Kwema Wakuu,
Mwezi uliopita nilihama rasmi kutoka kutumia RAV4 mpaka Subaru Forester ya 2011. RAV4 nliokua nikitumia ni "Kili time" ya mwaka 2000, engine 1ZZ, CC 1770, front wheel.
Sasa nimekuja kwenye Subaru, CC 2000 full time 4wd naona kama mambo hayaendi hivi kwa upande wangu. Yaan mazoea mabaya mafuta niliyokua naweka Kwa RAV4 nimeongeza consumption kwa kama 40% to 50% hapo ndio kwanza imported, likianza kuchoka si ndo itakua shida zaid?
Sina mishe nyingi sana, wala sio mzee wa masafa marefu. Sijatoka Dar Kwa Self Drive mwaka wa 7 labda huu. Makazi Makumbusho na kazi Posta, muda wote foleni hivyo hata speed 80 kama sio darajani pale tanzanite mara moja moja sikumbuki lini nilishawahi kuendesha hii speed.
Sasa naona nifunge mfumo wa CNG, nasoma promo zake kua unaokoa gharama za mafuta kwa % nyingi tu, mnanishauri vipi Wataalam? Ita athiri Chochote kwenye gari labda? Kuna Magari sio suitable labda kufunga huu Mfumo?
Na nikifunga nikaona ni miyeyusho si nikiutoa gari itarud kua poa tu kama mwanzo? Au ndio "nikishaharibu" ndo mwanzo huo nitegemee kua mgeni wa kudumu wa mafundi Subaru kila Leo?
Msaada wenu muhimu wakuu,
🙏🏾
NB;
Ukifunga CNG Ikapata Ajali (Kuungua Labda), Bima watalipa?
Au inabidi uwataarifu kabla ili mkubaliane upya terms na premium?
Mwezi uliopita nilihama rasmi kutoka kutumia RAV4 mpaka Subaru Forester ya 2011. RAV4 nliokua nikitumia ni "Kili time" ya mwaka 2000, engine 1ZZ, CC 1770, front wheel.
Sasa nimekuja kwenye Subaru, CC 2000 full time 4wd naona kama mambo hayaendi hivi kwa upande wangu. Yaan mazoea mabaya mafuta niliyokua naweka Kwa RAV4 nimeongeza consumption kwa kama 40% to 50% hapo ndio kwanza imported, likianza kuchoka si ndo itakua shida zaid?
Sina mishe nyingi sana, wala sio mzee wa masafa marefu. Sijatoka Dar Kwa Self Drive mwaka wa 7 labda huu. Makazi Makumbusho na kazi Posta, muda wote foleni hivyo hata speed 80 kama sio darajani pale tanzanite mara moja moja sikumbuki lini nilishawahi kuendesha hii speed.
Sasa naona nifunge mfumo wa CNG, nasoma promo zake kua unaokoa gharama za mafuta kwa % nyingi tu, mnanishauri vipi Wataalam? Ita athiri Chochote kwenye gari labda? Kuna Magari sio suitable labda kufunga huu Mfumo?
Na nikifunga nikaona ni miyeyusho si nikiutoa gari itarud kua poa tu kama mwanzo? Au ndio "nikishaharibu" ndo mwanzo huo nitegemee kua mgeni wa kudumu wa mafundi Subaru kila Leo?
Msaada wenu muhimu wakuu,
🙏🏾
NB;
Ukifunga CNG Ikapata Ajali (Kuungua Labda), Bima watalipa?
Au inabidi uwataarifu kabla ili mkubaliane upya terms na premium?