Kuhusu katiba mpya

haulecarolus

New Member
Apr 1, 2012
2
2
Ndugu zangu watanzania, nawaomba sana kuhusu suala hili la tume ya katiba tujaribu kuwa na uvumilivu wa kisiasa tukishaanza kupandikiza mambo ya udini hatari iliyo mbele yetu itakuwa kubwa sana, tume imeapishwa leo, watoa maoni ni sisi wananchi na waamuzi wa mwisho wa suala hili la katiba ni sisi wananchi, ndio tukakao piga kura za maoni kuikubali au kuikataa hiyo rasimu ya katiba itakayoletwa.

Sikatai maoni ya wanaoona kuna uwiano mdogo wa udini kwa wajumbe walioteuliwa yaani 9 kwa 21, labda nimshauri tu mh rais jk ameliona hili au lilimpita kushoto?

Kama ameliona basi alifanyie kazi kama alivyofanyia kazi musuada ule kule bungeni kwa kuwasikiliza wadau mapema ili hili nalo lisije likaleta kizazaa. Ila sisi wadau ebu tuwe na subira kidogo. Mungu ibariki tanzania, haule.
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Haule, karibu JamiiForums.

Leo hii nimekereka sana na suala la udini. Mimi ni Mkatoliki lakini siko tayari hata kwa kuning'inizwa kumtazama Dr Salim kama Mwislam. Dr Salim si Mwislam, si Mzanzibari, si Mwarabu, si Mwanaume. Dr Salim ni Dr Salim. Dr Salim ana-occupy special position katika nchi hii kwa identity inayoitwa "Dr Salim" fullstop. Niko tayari kuona Tanzania haipati katiba mpya ikiwa mawazo ya dini yatatakiwa ku-guide kupatikana kwake. Niko Tayari pia kuikosa Tanganyika yangu ikiwa nitaipata kwa kusaidiwa na Wakristo wenzangu. Huu ni uzoba wa hali ya juu. Waafrika wape silaha wataanza tu kupigana bila sababu. Nimekereka sana. Sana.
 
Ndugu zangu watanzania huu ni wakati wa kujitolea nafsi zetu kwa ajili ya tanzania yetu, kwani mchakato wa kuunda katiba si suala la dogo na la mzaa na sio suala la kumwachia mtu mmoja jukumu hili. Sasa ni fursa yetu watanzania kujenga nchi yenye falsafa inayoeleweka kwa kila moja wetu, na kwa ajili ya maendeleo yetu na vizazi vijavyo, Tusikubali waasi waendelee kuiangamiza nchi yetu na kutunyima macho yasiyo na viini vya kutuwezesha kuona, katiba hii mpya inayojengwa kutokana na roho za kizalendo za kitanzania ilete uhuru wa kweli katika nyanja zote za kiuchumi, kisiasa,kitamaduni na kifikra.kwani "DAGAA LA UGUVI HALITAKI UPUUZI SHARTI UACHE MAMBO NA BAADHI NDIPO UPATE MCHUZI".
 
Back
Top Bottom