Kuhusu CHADEMA kuwafuta/ kuwafukuza ubunge akina Lwakatare, Selasini, Komu na Silinde: Nakubaliana na Spika Ndugai

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,517
Nisiwe mnafiki wala wa maneno mengi, nakubaliana na Spika Ndugai kuwa CHADEMA haiwezi kumfuta au kumfukuza ubunge mtanzania yeyote. Kama maamuzi ya CHADEMA yaliyotangazwa na Karibu Mkuu wao Mnyika yalikuwa ya kuwafukuza ubunge akina Lwakatare, Spika Ndugai yuko sahihi kukemea.

Naamini Spika Ndugai anajua kuwa kikatiba na kisheria, sifa mojawapo ya lazima ya kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge ni kuwa mwanachama wa chama kimojawapo cha siasa hapa nchini na afadhiliwe na chama hicho katika kugombea. Hilo ni takwa la kikatiba na kisheria.

Naamini pia kuwa Spika Ndugai anajua fika kabisa kuwa kukoma kwa ubunge kumeainishwa kikatiba na kisheria kwa kuorodhesha mambo yanayofanya ubunge ukome. Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sura Nambari 2 ya Sheria za Tanzania, moja ya jambo la lazima linalokomesha ubunge ni kukoma/ kuacha/ kusita kuwa mwanachama wa chama ambacho Mbunge husika alikuwa mwanachama wakati akigombea(Ibara ya 71(1)).

Iko wazi kuwa, na imeshatokea mara nyingi hapa nchini, mara tu baada ya uanachama wa Mbunge kukoma, ubunge wake nao unakoma. Hiyo ndiyo sheria halali iliyopo hivi sasa na inatumika kila uchao. Ndiyo kusema, vyama vimepewa nguvu ya kuupeperusha ubunge kwa kumfukuza uanachama tu Mbunge.

Mchungaji Marahemu Christopher Mtikila aliiona kadhia hii ya kumlazimisha mgombea wa Urais, Ubunge, Udiwani na kadhalika kuwa mwanachama na kufadhiliwa na chama. Akapambana kimahakama kuanzia kule Dodoma na hata Dar es Salaam.

Alipata ushindi mara mbili Mahakama Kuu Dodoma na Dar es Salaam lakini akagonga mwamba Mahakama ya Rufani kwenye shauri maarufu kama la Mgombea Binafsi. Bunge liliachiwa mamlaka yake ya kubadili katiba na sheria ili kuruhusu jambo hilo. Bado tunasubiri hatma ya jambo husika.

Kikatiba na kisheria, kupoteza uanachama wa chama cha siasa kilichomfadhili Mbunge wakati akigombea kunampotezea moja kwa moja ubunge wake. Kinachopaswa kufanywa na chama husika ni kupeleka kwa Mamlaka husika maamuzi yake hayo ya kumfukuza uanachama Mbunge. Basi. Baada ya hapo, Katiba na sheria zinachukua mkondo wake. Maelezo au kauli au tamko la yeyote halifui dafu.

Naamini Spika Ndugai anajua kuwa kwa hali ya sasa ya kikatiba, kisheria na kisiasa, kufukuzwa uanachama wa chama ni jambo linalopaswa kuepukwa na kila aliyechaguliwa akiwa mwanachama na aliyefadhiliwa na chama husika. Na hapo ndipo nidhamu kwa chama inapojikita na kujidai.

Itoshe kusema kuwa kikatiba na kisheria, kuanzia Rais, Mbunge, Diwani na kadhalika, uanachama unapokoma na nafasi hiyo inapotea mara moja na mhusika hawezi tena kikatiba na kisheria kuwa Rais, Mbunge, Diwani na kadhalika. Hadi hapo mambo hayo yatakavyobadilishwa kwenye Katiba na sheria zetu, kwasasa uanachama ni lulu.

Kama CHADEMA wamewafukuza uanachama akina Lwakatare, Selasini, Komu na Silinde, ubunge wao unakoma mara moja. Na hawapaswi kuwa Wabunge. Kama wamewafukuza ubunge, ni kinyume na katiba na sheria kwakuwa hawana mamlaka hayo.
 
Mwanasheria Petro E. Mselewa wajua tamko la chama cha Chadema lilkuwa lipi?

Chadema katika tamko lao wamesema kuwa katika kikao chao cha chama cha Kamati Kuu, wameamua kuwavua uanachama wabunge wao 4

Kwa hiyo "automatically" na ubunge wao unakuwa umekoma, kwa kuwa hapa nchini, ni takwa la kisheria, ndani ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ibara ya 71(1)(e) kuwa kamwe huwezi kuwa Mbunge, bila kuwa mwanachama wa chama cha siasa
 
Naona una horoja tu hapa kama huyo Ndungai wako, Chadema hakijamfukuza mtu ubunge kimewafukuza uanachama. . Hilo la ubunge ni la Bunge na katiba ya Nchi.

Mambo ya Mtikila hata CCM waliyakataa na kuamua kuzuia kwa nguvu independent candidate.

Jiulize wakat Nyalandu anavuliwa ubunge baada ya kukoma kuwa mwanachama wa CCM huyo Ndungai hakuwepo?
 
Unapaswa kutumia akili huru, usilazimishe kuwa mfungwa wa mafungamano. Usilazimishe ku take sides.

Katika suala hili, ungeweza kutofautiana na CHADEMA bila ya kukubaliana na Ndugai. Kuna point gani aliyo make Ndugai hata ulazimike kufungamana na mawazo yake? Yaani kwa kuwa tu CHADEMA wamekosea basi unahamishie akili kwingine?
 
Safi ungemkumbusha pia spika wabunge waliofukuzwa na CCM na ubunge wao kukoma akiwemo yule wa Zbar na Sophia Simba. Mkumbushe pia wabunge 8 wa CUF waliopoteza ubunge baada ya kufukuzwa uanachama na Lipumba na yeye spika akabariki. Mkumbushe pia kisa cha Zitto na Nyalandu.

Inaonekana hana kumbukumbu kabisa. Sidhani kama CHADEMA wameandika barua kuwa wamewafukuza ubunge wabunge hao. Muulize pia kuhusu Mwambe aliyejiuzulu mwenyewe na kutokwenda bungeni amemrudishaje bungeni?

Mbona hakumrudisha Nyalandu. Topic yako nzuri lakini naona ingekuwa pana na nzuri zaidi kama ungeiongezea nyama kama hizo zaidi maana inaonekana spika dish limeyumba.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ulivyoanza sikukuelewa kabisa, almanusra nianze kukujibu. Nikijipa moyo konde acha nimalize kumsoma huyu Mh, nimekuelewa sana.

Ni kweli Chadema hawana uwezo wa kumfuta mtu ubunge, Ila wanauwezo wa kumfuta uanachama. Baada ya hapo ubunge unakoma mara moja" Nanukuu tena ubunge unakoma mara moja".

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sikiliza vizuri maelezo ya John Mnyika, katibu mkuu "Wamejifukuza uanachama" baada ya kukosa sifa za kuwa wanachama kwa katiba ya Chadema, hawajafukuzwa Ubunge.

Wajibu wa Katibu mkuu huyo ni kupeleka barua ya kuonesha ni jinsi gani wamejifukuza uanachama na vifungu vya katiba ya chama chake, nakala ya barua hiyo aiwasilishe tume ya uchaguzi
 
Chadema ni wahuni Wasubirie October wataiona hasira ya Watanzania
Una bidii sana ya maono mfu, yatakuezeesha bure na huo umri wako mdogo.
Kwa taarifa ni kuwa hata mlioko lumumba tu mmeshagawanyika, hautaamini.

Tegemeo lenu kubwa lililobaki ni NECCM, POLICCM na ma DED, ambao nao watz wamekwisha wachoka baada ya miaka 18 ya ubabaishaji, na tumejipanga kula nao sahani moja.

Jitahidi na muombe Mungu wako akulinde ili uwepo kuja shuhudia. Amen
 
Nawe naona umejaa mawenge kwenye hili sakata,

Cdm haijawafukuza wala kuwavua nyadhifa zao za ubunge wahusika! Bali imewafuta uwanachama wa CHADEMA.

Wamevuliwa uanachama hao na kuanzia sasa siyo wanachama wa cdm.

In God we Trust
 
Back
Top Bottom