Kufutwa Semina, Mikutano na Warsha zachochea hasira vijana kutaka mishahara iwe sawa kwa wote

seedfarm

JF-Expert Member
Feb 9, 2020
260
2,654
Kabla ya mwaka 2015 Vijana wengi walipata kazi serikalini na waliridhika kabisa na mishahara yao. Nyuma ya pazia kulikuwa ni siri kubwa zilizojificha ambazo ziliwafanya waone mishahara inatosha na kukidhi mahitaji.

Semina na Mikutano ndio chanzo kikubwa kilichowasaidia wazee wetu kusomesha na kujenga makazi ya kuishi. Lakini semina na mikutano ya wazee wa zamani ilisaidia kutatua changamoto za wakati huo

Semina na warsha ziligeuka kuwa eneo la upigaji enzi za Rais wetu mpendwa J Kikwete, Watu waligawana safari kuelekea bara ulaya, America kaskazini, Asia na Australia na pesa za semina hizi zilifanya watu walidhike na mishahara huku wakisomesha ndugu na jamaa

Spana na kishindo cha awamu ya tano maeneo kama Halmashauri za wilaya na manispaa hali imekuwa tete kwa vijana kwani mrija wa semina na warsha zimekata

Walimu wa sekondari na msingi wao maisha yao ni yale yale hawakutegemea warsha na mikutano kama taasisi zingine za Serikali

Mshahara wa mtu ni siri, Na kama ingekuwa sio siri basi taasisi zinazosemwa zinalipwa pesa nyingi utacheka sana, Ni kweli wale waliofikia level au hatua ya Ukurugenzui au Umanager wana unafuu kidogo sana

Wafanyakazi wa taasisi zinazosemwa kubwa basi watu wanaacha kazi huko na kwenda kwenye taasisi binafsi zenye mishahara mikubwa.

Watu wa taasisi zinatuhumiwa humu wanaishi kwa mikopo tu, Wamekopa kuanzia magari ya kutembelea, Nyumba na bado wanasubiri wakistaafu pension yao ikatwe kufidia mikopo ya nyumba na magari, Haya maisha yana siri kubwa sana usione watu wapo kwenye Landcruiser Vx V8 halafu ni wafanyakazi wa BOT au TRA kuna siri kubwa labda kama ni Mzee wa mangumasha, misheni town na mpiga dili hao hakuna shida

Tatizo ukiwa na gari haramu la kuzulumu watu, au nyumba umejenga haramu kwa kuzulumu watu roho huwa inauma sana sana maishani unakosa furaha kabisa, Mimi ni muhanga wa kununua kitu kwa kupiga deal hakika baada ya miaka kadhaa niliamua kukiuza kile kitu maana kila wakati roho ilinisuta kuwa nimepiga dili haramu na kuzulumu wengine

Ni kawaida kuwakuta vijana wameacha kazi BOT baada ya kupata uzoefu na kwenda CRDB ,CITi Bank au USAID kutafuta maslahi makubwa baada ya spana za awamu ya tano

Ni kawaida vijana wa TRA kukimbia kazi na kuelekea taasisi binafsi au kuamua kufanya biashara binafsi

Maneno ni mengi sana lakini ikumbukwe taasisi baadhi za serikali walijipangia wao mishahara kutokana na kuwa na uhakika wa kupata pesa

Hakuna siku mtu mshahara utamtosha maishani mwake ishu ni mpangilio na vipaumbele tu, Kuna vijana maofisini umemzidi mshahara mara 10 lakini mwisho wa mwezi ukikaribia unajikuta huna kitu lakini dogo yupo vizuri kila wakati na unamuazima pesa. Ishu hapa ni utunzaji wa fedha na hii kitu wachache wanaweza kutunza pesa labda wahindi na wakinga wana roho ngumu
 
Semina gani zimefutwa?? Mbona waganga na wahudumu mbalimbali wa afya wanaenda kila siku??
Semina na Safari zipo kwa kibali maalumu

Zile semina za halmashauri watu wakiona hawana pesa wanaenda kwa RAS au DED wanampa mchongo basi kesho utasikia semina ya wafanyabiashara

Baada ya hapo inaandaliwa Paylist ,Anatumwa Cashier Bank na Cheque anakuja na pesa maburungutu ya kutosha,Anatengewa Big boss kwenye bahasha ya kaki halfu sekretari anampelekea

Kiasi kilichobaki mnagawana na kinakuwa cha kutosha kinachokufanya uweze kununua Bajaji ndogo au pikipiki sita za mchina

Hii story naongelea enzi zile za JK, Marafiki na Jamaa ndio walichokuwa wanafanya weekend hasa hasa ijumaa entry inapita kwa ajili ya kula bata

Kwa sasa wamebaki vumbi tupu hata kandambili zinawapwaya baada ya kishindo cha awamu ya Tano

Poleni marafiki sana sana hakika semina zilileta umoja week end na undugu

Kwa mujibu wa story zao kwa sasa nasikia kila ofisi kumejaa Nyoka, Hakuna anayemuamini mwenzake kwa sasa, Ukianzisha story za semina unaona watu wanajifanya wanaenda msalani kumbe ndio kimoja hiyo hakuna kuaminiana tena bali hofuuuiii.... Uui

Na hofu ndio uzalendo wenyewe
 
Semina na Safari zipo kwa kibali maalumu

Zile semina za halmashauri watu wakiona hawana pesa wanaenda kwa RAS au DED wanampa mchongo basi kesho utasikia semina ya wafanyabiashara..
Haaaaaaa haaaaaa. Nimekuelewa kiungozi. Umenikumbusha mbali saaana. Watu walikuwa wakiona fedha ya maendeleo ya jimbo zikutumwa wahuni wahuni wanazitengenezea namna ya kuzigawana kwa vikao vya kikanjanja, huku wao mishahala yao hawajui imeingia lini. Kwakweli kulikuwa na wizi wa hali juuu saaaàaanaaaaa
 
Kukatwa kwa hizi fedha zilizokuwa zinaliwa hovyo kumesababisha hasira na kushuka kwa morali ya kufanya kazi kwa watumishi wa Serikali usipime!

Wengi wapo tu bora siku ziende maana wengi hawana pa kwenda wala cha kufanya maana maishani ni watu wa kutegemea vyeti tu!
Leo hii kazi iliyokuwa ikichukua siku 3 hadi 7 pale BRELA inachukuwa hadi Mwaka mzima kukamilika!

Ukipiga simu au ukienda kuulizia jambo pale BRELA watu wanahasira siyo za Nchi hii!
 
Hizo posho na semina za safari mara zote zimekuwa zinawahusu watu wachache tu kuanzia wakuu wa idara na wakurugenzi, asilimia kubwa ya watumishi wanategemea salary pekee, hawa wanaponyimwa kupandishwa madaraja na nyongeza zao za mishahara na pesa za likizo unakuwa unawaweka kwenye wakati mgumu sana....
 
Serikali imetoka katika akili za kijamaa; ila wananchi bado.

It’s a free market kama mtu anaona elimu yake ina thamani zaidi kuliko mshahara anaolipwa serikalini kitu gani kinamzuia asiamie private au ajiajiri mwenyewe au afungue biashara; kuliko kulamimika kila siku.

Kila mtu nchi hii biashara yake inayotegemea serikali akikosa tender au maslahi yake yanapobwana anaanza kuilalamikia serikali.

Hizo ndio fikra za wananchi kwenye soko huru kweli? wengi wetu bado wajamaa kiakili wakati serikali ishatoka huko kwa asilimia kubwa. Hapo ndio tatizo lilipo.
 
Semina zilikuwa na athari zake
Wengi walipata ukimwi kwenye hizo semina Tacaaids ikitaka ihoji wafanyakazi wanaoumwa ukimwi kuwa walipatia wapi na mimba kibao za nje ya ndoa zilitungwa huko kuanzia serikalini bungeni na mahakama !!!! Iwe ndani ya nchi au Watoto wengi mimba zao zimetungwa kwenye Semina na warsha!!!! Mitoto mingi inatakiwa ipewe majina ya Semina au Warsha

Semina yalikuwa madanguro ya watu kwenda kufanya ufusika kwa gharama za ofisi za posho za safari

Ndoa nyingi hizo semana na warsha zimezivunja

Pia kulikuwa na upendeleo wa juu na rushwa wengine unakuta hawaendi kabisa wengine kila siki airport au safari!!
Wengine kwa mwaka kukaa ofisi ilikuwa Nadra kutwa huko semina na warsha!


Semina na warsha walienda sana sana wakae wayafanyie kazi yale waliyopata kwenye Semina na warsha kipindi cha Kikwete
 
Kukatwa kwa hizi fedha zilizokuwa zinaliwa hovyo kumesababisha hasira na kushuka kwa morali ya kufanya kazi kwa watumishi wa Serikali usipime!
Wengi wapo tu bora siku ziende maana wengi hawana pa kwenda wala cha kufanya maana maishani ni watu wa kutegemea vyeti tu!
Leo hii kazi iliyokuwa ikichukua siku 3 hadi 7 pale BRELA inachukuwa hadi Mwaka mzima kukamilika!
Ukipiga simu au ukienda kuulizia jambo pale BRELA watu wanahasira siyo za Nchi hii!
Mmmh kumbe hasira
 
Kila kitu bado kipo utofauti ni kwamba wanaofaidi ni rank fulani tu.
Hata upigaji wa mali za umma bado upo mkubwa tu utofauti ni kwamba unaonjiniwa na mtu mmoja tu.
 
wachache wanaweza kutunza pesa labda wahindi na wakinga wana roho ngumu
Mm huwa nikipata pesa nataka initunze. Sitakagi kqbisa ujinga wa kutunza pesa. Nina kanuni yangu nimejiwekea kuwa "kula bata kufa kwaja".

BTW, roadmap ya maisha ya kila mwanadamu imeshaandaliwa na God, ndiyo maana kuna watu huwa wanaokota dhahabu ama kushinda biko kwasabb roadmap yao God aliiandaa kuwa one day watakuwa matajiri.


Fanya ufanyacho. Tunza pesa utunzavyo kama God kakuandikia umaskini kunuka hutoboi. Ndiyo maana unaona kuna watu wanatunza pesa halafu wakifikia hatua ya kutoboa ajali ya moto hutokea na kutekwteza mali ama magonjwa yasiyotibika huibuka na kuwaharibia mishe.
 
Mm huwa nikipata pesa nataka initunze. Sitakagi kqbisa ujinga wa kutunza pesa. Nina kanuni yangu nimejiwekea kuwa "kula bata kufa kwaja".

BTW, roadmap ya maisha ya kila mwanadamu imeshaandaliwa na God, ndiyo maana kuna watu huwa wanaokota dhahabu ama kushinda biko kwasabb roadmap yao God aliiandaa kuwa one day watakuwa matajiri.


Fanya ufanyacho. Tunza pesa utunzavyo kama God kakuandikia umaskini kunuka hutoboi. Ndiyo maana unaona kuna watu wanatunza pesa halafu wakifikia hatua ya kutoboa ajali ya moto hutokea na kutekwteza mali ama magonjwa yasiyotibika huibuka na kuwaharibia mishe.
Kula bata nasema kula bata
 
Kabla ya mwaka 2015 Vijana wengi walipata kazi serikalini na waliridhika kabisa na mishahara yao. Nyuma ya pazia kulikuwa ni siri kubwa zilizojificha ambazo ziliwafanya waone mishahara inatosha na kukidhi mahitaji.

Semina na Mikutano ndio chanzo kikubwa kilichowasaidia wazee wetu kusomesha na kujenga makazi ya kuishi. Lakini semina na mikutano ya wazee wa zamani ilisaidia kutatua changamoto za wakati huo

Semina na warsha ziligeuka kuwa eneo la upigaji enzi za Rais wetu mpendwa J Kikwete, Watu waligawana safari kuelekea bara ulaya, America kaskazini, Asia na Australia na pesa za semina hizi zilifanya watu walidhike na mishahara huku wakisomesha ndugu na jamaa

Spana na kishindo cha awamu ya tano maeneo kama Halmashauri za wilaya na manispaa hali imekuwa tete kwa vijana kwani mrija wa semina na warsha zimekata

Walimu wa sekondari na msingi wao maisha yao ni yale yale hawakutegemea warsha na mikutano kama taasisi zingine za Serikali

Mshahara wa mtu ni siri, Na kama ingekuwa sio siri basi taasisi zinazosemwa zinalipwa pesa nyingi utacheka sana, Ni kweli wale waliofikia level au hatua ya Ukurugenzui au Umanager wana unafuu kidogo sana

Wafanyakazi wa taasisi zinazosemwa kubwa basi watu wanaacha kazi huko na kwenda kwenye taasisi binafsi zenye mishahara mikubwa.

Watu wa taasisi zinatuhumiwa humu wanaishi kwa mikopo tu, Wamekopa kuanzia magari ya kutembelea, Nyumba na bado wanasubiri wakistaafu pension yao ikatwe kufidia mikopo ya nyumba na magari, Haya maisha yana siri kubwa sana usione watu wapo kwenye Landcruiser Vx V8 halafu ni wafanyakazi wa BOT au TRA kuna siri kubwa labda kama ni Mzee wa mangumasha, misheni town na mpiga dili hao hakuna shida

Tatizo ukiwa na gari haramu la kuzulumu watu, au nyumba umejenga haramu kwa kuzulumu watu roho huwa inauma sana sana maishani unakosa furaha kabisa, Mimi ni muhanga wa kununua kitu kwa kupiga deal hakika baada ya miaka kadhaa niliamua kukiuza kile kitu maana kila wakati roho ilinisuta kuwa nimepiga dili haramu na kuzulumu wengine

Ni kawaida kuwakuta vijana wameacha kazi BOT baada ya kupata uzoefu na kwenda CRDB ,CITi Bank au USAID kutafuta maslahi makubwa baada ya spana za awamu ya tano

Ni kawaida vijana wa TRA kukimbia kazi na kuelekea taasisi binafsi au kuamua kufanya biashara binafsi

Maneno ni mengi sana lakini ikumbukwe taasisi baadhi za serikali walijipangia wao mishahara kutokana na kuwa na uhakika wa kupata pesa

Hakuna siku mtu mshahara utamtosha maishani mwake ishu ni mpangilio na vipaumbele tu, Kuna vijana maofisini umemzidi mshahara mara 10 lakini mwisho wa mwezi ukikaribia unajikuta huna kitu lakini dogo yupo vizuri kila wakati na unamuazima pesa. Ishu hapa ni utunzaji wa fedha na hii kitu wachache wanaweza kutunza pesa labda wahindi na wakinga wana roho ngumu
Na hili litapita
 
Acha porojo wewe. Mwambie Mzee wako apandishe Wafanyakazi madaraja yao. Ni mwaka wa sita huu sasa, mnaleta tu porojo!

Mara uhakiki, mara tunanunua ndege, mara TIN NUMBER, mara warsha!!Hivi nyinyi ni watu wa aina gani? Hamna kabisa huruma na maisha ya wenzenu!!
 
Mlio
Kabla ya mwaka 2015 Vijana wengi walipata kazi serikalini na waliridhika kabisa na mishahara yao. Nyuma ya pazia kulikuwa ni siri kubwa zilizojificha ambazo ziliwafanya waone mishahara inatosha na kukidhi mahitaji.

Semina na Mikutano ndio chanzo kikubwa kilichowasaidia wazee wetu kusomesha na kujenga makazi ya kuishi. Lakini semina na mikutano ya wazee wa zamani ilisaidia kutatua changamoto za wakati huo

Semina na warsha ziligeuka kuwa eneo la upigaji enzi za Rais wetu mpendwa J Kikwete, Watu waligawana safari kuelekea bara ulaya, America kaskazini, Asia na Australia na pesa za semina hizi zilifanya watu walidhike na mishahara huku wakisomesha ndugu na jamaa

Spana na kishindo cha awamu ya tano maeneo kama Halmashauri za wilaya na manispaa hali imekuwa tete kwa vijana kwani mrija wa semina na warsha zimekata

Walimu wa sekondari na msingi wao maisha yao ni yale yale hawakutegemea warsha na mikutano kama taasisi zingine za Serikali

Mshahara wa mtu ni siri, Na kama ingekuwa sio siri basi taasisi zinazosemwa zinalipwa pesa nyingi utacheka sana, Ni kweli wale waliofikia level au hatua ya Ukurugenzui au Umanager wana unafuu kidogo sana

Wafanyakazi wa taasisi zinazosemwa kubwa basi watu wanaacha kazi huko na kwenda kwenye taasisi binafsi zenye mishahara mikubwa.

Watu wa taasisi zinatuhumiwa humu wanaishi kwa mikopo tu, Wamekopa kuanzia magari ya kutembelea, Nyumba na bado wanasubiri wakistaafu pension yao ikatwe kufidia mikopo ya nyumba na magari, Haya maisha yana siri kubwa sana usione watu wapo kwenye Landcruiser Vx V8 halafu ni wafanyakazi wa BOT au TRA kuna siri kubwa labda kama ni Mzee wa mangumasha, misheni town na mpiga dili hao hakuna shida

Tatizo ukiwa na gari haramu la kuzulumu watu, au nyumba umejenga haramu kwa kuzulumu watu roho huwa inauma sana sana maishani unakosa furaha kabisa, Mimi ni muhanga wa kununua kitu kwa kupiga deal hakika baada ya miaka kadhaa niliamua kukiuza kile kitu maana kila wakati roho ilinisuta kuwa nimepiga dili haramu na kuzulumu wengine

Ni kawaida kuwakuta vijana wameacha kazi BOT baada ya kupata uzoefu na kwenda CRDB ,CITi Bank au USAID kutafuta maslahi makubwa baada ya spana za awamu ya tano

Ni kawaida vijana wa TRA kukimbia kazi na kuelekea taasisi binafsi au kuamua kufanya biashara binafsi

Maneno ni mengi sana lakini ikumbukwe taasisi baadhi za serikali walijipangia wao mishahara kutokana na kuwa na uhakika wa kupata pesa

Hakuna siku mtu mshahara utamtosha maishani mwake ishu ni mpangilio na vipaumbele tu, Kuna vijana maofisini umemzidi mshahara mara 10 lakini mwisho wa mwezi ukikaribia unajikuta huna kitu lakini dogo yupo vizuri kila wakati na unamuazima pesa. Ishu hapa ni utunzaji wa fedha na hii kitu wachache wanaweza kutunza pesa labda wahindi na wakinga wana roho ngumu
Mliigeuza nchi Shana la Bibi Sasa kazi kwenu
Ukitaka kufaidi awamu hii ya Rais mwema mwenye Moyo wa huruma na upendo kwa RAIA wake
Tii sheria bila shuruti
Lipa kodi
Vinginevyo utaumia sana maana mianya ya wapiga dili imeziba kabisa
 
Mk
Acha porojo wewe. Mwambie Mzee wako apandishe Wafanyakazi madaraja yao. Ni mwaka wa sita huu sasa, mnaleta tu porojo!

Mara uhakiki, mara tunanunua ndege, mara TIN NUMBER, mara warsha!!Hivi nyinyi ni watu wa aina gani? Hamna kabisa huruma na maisha ya wenzenu!!
Mkuu ni kweli nchi hii iligeuzwa shamba la Bibi
Kwa sasa Ukitaka kuishi kwa raha katika awamu hii ya Rais mwema mwenye Moyo wa huruma na upendo kwa RAIA wake
Tii sheria bila shuruti
Lipa kodi
Utafaidi sana
Vinginevyo lazima uumie maana mianya yote ya wapiga dili imeziba kabisa
 
Kukatwa kwa hizi fedha zilizokuwa zinaliwa hovyo kumesababisha hasira na kushuka kwa morali ya kufanya kazi kwa watumishi wa Serikali usipime!

Wengi wapo tu bora siku ziende maana wengi hawana pa kwenda wala cha kufanya maana maishani ni watu wa kutegemea vyeti tu!
Leo hii kazi iliyokuwa ikichukua siku 3 hadi 7 pale BRELA inachukuwa hadi Mwaka mzima kukamilika!

Ukipiga simu au ukienda kuulizia jambo pale BRELA watu wanahasira siyo za Nchi hii!
Lumumba wanakuambi ufanisi umeimarika makazini
 
Back
Top Bottom