Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2020

Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2020

Daisam

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2016
Posts
2,622
Reaction score
3,144
Kwa hiki kipindi kifupi ambacho viongozi wa vyama mbalimbali wamekuwa wakitoa hotuba zao majukwaani, nimejifunza yafuatayo:-

(1)Kuna wagombea waliojiandaa kushinda Uchaguzi.
(2)Kuna wagombea waliojiandaa kushindwa Uchaguzi.

Wagombea waliojiandaa kushinda Uchaguzi mkuu wa mwaka huu 2020 wanaeleza sera zao kwa ustaarabu na unyenyekevu mkubwa sana. Kwa kufanya hivyo tu, wameshashinda tayari kwani Watanzania wanapenda zaidi amani.

Kwa wagombea waliojiandaa kushindwa Uchaguzi huu wa 2020, wao hawana mpango kutoa sera zao, bali hutumia muda mwingi(95%) . KUKEJELI, KUBEZA, KULAUMU, KULALAMIKA, KUTUKANA, KULETA VITISHO, KULIA LIA NA HATA KUSHAWISHI WATANZANI KUANDAMANA.

Hayo yote hutolewa kwa lugha kali za kutisha na kuwaogofya Watanzania. Maoni yangu ni kwamba, WATANZANI wa leo si wajinga kiasi hicho. Wanasikiliza na kupima hoja kwa kina. Kama kweli wagombea wanataka kuchaguliwa katika Uchaguzi huu, hawanabudi kubadili staili ya Kampeni zao majukwaani, yaani kupiga Kampeni za kistaarabu.

Amimi, Amimi nawaambia, hakuna mtanzania hata mmoja atakayekubali kuacha shughuli zake zinazomwingizia kipato na kwenda kushiriki MAANDAMANO yasiyo na kichwa wala miguu.
 
Hawaendi na Wakati watanzania wa Sasa ni more educated kuliko wale wa miaka ya Kikwete .Lile kundi la vijana wa waliotumiwa na Upinzani wengi waneshmaliza vyuo vikuu uelewa wao uko juu mno.Upinzani wanadhani watu Ni wale wale wa enzi za Kikwete !!! Za Hadi 2015

Wa Sasa Ni more knowledgeable Huwezi ongea Kama miaka ile porojo uka win their hearts
 
maandamano ni sehemu ya haki za watanzania, kwani ccm mnavyoandamana kuunga mkono juhudi mnakuwa mmekosa kazi.
 
Ukisikia mtawala anataka wananchi wawe wapole na wadumishe Amani sio kwa sababu ya nchi bali kwa maslahi yake kubakia madarakani.


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Miaka yote ya uchaguzi Mkuu, Kuna kashfa za uchotaji Pesa serikalini na huibuliwa baadae. Safari hii 1.5 Trillion ilichotwa mapema.
Tukumbuke EPA Ni ya mwaka gani

Meremeta, KAGODA, etc

ESCROW Ni 2005

Pesa za kuweka Mabango nchi Nzima

Kununua vitenge na kifua

Kulipa wasanii
 
Hawaendi na Wakati watanzania wa Sasa ni more educated kuliko wale wa miaka ya Kikwete .Lile kundi la vijana wa waliotumiwa na Upinzani wengi waneshmaliza vyuo vikuu uelewa wao uko juu mno.Upinzani wanadhani watu Ni wale wale wa enzi za Kikwete !!! Za Hadi 2015

Wa Sasa Ni more knowledgeable Huwezi ongea Kama miaka ile porojo uka win their hearts
Hao watu bado wapo. Angalia humu mitandaoni lugha zilizotapakaa na hata huko majukwaani kwao katika kampeni ni HADI KIELEWEKE, TUSIKUBALI, TOKENI BARABARANI, NA MWINGINER HADI ANASEMA WATU WATOKE NA MUNDU, PANGA, MKUKI, JIWE. Sasa hizo sio siasa.
 
Magufuli ajiandae kukabidhi Ikulu Tarehe 28 October 2020 Kwa Lissu.
 
Back
Top Bottom