Supervision
JF-Expert Member
- Jun 16, 2016
- 265
- 203
Faida ya kuwaongezea walimu mishahara mizuri!Habarini ndugu zangu wa JF.Nimeamua kuleta bandiko langu baada ya tathimini niliyoifanya kwa hawa ndugu zetu walimu.
Bila kupoteza muda naomba nirudi kwenye hoja,faida za kuongezea mishahara waalimu ambazo ni kama ifuatavyo:
01.Kuinua mtu wa chini.Ikumbukwe kuwa walimu wapo kila kijiji hivyo unapoongeza mshahara kwa walimu unaongeza kitu kikubwa.Ujue kama kijiji kina waalimu kumi au ishirini na ukawapa shilingi milioni moja na kuendelea ujue kuna milioni zaidi ya kumi zipo kijijini hapo.Walimu hawa watapeleka pesa zao kwa wafanya biashara wadogowadogo watanunua mafuta ya kupikia,soda,sukari na vingine vingi.Lakini kama haitoshi waalimu wengi hujihusisha na kilimo hivyo wale watu wanaowalimia kupanda na kuvuna watajipatia pesa,na kadiri anavyoongezewa pesa ndivyo atakavyo lima zaidi.
Hapa mtu wa chini atakuwa anajipatia kipato na kuongeza mzunguko wa pesa mjini na kijijini kwani hata mjini waalimu ni wengi zaidi.Watu wanaotegemea ajira kutokana na mishahara ya walimu wataongezeka kwani sasa mwalimu anapata zaidi hivyo anapofanya zaidi katika kilimo au kazi nyingineyo ujue vibarua wake wanaomfanyia huongezeka na kujipatia pesa ama wanaomuuzia vitu watapata zaidi na kupelekea kuongeza mzunguko wa pesa.
02.Kuwaongezea walimu mishahara mizuri kutafanya wengi kusomea ualimu na kufanya walimu wawe kila mahali.Yaani siku zote waalimu hukubali kuwa kinachowafanya wawe chini siyo kazi mbaya,bali hudharaulika kwasababu ya maslahi madogo.Uchumi mdogo huwafanya wadharaulike.
03.Itaongeza hamu ya kazi.Siku zote maslahi humfanya mtu awe tayari kufanya kazi usiku na mchana.Naukitaka kuamini tazama walimu wa private hupenda kazi zao na kufanya kwa mashindano lakini mwalimu huyohuyo wa private aliyekuwa akafaukusha saba ukimpeleka shule za serikali hufanya kazi chini ya kiwango tatizo ni maslahi.
04.Kuongeza pato la taifa kupitia kodi kwani mwalimu anapolima mazao na kuuza ataongeza pato kupitia kodi na akianzisha mradi endapo ataweza kupata pesa nzuri kutokana na mshahara wake ataajiri watu katika mradi wake na kulipa kodi.Kama kila kijiji kati ya waaalimu kumi,watano watafungua biashara basi ajira nyingi zitatengenezwa na kodi kuongezeka.
Jamani hata posho kila katikati ya mwezi kama kada zingine hakuna!Ngoja niendelee;
05.Kuongeza ufaulu.Jamani kuna watu wengi waliingia kazini kwa kuupenda ualimu yaani tulikuwa na mwalimu anafurahia kufundisha hadi raha na anaeleweka ila baadaye akaonekana kukatishwa tamaa.Sasa watu hawa wapo wengi kama mwalimu wa shule ya msingi angekuwa na uhakika wa kupata milioni nina uhakika kunawalimu wangelala darasani wanakesha wakifundisha.<br />SALAMU KWA mama yetu Profesa Ndalichako.<br /><br />
06.Kusaidia mapinduzi ya viwanda nchini.Pale anapopata mshahara mzuri atalima sana yaani kama hupenda kulima pamba atalima mara dufu,kahawa,korosho,miti,na vingine Vingi.Kumbe basi hata malighafi za viwanda zitaongezeka na kuifanya nchi iharakishe katika mapinduzi ya viwanda.Chamsingi ni kufanya kilimo na biashara bila kukiuka sheria za Utumishi wao.
SAIDIA MWALIMU,USAIDIE TAIFA
Bila kupoteza muda naomba nirudi kwenye hoja,faida za kuongezea mishahara waalimu ambazo ni kama ifuatavyo:
01.Kuinua mtu wa chini.Ikumbukwe kuwa walimu wapo kila kijiji hivyo unapoongeza mshahara kwa walimu unaongeza kitu kikubwa.Ujue kama kijiji kina waalimu kumi au ishirini na ukawapa shilingi milioni moja na kuendelea ujue kuna milioni zaidi ya kumi zipo kijijini hapo.Walimu hawa watapeleka pesa zao kwa wafanya biashara wadogowadogo watanunua mafuta ya kupikia,soda,sukari na vingine vingi.Lakini kama haitoshi waalimu wengi hujihusisha na kilimo hivyo wale watu wanaowalimia kupanda na kuvuna watajipatia pesa,na kadiri anavyoongezewa pesa ndivyo atakavyo lima zaidi.
Hapa mtu wa chini atakuwa anajipatia kipato na kuongeza mzunguko wa pesa mjini na kijijini kwani hata mjini waalimu ni wengi zaidi.Watu wanaotegemea ajira kutokana na mishahara ya walimu wataongezeka kwani sasa mwalimu anapata zaidi hivyo anapofanya zaidi katika kilimo au kazi nyingineyo ujue vibarua wake wanaomfanyia huongezeka na kujipatia pesa ama wanaomuuzia vitu watapata zaidi na kupelekea kuongeza mzunguko wa pesa.
02.Kuwaongezea walimu mishahara mizuri kutafanya wengi kusomea ualimu na kufanya walimu wawe kila mahali.Yaani siku zote waalimu hukubali kuwa kinachowafanya wawe chini siyo kazi mbaya,bali hudharaulika kwasababu ya maslahi madogo.Uchumi mdogo huwafanya wadharaulike.
03.Itaongeza hamu ya kazi.Siku zote maslahi humfanya mtu awe tayari kufanya kazi usiku na mchana.Naukitaka kuamini tazama walimu wa private hupenda kazi zao na kufanya kwa mashindano lakini mwalimu huyohuyo wa private aliyekuwa akafaukusha saba ukimpeleka shule za serikali hufanya kazi chini ya kiwango tatizo ni maslahi.
04.Kuongeza pato la taifa kupitia kodi kwani mwalimu anapolima mazao na kuuza ataongeza pato kupitia kodi na akianzisha mradi endapo ataweza kupata pesa nzuri kutokana na mshahara wake ataajiri watu katika mradi wake na kulipa kodi.Kama kila kijiji kati ya waaalimu kumi,watano watafungua biashara basi ajira nyingi zitatengenezwa na kodi kuongezeka.
Jamani hata posho kila katikati ya mwezi kama kada zingine hakuna!Ngoja niendelee;
05.Kuongeza ufaulu.Jamani kuna watu wengi waliingia kazini kwa kuupenda ualimu yaani tulikuwa na mwalimu anafurahia kufundisha hadi raha na anaeleweka ila baadaye akaonekana kukatishwa tamaa.Sasa watu hawa wapo wengi kama mwalimu wa shule ya msingi angekuwa na uhakika wa kupata milioni nina uhakika kunawalimu wangelala darasani wanakesha wakifundisha.<br />SALAMU KWA mama yetu Profesa Ndalichako.<br /><br />
06.Kusaidia mapinduzi ya viwanda nchini.Pale anapopata mshahara mzuri atalima sana yaani kama hupenda kulima pamba atalima mara dufu,kahawa,korosho,miti,na vingine Vingi.Kumbe basi hata malighafi za viwanda zitaongezeka na kuifanya nchi iharakishe katika mapinduzi ya viwanda.Chamsingi ni kufanya kilimo na biashara bila kukiuka sheria za Utumishi wao.
SAIDIA MWALIMU,USAIDIE TAIFA