Kuchoma majani ni ibada au mazoea?

Kuchoma majani ni ibada au mazoea?

Jacobus

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2011
Posts
4,707
Reaction score
1,729
Wakuu, moja ya mambo yanayoharibu mazingira ya ulimwengu wetu ni kuchoma majani hasa wakati masika inapoisha na kiangazi kuanza. Tabia hii imezidi hasa mkoa wa Tabora kwani hali ya hewa ni hatari watu wanajichomea majani kama ni mashindano vile! Kama ningekuwa kiongozi wa serikali ningeweka sheria kali kwa atakae fanya kitendo hicho. Lakini labda ni jambo la imani kufanya hivo, kama inaefahamu vema tabia hii atujuze na kwa nini mkoa wa Tabora tuu?
 

Attachments

  • IMG_20160628_191153_0.jpg
    IMG_20160628_191153_0.jpg
    30.6 KB · Views: 38
  • IMG_20160629_085214_0.jpg
    IMG_20160629_085214_0.jpg
    40.6 KB · Views: 38
  • IMG_20160628_085348_0.jpg
    IMG_20160628_085348_0.jpg
    94 KB · Views: 40
Ni yale maeneo wavivu wa kulima. Ni mwendo wa kuchoma na kupanda.
 
Wengine wanasema kufanya hivyo ni kuwakimbiza wadudu wenye hatari kwa jamii, kwa mfano nyoka, ng'e na wengineo
 
Wengine wanasema kufanya hivyo ni kuwakimbiza wadudu wenye hatari kwa jamii, kwa mfano nyoka, ng'e na wengineo
Hao viumbe vina haki ya kuishi mkuu. Kama ni usafi wa mazingira pana njia mbili za kufanya, 1 ni kupalilia na kuchimba shimo la kutupia na kufunika na 2 ni kufyeka hayo majani na kuyazoa na kutupia ndani ya shimo. Hali ya hewa inabaki nzuri tu.
 
Back
Top Bottom