bigmind
JF-Expert Member
- Oct 28, 2015
- 12,457
- 12,668
Mh. Rais hongera kwa kuamua kuchepuka na kuachana na njia kuu.
Niseme kwa dhati kabisa na nikupongeze mh. Rais Magufuli kwa ujasiri wako, bila kupepesa macho ulivyoamua kuchepuka mchana kweupe na kuacha njia kuu nakusihi baki huko kwa mchepuko mpaka njia kuu izibe kabisa.
Tangu nchi yetu ipate uhuru mwaka 1961, watanzania chini ya uongozi JK Nyerere tulianza kazi kuchimba njia za kupita ili kujiepusha na mbigili na miba iliyokuwa imetoboa nyayo za miguu yetu kwa kipindi kirefu sana.
Ghafla mwalimu Nyerere mwaka 1977, akamua tuachane na kuchimba njia nyingi na badala yake tujenge barabara moja kubwa itakayotutosha wote kupita kwa urahisi haikuwa kazi kubwa watanzania tulimuunga mkono tukaachana na MICHEPUKO tukaingia NJIA KUU.
Miaka 1980s, baada ya vita ya Uganda, lahaula njia yetu kuu ilitokea kuota MBIGILI ambazo zilitutoboa miguu yetu kuliko ata zile za njia za kabla ya uhuru..! 1985 alikuja mzee MWINYI kwa kuwa yeye alikuwa amevaa viatu alitutangulia mbele sisi tukamfuata nyuma vilio vyetu vya kuumizwa na mbigili za njia kuu hakuzisikia.
1995 Mzee BEN alipoingia alikuwa kavaa GHAMBUTI hakujali tulio nyuma yake tulikuwa PEKU akatuhimiza tukimbie njia kuu ilikuwa sasa haina mbigili tena isipokuwa MISUMARI SASA, hakika majeraha ni makubwa yalitupata.
2000 JK WA PILI, bila kujua na kujali majeraha ya miaka 10 kutembea njia ya misumari peku, alisema hapa KASI MPYA akaamua lazima twende kasi ya MITA 100 akasahau wenziwe tuko PEKU na njia ina misumari.
Ponapona yetu, MUNGU SI ATHUMANI 1990s ziliundwa NJIA ZA PANYA ila nako kukawa kuna MBIGILI ingawa siyo nyingi walichoka mateso ya NJIA KUU wakachepuka na kijistili na maumivu ya misumari.
Katika hali ya kukata tamaa 2015, ghafla mh. Rais JP Magufuli akaokota dodo chini ya mnazi, alivyokaa chini alimenye akagundua WATANZANIA tulikuwa na vilio vya maumivu makubwa yaliyotkana na MAJERAHA YA MISUMARI YA NJIA KUU kwa miaka 30, huruma ilimjaa haikuwa rahis kutuponya ila akachukua hatua ya kwanza KUCHEPUKA akaingia SERVICE ROAD watanzania tukamfuata nyuma huku akaomba MISUMARI itolewe kwanza NJIA KUU, kabla ya watanzania hatujarudi kuendelea na safari kupitia njia kuu.
Wamiliki wa NJIA ZA PANYA sababu ya mateso ya NJIA KUU (misumari) basi walipata wapita njia na wao wakavimba kichwa na kusahau kuokota MBIGILI chache zinazowaumiza wapita njia wao GHAFLA sasa wapita njia wanaona bora warudi SERVICE ROAD kwa matumaini kuwa NJIA KUU itasafika siyo muda mrefu.
Mwisho nikuombe mh. Rais Magufuli ongeza kasi ya kuokota MISUMARI NJIA KUU, sisi na majeraha yetu bado tunaumia maana SERVICE ROAD ina CHANGALAWE inayotuumiza tulio PEKU na MAJERAHA YA MISUMARI ya miaka 30.
Nitoe heko na kukupa kongole mh. rais Magufuli, ila niombe kitu (OMBI BINAFSI) NINALO WAZO LANGU KWA VIJANA WAHITIMU ELIMU YA JUU (GRADUATES) LA KUWEZA KUTUSAIDIA TUJISAIDIE ANGALAU TURUDISHE MIKOPO YA BODI YA MIKOPO ELIMU YA JUU.
UKIPENDEZWA WASAIDIZI WAKO WANIFUATILIE NITOE HUO MPANGO UTUSAIDIE VIJANA NA WATANZANIA KWA UJUMLA.
Niseme kwa dhati kabisa na nikupongeze mh. Rais Magufuli kwa ujasiri wako, bila kupepesa macho ulivyoamua kuchepuka mchana kweupe na kuacha njia kuu nakusihi baki huko kwa mchepuko mpaka njia kuu izibe kabisa.
Tangu nchi yetu ipate uhuru mwaka 1961, watanzania chini ya uongozi JK Nyerere tulianza kazi kuchimba njia za kupita ili kujiepusha na mbigili na miba iliyokuwa imetoboa nyayo za miguu yetu kwa kipindi kirefu sana.
Ghafla mwalimu Nyerere mwaka 1977, akamua tuachane na kuchimba njia nyingi na badala yake tujenge barabara moja kubwa itakayotutosha wote kupita kwa urahisi haikuwa kazi kubwa watanzania tulimuunga mkono tukaachana na MICHEPUKO tukaingia NJIA KUU.
Miaka 1980s, baada ya vita ya Uganda, lahaula njia yetu kuu ilitokea kuota MBIGILI ambazo zilitutoboa miguu yetu kuliko ata zile za njia za kabla ya uhuru..! 1985 alikuja mzee MWINYI kwa kuwa yeye alikuwa amevaa viatu alitutangulia mbele sisi tukamfuata nyuma vilio vyetu vya kuumizwa na mbigili za njia kuu hakuzisikia.
1995 Mzee BEN alipoingia alikuwa kavaa GHAMBUTI hakujali tulio nyuma yake tulikuwa PEKU akatuhimiza tukimbie njia kuu ilikuwa sasa haina mbigili tena isipokuwa MISUMARI SASA, hakika majeraha ni makubwa yalitupata.
2000 JK WA PILI, bila kujua na kujali majeraha ya miaka 10 kutembea njia ya misumari peku, alisema hapa KASI MPYA akaamua lazima twende kasi ya MITA 100 akasahau wenziwe tuko PEKU na njia ina misumari.
Ponapona yetu, MUNGU SI ATHUMANI 1990s ziliundwa NJIA ZA PANYA ila nako kukawa kuna MBIGILI ingawa siyo nyingi walichoka mateso ya NJIA KUU wakachepuka na kijistili na maumivu ya misumari.
Katika hali ya kukata tamaa 2015, ghafla mh. Rais JP Magufuli akaokota dodo chini ya mnazi, alivyokaa chini alimenye akagundua WATANZANIA tulikuwa na vilio vya maumivu makubwa yaliyotkana na MAJERAHA YA MISUMARI YA NJIA KUU kwa miaka 30, huruma ilimjaa haikuwa rahis kutuponya ila akachukua hatua ya kwanza KUCHEPUKA akaingia SERVICE ROAD watanzania tukamfuata nyuma huku akaomba MISUMARI itolewe kwanza NJIA KUU, kabla ya watanzania hatujarudi kuendelea na safari kupitia njia kuu.
Wamiliki wa NJIA ZA PANYA sababu ya mateso ya NJIA KUU (misumari) basi walipata wapita njia na wao wakavimba kichwa na kusahau kuokota MBIGILI chache zinazowaumiza wapita njia wao GHAFLA sasa wapita njia wanaona bora warudi SERVICE ROAD kwa matumaini kuwa NJIA KUU itasafika siyo muda mrefu.
Mwisho nikuombe mh. Rais Magufuli ongeza kasi ya kuokota MISUMARI NJIA KUU, sisi na majeraha yetu bado tunaumia maana SERVICE ROAD ina CHANGALAWE inayotuumiza tulio PEKU na MAJERAHA YA MISUMARI ya miaka 30.
Nitoe heko na kukupa kongole mh. rais Magufuli, ila niombe kitu (OMBI BINAFSI) NINALO WAZO LANGU KWA VIJANA WAHITIMU ELIMU YA JUU (GRADUATES) LA KUWEZA KUTUSAIDIA TUJISAIDIE ANGALAU TURUDISHE MIKOPO YA BODI YA MIKOPO ELIMU YA JUU.
UKIPENDEZWA WASAIDIZI WAKO WANIFUATILIE NITOE HUO MPANGO UTUSAIDIE VIJANA NA WATANZANIA KWA UJUMLA.