Kuchagua mawaziri kuwa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa bunge la Katiba tunajifunza nini?

Tunapokubali kuwa kazi ya kuimarisha upinzani bado ni kubwa, tukubali pia kuwa usalama wa Taifa hili, unaopaswa kusimamia maslahi ya wananchi bado nao unahitaji kuimarishwa kwa kuongezewa ari ya uzalendo. Katika Mchakato huu tulikosea katika kutunga sheria. Laiti sheria ingetamka kuwa Mwenyekiti wa Bunge awe ni mtu asiyetokana na chama cha siasa na awe Jaji wa Makahama Kuu au ya Rufaa, ni dhahiri tungepata Katiba nzuri maana maadili ya Jaji yanafahamika kama kweli akiamua kutenda haki kwa mjibu wa maadali ya nafasi yake. Katiba iliyotawaliwa na ushabiki wa kisiasa, tutapata katiba ya wanasiasa!

Hili la Jaji kuwa mwenyekitii ndoo kabisaaa uozoo...wajua majaji wote ni wateule wa Raisi huku wengi wao wakipewa kama fadhila, ukada na urafikii??
Kosa kubwa hata Rasimi hii imekosa sana misingi ya utawala na maadili yake. Yahitajikaa Katiba itakayojalii sana Maadili na Uongozi hasa upatikanaji wa viongozi kama Majaji, mawaziri, wakuu wa taasisi za umma, usimamizi wa mapato na matumizi ya umma, na rasilimali zetu.
 
mchakato ulipofikia haususiki tena - tumeshayavulia nguo.....
Wenzetu jirani zetu Kenya waliususa mchakato wa kwanza wakaanza upya. Sasa hivi pamoja na tatizo lao kubwa la ukabila wana moja ya KATIBA nzuri sana barani Africa.
 
Hili la Jaji kuwa mwenyekitii ndoo kabisaaa uozoo...wajua majaji wote ni wateule wa Raisi huku wengi wao wakipewa kama fadhila, ukada na urafikii??
Kosa kubwa hata Rasimi hii imekosa sana misingi ya utawala na maadili yake. Yahitajikaa Katiba itakayojalii sana Maadili na Uongozi hasa upatikanaji wa viongozi kama Majaji, mawaziri, wakuu wa taasisi za umma, usimamizi wa mapato na matumizi ya umma, na rasilimali zetu.
Wapo Majaji wazuri tu nchi hii akina Robert Kisanga, Barnabas Samatta, etc., ambao wangeweza kulisimamia jambo hili bila bias yoyote kwa mtu wala kundi lolote.
 
Wapo Majaji wazuri tu nchi hii akina Robert Kisanga, Barnabas Samatta, etc., ambao wangeweza kulisimamia jambo hili bila bias yoyote kwa mtu wala kundi lolote.

Natumai hao uliowataja (Kisanga na Samatta) wajua watawala hawakuwafurahiaa kwa misimamo yao na kamwe hawawezi kuwashirikisha uongozi katika utungaji wa Katiba hii..
 
Mleta mada,

Fact 1: CCM ndio ilikuwa na watu wenye sifa kugombea nafasi zote mbili, uenyekiti na makamu mwenyekiti. Sifa hizo zili-range kuanzia elimu mpaka uzoefu wa kuendesha mabunge. Wapinzani siwalaumu kushindwa kwao kusimamisha mgombea kwa kuwa hawana, narudia, hawana mtu mwenye sifa.

Fact 2: CCM ni chama tawala na probably ndio chama chenye kuaminiwa zaidi na wale wajumbe 201. Hivyo, mbali na wale wajumbe kuwa ni wana CCM huenda kabisa wakawa wapenzi wakubwa wa CCM. Hivyo, kivyovyote mgombea wa CCM alikuwa ashinde kwa kishindo.

Fact 3: Wapinzani wana jiaminisha kuwa mhe. Sitta ni msimamia usawa bungeni na hana upande hivyo atatoa fursa sawa kwa wote. Jamani, hata mzee Kificho mwenyewe alikua akitoa fursa kwa mawaziri na wabunge wa CCM kwa kiasi kikubwa na hata maamuzi yake yaliendeshwa kwa misingi hiyo. Hakuna usawa pale, ni kusimamia msimamo wa chama tu.

Hamy-D, naomba usome vizuri uzi wangu. Nilisema mtu ambaye ni waziri. Kificho ni spika wa baraza la wawakilishi nafasi ambayo inamfanya asimamie mhimili mwingine wa dola na siyo waziri. Sitta na Samia ni wajumbe wa baraza la Mawaziri kwa hiyo wako chini ya muhimili mmoja wa dola na wanakwenda kuongoza mhimili mwingine. Hilo ndilo lilikuwa suala langu
 
Hamy-D, naomba usome vizuri uzi wangu. Nilisema mtu ambaye ni waziri. Kificho ni spika wa baraza la wawakilishi nafasi ambayo inamfanya asimamie mhimili mwingine wa dola na siyo waziri. Sitta na Samia ni wajumbe wa baraza la Mawaziri kwa hiyo wako chini ya muhimili mmoja wa dola na wanakwenda kuongoza mhimili mwingine. Hilo ndilo lilikuwa suala langu
Watakwambia hili ni BUNGE MAALUM hivyo WAJUMBE wote walioko mle wana hadhi sawa ingawa tunawaona wanaitana kwa hadhi na vyeo vyao. Watakwambia pia kwamba Sheria ya Mabadiliko ya Katiba iko kimya juu ya hili.

Ni mambo kama haya ndio yanayotushangaza kuwa watu makini kama akina Tundu Lissu hawakuyaona haya hata walipopata fursa ya kuonana na Jakaya wetu ana kwa ana. Niliwaona juzi wakisifiana kwa kutengeneza KANUNI nzuri zitakazo liongoza bunge hili ambalo tayari limetekwa na CCM.


Historia haitawaacha watu hawa.
 
Watakwambia hili ni BUNGE MAALUM hivyo WAJUMBE wote walioko mle wana hadhi sawa ingawa tunawaona wanaitana kwa hadhi na vyeo vyao. Watakwambia pia kwamba Sheria ya Mabadiliko ya Katiba iko kimya juu ya hili.

Ni mambo kama haya ndio yanayotushangaza kuwa watu makini kama akina Tundu Lissu hawakuyaona haya hata walipopata fursa ya kuonana na Jakaya wetu ana kwa ana. Niliwaona juzi wakisifiana kwa kutengeneza KANUNI nzuri zitakazo liongoza bunge hili ambalo tayari limetekwa na CCM.


Historia haitawaacha watu hawa.

Teh teh teh nimecheka sana ulivyosema wataniambia kuwa hili ni bunge maalum. Hivi katika siku zote hizo baraza la mawaziri halitakutana? Je likikutana nani ataongoza vikao vya bunge maalum au watakuwa wanapeana zamu? Nadhani kama unavyosema kuna wakati inatakiwa tuwe makini kidogo na mambo tunayoyafanya.
 
Mkuu hapa hakuna suala la endapo. Ni dhahiri kwamba tayari CCM walishavuruga Mchakato huu kwa kuhakikisha wanapanga safu yao kuanzia kutungwa kwa sheria, kanuni za Bunge na sasa uchaguzi. Huwezi kuwa na Spika ambaye ni Waziri na Makamu wake ni waziri tena wa Muungano ukategemea Katiba inayotakiwa na wananchi. Tutapata Katiba inayotakiwa na watawala.
Asante studioo, Samia hakupenda katiba mpya tangu akiwa makamu wa mwenyekiti wa bunge la katiba
 
Back
Top Bottom