demigod
JF-Expert Member
- Jan 2, 2015
- 8,222
- 15,073
"Nataka wananchi wenzangu wa Ubungo na Dar es Salaam pamoja na jitihada kubwa zinazofanywa na viongozi zinapaswa kuungwa mkono na jamii ili wananchi wajue madhara ya ugonjwa huu wa Corona tufuate ushauri wa wataalam.
Kuna hatari za kiafya kutoka nchi tajiri duniani juu ya gonjwa hili la Corona sembuse sisi?, Mungu atunusuru na haya mambo ya kufanya mzaha.
Nimshukuru Spika Ndugai kwa kupunguza idadi ya wabunge Bungeni ametumia mamlaka yake kwa mujibu wa Katiba kulinda afya za wabunge lakini haitoshi, ni vizuri bunge likafungwa kama maambukizi yataendelea, kuokoa maisha ya watu.
Mapato ya serikali yanategemea kodi na mapato makubwa ni ya utalii, tutegemee uwepo wa mdororo wa uchumi duniani kwa sababu ya gonjwa hili.
Huu sio wakati wa kurushiana vijembe na kuonyeshana ubabe, hii vita vi yetu sote, wakati wa vita ya Kagera, Taifa lilikuwa pamoja na huu ugonjwa ni lazima tushikamane pamoja kuhamasisha jamii inaelimika na Serikali isaidie.
Inawezekana taarifa zinazotolewa sasa sio za kweli kwa sababu kuna shida pia ya utambuzi ambayo ni jambo serious kabisa, serikali iwekeze katika maeneo ya kuhudumia wagonjwa.
Ni jambo jema shule zilivyofungwa kwa sababu mzazi unakuwa karibu na mwanao lakini kwa misongamano iliyopo kwenye madaladala unaona bora huyo mtoto angebaki shuleni.
Baada ya Anthony Komu kutangaza kuondoka Chadema yamekuwepo maneno mengi nikitajwa na mimi nitamfuata Komu, Komu ni ndugu yangu kabisa, lakini urafiki wangu na Komu haunifanyi kila anachofanya nami nifanye, mimi bado mbunge wa Chadema.
Mimi nimeshaenda mahakamani mara nyingi sana, lakini inategemea na nafasi yangu na mimi naamini sio lazima watu wote kukusanyika katika tukio moja, mimi nashiriki kwenye shughuli za Chadema, sina shida na chama na nipo pamoja na viongozi wangu," Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo
Kuna hatari za kiafya kutoka nchi tajiri duniani juu ya gonjwa hili la Corona sembuse sisi?, Mungu atunusuru na haya mambo ya kufanya mzaha.
Nimshukuru Spika Ndugai kwa kupunguza idadi ya wabunge Bungeni ametumia mamlaka yake kwa mujibu wa Katiba kulinda afya za wabunge lakini haitoshi, ni vizuri bunge likafungwa kama maambukizi yataendelea, kuokoa maisha ya watu.
Mapato ya serikali yanategemea kodi na mapato makubwa ni ya utalii, tutegemee uwepo wa mdororo wa uchumi duniani kwa sababu ya gonjwa hili.
Huu sio wakati wa kurushiana vijembe na kuonyeshana ubabe, hii vita vi yetu sote, wakati wa vita ya Kagera, Taifa lilikuwa pamoja na huu ugonjwa ni lazima tushikamane pamoja kuhamasisha jamii inaelimika na Serikali isaidie.
Inawezekana taarifa zinazotolewa sasa sio za kweli kwa sababu kuna shida pia ya utambuzi ambayo ni jambo serious kabisa, serikali iwekeze katika maeneo ya kuhudumia wagonjwa.
Ni jambo jema shule zilivyofungwa kwa sababu mzazi unakuwa karibu na mwanao lakini kwa misongamano iliyopo kwenye madaladala unaona bora huyo mtoto angebaki shuleni.
Baada ya Anthony Komu kutangaza kuondoka Chadema yamekuwepo maneno mengi nikitajwa na mimi nitamfuata Komu, Komu ni ndugu yangu kabisa, lakini urafiki wangu na Komu haunifanyi kila anachofanya nami nifanye, mimi bado mbunge wa Chadema.
Mimi nimeshaenda mahakamani mara nyingi sana, lakini inategemea na nafasi yangu na mimi naamini sio lazima watu wote kukusanyika katika tukio moja, mimi nashiriki kwenye shughuli za Chadema, sina shida na chama na nipo pamoja na viongozi wangu," Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo