Kubadilisha engine na gearbox ya Mitsubishi RVR

Kubadilisha engine na gearbox ya Mitsubishi RVR

Mkuu Dingswayo,
Asante kwa kuuliza swali hili. Nami nina shida kama ya kwako. RvR yangu imelala mwaka wa pili sasa...
Ama kweli kijiwe hiki tunajifunza mengi!
 
Kwa wale wataalam naomba msaada. Nina gari yangu aina ya mitsubishi RVR ambayo nimeipark kwa muda mrefu kutokana na matatizo yake ya gear box. Kuna mtu alishawahi kunidokeza kuwa inawezekana kubadilisha engine/gearbox na kuweka nyingine ya Toyota. Ni siku kiasi zimepita na zile details zimenipotea kidogo. Hivyo basi nakuja hapa jamvini kuuliza kama kuna yeyote mwenye ujuzi au habari kuhusu ubadilishaji huo? je kama inawezekana, engine hizo na gearbox zinapatikana wapi na kwa bei gani?

Natanguliza shukrani.

Mkuu Dingswayo kupunguza hizo cost za kununua gearbox mpya na kuifix kwa nn usitafute mkebe mwingine ukauweka barabarani kaka?
Sasa hv mikebe mingi sana na bei ziko mwake hazina noma sana.
Au bado una hamu na RVR?
Ushauri tu mkuu

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Shaurimoyo, Ilala lakini kuwa makini sana na wale jamaa.

Lakini kama umefikia stage ya kubadili injini, naona kama vile ni bora kutafuta gari nyingine tuu.

Personally, I won't risk to that extent.
 
Mkuu inawezekana kabisa,nunua engine complete ya Toyota Corolla Model Ae91 au Ae100 hizo zipo mara mbili ambazo ni 4A-FE na 5A-FE,hiyo ya kwanza ndo nzuri zaidi mana ni economic nadhan itakufaa

Asante Mkuu Sir Mimi- Ukisema engine complete una maana gani. Na ukisema ya kwanza ndio nzuri una maana 4A-FE?
 
Mkuu Dingswayo kupunguza hizo cost za kununua gearbox mpya na kuifix kwa nn usitafute mkebe mwingine ukauweka barabarani kaka?
Sasa hv mikebe mingi sana na bei ziko mwake hazina noma sana.
Au bado una hamu na RVR?
Ushauri tu mkuu

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

In fact ni gari ambalo silitumii, nilimnunulia Mzee wangu. Nina gari lingine ambalo natumia na hiyo rvr niliingiza duty free. Kama siwezi kuliuza option nyingine ni kuliacha lioze, na mimi naona si vizuri. Unanishauri vipi?
 
Injini nzuri zaifi ni ya suzuki vitara. Hiyo hata Ulaya wanaijua hiyo.
 
Complete kwamba na gear box yake mkuu,ukiichukua fundi anenda kuipachika tu,sema atabadisha engine mounting na gear box mounting coz RvR nitofauti na za Toyota,ya kwnza ni hiyo 4A-FE ni nzuri sana kwa ulaji wa mafuta na hata kufit kwenye RvR inapendeza mtu haezi'jua labda umwambie,bei zake ni 1.5mil au 1.4mil.
 
Kama upo dar kuna fundi mmoja maarufu sana ila mimi jina nimemsahau gereji yake ipo kati ya junction ya africana (mbezi beach) na round about ya kwenda white sands. Huyo jamaa ni mtaalam wa hiyo makitu balaa. Mtafute mwenyewe utamkubali.
 
Watu8 keleza vema pia wacheki hao jamaa hapo shhauri moyo Kiokote,Kizibo au mkuu wao Mbegu wapo pembezoni mwa Machinga complex

Kwa engine pia cheki ya 4e-Fe very economic inakuja san a kwenye starlet

Ukifikia uamuzi wa kununua engine pm mkuu kwa utekelezaji
 
Kwa wale wataalam naomba msaada. Nina gari yangu aina ya mitsubishi RVR ambayo nimeipark kwa muda mrefu kutokana na matatizo yake ya gear box. Kuna mtu alishawahi kunidokeza kuwa inawezekana kubadilisha engine/gearbox na kuweka nyingine ya Toyota. Ni siku kiasi zimepita na zile details zimenipotea kidogo. Hivyo basi nakuja hapa jamvini kuuliza kama kuna yeyote mwenye ujuzi au habari kuhusu ubadilishaji huo? je kama inawezekana, engine hizo na gearbox zinapatikana wapi na kwa bei gani?

Natanguliza shukrani.

Kuna RVR moja niliiona miaka kadhaa iliyopita ikiwa imefungwa injini ya 4S-FE ya Toyota. Injini hizi zinatumika katika Toyota zinazoendeshwa na magurudumu ya mbele (front wheel drive) na magurudumu ya nyuma (rear wheel drive). Itakayokufaa ni ile iliyofungwa automatic gearbox ya front wheel drive, kwa hiyo utalazimika kununua injini ya 4S-FE ikiwa na gearbox yake. Hizi zipo Ilala na ni vizuri kwenda moja kwa moja katika maduka badala ya kutumia madalali ambao wengi ni matapeli.
 
Back
Top Bottom