Hivi kile kiapo wabunge wateule wanachofanya bungeni mbele ya spika si kina maana baada ya hapo wanakuwa wabunge kamili na si wateule tena ili waweze kikatiba kufanya kazi zao. <br />
SASA inakuwaje akina Shamsi Nahodha ambao ni wateule tu na hawajala kiapo bungeni wanaapa kuwa mawaziri wakati ILI uwe waziri ni lazima uwe mbunge kwanza!!!<br />
<br />
Kama hivyo ndivyo, je kile kiapo Rais anachokula uwanja wa Taifa ni kulinda katiba kwa baadhi tu ya mambo, hasa makubwa na si ku-observe each and every thing in constitution?<br />
Je, mwanasheria mkuu na wanasheria washauri wa Rais wanamtakia mema kwa hilo?<br />
<br />
kuvunja vipengele vidogo kunapelekea kutokuwa na uwoga tena wa kuvunja vipengere hata vikubwa. Ni mtizamo wangu tu na naomba tukemee na ku-highlight hili ili katiba isinyanyaswe this much.<br />
<br />
Asanteni!