Kuanguka kwa CCM ni unabii unaotimia. Unabii wa MM Mwanakijiji

Hivi kwenye siasa kuna consistency?

Tatizo unaongelea siasa wakati mimi naongelea principled leadership.

Consistency gani unayoiongelea hapa. Kuwa specific.

Mimi naongelea consistency ya kumpinga Lowassa kama fisadi.

Mwanakijiji alimsema Lowassa fisadi kitambo sana. Kaandika mengi sana kuanzia vibahasha walivyokuwa wakipewa waandishi wa habari mpaka Richmond. CHADEMA walipenda kusikia hilo kwa sababu Lowassa alikuwa CCM. CHADEMA wakamuita Lowassa fisadi mkubwa. Na list of shame akawekwa.

Leo Lowassa kaenda CHADEMA. Mwanakijiji anaendelea kusema Lowassa fisadi. Na mimi sioni Lowassa kaacha vipi au lini kuwa fisadi. Kwa hiyo katika hili Mwanakijiji yupo consistent.

Huko CHADEMA sio tu mmemkaribisha, mmempa na nafasi ya kugimbea urais bula ya kutueleza Lowassa kaacha ufisadi lini?

CHADEMA is not consistent in this.
 
Lowassa akishinda hawi Mwenyekiti wa chama,chama na dola haitokuwa kama CCM,Chama kitaisimamia serikali na kuiwajibisha wakati maCCM serikali inakitia chama mfukoni na hakina sauti wala mlio wa huzuni!!!

Lowassa akishinda,Mawaziri baathi yao ni Mbowe,Mbatia,Tundu Lissu,Mnyika,Halima Mdee,Kafulila,Silinde,Habib Mnyaa,Mbarouk etc

Kwenye orodha tajwa hapo,wabunge gani wa maCCM wanawazidi hao tajwa hapo kwa uchapa kazi na uadilifu??!! Utasema January Makamba,Ridhiwani,Ummy Mwalimu,Angela KairukinChenge na kina Mama Sita?!!

Lowassa atarudisha katiba ya Warioba,Magufuli ataweza?! Lowassa atavunja mkataba wa bandari ya Msoga/Bagamoyo na kupeleka mradi Tanga au Mtwara,Magufuli atathubutu?!

Serikali ya UKAWA itatunga upya sheria ya mafuta na gesi na kufuta ile ya CCM ambayo imepitishwa na wabunge 80 tu wa maCCM kati wabunge 400,Magufuli atathubutu au ataishia kuleta ukasuku tu?!!

Huu uchambuzi ni mzuri sana mkuu natamani ungeuanzishia uzi wake
 
CCM (idea, deeper kuliko chama) ni lazima ishinde mwaka huu.

Ama kwa mgombea wake Magufuli, ama kwa mgombea wake Lowassa.

Upinzani hauna mgombea.

Kwa hivyo, CCM haiwezi kuanguka mwaka huu.

Huwezi kuleta mabadiliko ya kweli kwa kutumia makapi ya CCM ambayo hata hayajapata muda wa kuangaliwa ndani ya upunzani.

CHADEMA hamjajifunza kwa Shibuda tu?

Mimi namuelewa Mwanakijiji.

Kimoyomonyo nakuona unajaribu kuponda huku unadai umemwelewa MMM.Kweli ndege wafananao huruka pamoja.
Vipi yasiyo kuwa makapi ni yapi?
Shibuda alinufaika na CDM ilinufaika kwa uwapo wake tatizo iliko wapi?
 
mwanakijiji ni mfano wa mwanaume aliyemtongoza msichana kisha akakubaliwa na kuanza kutoamini kukubaliwa. pengine anaamini katika mitama na niangusage
 
Unabii huu ulitabiriwa Na Mzee mwanakijiji, na sasa ni wazi kabisa unatimia. .


Kwa vile unabii utatimia ulivyo, nawasihi wale wote waliofunguliwa kuwa tayari kwa lolote kwani vichaa wamepewa sime sokoni! Tutakiona cha moto! Kama walivyowahi kusema wengine – ni bora kufa kwa heshima kuliko kuishi kwa aibu! Tuendelee kuwaamsha watu wengi zaidi ili kuhakikisha kuwa pigo la kwanza takatifu, pigo lisilo na huruma, pigo lisilo na onyo liangukie CCM kwenye chaguzi zote zinazokuja kuanzia sasa.


Kwani unabii utatimia; ndivyo ilivyopaswa kuwa, nayo itakuwa kwani hivyo ndivyo ilitakiwa iwe. NA ITAKUWA.


Nitafute Facebook: “Mimi Mwanakijiji
Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com


Hapo red MMM asante sana!
Kwa taarifa tu-hicho ndicho anachotaka kulitimiza Mhe.Edward G.Lowassa.Kuwa Raisi bora kuliko wengine wote mliopata kuwa nao.
Kwa Umri wake wa miaka 60 kuna mengine mazuri na mabaya ameyafanya na kuna mengi mmeamua kutokumsamehe au kumshitaki Mahakamani aonekane kweli ni fisadi lakini hamfanyi chochote ila mmebaki kumchafua miaka 20 yote hii .
 
Kama wewe ni mfuatiliaji utagundua kuwa katika ile list of shame haikuwa na Lowasa peke yake.. pamoja na wengine Mkapa alikuwemo, Kikwete pia alikuwemo, licha ya Lowasa mwenyewe kukiri kuwa ile dili ilikuwa na ya Mamlaka ya juu, na juzi Lisu kuthibitisha hadharani kuwa Richmond ni ya Kikwete kwa nini sasa anaandamwa Lowasa peke yake?
Tatizo lilikuwa uwaziri mkuu au Richmond? Kama tatizo lilikuwa Richmond kwa nini kamati ya Mwakyembe haikumhoji? TAFAKARI

Hata wahusika wa ESCROW ya juzi tu ambayo inamhusisha pia Mkuu wa Kaya nayo imesahauliwa kisa LOWASA ameamua kujiunga upande wa pili. Wakiulizwa ushahidi hawana wamebaki kupiga domo tu. Mambo mengine yanafanywa kwa unafiki Zaidi na sio kwa minajili ya kulinasua taifa letu, hata wale tuliowaamini kuwa ni wapambanaji wa kweli nao wamejionesha wazi kuwa wanapigania masilahi yao binafsi kwa kivuli cha kuwakomboa wananchi.

Wanafiki, walaghai na wavurugaji wa fikra na maamuzi ya wananchi waliowengi wapigwe vita muda wote na kamwe wasipewe nafasi ya kucheza na fikra za wananchi wa taifa hili
 
Tatizo unaongelea siasa wakati mimi naongelea principled leadership.

Consistency gani unayoiongelea hapa. Kuwa specific.

Mimi naongelea consistency ya kumpinga Lowassa kama fisadi.

Mwanakijiji alimsema Lowassa fisadi kitambo sana. Kaandika mengi sana kuanzia vibahasha walivyokuwa wakipewa waandishi wa habari mpaka Richmond. CHADEMA walipenda kusikia hilo kwa sababu Lowassa alikuwa CCM. CHADEMA wakamuita Lowassa fisadi mkubwa. Na list of shame akawekwa.

Leo Lowassa kaenda CHADEMA. Mwanakijiji anaendelea kusema Lowassa fisadi. Na mimi sioni Lowassa kaacha vipi au lini kuwa fisadi. Kwa hiyo katika hili Mwanakijiji yupo consistent.

Huko CHADEMA sio tu mmemkaribisha, mmempa na nafasi ya kugimbea urais bula ya kutueleza Lowassa kaacha ufisadi lini?

CHADEMA is not consistent in this.

Kiranga

Wote walikuwa wakimtuhumu Lowasa kuwa ni Fisadi. . Hakuna mahali walithibitisha ufisadi wake.. Na hata hiyo Richmond iliyoundiwa tume. Mwakyembe na tume yake, pamoja na kwamba hawakumuhoji lakini HAKUNA mahali ilipothibitisha kuhusika kwake moja kwa moja. Kuja kwake Chadema ilibidi aeleze mwenye Richmond ni nani ndipo alipothibitisha kuwa Ni Mamlaka ya Juu. Zingatia alipotaka kuuvunja ule mkataba alikatazwa na hiyo Mamlaka ya juu. Kwa hiyo si kwamba Mbowe alimeza matapishi yake bali Lowasa alieleza mwenye huo mzigo ni Kikwete na maelezo yake yakaeleweka . Na kwa mvuto alionao Lowasa ikathibitika kuwa hakuna mwingine kwa sasa ambaye angeisumbua na kuiangusha ccm is ipokuwa Lowasa. Rejea maneno ya Baba wa Taifa, Upinzani wa kweli utatoka CCM. Na hata hivyo bila ccm kupasuka usitegemee kuiondoa madarakani.
 
...Mimi namuelewa Mwanakijiji.
Kweli Kiranga? Labda utakuwa hukumsoma Mzee Mwanakijiji mwaka 2010 na harakati zake katika kuinadi CCJ ya Nape, Sitta na Mwakyembe waliodaiwa kuwa wapiganaji ndani ya CCM. Hawa Mzee Mwanakijiji aliwapenda sana tu na hata siku moja hakuwaponda. Ikumbukwe kwamba kabla ya kashfa ya Richmond zilikuwepo pia kashfa zingine kama za CDA, TIC na zinginezo ambazo zote zilimhusisha mtu moja naye ni Samwel Sitta.

Kinachonishangaza ni kwamba wote waliowahi kuwa na tuhuma katika nchi hii tukianza na Kikwete, mkataba wa IPTL akiwa Waziri wa Nishati, hadi Mwakyembe, Umeme wa Upepo, wanafumbiwa macho lakini si Lowassa. Bahati nzuri tuko wengi, on record, tuliosema na tunazidi kusema, adui wa taifa hili ni CCM na si individuals, ni mfumo. Kinachomsukuma Mzee Mwanakijiji ni chuki abayo imekomaa na kugeuka obsession dhidi ya Lowassa.
 
Last edited by a moderator:
Kweli Kiranga? Labda utakuwa hukumsoma Mzee Mwanakijiji mwaka 2010 na harakati zake katika kuinadi CCJ ya Nape, Sitta na Mwakyembe waliodaiwa kuwa wapiganaji ndani ya CCM. Hawa Mzee Mwanakijiji aliwapenda sana tu na hata siku moja hakuwaponda. Ikumbukwe kwamba kabla ya kashfa ya Richmond zilikuwepo pia kashfa zingine kama za CDA, TIC na zinginezo ambazo zote zilimhusisha mtu moja naye ni Samwel Sitta.

Kinachonishangaza ni kwamba wote waliowahi kuwa na tuhuma katika nchi hii tukianza na Kikwete, mkataba wa IPTL akiwa Waziri wa Nishati, hadi Mwakyembe, Umeme wa Upepo, wanafumbiwa macho lakini si Lowassa. Bahati nzuri tuko wengi, on record, tuliosema na tunazidi kusema, adui wa taifa hili ni CCM na si individuals, ni mfumo. Kinachomsukuma Mzee Mwanakijiji ni chuki abayo imekomaa na kugeuka obsession dhidi ya Lowassa.

Mie sijawatetea hao wengine.

Na wala sijasema kwamba nakubaliana na Mwanakijiji katika yooote.

Ila katika la kumsema Lowassa, siwezi kushangaa Mwanakijiji akishindwa kumpa support Lowassa leo, kwa sababu hajawahi kumpa support.

Ninachoshangaa ni CHADEMA kumpa nafasi ya kugombea urais bila maelezo ya kueleweka kuhusu ufisadi wake.

Lowassa anapata prominence sasa kwa sababu anagombea urais.
 
Last edited by a moderator:
Mie sijawatetea hao wengine.

Na wala sijasema kwamba nakubaliana na Mwanakijiji katika yooote.

Ila katika la kumsema Lowassa, siwezi kushangaa Mwanakijiji akishindwa kumpa support Lowassa leo, kwa sababu hajawahi kumpa support.

Ninachoshangaa ni CHADEMA kumpa nafasi ya kugombea urais bila maelezo ya kueleweka kuhusu ufisadi wake.

Lowassa anapata prominence sasa kwa sababu anagombea urais.
kashaeleza kwamba mwenye Richmond ni rais. maelezo gani ya kueleweka unataka?
 
kashaeleza kwamba mwenye Richmond ni rais. maelezo gani ya kueleweka unataka?

Just like that? Na rais naye kasema mwenye Richmond anatembea na Tundu Lissu.

Kwa nini hajatoa documents siku zote hizo?
 
Just like that? Na rais naye kasema mwenye Richmond anatembea na Tundu Lissu.

Kwa nini hajatoa documents siku zote hizo?

And to Lowassa just like that!?

Unataka mpaka aje kutoa hata minutes za baraza la mawaziri ambaye mwenyekiti wake ni Rais mkuu?

Jamaa anaposema waende mahakamani ana maanisha kweli kuwa serikali ilipeleke hilo mahakamani ili kila kitu kikaagizwe kiende huko!!
 
Just like that? Na rais naye kasema mwenye Richmond anatembea na Tundu Lissu.

Kwa nini hajatoa documents siku zote hizo?
ni rais huyo alisema hamjui mwenye richmond na hajawahi muona, ni huyo alimleta muoman aliyejieleza kwamba ndiye mmiliki wa richmond, ni huyo leo anasema mwizi yuko na na lissu. lazima tukubali kuwa kwenye richmond tulitakke sides kwa mapenzi tu siyo facts. facts zinapoanza kujionyesha kuna watu kama mwanakijiji wanaona aibu kubadilika kwasababu kipindi kile waliongea kana kwamba wanaujua ukweli wote.

hakutoa documents zote kama tu mwakyembe alivyosema serikali ingeanguka. bado hatujui ukweli wote wa richmond hivyo tusione aibu kubadilika mara mambo yanavyojifunua.
 
And to Lowassa just like that!?

Unataka mpaka aje kutoa hata minutes za baraza la mawaziri ambaye mwenyekiti wake ni Rais mkuu?

Jamaa anaposema waende mahakamani ana maanisha kweli kuwa serikali ilipeleke hilo mahakamani ili kila kitu kikaagizwe kiende huko!!

Serikali hawawezi kumpeleka mahakamani kwa sababu deal walisuka wote.

Sasa mnabadilisha nini kama mnamtoa mwozi mmoja na kumuingiza mwingine?
 
ni rais huyo alisema hamjui mwenye richmond na hajawahi muona, ni huyo alimleta muoman aliyejieleza kwamba ndiye mmiliki wa richmond, ni huyo leo anasema mwizi yuko na na lissu. lazima tukubali kuwa kwenye richmond tulitakke sides kwa mapenzi tu siyo facts. facts zinapoanza kujionyesha kuna watu kama mwanakijiji wanaona aibu kubadilika kwasababu kipindi kile waliongea kana kwamba wanaujua ukweli wote.

hakutoa documents zote kama tu mwakyembe alivyosema serikali ingeanguka. bado hatujui ukweli wote wa richmond hivyo tusione aibu kubadilika mara mambo yanavyojifunua.

Mimi tangu siku ya kwanza nilisema haiyumkiniki Tanzania PM afanye mambo makubwa kwenye mikataba kama tuliyosema kafanya Lowassa bila rais kukubali.

Nilisema culprit number one ni Kikwete.

Juzi nilikuwa nabishana na Mwakyembe alipokuwa anasema anataka mjadala na Lowassa. Mwakyembe akasema ana ushahidi zaidi alikuwa anangoja tu sasa kuna watu wa Lowassa wanaleta kidomodomo atawaonyesha.

Nikamuuliza, kwa nini anakalia ushahidi wa mtu fisadi miaka yote hiyo? Mpaka sasa huyu fisadi anataka kuaminiwa na watu kupewa nchi? Haoni kwamba kwa kukaa na ushahidi mpaka asubiri uchaguzi amewanyima Watanzania haki yao ya kujua habari nzima na anautumia uchunguzi wa tume kisiasa zaidi?

Akanyamaza. Nikamuuliza, na zaidi ya hapo, ulikuwa na maana gani uliposema kwamba mliyoyasema bungeni si yote, kuna mengine mmeyabakiza kwa kuhofia kuvunjika kwa serikali? Hakujibu.

Nikambana zaidi, nikamwambia mlihofia nini kama maneno ni ya ukweli? Au mlihofia maneno yatamu implicate Kikwete?

Nilivyosema hivyo nikawa kama nimemfukuza. Kijiwe kile akawa hakanyagi kabisa. Na hata huo mdahalo wenyewe waliokuwa wanataka kufanya kumuumbua Lowassa sijausikia tena. Ilikuwa ufanyike wiki iliyopita nafikiri.

Kwa hiyo najua Kikwete anahusika.

Tatizo langu si Kikwete. Kikwete anajistaafia. Hao liutenants wake. Tatizo langu hawa watu wanaoenda kuwania urais sasa.
 
Back
Top Bottom