Kuangamiza panya

Kuangamiza panya

Kambaku

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2011
Posts
8,710
Reaction score
32,483
Asalam aleikum waungwana, jamani naomba msaada wa haraka kwa mwenye uelewa wa kuangamiza hawa wadudu (Panya). Ndani ya wiki mbili imekuwa tishio kwangu, walianza kama utani mmoja mmoja sasa wameingia kila mahali. Tunajitahidi sana usafi wa kila siku na kila mahali lakini wanazidi, msaada jamani. Tumewawekea sumu wakala siku ya kwanza baada ya hapo hawali ng'o!

Najua kuwa na paka ni suluhisho moja wapo, natafuta sana paka kwa mwenye nae pia wakuu.
 
Vinauzwa wapi mkuu? Asante kwa jibu la matumaini
 
Hao panya wategee sumu ila badilisha vyakula vya kutegea mana siku ya kwanza unasema walikula hawakuka tena wamechoka wabadilishie diet
Shukrani mkuu, nitajaribu kubadili
 
Kuna sumu flani ivi nimeisahau jina iyo unamix na karanga za kukaanga panya akila anakufa lakini haozi
 
sorry... ni kosa kumuita panya mdudu alafu yule ni mnyama kama wanyama wengine na ana haki ya kuishi kama wengine, familia yake inamtegemea. Hivi kwenye vitabu vya dini viimeandikaje kuhusu kuua? kuua sio binadam tu hata wanyama wanaonyonyesha kama panya wanahusika pia.....





380783297cbbbbe95003884cf1cb5120.jpg



(jokes)
 
sorry... ni kosa kumuita panya mdudu alafu yule ni mnyama kama wanyama wengine na ana haki ya kuishi kama wengine, familia yake inamtegemea. Hivi kwenye vitabu vya dini viimeandikaje kuhusu kuua? kuua sio binadam tu hata wanyama wanaonyonyesha kama panya wanahusika pia.....








(jokes)
Hata kumfukuza tu ni poa aisee ila mabishi balaa
 
Hayali aisee, yalikula siku ya kwanza yakafa manne baada ya hapo hayagusi ng'o!
Panya ni mnyama mjanja sana na ndiyo sababu katuni nyingi za watoto zinamhusu panya. Unapotumia sumu au mtego wowote ile hakikisha mara tu alapo au anasapo unamuondoa mtuhumiwa kabla wenzake hawajamuona na uhamishie sehemu nyingine; Na kama ni sumu usiirembe sana kwa mapochopocho udugu huo hana, hatakula huwa wanajiuliza kama kitamu kwanini wewe haukula? Na ukiwabughudhi sana watahama wakuachie nyumba yako kama umeiona ni ya maana sana. Ukifuga paka hakikisha haumpi chakula chochote kile vinginevyo utawakuta wanacheza pamoja huku wakivutana sharubu.
Mwisho ukiwanasa kwa kitabu huwa hakina sumu na unaweza ukawabanika kwa chai ya asubuhi na chapati.
 
Panya ni mnyama mjanja sana na ndiyo sababu katuni nyingi za watoto zinamhusu panya. Unapotumia sumu au mtego wowote ile hakikisha mara tu alapo au anasapo unamuondoa mtuhumiwa kabla wenzake hawajamuona na uhamishie sehemu nyingine; Na kama ni sumu usiirembe sana kwa mapochopocho udugu huo hana, hatakula huwa wanajiuliza kama kitamu kwanini wewe haukula? Na ukiwabughudhi sana watahama wakuachie nyumba yako kama umeiona ni ya maana sana. Ukifuga paka hakikisha haumpi chakula chochote kile vinginevyo utawakuta wanacheza pamoja huku wakivutana sharubu.
Mwisho ukiwanasa kwa kitabu huwa hakina sumu na unaweza ukawabanika kwa chai ya asubuhi na chapati.
Asante mkuu kwa mawazo
 
Pole mkuu, nunua hii sumu huchanganyi na kitu chochote, wakila inawakausha ila hakikisha umefunika vyombo vya maji, sababu wakinywa maji inapungua nguvu
Ni Nzuri sana
20190521_114748.jpeg
20190521_114757.jpeg
 
Yameanza kula nguo usiku wa leo! Baada ya kukosa kitu jikoni
Yani panya waingie kote lkn si kabati la Nguo wanatafuna kidogokidogo kiac kwamba huwez kuivaa tena, ukiweka sumu badilisha chakula kila siku na uangalie sehem wanakoingilia uzibe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom