Kuajiriwa na mafanikio tunayotaka

Kuajiriwa na mafanikio tunayotaka

Asante kwa maneno mazuri! mfano mimi nafuga kuku wa asili nazalisha mayai. soko limekuwa shida! mtu anaona bora anunue mayai toka Kenya kwa 4000 au 5000, nakuacha mayai ya asili kwa sababu yanauzwa ghali! lakini kama waagizaji wangetozwa kodi kubwa wasinge agiza.

Narundia tena kutoa shukuran za dhata kwa mkuu ego amefafanua vizur sana.
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli kabisa,lakini kumbuka kuwa mfumo wetu sisi wa-TZ,ni mgumu sana hadi ukatoke siyo rahisi,halafu jambo jingine ni kwamba Ajira hutumika km mtaji tu! wa kuweza kusonga mbele,kwasababu huwezi kuanza hivi hivi tu bila mtaji.hata hao wameendelea kwa kuwa na mitaji hapo mwanzo.
 
Wote wakiajiriwa nani atafanya biashara?

Na wote wakifanya biashara nani ataajiliwa?,MUNGU,aliweka hivyo kwa makusudi maalumu,ukijifanya eti unataka kila mtu awe unavyotaka,basi NATURE haiwezi kuwa-balanced.
 
~~Rejea andiko lako na ufanye utafiti wa kina katika fikra na uhalisia wa kimazingira uone mapungufu ya ulicho kiandika.
JE:
1.Nikweli kwamba mfumo wa elimu ya Tanzania hauna faida yoyote na humuandaa mwanafunzi kuajiriwa kwa 100%?Thibitisha hoja yako kwa ushahidi wa kimfumo.
Asilimia kubwa ya wasomi wa tanzania wameajiriwa katika sekta mbalimbali, na ninaposema mfumo wa elimu ya tanzania ni duni nimezigatia hoja ya mwanafunzi wa kitanzania kukosa plan "b" yakuyaendesha maisha yake kama hatoajiriwa.[/puote]
2.Umhimu wa Elimu ni kumfanya msomi kutajirika tu.?
wapi nilipoandika hivyo?
3.Wewe upo namba ngapi katika orodha ya matajiri wasiokuwa na Elimu duniani.?
labda ni aina gan ya elimu unayozugumzia hapa. mimi nina elimu
4.Wajua biashara nyingi za matajiri uliowataja zinaendeshwa na mifumo iliyobuniwa na wasomi.?
wasomi waliotoka katika mifumo mizuri ya elimu ila siyo
tanzania
 
lipo tatizo katika nchi kununua bidhaa za nje nalo ni fedha kutoka katika mzunguko. lakini huwezi kumshawishi mnunuzi kuwa nunua kwa bei ghali hiki kinatoka hapa hapa hivyo inakuwa ni kazi ya serikali kulinda fedha zake zisipotee kutoka nje.

yaani wewe ukiza mayai hata kwa bei ghali kutoka hapa tanzania ni kwamba mteja mayai amepata na fedha ni mali ya serikali tanzania bado iko katika mzunguko wa fedha ya tanzania. lakini kwa kununua mayai ya bei nafuu ya kenya tanzania tunakuwa na mayai tu fedha ndio imeondoka hivyo mteja akisha kula yale mayai hatuna kitu tena.

wapo viongozi wasiojua mantiki za uchumi, kwa wao wanachotaka ni bidhaa kuporomoka bei na bei zikiwa chini basi wanaona wamekuwa viongozi bora kwa maana bei za vyakula hazikupanda. kwa ajiri ya kushusha bei wanazuia wakulima kuuza vyakula nje. viongozi wa namna hii ndio wamedidimiza kilimo ndio wanadidimiza uchumi. ili kilimo kiendelee kukua tuwe na wazalishaji wakubwa kitu cha kwanza ni soko. kama nchi mnabaini kilimo kinaanza kushika kasi mnazalisha sana hasa kutokana na ruzuku za mbolea na vitu vingine mnaondoa kodi katika vyakula vivyouzwa nje ya nchi. hapo sio kuwa serikali inakuwa haipati fedha bali fedha ambayo mkulima anapata inakuwa inaingia kwenye mzunguko wa serikali na serikali itaipata kupitia kodi na tozo mbalimbali. lengo la kuondoa kodi ni kufanya mazao yako yawe bei nafuu kule kwa wageni na uteke soko lao kwa maana wakulima wetu watuzalishie sisi ndani na kuwazalishia mataifa mengine kama mataifa jirani. sasa lipi linaondoa umasikini wakulima kuzalisha tukazuia soko ili bei ziporomoke na sisi tununue kwa bei ambazo wao wanaendelea kuwa masikini na wengine wakikosa soko na kukata tamaa ya kulima au kutuuuzi kwa bei zenye tija kwao na kuwauzia wanunuzi wa nje?

Asante kwa maneno mazuri! mfano mimi nafuga kuku wa asili nazalisha mayai. soko limekuwa shida! mtu anaona bora anunue mayai toka Kenya kwa 4000 au 5000, nakuacha mayai ya asili kwa sababu yanauzwa ghali! lakini kama waagizaji wangetozwa kodi kubwa wasinge agiza.
 
learnin

Umenena vyema sana.

Haiwezekani kila mtu akajiajiri. Watu wengine wanafanya vizuri zaidi wakiajiriwa. Mimi ninaamini mtu anaweza kuwa mjasiriamali kwenye ajira yake au ya mtu mwingine.

Nina kaka ni mwalimu wa sekondari. Ana kipaji kikubwa sana cha kufundisha na ni mstaarabu. Anagombaiwa sana na wenye mashule na pale alipoamua ku"settle" analipwa mshahara mkubwa na marupurupu mengine tofauti na walimu wengine. Anakoishi ana shamba kubwa anafuga kuku wengi na mbuzi. Hana shida ya hela.

Binafsi sipendi aache hi huduma kazi anayofanya ya kufundisha kwani ni huduma muhimu sana na anazalisha kikubwa na cha maana kuliko wafanyabiashara.

Tafsiri ya entrepreneur ndiyo iliyokosewa kwa kuwekwa -mali kule mwishoni, lakini mtu yeyote anaweza kuwa entrepreneur kwenye siasa, ualimu, udaktari, ukulima, utangazaji, biashara n.k.
 
Last edited by a moderator:
Kama kila mtu angejiajiri na kua mfanya biashara, tungekua na.madaktari? Tungekuwa na waalimu? Tungekuwa na wasafishaji wa miji? Na.kazi.nyingine nyiiingi za.muhimu. Sio kila mtu anaweza kujiajiri.
 
nimesoma ili niajiriwe acheni mambo yenu ya kutishana,kila mtu na maisha yake
mimi furaha yangu ni kuajiriwa,kikubwa maisha yanasonga tu
Duniani tupo watu wa aina tatu. Wanaouliza nini kilitokea, wanaoshuhudia kinachotokea na wanaosababisha kitokee. Kila mtu ana nafasi yake katika hayo makundi matatu. Lakini kwa jitihada binafsi unaweza kutoka kundi moja ukajipeleka kundi lingine. Ukipenda.
 
~~Rejea andiko lako na ufanye utafiti wa kina katika fikra na uhalisia wa kimazingira uone mapungufu ya ulicho kiandika.
JE:
1.Nikweli kwamba mfumo wa elimu ya Tanzania hauna faida yoyote na humuandaa mwanafunzi kuajiriwa kwa 100%?Thibitisha hoja yako kwa ushahidi wa kimfumo.
2.Umhimu wa Elimu ni kumfanya msomi kutajirika tu.?
3.Wewe upo namba ngapi katika orodha ya matajiri wasiokuwa na Elimu duniani.?
4.Wajua biashara nyingi za matajiri uliowataja zinaendeshwa na mifumo iliyobuniwa na wasomi.?
5.Kwakuwa kigezo cha kujiajiri ni kutoelimika (yaani kuwa na kiwango duni cha elimu mfano.darasa la saba)kwanini watanzania wengi wenye akili (walio ishia darasa la saba na kujiajiri) ni maskini kuliko wachache wenye elimu walioajiriwa?
~~~~
Baada ya kujibiwa hayo maswali ntarudi kutoa mchango wangu.

jibu la 1.ni kweli mfumo wa elimu haumuandai vya kutosha mwanafunzi kujiajiri tofauti na technical schools. mfumo uliopo sehemu nyingi duniani unabase na kumpa mwanafunzi technical skills za kufanya kazi na zikipromote ajira tu.ubaya tena kila unavyozidi soma sana ndio unazidi specialize sehemu fulani tu.hii ni kinyume na ujasiliamali halisi.
kutokana na mfumo huu ni vigumu kumpa mwanafunzi softskills za what to do with my education?. wengi waliofanikiwa sana duniani utakuta kilichomsaidia sana ni background ya kwao .elimu anayopewa na wazazi kuhusu biashara huu ndio msingi mkuu .mfano warren buffet,bill gates, mark zuckerberg wote hawa fuatilia utagundua nyumbani kwao wazazi wao waliwapa kitu cha ziada.ndio maana hata walipodrop out lakini walikuwa na kitu cha ziada baada ya kupata elimu ya darasani kidogo tu. vilevile aliko dangote babu yake na mjomba wake walimpa elimu ya ziada ya kiujasiliamali so sio elimu ya darasani pekee(elimu ya ziada inahitajika kuwekwa mashuleni japokuwa ni vigumu sana kuiweka,vivyo ni muhimu wazaazi pia kuwa na mchango) nashangaza sana baba ni mfanya biashara baada ya kumfundisha mtoto japo kwa saa tu kuhusu biashara utakuta akimfokea "kafanye assignment ,au nenda kalale hayawahusu watoto nyie"

2.umuhimu wa elimu unamchango mkubwa kumfanya mtu kuajirika sababu jinsi unavyoongea elimu ndio zaidi ndivyo unazidi kuspecialize kwenye kitu kimoja ,mfano PHD holder wengi zaidi kuwa mkufunzi au researcher ndio wanapoishia.unakuta mtu ana phd ya entrepreneurship lakini hata duka hana .(hapa wengi wao waliofanikiwa wanakuwa na elimu ya ziada walioipata mtaani au sehemu tofauti kwa kutumia ujuzi wao kawa njia ya kuanzisha huduma au biashara fulani mfano consultation,financial services agency na zinginezo)
3. wewe upo namba ngapi kwa matajiri wasiokuwa na elimu? Mtoa maada hajamaanisha kwamba mtu asiwe na elimu hapana.bali alikuwa anamaanisha utofauti kati ya elimu rasmi na elimu ya ziada ambayo isio rasmi. kuna ambao hawana elimu rasmi kiwango kikubwa lakini wanaelimu isiyo rasmi ambayo imewasaidia .
4. ni kweli biashara nyingi za matajiri zilizokubwa zime kuwa designed na watu wenye elimu rasmi kubwa. hapa kuna utofauti kati ya intrapreneurship v entrepreneurship ,wewe ukiajiriwa na kampuni ni muhmu kama una idea ukampa bosi wako au mkurugenzi akaimplement na kuleta matunda na wewe ukapewa commission kubwa kabisa sababu huna fedha au uwezo wa kulitumia binafsi. lakini muhimu aidi ni mjasiliamali kuwa na kitu chake alichobuni halafu baadae akaanza kununua makampuni au uvumbuzi wa wengine aautumia kama wake(merger and acquisition mfano facebook founder alinunua whatsapp)."Most of richest people employ the people who are more intelligent that they are"
5.mwisho si kila mtu ataweza kujiajiri.bali kila mtu na wakati wake. watu wengi ambao wamejiajiri walikuwa waajiliwa wazuri sana.mfano wengi nawafahamu waliokuwa wahasibu wazuri ,Human resourses wamefungua makampuni ya auditing na consultation makubwa kabisa BAADA YA KUPATA EXPERIENCE KUBWA KABISA(huu pia ni ujasiriamali bora kabisa )


NOTE; si kila aliefanikiwa duniani ni kutokana na elimu,wengine wamerithi utajiri ,pia wengine wanabahati tu.wengine ni wezi tu. na wengine ni mafisadi. kujiajiri moja kwa moja after school si kitu rahisi inabidi uwe vizuri kweli na KILA UNAPOKUWA DARASANI USOME KWA MELENGO NA KILA KITU UJUE KWANINI UNASOMA NA NINI NI MATUMIZI AU UMUHIMU WA UNACHOSOMA UKIRINGANISHA NA MALENGO YAKO. MDA MWINGINE NI PERCEPTION TU ,JINSI UNAVYO PERCEIVE UNAPOSOMA KITU. pia waalimu wenyewe wnapomfundisha mwanafunzi ni muhimu kumfundisha mwanafunzi kama anampa maarifa sio ilimradi afaulu mtihani tu.
lazima watu waajiriwe ili kazi zifanyike.kosa kubwa ni kuajiriwa miaka mingi au almost maisha yote umekaa kuajiriwa tu.
WORK TO LEARN ,DONT WORK FOR MONEY .


Samahani na naomba kurekebishwa kama nimekosea sehemu kimaandishi na nilichoandika.hayo ni maoni tu.
 
Duniani tupo watu wa aina tatu. Wanaouliza nini kilitokea, wanaoshuhudia kinachotokea na wanaosababisha kitokee. Kila mtu ana nafasi yake katika hayo makundi matatu. Lakini kwa jitihada binafsi unaweza kutoka kundi moja ukajipeleka kundi lingine. Ukipenda.
upo sawa KABISA MKUU,BIG UP UMUHIMU NI KUKAA KWA MDA KWENYE KUNDI MOJA NA KUHAMA.
KOSA NI KUWA KWENYE KUNDI MOJA MAISHA YAKO YOTE.
 
upo sawa KABISA MKUU,BIG UP UMUHIMU NI KUKAA KWA MDA KWENYE KUNDI MOJA NA KUHAMA.
KOSA NI KUWA KWENYE KUNDI MOJA MAISHA YAKO YOTE.

Je? elimu yenu ya tz inatoa elimu kulingana na mgawanyo wa hayo makundi???
 
Nashangaa mnailaumu serikali wakati kuna wafanyabiashara wanatoboa humu humu na kwa mazingira magumu haya haya, huo wote ni uoga wa maisha tu
 
Danp36 hongera sana kamanda nimekusoma vizuri sana!
 
Last edited by a moderator:
Je? elimu yenu ya tz inatoa elimu kulingana na mgawanyo wa hayo makundi???
Elimu ya tanzania inatoa elimu ya kubakikundi moja kwa ujumla,ambayo inampelekea mtu kuwa mwajirwa mpaka anazeeka.akipata mafao anafikiria nunua daladala,baada ya mda anafilisika sababu hajawahi kuwa hata na duka,baada ya mda tena anapata presha.mda mfupi mara hatunaye duniani sababu ya presha na kuishi maisha y stress.ni vizuri hata waajiriwa wakafanya kazi kwa kupata maarifa huku wakijua kuajiriwa ni kwa muda tu.kabla ya kustaafu lazima mtu awe na huuduma au biashara. kila mtu kaumbwa na element za ujasiliamali katika sektatofauti tofauti , kwahiyo hata charles kimei (ceo wa crdb bank anapray part yake,diamond platnam(musicisian anapray part) huo pia ni ujasiriamali.
 
Back
Top Bottom