rasomaka
Senior Member
- Dec 26, 2013
- 115
- 139
Yaani sina hata hamu. Gari yangu niliyoagiza sbtjapan mwezi wa Feb mwanzoni limefika dar tangu Ijumaa tarehe 20 Machi, lakini huo ukilitimba wa Agent wa Clearing and Forwarding niliyemchagua mbona kasheshe. Yaani yupo very manually au sijui nisemeje. Hanipi update zozote wala nini, ukimpigia simu au meseji hajibu mpaka ajisikie yeye. Kodi nimeshalipa Tsh 6,200,000, charges zingine bado (shipping line, port charges, reg fees etc) kwa madai kuwa atazilipa yeye mwenyewe kwanza halafu nitam-refund.
Yaani kiufupi hajali kabisaaa kwamba mwenzake nna moto na mkoko mpya halafu yeye anarembaremba tu. Nina hasira hapa hadi nataka nipasuke. Siku nyingine nitaagiza gari na kufanya Clearing mwenyewe nitembee na file hadi kiatu kiishe.
Clearing and Forwarding agents oyeeeeeeee...
Yaani kiufupi hajali kabisaaa kwamba mwenzake nna moto na mkoko mpya halafu yeye anarembaremba tu. Nina hasira hapa hadi nataka nipasuke. Siku nyingine nitaagiza gari na kufanya Clearing mwenyewe nitembee na file hadi kiatu kiishe.
Clearing and Forwarding agents oyeeeeeeee...