Maji safi kuna kozi special za maji... zipo chuo maji na SUA.
Kongole kwao.
Environmental kwenye water supply anaiba tu yeye kwake ni maji machafu.
Environmental Engineer kazi yake ni kupigia debe upandaji miti ya kivuli ili kuzuia jangwa; walipata kusikika watu fulani
😀 . Wewe umeenda hatua moja mbele angalau umetaja maji machafu. Ninyi nyote hujiweka wazi kutozingatia kwenu uhalisia.
Kozi ya Environmental Engineering hapa Tanzania ilianzishwa miaka ya enzi za Nyerere ikiitwa
Public Health Engineering (PHE). Kozi hiyo ililenga kuandaa wataalam watakaoweza kwenda vijijini na mijini kama maaskari walio mstari wa mbele katika kutumia afya ya jamii kama mbinu ya kupambana na magonjwa, moja ya maadui wakubwa watatu wa taifa. Kazi kuu ya wahandisi wale ilikuwa ni ya majisafi, majitaka, taka-ngumu na udhibiti wa uchafuzi wa mazingira.
Kutokana na maboresho kwenye fani, na mahitaji ya kitaifa na kimataifa, kozi hiyo iliboreshwa na kuitwa
Environmental Engineering, jina ambalo liko mpaka leo.
Kusema Environmental Engineers tunaibia kuhusu masuala ya majisafi, hakuzingatii uhalisia wa yaliyomo kwenye kozi yenyewe ya Uhandisi Mazingira. Siyo lazima kozi iwe na neno
Maji au Water ili mhitimu awe mtaalam wa maji. Wajemeni!
Na tunako enda kazi za water supply atakua hapewi tena maana kuna watu walio base kwenye hiyo sector (ambao hawajaunga unga).
Huo utakuwa uamuzi wa kijuha kuwahi kutokea hapa nchini.
Huwezi kuzuia watu mahiri kwenye tasnia ya maji kutumia ujuzi wao ambao taifa limetumia gharama nyingi kuwaandaa, eti tu kuridhisha watu fulanifulani wanaotaka kutafutia soko wahitimu wa kozi zao kwa mbinu ya kizembe ya kuzuia wahitimu wa kozi zingine.
Sote tunajenga taifa moja, ni wehu kuanza kunyang'anyana fito.