Omusolopogasi
JF-Expert Member
- Aug 31, 2017
- 7,105
- 18,005
WanaJF - wakati mwingine ni vizuri kusema jambo linalokukwaza katika maisha kwa watu wengine - si kwa sababu utapata ufumbuzi, ila kwa sababu ukilisema kwa watu wengine inakupunguzia msongo wa mawazo na kichwa kuuma.
Kuna huyu mwenza wangu. Tuna watoto pamoja na tunakaa pamoja. Ni mume na mke. Mambo ya kawaida sana kama usafi wa nyumbani yanamshinda. Hawezi kabisa kujifunza, akabadilika. Miaka nenda rudi. Akiosha vyombo, ataacha mabaka ya chakula juu yake.
Siyo kwamba kuna tatizo la maji ama sabuni nyumbani - la hasha! Akienda kununua chakula, atanunua vitu kama matunda ya juma zima na yote ukiyaangalia, yako tayari kuliwa siku hiyo hiyo. Kwa sababu yamenunuliwa mengi kwa ajili ya juma zima, baada ya siku 2-3 hivi, yote yanaoza. Yakishaoza, atayakata hivyo hivyo na kuyaweka mezani kwa ajili ya kula. Ukishaweka mdomoni, ndio unapambana na ladha ya kitu kilichooza.
Hata watoto, ambao bado ni wadogo, tayari wanajua na kuepuka kitu kisichostahili kuliwa na binadamu lakini mama yao hawezi kabisa. Nimejaribu kumwelewesha lakini wapi. Kuna wakati ilibidi tuwe tunakwenda wote sokoni ili ajifunze baada ya mwaka mmoja nikamwacha awe anakwenda peke yake. Kwa sababu ya kazi, haiwezekani siku zote kwenda naye. Siku hizi nimemwacha afanye manunuzi mwenyewe. Lakini hakuna mabadiliko kabisa.
Hapa naongelea mwanamke mwenye elimu ya chuo kikuu lakini kwa sababu watoto bado ni wadogo, ni mama wa nyumbani kwa sasa. Hata kama haukwenda shule, je, kweli ni vigumu kujua kuwa haya mananasi/mapapai niliyonunua kwa ajili ya kutumia kwa siku 7 kwa hali yake ya kuiva hayawezi kukaa siku 7? Kama kuna umuhimu wa kununua ya juma zima basi nichanganye yaliyoiva na magumu? Yaliyoiva ya kula leo na kesho na magumu ya kula baadae?
Vijana wa sasa - kosea kitu kingine lakini usikosee kuchagua mwenza wa maisha ambaye unaapa kukaa naye hadi kifo kiwatenganishe. Ukikosea, utakufa kabla ya wakati wako. Tafadhali zingatieni hili. Waingereza wanasema, "to be forewarned is to be forearmed".
Kuna huyu mwenza wangu. Tuna watoto pamoja na tunakaa pamoja. Ni mume na mke. Mambo ya kawaida sana kama usafi wa nyumbani yanamshinda. Hawezi kabisa kujifunza, akabadilika. Miaka nenda rudi. Akiosha vyombo, ataacha mabaka ya chakula juu yake.
Siyo kwamba kuna tatizo la maji ama sabuni nyumbani - la hasha! Akienda kununua chakula, atanunua vitu kama matunda ya juma zima na yote ukiyaangalia, yako tayari kuliwa siku hiyo hiyo. Kwa sababu yamenunuliwa mengi kwa ajili ya juma zima, baada ya siku 2-3 hivi, yote yanaoza. Yakishaoza, atayakata hivyo hivyo na kuyaweka mezani kwa ajili ya kula. Ukishaweka mdomoni, ndio unapambana na ladha ya kitu kilichooza.
Hata watoto, ambao bado ni wadogo, tayari wanajua na kuepuka kitu kisichostahili kuliwa na binadamu lakini mama yao hawezi kabisa. Nimejaribu kumwelewesha lakini wapi. Kuna wakati ilibidi tuwe tunakwenda wote sokoni ili ajifunze baada ya mwaka mmoja nikamwacha awe anakwenda peke yake. Kwa sababu ya kazi, haiwezekani siku zote kwenda naye. Siku hizi nimemwacha afanye manunuzi mwenyewe. Lakini hakuna mabadiliko kabisa.
Hapa naongelea mwanamke mwenye elimu ya chuo kikuu lakini kwa sababu watoto bado ni wadogo, ni mama wa nyumbani kwa sasa. Hata kama haukwenda shule, je, kweli ni vigumu kujua kuwa haya mananasi/mapapai niliyonunua kwa ajili ya kutumia kwa siku 7 kwa hali yake ya kuiva hayawezi kukaa siku 7? Kama kuna umuhimu wa kununua ya juma zima basi nichanganye yaliyoiva na magumu? Yaliyoiva ya kula leo na kesho na magumu ya kula baadae?
Vijana wa sasa - kosea kitu kingine lakini usikosee kuchagua mwenza wa maisha ambaye unaapa kukaa naye hadi kifo kiwatenganishe. Ukikosea, utakufa kabla ya wakati wako. Tafadhali zingatieni hili. Waingereza wanasema, "to be forewarned is to be forearmed".