lazima ukae
JF-Expert Member
- May 15, 2013
- 788
- 380
Nina mpenzi wangu ambae tuna miezi mitatu toka tuanzishe uhusiano wetu mimi nampenda na yeye nina imani ananipenda ingawa sina uhakika kama na yeye ananipenda kwa kiwango kilekile ninachompenda mimi mana sina uwezo wa kuufungua moyo wake na kungalia ananipenda kwa kiasi gani.
Kwa kipindi chote hicho cha takribani miezi mitatu tumekua na maelewano mazuri na mpenzi wangu ingawa kuna kule kupishana maneno mara chachechache ambapo ni jambo la kawaida kutokea kwenye mahusiano mana hata vikombe tu kabatini hugongana.
Jana mida ya jioni alinipigia simu kwamba anashida na kiasi fulani cha pesa hivyo anaomba nimsaidie, kwakua nilikua safarini toka mkoani nikamwambia asubiri kama lisaa limoja nitakua nishafika mjini na nitamtumia hicho kiasi cha pesa mana kipo ndani ya uwezo wangu.
Nilivyofika mjini haraka sana nikamtumia hiyo pesa kupitia mitandao ya simu na akanijulisha kuwa ameipata na anashukuru sana baaada ya kupita kama lisaa limoja akanipigia simu kwamba ameenda kwa wakala lakini kwa bahati mbaya amekosea namba ya wakala hivyo pesa imeenda kwa wakala mwingnine na hawezi kuipata siku hiyohiyo hivyo anaomba nimtumie pesa nyingine ikibidi nikope hata kwa mtu kitu ambacho sikukubaliana nacho mana yeye ndo amefanya uzembe na siwezi kujiingiza kwenye madeni yasiyokua na ulazima.
Hivi ninavyoongea toka jana kanichunia na mimi nimekaa zangu kimya na nishaamua kama akiendelea kukaa kimya basi na mapenzi yenyewe yafe tu huenda haikua ridhiki mana najua tu atakua amenikasirikia kwa kosa ambalo sio langu.
Je hapa mimi nina kosa waungwana ?
Kwa kipindi chote hicho cha takribani miezi mitatu tumekua na maelewano mazuri na mpenzi wangu ingawa kuna kule kupishana maneno mara chachechache ambapo ni jambo la kawaida kutokea kwenye mahusiano mana hata vikombe tu kabatini hugongana.
Jana mida ya jioni alinipigia simu kwamba anashida na kiasi fulani cha pesa hivyo anaomba nimsaidie, kwakua nilikua safarini toka mkoani nikamwambia asubiri kama lisaa limoja nitakua nishafika mjini na nitamtumia hicho kiasi cha pesa mana kipo ndani ya uwezo wangu.
Nilivyofika mjini haraka sana nikamtumia hiyo pesa kupitia mitandao ya simu na akanijulisha kuwa ameipata na anashukuru sana baaada ya kupita kama lisaa limoja akanipigia simu kwamba ameenda kwa wakala lakini kwa bahati mbaya amekosea namba ya wakala hivyo pesa imeenda kwa wakala mwingnine na hawezi kuipata siku hiyohiyo hivyo anaomba nimtumie pesa nyingine ikibidi nikope hata kwa mtu kitu ambacho sikukubaliana nacho mana yeye ndo amefanya uzembe na siwezi kujiingiza kwenye madeni yasiyokua na ulazima.
Hivi ninavyoongea toka jana kanichunia na mimi nimekaa zangu kimya na nishaamua kama akiendelea kukaa kimya basi na mapenzi yenyewe yafe tu huenda haikua ridhiki mana najua tu atakua amenikasirikia kwa kosa ambalo sio langu.
Je hapa mimi nina kosa waungwana ?