plan z
JF-Expert Member
- Jun 10, 2019
- 1,395
- 1,439
SIMU/WHATSAPP 0768571786
Ilipoishia..
kila mtu chuoni alijua kua nilikua nikimpenda Leyra hata yeye mwenyewe alijua hilo kwa sababu kila mtu alisema tunapendezana kama tungekua pamoja.
Songa nayo..
Nilitamani sana iwe hivyo lakini nilishindwa, nilikua mgonjwa wa aibu, ujanja na ucheshi wangu kwa watu wote ulikua bure sikua nimewahi kutongoza msichana yoyote toka utoto wangu, wala kua katika uhusiano wowote wa kimapenzi licha ya kutakwa na wanawake kadhaa hapo nyuma. Nilifanya hivyo sio kwa sababu sikua nimekamilika, hapana mimi ni mwanaume rijali niliyekamilika lakini nilifanya hivyo kwa sababu elimu yangu yote ya awali nilisoma seminari maadili na aina ya maisha niliyoishi yalichangia mimi kua hivyo, pia nilifanya hivyo kwa ajili ya masomo, mawaidha ya baba yangu hayakutoka masikioni mwangu hata siku moja pia nilikua nimetoka mbali sana sikutaka kusongwa na mapenzi, lengo langu kubwa lilikua kua daktari bingwa wa magonjwa sugu ya wanawake na watoto pamoja na mifupa ili nimsaidie bibi yangu ambaye toka napata akili sikuwahi kumuona akitembea kwa miguu yake zaidi ya kutumia kiti cha magurudumu.
Mpaka muda huo nakubali kweli nilikua domo zege kwani licha ya kumpenda Leyra sikua nimewahi kumsemesha neno lolote, sikumuogopa bali nilimuonea sana aibu kila nilipo jiringanisha nae niliona mimi sio hadhi yake tabia yake ya kutopenda wanaume ndio ilinimaliza kila nilipowaza kumwambia jibu la kukataliwa lilikuja kichwani kwangu, sikua na jinsi niliishia kukata tamaa na kuumia mwenyewe.Haikua siri tena kila mtu alijua kua nilikua namuogopa Leyra, marafiki zangu wote walijua hata yeye mwenyewe alijua lakini hakufanya kitu chochote nadhani alikua akinicheka kimoyo moyo.
Umaarufu wangu wote ulibadilikia hapo, jina la Alfred Kamba liliacha kusikika tena kwa sababu ya kushuka kwa maendeleo yangu ya kitaaluma. Lakini hii haikunizuia kufahamika kwani kama Yohane mbatizaji nilibatizwa jina la utani Domo Gundi kwa sababu ya kushindwa kumtongoza Leyra.
Jina hili lilikaa mdomoni mwa watu wengi kama sala za asubuhi, lilikaririwa na kila mtu kama orodha za kuzidisha ma lecture tu ndio watu pekee ambao hawakulijua.
Nilikosa raha, akili yangu ilivurugika kiasi cha kupoteza muelekeo wangu mzima wa kitaaluma.
Lucyra Rustin alikua miongoni mwa wasichana warembo sana ambao mwanaume yoyote hawezi kujutia muda wake kua nao. Mvuto wa sura na umbo lake viliuelezea wazi uzuri aliokua nao, kwa wasichana wote Lucyra alifua dafu kasoro kwa Leyra tu ndipo aligonga mwamba nadhani kama sio robo basi aliufikia uzuri wa Leyra kwa theluthi moja.
Lucyra alikua jirani yangu nyumba zetu zilikua pua na mdomo. Tulitoka sehemu moja, tulikua na kucheza pamoja toka utotoni. Wazazi wetu walikua ni marafiki wakubwa sana kwa sababu ya ujirani wetu wa muda mrefu, walisaidiana pamoja kwenye shida na raha, upendo wao ulifanya tuwe kama ndugu.
Toka utotoni Lucyra alitokea kunipenda sana labda kwa sababu wazazi wetu walitutania kwa kutuita mtu na mkewe. Mara kwa mara Lucyra alikua akishinda kwetu, tulicheza michezo yote ya kitoto kwa furaha bila wazazi wetu kutuingilia.
Nilipokua sipo alikua akija nyumbani kuniulizia, muda mwingi alijali kuhusu mimi kuliko hata alivyojijali yeye mwenyewe.
Kila siku Lucyra alikua akiniletea pipi na ice cream za maziwa kutoka dukani kwao, sikujali kama ameiba au amepewa nilikua kama kupe, nilijenga ukaribu mkubwa ili nizidi kuzifaidi zile zawadi zake.
Tulikua watoto lakini nilikua mkatili sana siku ambayo hakuniletea kitu nilinuna maskini ya Mungu mtoto wa watu alikua anatoa machozi kunililia na kuniomba msamaha utasema alikua amenikosea.
Ukaribu wetu ulikua kivutio kwa watu wengi harusi nyingi za mtaani kwetu walitutumia sisi kama baba harusi na bibi harusi wadogo, tulikua kielelezo na maana halisi ya upendo kwa kila mtu, hata wazazi wetu wote walijisikia fahari.
Polepole muda ulianza kututenganisha, nilikua nimemzidi Lucyra miaka miwili. Umri wangu wa kuanza shule ya msingi ulifika, baba yangu Mzee Kamba aliachana na utani wote wa huko nyuma wa kutuita mke na mume, alinipeleka seminari ndogo ya Mtakatifu Don Bosco iliyopo jijini Nairobo nchini Kenya, ambapo nilianza elimu yangu ya msingi, darasa la kwanza.
Nilikua na miaka saba lakini baba yangu hakujali umri wangu wala mimi kua mbali na nyumbani alichojali ni ubora wa elimu na malezi niliyokua ninaenda kuyapata. Nililia sana siku baba yangu aliponiacha seminarini na kurudi Tanzania, sikua nikinyonya lakini nilimkumbuka sana mama yangu kuliko kitu chochote, siku ya kwanza tu niliona ni kama nimekaa huko mwaka mmoja. Seminari nzima darasa la kwanza hadi la saba tulikua watu wanafunzi mia tatu tu. Tulikua wachache sana hivyo huduma zote tulizopata pale zilikua bora kuliko hata huduma za taasisi zingine binafsi.
Ukiacha pipi na ice cream za Lucyra, kitu kingine ninachokikumbuka seminarini hapo tulifundishwa upendo, uaminifu na nidhamu ya juu kabisa, tulikua wadogo lakini mapadri hawakua na masihara hata kidogo lilipokuja suala la nidhamu na uaminifu, kwa macho yangu nilishuhudia mwanafunzi mmoja akifukuzwa kwa kosa la kuokota tunda bustanini na kulila bila kupewa ruhusa.
Tulikua tunaandaliwa kua mapadri wa baadae kama yalivyokua malengo ya seminari zote duniani kote. Hivyo tulifundishwa utii wa hali ya juu mno, mapadri hawakujali umri wala darasa unalosoma, muda wa sala ukifika saa 11 na nusu asubuhi lazima wote muwepo kanisani, muda wa darasani lazima muwepo darasani, muda wa michezo lazima muwepo uwanjani, bila kusahau muda wa kazi lazima wote mshiriki.Tulikua kama siafu kila kitu kilifanyika pamoja kwa ushirikiano, tulioga muda mmoja wote maji ya baridi, tulikula chumba kimoja, tulivaa sare moja hatukuruhusiwa kubeba nguo zozote kutoka nyumbani, kifupi tulikua kama watoto wa mama na baba mmoja.
Hii ndio ilikua aina yangu ya maisha kutoka nikiwa na miaka saba mpaka ninamaliza kitado cha sita nikiwa na miaka karibu kumi na saba hivi. Kwa maisha ya aina hii unaanzaje kuwaza wanawake?, muda wote mtu upo bize, upende usipende kanisani utaenda, utake usitake kuamka utawahi, uwanjani michezo hutashiriki hata kama upendi, kazi utafanya na mwisho wa siku maji ya baridi utaoga.
Eti ndugu zangu kwa hali hii kwanini nisiwe domo geze?, naanzaje kwa mfano ikiwa tu sketi na wasichana unawaona mara 2 kwa mwaka wakati wa likizo kila baada ya miezi sita.
Maisha ya shule ya seminari yalifanya nimsahau Lucyra ilifika hatua hata pipi na ice cream zake nikazisahau, nilikua napambana ili niwepo shuleni hapo kwani mchujo ulianzia darasa la kwanza mpaka kidato cha sita, usipofikisha wastani wa 75 hata uwe mtoto wa raisi wa nchi utarudi kwenu. Nilisahau kila kitu kuhusu Lucyra, marafiki zangu wakubwa walikua ni chakula (ninapenda sana kula), kitabu na maji ya baridi muda wa kuoga.
Lucyra tulionana nae tu wakati wa likizo nilipokua nikirudi nyumbani nchini Tanzania.
Kipindi cha likizo yangu ndio kilikua kipindi cha Lucyra
kunenepa kila aliposikia nimerudi alikua akija nyumbani na kushinda kila siku. Kuonana na kuongea na mimi ndio ilikua furaha yake kubwa kuliko kitu chochote nakumbuka kila muda tuliokua pamoja Lucyra hakuchoka kuniambia kua ananipenda sana, hata tulipokua kua wakubwa hakuchoka kunipenda, nilipomsahau alinikumbuka kwa simu, jumbe nzuri za mapenzi pamoja na email zisizokua na idadi.
.....Itaendelea....
Ilipoishia..
kila mtu chuoni alijua kua nilikua nikimpenda Leyra hata yeye mwenyewe alijua hilo kwa sababu kila mtu alisema tunapendezana kama tungekua pamoja.
Songa nayo..
Nilitamani sana iwe hivyo lakini nilishindwa, nilikua mgonjwa wa aibu, ujanja na ucheshi wangu kwa watu wote ulikua bure sikua nimewahi kutongoza msichana yoyote toka utoto wangu, wala kua katika uhusiano wowote wa kimapenzi licha ya kutakwa na wanawake kadhaa hapo nyuma. Nilifanya hivyo sio kwa sababu sikua nimekamilika, hapana mimi ni mwanaume rijali niliyekamilika lakini nilifanya hivyo kwa sababu elimu yangu yote ya awali nilisoma seminari maadili na aina ya maisha niliyoishi yalichangia mimi kua hivyo, pia nilifanya hivyo kwa ajili ya masomo, mawaidha ya baba yangu hayakutoka masikioni mwangu hata siku moja pia nilikua nimetoka mbali sana sikutaka kusongwa na mapenzi, lengo langu kubwa lilikua kua daktari bingwa wa magonjwa sugu ya wanawake na watoto pamoja na mifupa ili nimsaidie bibi yangu ambaye toka napata akili sikuwahi kumuona akitembea kwa miguu yake zaidi ya kutumia kiti cha magurudumu.
Mpaka muda huo nakubali kweli nilikua domo zege kwani licha ya kumpenda Leyra sikua nimewahi kumsemesha neno lolote, sikumuogopa bali nilimuonea sana aibu kila nilipo jiringanisha nae niliona mimi sio hadhi yake tabia yake ya kutopenda wanaume ndio ilinimaliza kila nilipowaza kumwambia jibu la kukataliwa lilikuja kichwani kwangu, sikua na jinsi niliishia kukata tamaa na kuumia mwenyewe.Haikua siri tena kila mtu alijua kua nilikua namuogopa Leyra, marafiki zangu wote walijua hata yeye mwenyewe alijua lakini hakufanya kitu chochote nadhani alikua akinicheka kimoyo moyo.
Umaarufu wangu wote ulibadilikia hapo, jina la Alfred Kamba liliacha kusikika tena kwa sababu ya kushuka kwa maendeleo yangu ya kitaaluma. Lakini hii haikunizuia kufahamika kwani kama Yohane mbatizaji nilibatizwa jina la utani Domo Gundi kwa sababu ya kushindwa kumtongoza Leyra.
Jina hili lilikaa mdomoni mwa watu wengi kama sala za asubuhi, lilikaririwa na kila mtu kama orodha za kuzidisha ma lecture tu ndio watu pekee ambao hawakulijua.
Nilikosa raha, akili yangu ilivurugika kiasi cha kupoteza muelekeo wangu mzima wa kitaaluma.
Lucyra Rustin alikua miongoni mwa wasichana warembo sana ambao mwanaume yoyote hawezi kujutia muda wake kua nao. Mvuto wa sura na umbo lake viliuelezea wazi uzuri aliokua nao, kwa wasichana wote Lucyra alifua dafu kasoro kwa Leyra tu ndipo aligonga mwamba nadhani kama sio robo basi aliufikia uzuri wa Leyra kwa theluthi moja.
Lucyra alikua jirani yangu nyumba zetu zilikua pua na mdomo. Tulitoka sehemu moja, tulikua na kucheza pamoja toka utotoni. Wazazi wetu walikua ni marafiki wakubwa sana kwa sababu ya ujirani wetu wa muda mrefu, walisaidiana pamoja kwenye shida na raha, upendo wao ulifanya tuwe kama ndugu.
Toka utotoni Lucyra alitokea kunipenda sana labda kwa sababu wazazi wetu walitutania kwa kutuita mtu na mkewe. Mara kwa mara Lucyra alikua akishinda kwetu, tulicheza michezo yote ya kitoto kwa furaha bila wazazi wetu kutuingilia.
Nilipokua sipo alikua akija nyumbani kuniulizia, muda mwingi alijali kuhusu mimi kuliko hata alivyojijali yeye mwenyewe.
Kila siku Lucyra alikua akiniletea pipi na ice cream za maziwa kutoka dukani kwao, sikujali kama ameiba au amepewa nilikua kama kupe, nilijenga ukaribu mkubwa ili nizidi kuzifaidi zile zawadi zake.
Tulikua watoto lakini nilikua mkatili sana siku ambayo hakuniletea kitu nilinuna maskini ya Mungu mtoto wa watu alikua anatoa machozi kunililia na kuniomba msamaha utasema alikua amenikosea.
Ukaribu wetu ulikua kivutio kwa watu wengi harusi nyingi za mtaani kwetu walitutumia sisi kama baba harusi na bibi harusi wadogo, tulikua kielelezo na maana halisi ya upendo kwa kila mtu, hata wazazi wetu wote walijisikia fahari.
Polepole muda ulianza kututenganisha, nilikua nimemzidi Lucyra miaka miwili. Umri wangu wa kuanza shule ya msingi ulifika, baba yangu Mzee Kamba aliachana na utani wote wa huko nyuma wa kutuita mke na mume, alinipeleka seminari ndogo ya Mtakatifu Don Bosco iliyopo jijini Nairobo nchini Kenya, ambapo nilianza elimu yangu ya msingi, darasa la kwanza.
Nilikua na miaka saba lakini baba yangu hakujali umri wangu wala mimi kua mbali na nyumbani alichojali ni ubora wa elimu na malezi niliyokua ninaenda kuyapata. Nililia sana siku baba yangu aliponiacha seminarini na kurudi Tanzania, sikua nikinyonya lakini nilimkumbuka sana mama yangu kuliko kitu chochote, siku ya kwanza tu niliona ni kama nimekaa huko mwaka mmoja. Seminari nzima darasa la kwanza hadi la saba tulikua watu wanafunzi mia tatu tu. Tulikua wachache sana hivyo huduma zote tulizopata pale zilikua bora kuliko hata huduma za taasisi zingine binafsi.
Ukiacha pipi na ice cream za Lucyra, kitu kingine ninachokikumbuka seminarini hapo tulifundishwa upendo, uaminifu na nidhamu ya juu kabisa, tulikua wadogo lakini mapadri hawakua na masihara hata kidogo lilipokuja suala la nidhamu na uaminifu, kwa macho yangu nilishuhudia mwanafunzi mmoja akifukuzwa kwa kosa la kuokota tunda bustanini na kulila bila kupewa ruhusa.
Tulikua tunaandaliwa kua mapadri wa baadae kama yalivyokua malengo ya seminari zote duniani kote. Hivyo tulifundishwa utii wa hali ya juu mno, mapadri hawakujali umri wala darasa unalosoma, muda wa sala ukifika saa 11 na nusu asubuhi lazima wote muwepo kanisani, muda wa darasani lazima muwepo darasani, muda wa michezo lazima muwepo uwanjani, bila kusahau muda wa kazi lazima wote mshiriki.Tulikua kama siafu kila kitu kilifanyika pamoja kwa ushirikiano, tulioga muda mmoja wote maji ya baridi, tulikula chumba kimoja, tulivaa sare moja hatukuruhusiwa kubeba nguo zozote kutoka nyumbani, kifupi tulikua kama watoto wa mama na baba mmoja.
Hii ndio ilikua aina yangu ya maisha kutoka nikiwa na miaka saba mpaka ninamaliza kitado cha sita nikiwa na miaka karibu kumi na saba hivi. Kwa maisha ya aina hii unaanzaje kuwaza wanawake?, muda wote mtu upo bize, upende usipende kanisani utaenda, utake usitake kuamka utawahi, uwanjani michezo hutashiriki hata kama upendi, kazi utafanya na mwisho wa siku maji ya baridi utaoga.
Eti ndugu zangu kwa hali hii kwanini nisiwe domo geze?, naanzaje kwa mfano ikiwa tu sketi na wasichana unawaona mara 2 kwa mwaka wakati wa likizo kila baada ya miezi sita.
Maisha ya shule ya seminari yalifanya nimsahau Lucyra ilifika hatua hata pipi na ice cream zake nikazisahau, nilikua napambana ili niwepo shuleni hapo kwani mchujo ulianzia darasa la kwanza mpaka kidato cha sita, usipofikisha wastani wa 75 hata uwe mtoto wa raisi wa nchi utarudi kwenu. Nilisahau kila kitu kuhusu Lucyra, marafiki zangu wakubwa walikua ni chakula (ninapenda sana kula), kitabu na maji ya baridi muda wa kuoga.
Lucyra tulionana nae tu wakati wa likizo nilipokua nikirudi nyumbani nchini Tanzania.
Kipindi cha likizo yangu ndio kilikua kipindi cha Lucyra
kunenepa kila aliposikia nimerudi alikua akija nyumbani na kushinda kila siku. Kuonana na kuongea na mimi ndio ilikua furaha yake kubwa kuliko kitu chochote nakumbuka kila muda tuliokua pamoja Lucyra hakuchoka kuniambia kua ananipenda sana, hata tulipokua kua wakubwa hakuchoka kunipenda, nilipomsahau alinikumbuka kwa simu, jumbe nzuri za mapenzi pamoja na email zisizokua na idadi.
.....Itaendelea....