Kosa Langu - 2

Kosa Langu - 2

plan z

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2019
Posts
1,395
Reaction score
1,439
SIMU/WHATSAPP: 0768571786

Furaha hii na salamu za pongezi za kila mara kutoka nyumbani vilidumu kwa semista kadhaa, lakini polepole kama mwendo wa kinyonga mambo yalianza kubadilika ufaulu wangu ulianza kupungua kila mtu aliliona hilo mimi pia nilijiona kua ninafeli lakini sikufanya chochote kwani muda huo akili, mawazo na kila kitu changu kilikua kina muwaza Leyra, msichana nilietokea kumpenda ghafla kwa sababu ya uzuri aliokua nao.

Nimewaona wasichana wengi warembo mitandaoni na kwenye filamu nzuri za mapenzi lakini sijaona msichana kama Leyra.
Leyra alikua msichana mrembo pengine kuliko wote niliowahi kuwaona kwa macho yangu yote mawili tena yakisaidiwa na nguvu miwani yangu ya macho ambayo kutwa nzima haikubanduka machoni mwangu.

Tabasamu lake lilikua ni tiba tosha ya magonjwa mengi pengine kuliko hata madawa tuliyoyasoma hapo chuoni, sio tu tiba bali tabasamu lake lingeweza kumfanya mdaiwa sugu akalipe deni lake, na mkwepa kodi ajipeleke mwenyewe tra.
Jina lake lilisanifu uzuri wake toka lini mtu akaitwa Leyra akawa mmbaya?, ubaya, umbea na ubondia ulikua na majina yake, majina kama Chausiku, Kurusumu, Mwantumu, Asha ngedere, Mwajuma ndala ndefu, chakubimbi na kuendelea.
Sauti yake ilikua tamu kama sauti za vinubi, kama angelikua mwanakwaya nadhani watu wote wangemrudia Mungu mapema maana wasingechoka kumsikiliza.

Nikisema niiongelee sura yake iliyobarikiwa uso mwembamba, pua ndefu, midomo miekundu, macho makubwa ya duara, ngozi nyeupe isiyokua na kovu wala chunusi hata moja bila kusahau nywele zake ndefu alizozifunga kwa nyuma nahisi unaweza ukameza simu yako nikisema niongeze na umbo lake namba nane unaweza ukameza na chaja pia.
Unashindwaje kumpenda mtoto kama huyu labda uwe umelogwa na wachawi wakuu wa kijiji.

Kwa kua sikua nimelogwa, nilijikuta nimekufa na kuoza kwa Leyra, nilimuwaza kila sekunde iendayo kwa Mungu, muda wote moyo wangu uliyalaumu macho yangu kwa kuchelewa kumuona tokea siku ya kwanza tulipowasili hapo chuoni.
Muda mwingi macho yangu yalikua yakitua juu uso wake ni kama yalivutwa na sumaku. Kwenye mawazo yangu nilimvua nguo zote na kulala nae, nilimkunja aina zote nilizozitaka, kama ingekua ni kweli basi naamini ni lazima angelazwa hospitali kwa uchovu au majirani wangekuja kuamua maana kwa uzuri wake hata mwanaume mwenye kibamia angejitutumua kuweka heshima.

Wapo wasichana waliotamani wangekua wanaume ili waufaidi uzuri wake lakini kwa bahati mbaya haikuwezekana.
Lakini pamoja na uzuri wote aliokua nao, Leyra hakua kama wasichana wa uswahilini unakuta msichana sura ngumu kama mkasi wa kupunguzia maua lakini anaringa utasema hatoi kitu cha ushuzi au hakati gogo.
Leyra alikua mtu wa watu kwao walikua matajiri wakubwa lakini hakuchagua marafiki, alicheka na kila mtu si masikini si tajiri kwake watu wote walikua sawa. Tofauti na tabia za kina Cheusi mangala ambao wakipewa tu uzuri inakua kosa.
Leyra kwake ilikua tofauti alijiheshimu kupita kiasi, hakua mtu wa wanaume hata kidogo japo wapo wengi wenye pesa zao waliomtaka lakini wote waliambulia hewa, hewa ambayo huenda ingetosha kujaza mipira yote toka ligi kuu ya Uingereza tokea ikiwa inaanza hadi inaisha kwa muda wa miezi nane.

Sikua nikichoka kumuangalia Leyra nilisikia raha kufanya hivyo, alinishtukia aligundua kua nilikua nikimuangalia sana lakini hakunizuia. Kila mara macho yetu yalikua yakigongana lakini hakunisemesha neno aliishia kutabasamu bila kukasirika jambo lililofanya nizidi kumpenda siku hadi siku.
Kadri siku zilivyosonga mbele ndivyo nilivyozidi kumpenda sikujali tena maneno ya baba yangu wala ratiba yangu ya masomo.
Muda mwingi niliutumia kuuwaza uzuri wake jambo ambalo nilishindwa kujizuia kabisa, kwani kila nilipojaribu kujizuia ni kana kwamba nilikua nikijiumiza mwenyewe.

Hali hii ilidumu kwa muda miezi kadhaa hatimaye kama upepo taarifa zilizagaa kila kona, kila mtu chuoni alijua kua nilikua nikimpenda Leyra hata yeye mwenyewe alijua hilo kwa sababu kila mtu alisema tunapendezana kama tungekua pamoja.

Je nitafanikiwa kua na mtoto Leyra?
Tukutane alhamisi.

...Itaendelea. ..
 
Back
Top Bottom