Waziri mkuu alipokuwa kwenye ziara ya kikazi mkoani Tabora aliwashauri wakulima wa mkoa huo kuanza kulima zao la korosho kwani hali ya hewa na tafiti zilizofanywa zinaonyesha zao hilo linastawi vizuri katika eneo hilo. Hali ya hewa ya Tabora, Shinyanga, Singida na Mwanza zinafanana hivyo unaweza kuwasiliana na bodi ya korosho au kituo cha utafiti cha Naliendele kuomba kupatiwa mbegu ambazo wanagawa bure kwa wakulima.