toghocho
JF-Expert Member
- Mar 16, 2011
- 1,172
- 198
jamani nina tatizo ambalo mwanzo sikuliona kubwa, lakini sasa naanzza kuji doubt, mwanzoni mwa february mwaka huu nilianza kusikia kooni kwangu kama kuna kitu kimekwama, nikajua kawaida labda msosi, baadae kikawa kama kinakua hivi yaani naanza kusikia kooni karia pote pamekabwa, nikaenda hospitali, dokta akanambia ni minyoo akanipa dawa za minyoo nikatumia,nikapata nafuu au tuseme nikawa sisikii tena kitu chochote kooni, baada kama ya wiki tatu, tatizo likajirudia, nikajua minyoo tena, nikanunua dawa nikameza, baadae nikapata nafuu kama wiki mbili, likaanza tena nikaenda hospitali tena april(mwezi wa nne) . nikamwelezea daktari(ambaye alikuwa mwingine sio yule wa kwanza) maelezo yote ikiwemo dawa nilizotumia na jinsi zilivyonisaidia kwa muda, akanambia tatizo langu sio minyoo, akasema ni kuchafuka kwa njia ya hewa, akaniandikia dawa kama sikosei zinaitwa broadcloax nikazitumia zikaisha nikaanza kujisikia nafuu baadae tatizo hilo likapotea, wakati nikijua limeisha miezi kama miwili baadae, kwenye wiki iliyopita nikaanza kujisikia tena tatizo hilohilo, leo nimeenda hospitali tena(ileile ya siku zote) dokta baada ya kusoma historia ya mgonjwa(patient history) eti anashangaa, mbona hilo tatizo (lako) linakuruduarudi? asa mi ntajuaje jamani si ndio maana niko hapa?
wamenipa dawa tena, safari hii ni ampicilin na nyingine za minyoo, sasa najiuliza nina tatizo gani hasa? na nini ufumbuzi (solution) yake ya kudumu, maana inaonekana hospitali wanabahatisha na wananipa dawa za kupoza tu, sio kutibu... msaada wadau tafadhali maana hata raha sina nasikia kitu kimekwama natamani ningekimeza..yaani...wakati mwingine najisikia maumivu yaani kama nimekabwa...nisaidieni
wamenipa dawa tena, safari hii ni ampicilin na nyingine za minyoo, sasa najiuliza nina tatizo gani hasa? na nini ufumbuzi (solution) yake ya kudumu, maana inaonekana hospitali wanabahatisha na wananipa dawa za kupoza tu, sio kutibu... msaada wadau tafadhali maana hata raha sina nasikia kitu kimekwama natamani ningekimeza..yaani...wakati mwingine najisikia maumivu yaani kama nimekabwa...nisaidieni