Kongamano la Pili la Katiba: Jumamosi, 02 Aprili 2011

Kitila Mkumbo

JF-Expert Member
Feb 25, 2006
3,354
1,943
Jumuiya ya Wanataaluma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA) imeandaa Kongamano la Pili la Katiba litakalofanyika katika ukumbi wa Nkrumah Chuo Kikuu cha Dar es Salaam siku ya Jumamosi, tarehe 02 Aprili 2011 kuanzia saa 4 asubuhi. Mada kuu katika kongamano hili ni: Maudhui na Misingi ya Katiba Mpya.
Tangu Kongamano la Kwanza la Katiba lilipofanyika tarehe 15 Januari 2011, ambalo lilijadili kwa kina haja na mchakato wa Katiba Mpya, maendeleo mbalimbali yamepatikana kuelekea hatua za kupata Katiba Mpya, ikiwemo Serikali kukiri kwa dhati juu ya umuhimu na haja ya kuwa na Katiba Mpya. Aidha, Serikali imeshaandaa Mswada Maalumu wa Sheria unaopendekeza kutungwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Nchi.
Kwa hivyo basi, kwa kiasi cha kutosha, mjadala juu ya haja na mchakato wa Katiba Mpya unaelekea kuitimishwa baada ya kuwa kila mtanzania mwenye uzalendo na mapenzi mema kwa nchi yetu kutambua umuhimu na haja hiyo. Hata hivyo, swala la maudhui na misingi ya Katiba Mpya limebaki kuwa tata. Kwa sababu hii, Kongamano hili la pili litajikita katika kuanisha na kutoa fursa kwa washiriki kutoa maoni yao juu ya maudhui na misingi ambayo wanafikiri ni muhimu ikazingatiwa katika Katiba Mpya.

Kwa kuwa Serikali imetoa Mswada maalumu wa Katiba wenye kulenga kutunga sheria itakayotoa mwongozi wa kufikiwa kwa Katiba Mpya, Kongamano hili pia litaupitia na kuujadili kwa kina Mswada huu.
Katika kufikia lengo hili, UDASA imewaomba na wamekubali wananchi wawili waliobobea na wenye uzoefu wa muda mrefu katika mambo ya sheria na siasa za katiba. Wananchi hawa ni Jaji Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Barnabas Samata na Ndugu Francis Kiwanga ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu. Mbali na watoa mada hawa wakuu, vyama vya siasa vyenye uwakilishi bungeni vitapatiwa dakika 10 kwa ajili ya kutoa maoni ya vyama vyao kuhusu mada hii. Aidha, tumemuomba Ndugu Onesmo Kyauke, Mhadhiri Mwandamizi katika Shule Kuu ya Sheria Chuo Kikuu cha DSM, kuzungumiza juu ya Mswada Maalumu wa Sheria kuhusu Katiba Mpya ya Nchi.
Tunarajia kuwa kongamano hili litatoa mwongozo kuhusu maudhui na misingi inayofaa kuwamo katika Katiba Mpya ili Katiba hiyo iwe na tija pana na endelevu katika ujenzi wa demokrasia hapa nchini na mustakabali mpya wa Taifa letu. Aidha, Kongamano hili litatoa fursa kwa wananchi kutoa maoni yao kuhusu Mswada Maalumu yatakayowasaidia wabunge kuneemesha michango yao katika kuboresha mswada huo kabla haujawa sheria kamili.
Kwa taarifa zaidi kuhusu Kongamano hili, tafadhali tuwasiliane kwa simu 0754 301 908 au email kitilam@udsm.ac.tz
Wananchi wote wanaalikwa kuhudhuria kongamano hili.

Dk Kitila Mkumbo
Makamu Mwenyekiti wa UDASA na Mratibu wa Kongamano

 
Shukrani. Natumaini litaendeliea kuwafungulia watanzania mwanga kuhusu katiba. Ningependa watakaopata nafasi ya kuchangia wasisitize umuhimu wa kusoma katiba iliyopo ili kubaini mapungufu yake.

Ni watanzania wachache sana walioisoma hii iliyopo.
 
Niseme jambo moja.
Kwenye Katiba ya sasa kuna baadhi ya vipengele ambavyo vizuri sana(havipaswi kubadilika) Je mbona wachangiaji hawavisemi.
 
Hivi UdaSa haina Katibu? Au Mwenyekiti ? Naona makamu ndio Yuko busy kuliko wengine maana ndio anatoa mialiko si ajabu ndiye atakuwa Mwenyekiti Wa kongamano nijuze wenzangu
 
Hongera sana UDASA kwa jitihada zenu zenye kuwa na tija elekezi na chanya!

Ni zamu ya vyuo vikuu pamoja na taasisi nyingine kanda ya kaskazini kuchukua hatua na kuitisha makongamano yatakayotakiwa kujadili hal ya kisiasa kwa kuzingatia mstakabal wa mwananchi juu ya maendeleo ya nchi yake zaid tukitupia jicho pevu juu ya katiba mpya!

Tusaidieni ili nasi pia wadau na wachangiaji juu ya katiba tulioko huku kanda ya kaskazini hasa Arusha tupate sehem ya kutoa mawazo yetu!
 
Nawapongeza saana UDASA kwa juhudi zenu za kuwaelimisha wananchi kuhusu katiba, je midahalo hiyo itakuwa inafanyika dar tu? Na sisi wa mikoani tutapata lini fursa ya kuchangia mawazo yetu? Coz na sisi tuna vya kwetu tunataka kuexpress kama la kuzunguka mikoani halitawezekana ningeshauri mtafute njia ya wale tulio mbali kuparticipate labda kwa njia ya simu au internet ili na sisi views zetu kuhusu katiba zijadliwe na wadau ni hayo tu akhasanteni.

Jah Bless
 
Dr.Mkumbo tunashukuru kwa taarifa yako. Aidha naomba utusaidie sisi ambao tulikuwa nje ya dar kupata nakala vcd/dvd ya komgamano la kwanza.

Ingekuwa vema mkawa na utaratibu wa kunakili na kutuuzia nakala za makongamano haya hasa sisi ambao kwa namna yoyote tunashindwa kujumuika kwa sababu mbalimbali ikiwemo ya kikazi nje ya dar. Mfano, tar.20 Januari nilimwagiza mwanafunzi wa sheria hapo chuoni mwenu aweze kunipatia nakala ya kongamano la kwanza ila aliishia kupata ahadi kwa wahusika, mara subiri,mara nenda faculty fulani mpaka nkaondoka dar tena sikuipata.

Nategemea kwa kongamano la pili ambalo ntajumuika, tutaweza kuuziwa/kupata nakala za kongamano la kwanza ili tuweze kuweka kumbukumbu za rejea zikae sawa.

Mwisho, nakushukuru tena na UDASA kwa ujumla kwa uzalendo ila kwa taarifa ya serikali ya kupanga kuwapa watanzania katiba mpya mwaka 2014 nauona kama mchezo mchafu. Kama hatua za kuiandika katiba mpya hazijaanza,iweje ujue ugumu wa kuwa nayo hadi ifike 2014. Kwa iyo hata kama katiba ikikamilika january2013 wataiweka kapuni mpaka 2014? Au wanataka uchaguzi mwingine ufike ufanyike kwa mizengwe?na je ikifika 2014 haijakamilika wataanza kuitumia ivo ivo?au kalenda tena? Hapana. Hapa mchakato uanze ndn tutajua itakamilika lini na si kuanza kupanga tarehe.

Nawatakia wikendi njema watanzania wote. Gsana.
 
Gsana: Tuna DVD za kongamano la kwanza. Zinauzwa sh 10,000/=. Mwagizie kijana wako anione au aende ofisi ya PRO pale utawala (UDSM) atapatiwa. Ahsante.
 
Ili kuwahimiza vyama vya siasa kushiriki,jaribu kuwaandikia barua kuwataka waandae hoja zao waje kuwasilisha siku hiyo ili kujenga mazingira shirikishi kwa political actors ,pia serikali kupitia kongamano hilo ipate salaam kuwa wananchi wangependa KATIBA MPYA ipatikane mapema ili wananchi wawe na muda mpana zaidi wa kujipanga katika kuitekeleza kabla ya uchaguzi mkuu 2015 maana itabadilisha maisha yetu kisiasa,kiuchumi,kijamii,n.k.

Vile vile NGOs zenye nguvu zipeni fursa maalum zitoe hoja zao ili finally kuwe na strong solidarity kwa wadau mbalimbali katika nchi yetu maana suala la katiba sio suala la vikundi vidogo vidogo, linahitaji nguvu ya pamoja kwa maslahi makubwa zaidi ya Watanzania na sio siasa na wanasiasa pekee.

Kazi njema Dr.kitila Mkumbo na timu yako yote katika hili,mwisho mjiepushe na ushabiki wa kisiasa usio wa lazima ili kulinda professionalism na heshima ya UDSM as a great university katika Dunia hii.

Mussa Mnyeti,
Mdau.
 
TANESCO wamekwisha chakachua umeme huku kwetu.......

Tafadhali mnaoipata live tujuzeni hapa jamvini.
 
Naona DK Slaa yupo pamoja na PROF Safari wakiwa ndani ya gwanda, jaji mstaafu Samatta nadhani ndie mmoja ya wazungumzaji wakuu.
 
Wawakilishi wa vyama
1.CHADEMA-Dr.Wilbroad Peter Slaa, Freeman Mbowe na Mabere Marando
3.NCCR-Dr.Mvungi
2.CCM-Prince Bagenda
 
Eti Bagenda ndie mwakilishi wa ccm, wapi Makamba na wengine!
 
Back
Top Bottom