Kongamano la kujadili hali ya siasa nchini kufanyika Mwanza

Izack Mwanahapa

JF-Expert Member
Apr 21, 2011
497
236
Taasisi ya Jitambue Foundation inawakaribusha kwenye kongamano la wazi la kujadili hali ya siasa nchini kuelekea 2015. Kongamano hili litafanyika Alhamisi Tarehe 05/12/2013 kuanzia saa 3 kamili asubuhi katika ukumbi wa Mwanza Hotel. Kongamano hili litahusisha Wanaharakati, Viongozi na wananchi wote kwa ujumla. Mada kuu itakuwa ” Kuelekea 2015, migogoro ndani ya vyama vya siasa je, ninajenga demokrasia?” Hakutakuwa na kiingilio wote mnakaribishwa.
Malengo ya Kongamano


1. Kutoa fursa kwa wananchi wa kawaida kutoa maoni yao kuhusu hali ya siasa nchini
2. Kutafakari nafasi ya wananchi katika utatuzi wa migogoro ya vyama
3. Kutoa fursa ya wananchi kujielimisha na kubadilishana mawazo.

WOTE MNAKARIBISHWA
 
Back
Top Bottom