Tutalumbana weee humu JF na kwenye majukwaa ya kisiasa,lakini ukweli ni kwamba sheria ilishapita bungeni,imesainiwa na Rais huyuhuyu ambaye naye amengia katika orodha ya walalamikaji kama mimi na wewe....(USANII MTUPU) na imeshaanza kutekelezwa!!
Na jamaa hawa CCM ndani ya miezi miwili tu (Julai & Agosti) watakuwa wameingiza Bil 56!!....Na kama ni kweli wanatafuta fedha za kugharamia kampeni za uchaguzi mkuu wa 2015 ktk chama chao,basi watakuwa wamefanikiwa kwa kiwango flani na kama kweli wamedhamiria kuifuta,basi itakuwa kuanzia mwezi Septemba baada ya bunge kukaa kuanzia mwishoni mwa mwezi wa 8!!
ON CONTRARY TO THAT; na nionavyo mimi ni kuwa tatizo si watu kulipa kodi hii na zingine zozote zile zinazoaanzishwa na serikali, ila tatizo liko kwenye pesa tunazolipa katika kodi hizo zinafanya kazi gani( And please don't tell me kuwa tumejenga barabara za rami kilometa 8000 nchi nzima au tumejenga shule za sekondari za kata na nyimbo zingine zinazofanana na hizo mnazoziimba kila siku kuwadaa wachache wanaofikiri kwa makario kwani haya mliyofanya CCM hayalingani na umri wenu wa kushika dola wa miaka zaidi ya 50 sasa!!)....Mpaka sasa tulitakiwa tuwe na barabara za rami za zaidi ya kilometa 30,000 na kila shule kila mwanafunzi kitabu kimoja,dawati lake,laptop moja,walimu wa kutosha,maabara za sayansi katka sekondari zetu,madawa ya kutosha katk zahanati na vituo vyetu vya afya na pasipokuwapo na mtumishi wa umma eti anayeidai serikali ya CCM iliyo madarakani kwa miaka zaidi ya 50 hela ya uhamisho,malimbikizo ya mishahara nk nk. Ni upuuzi na ni kukosa kujenga mifumo imara na thabiti and THIS IS A TOTAL FAILURE!!
Kwani pamoja na makusanyo makubwa ya kodi toka TRA yanayokimbilia bil. 800 kwa mwezi, bado hali za wananchi ni mbaya na umaskini unaongezeka badala ya kupungua; angalia na tembelea barabara za vijijini hazipitiki,mashule hayana vifaa vya kujifunzia na kufundishia,mashule hayana maabara,watumishi wa serikali (rejea madai ya walimu,madaktari,manesi nk nk) wanadai madeni ya miaka na miaka, zahanati,hospitali na vituo vya afya havina madawa na vifaa tiba na vitendea kazi vingine, miradi mingi ya maendeleo ina miaka imesimama kwa sababu eti serikali haina pesa!!......Hiki Bwana Nape ndicho kinachogomba na ndicho kinachowafanya CCM ionekane ovyo. Tatizo lenu kuu liko kwenye SERA na MIPANGO yenu na namna yaani MIFUMO mnayotumia kutekeleza mipango yenu ni ya hovyo na iko SO CORRUPTED na huu UFISADI umeshafikia ktk kiwango kibaya kiasi cha sasa damu ya binadamu zinamwagika kama sacrifice ya kuendelea ku-survive kwa mafisadi (rejea tukio la bomu la Soweto - Arusha ktk mkutano wa CHADEMA).
Kwa sasa dawa yake si ninyi kujirekebisha bali kulazimishwa kujirekekisha kwa KUONDOKA madarakani na kuwaachia wengine wenye mawazo mapya nao TUWAJARIBU!!...Kwani ilivyo sasa ni kuwa kuanzia IKULU ya JAKAYA KIKWETE(rejea kashfa ya kamuni hewa ya kufua umeme kama mfano ulio wazi ya Richmond) hadi ofisi ya kitongoji cha kijiji ni RUSHWA na UFISADI mtupu. Ni wazi katika hali kama hii, serikali lazima ipate taabu sana kuweka mipango yake na kuungwa mkono na wananchi bila kulalamika kwani HAIAMINIKI!!....Ona mnavopingana ninyi kwa ninyi katk suala hili la sim card tax na bado mengi mengine yatakuja na kila mtu ktk CCM na serikali yenu atakuwa anaruka ki-manga!!
To me, bwana Nape, hii ndiyo problem yangu na pengine hii ndiyo problem ya kila mtu anayepinga kodi hizi za ajabu ajabu na ni mara mia mngetafutia fedha hizi kwenye maeneo mengine kama migodi ya madini,mafuta na gesi yaliyojificha ambako hayagusi maisha ya kila siku ya watu moja kwa moja