Kodi ya ongezeko la thamani (VAT)

Mwenekaya Nkulu

Senior Member
Jul 16, 2014
142
169
Habari ya leo waungwana, naomba mwenye uelewa juu ya kitu kinachoitwa kodi ya ongezeko la thamani almaarufu VAT, ni kodi inayopaswa kulipwa na nani na kwa utaratibu upi, pia naomba kujulishwa ni biashara ya ukubwa gani ambayo mmiliki wake anapaswa kuwa na namba ya usajili ya VAT yaani VRN, kwa waelewa tafadhali naomba msaada wenu katika hilo na lolote lile ambalo linahusisha tozo za kodi, wasalaam.
 
Kodi ya ongezeko la thamani yaani VAT hutozwa kwa walaji kwa kuongeza 18% kwenye bei za bidhaa au huduma. Kodi hii hukusanywa na muuza bidhaa au mtoa huduma na hupelekwa TRA baada ya kuondoa kodi aliyolipa muuza bidhaa au mtoa huduma.

Mfanyabiashara yoyote mwenye mauzo yanazidi TZS 100 million kwa mwaka au TZS 25 million kwa miezi mitatu anatakiwa kujiandikisha na kodi hii, kutokufanya hivyo ni kosa kwa mujibu wa sheria ya VAT.

Kwa elimu na ushauri zaidi tuma email vabusiness@habari.co.tz au tembelea website yetu www.vabusiness.co.tz
 
Kodi ya ongezeko la thamani yaani VAT hutozwa kwa walaji kwa kuongeza 18% kwenye bei za bidhaa au huduma. Kodi hii hukusanywa na muuza bidhaa au mtoa huduma na hupelekwa TRA baada ya kuondoa kodi aliyolipa muuza bidhaa au mtoa huduma.

Mfanyabiashara yoyote mwenye mauzo yanazidi TZS 100 million kwa mwaka au TZS 25 million kwa miezi mitatu anatakiwa kujiandikisha na kodi hii, kutokufanya hivyo ni kosa kwa mujibu wa sheria ya VAT.

Kwa elimu na ushauri zaidi tuma email vabusiness@habari.co.tz au tembelea website yetu www.vabusiness.co.tz
Asante sana kwa maelezo mazuri na yaliyojitosheleza mkuu.
 
Back
Top Bottom