Kodi mpya

Kodi mpya

lusitu

Member
Joined
Jul 29, 2015
Posts
43
Reaction score
10
Wakuu nimeangalia kwenye kikokotozi cha TRA kinachohusu kodi za magari, nimekutana na kodi ya Custom processing fees, na Railway Dev.levy ambazo zinatozwa tofauti kulingangana na aina ya Gari.

Kodi hizi hapo kabla hazikuwapo naomba kufahamishwa wale wajuzi wa masuala ya kodi. Utaratibu upi unaotakiwa kufuatwa katika uanzishwaji wa kodi mpya?

Je wadau hatupaswi kufahamishwa, uwepo wa kodi hizi tayari utaaribu bajeti za wadau ambao wamekwishaagiza magari yao .

Naomba msaada tafadhali.
 
Wakuu nimeangalia kwenye kikokotozi cha Tra kinachohusu kodi za magari,nimekutana na kodi ya Custom processing fees, na Railway Dev.levy ambazo zinatozwa tofauti kulingangana na aina ya Gari,Kodi hizi hapo kabla hazikuwapo naomba kufahamishwa wale wajuzi wa masuala ya kodi.Utaratibu upi unaotakiwa kufuatwa katika uanzishwaji wa kodi mpya? Je wadau hatupaswi kufahamishwa, uwepo wa kodi hizi tayari utaaribu bajeti za wadau ambao wamekwishaagiza magari yao . Naomba msaada tafadhali.

Kabla ya kupitishwa, kodi na tozo hujadiliwa bungeni, hizo kodi za kuchangia ujenzi wa reli mbona zipo tangu mwaka huu wa fedha uanze (July)!
 
Customs Processing fees na railway Development levy zipo tangu mwaka huu wa fedha yaani kuanzia Julai 2015 hadi June 2016 hivyo sio kodi mpya mkuu kilichofanyika kwenye calculator zilikuwa hazionekani ila baada ya kufanya maboresho kwenye calculator ndio sasa zinaoneka mkuu

Kwa maelezo ya ziada wapigie TRA
kwa namba

Simu za Bure

0800 750 075 (Vodacom)
0800 780 078 (Airtel)
0713 800 333 (Tigo)
 
Shukrani kwa ufafanuzi maana kwangu zilikuwa zinaonekana kama mpya.
 
Back
Top Bottom