Kocha wa Taifa Star si lolote wala chochote!

Kocha wa Taifa Star si lolote wala chochote!

Tango73

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2008
Posts
2,227
Reaction score
1,362
Huyu kocha kafundisha mpira msumbiji na ethiopia ambako hajaleta mafanikio yeyote iwe kwa timu ya taifa wala vilabu alivyofundisha. Ni moja makocha wababaishaji ambao bara hili halijaoona mfano wake.

TFF ni hovyo kupindukia. Yaani wao wanategemea kocha mbovu na kamati ya saidia taifa star ishinde ndivyo nigezo vya kutuwezesha timu yetu ikacheze Afcon mjini moroco mwakani. hawa TFF walipeleka kesi ya kufuta uchaguzi wa TFF mpaka huko Zurish na sisi tulitegemea makubwa wakipata uongozi. Lakini kumbe TFF nao ndio wabovu na wachovu kupindukia.

wananchi lazima tususie kuishangilia Tifa stars ikiwa inacheza mpaka tuletewe kocha wa maana kama vile napomniac aliyeipeleka robo fainali cameroo world cup mwaka 1996.
Ubovu wetu sisi watanzani tunangojea mpaka kocha ashindwe kazi na tumetolewa kuingia ligi ya afcon mwakani huko moroco, ndipo tutaanza kulalamika.

wakati wa kulalamika ndio huu na sio mwingine. halafu utagundua kuwa TFF imeficha hata kutuelezea backgraund za kocha huyu na mafanikio yake.

Hivi sasa hivi mashabiki wa timu wa Gremio hawaendi uwanjani kuishangilia timu yao mpaka ibadili kocha na icheze vizuri. Je sisi tunangoja nn kuiadabisha TFF?
 
Maximo pekee ndio kocha angalau alikuwa anaweka nchi kwenye chati, wte wanaokuja ni uozo tu, tangu aondoke Maximo tafa stars ndio inazidi kurudi nyuma
 
taifa strs imeishatolewa kucheza fainali za Afcon huko moroco baada ya kuajili kocha bomu kupindukia. Huu ni ukweli kabisa na wala tusilogwe kuweka matumaini ya kitoto eti kamati ya saidia taifa stars itatusaidia. tususie mechi za taifa kama vile timu ya gremio ya daraja la kwanza brazil inavyolizwa na mashabiki wake.
 
Niloposoma cv yake nilishangaa sana, ila uongozi huu umefanya mambo mengi kinyume na matarajio ya wengi ukiachilia mbali kujaza nafasi za watendaji wake
 
sasa hilo nyeti na la ukweli umeliona wewe, je mtu kama malinzi kiongozi wa TFF kwa nn asilione na kulilekebisha mapema? hapo ndipo utagundua kuwa watanzania hatujui nn maana ya kupiga hatua ya kimaendeleo.
 
Shida matumizi mabaya kura tujilaumu wenyewe ndo tumewapa kura
 
Mnamsingizia kocha hakuna timu inaofanya vizuri bila kuwa na maandalizi kwa ngazi ya chini.

Hii mijitu inayofundishwa sasa ishakomaa na wao malengo yao ni kuchezea simba na yanga tu.

Ata mumlete kosha toka brazil au england kama hatutoendeleza soka la watoto na vijana ni kazi bure ni sawa na kujenga msingi mbovu na kupandisha matofali mabovu harafu finishing ndio ukapiga vizuri
 
Mleta mada utakua unasumbuliwa na homa ya degue...!!?umeandika mambo mengi ila yote pumba tupu...hivi hao makocha waliopita wameleta mabadiliko yapi.?umesahau kua mpira aujifunzi ukubwani tanzania hatuna mfumo mzuri wa kupata vijana ktka glass roots hata mgemleta van gaal hakuna kitachbadilika..kma. ni lawama zipeleke kwa viongoz waliomtamgulia malinzi walioshindwa kuweka mfumo nzur kwa vijana tatizo lako unafananisha kocha anaefundisha timu ya taifa na yule anaefundisha club..hawa ni watu tofauti,kimbinu na kimfumo hata ungefanyaje gootball inafunzwa udogoni na si ukubwani kma mnavofamya hapa bongo..
 
Kigezo kimojawapo cha kocha mzuri ni kuwindwa na timu nyingine, hata kama alimaliza vibaya au kufukuzwa huko alikotoka. Akina Macini, scolari, Mourinho, Van Gaal, Rijkaard, AVB na wengine ni mifano michache. Kigezo chengine kikuu ni mafanikio. Kwa huyu wa Taifa Stars, TFF imevutiwa na kuiwezesha Msumbiji, nchi isiyopishana sana na sisi kwa viwango na vipaji, kucheza AFCON. Sina hakika iwapo ni kocha mzuri ama la. Wasiwasi wangu ni huku kuhamishia sera za UKAWA mpirani!
 
Tatizo si kocha bali ni wachezaji kuwa hawakidhi viwango vya mashindano.

Tungefanya maandalizi yasiyojawa na propaganda na wizi wa pesa,tukaweka uzalendo tungeweza kuwa na timu bora.
 
Huyu kocha kafundisha mpira msumbiji na ethiopia ambako hajaleta mafanikio yeyote iwe kwa timu ya taifa wala vilabu alivyofundisha. Ni moja makocha wababaishaji ambao bara hili halijaoona mfano wake.

TFF ni hovyo kupindukia. Yaani wao wanategemea kocha mbovu na kamati ya saidia taifa star ishinde ndivyo nigezo vya kutuwezesha timu yetu ikacheze Afcon mjini moroco mwakani. hawa TFF walipeleka kesi ya kufuta uchaguzi wa TFF mpaka huko Zurish na sisi tulitegemea makubwa wakipata uongozi. Lakini kumbe TFF nao ndio wabovu na wachovu kupindukia.

wananchi lazima tususie kuishangilia Tifa stars ikiwa inacheza mpaka tuletewe kocha wa maana kama vile napomniac aliyeipeleka robo fainali cameroo world cup mwaka 1996.
Ubovu wetu sisi watanzani tunangojea mpaka kocha ashindwe kazi na tumetolewa kuingia ligi ya afcon mwakani huko moroco, ndipo tutaanza kulalamika.

wakati wa kulalamika ndio huu na sio mwingine. halafu utagundua kuwa TFF imeficha hata kutuelezea backgraund za kocha huyu na mafanikio yake.

Hivi sasa hivi mashabiki wa timu wa Gremio hawaendi uwanjani kuishangilia timu yao mpaka ibadili kocha na icheze vizuri. Je sisi tunangoja nn kuiadabisha TFF?
Tango 73 Mwalimu Nooij aliipeleka Msumbiji fainali za Africa zilizofanyika Angola,it is not a small feat kwa mpira wetu wa Africa.
katika kukuza mpira yapo ya kufanywa na kocha na yapo ya kufanywa na Federation.Timu ya Taifa ni finished good,misingi lazima iwekwe ya kuibua ,kuendeleza na kukuza vipaji.Kizuri gharama,grassroot na youth development ni gharama kubwa sana ,waliowekeza kina Misri,Ghana ,Nigeria ambao waliliona hili miaka mingi iliyopita sasa hivi kila msimu wanavuna,wanashinda vikombe vya dunia kuanzia umri chini ya miaka 17 na kama sio kushinda wanashiriki fainali.Tujiulize watanzania tumewekeza kiasi gani katika mpira wa awali ( grassroot) na wa vijana? Au tunataka tukusanye pale ambapo hatujatawanya. Ndio maana TFF sasa hivi inaandaa mkakati wa Taifa wa maendeleo ya mpira wa vijana na bajeti yake na ushauri tutakavyoweza kupata hizo fedha kila mwaka.Tukijaliwa mkakati huu utazinduliwa rasmi mwezi oktoba,huu mkakati utatoavdira na kueleza kina Tango73 nao watashiriki vipi katika programu hii.
 
Wenzenu walimpata kocha mzuri Brazil naona tukumbuke kuwa asali aichovwi mara moja. Kwa Brazil tulichovya asali. inakuaje sie twachovya mara moja? hivyo haitokuwa vibaya kumtafuta maximo tena iwe kumtaka arud yeye au asaidie kumpata kocha mwingine mwenye falsafa kama zake
 
sasa hilo nyeti na la ukweli umeliona wewe, je mtu kama malinzi kiongozi wa TFF kwa nn asilione na kulilekebisha mapema? hapo ndipo utagundua kuwa watanzania hatujui nn maana ya kupiga hatua ya kimaendeleo.

taifa stars 0 vs burundi 3 nation stdium
ngorongoro heroes 0 vs nigeria 2 nation stadium
movie linaendelea................
 
Watu wengi wanashindwa kuelewa kwmba tatizo la timu ya taifa stars siyo kocha ni wachezaji hawajitambui na pia mifumo yetu ya kupata wachezaji pia ni shida ligi mbovu wachezaji wetu hawatak exposure kwenda kucheza nje wameng'angania kucheza simba na yanga hta wakipelekwa nje huwa wanarudi na visingizio kbao kwa style hii hta tukileta kocha mwenye mafanikio vp hatuwez kufanikiwa
 
Bila kuwekeza kuwa na mashindano bora kwa kila ligi..........Timu imara kila kila ngazi.......timu ya taifa ni matokeo ya mwisho kabisa.......Unahitajika mkakati wa kuziwezesha Club zetu kifedha......si kwa mkataba wa Vodacom tu bali taasisi nyingi ziwekeze kwenye mpira tena si uwekezaji wa kugawa jezi na mipira........Ushindani wa zamani ulichangiwa na ushiriki wa taasisi za umma kama Bandari,Pamba,Reli,Ndovu,Ushirika,Sigara,Kurugenzi n.k ......sasa tunahitaji watu wenye fedha waweke pesa kwenye soka kwa ushawishi wa uwezekano wa faida.....AZAM anaweza kuwa mfano bora....lakini si vibaya tukatumia case study za matajiri wa mataifa mengine hasa hapa hapa Afrika wenye timu zenye mafaniko makubwa kama TP Mazembe kushawishi makampuni binafsi kama Vodacom kuwa na timu rasmi........utengenezwe mfumo rahisi kuingia kwenye mashindano kuongeza ushindani ili pia return za wawekezaji hawa zisiwe in a very long term........
 
Maximo pekee ndio kocha angalau alikuwa anaweka nchi kwenye chati, wte wanaokuja ni uozo tu, tangu aondoke Maximo tafa stars ndio inazidi kurudi nyuma

No, Kim ndie kocha. Maksimo alikuja kipindi cha neema, kilichoifanya Stars iwe juu ni sapoti kubwa ya Serikali na sio kocha yule. Kama ana huo ubora unaodai sasa hivi anafundisha timu gani, na mafanikio yake yakoje huko?
 
No, Kim ndie kocha. Maksimo alikuja kipindi cha neema, kilichoifanya Stars iwe juu ni sapoti kubwa ya Serikali na sio kocha yule. Kama ana huo ubora unaodai sasa hivi anafundisha timu gani, na mafanikio yake yakoje huko?

mtabaki kutambiana lkn ukwel mnaujua lkn hamtak kuuweka wazi mfumo ndyo tatizo simba na yanga klabu kongwe zaid hpa nchini lkn hawana academy za kukuza vipaji vya wachezaji kila cku wanapigana vikumbo kugombea wachezaji wazee
 
Matatizo ni mengi poti na ulilotaja pia lipo., hapa huyu alikuwa amesema ubora wa kocha Maksimo na mimi nikawa naumeleza kwanini yule sio bora. Hao Simba na Yanga wasio na akademi tunaweza kufanya yetu bila hata kuwahusisha lakini shida ni nani amfunge paka kengele ikiwa walio TFF karibu wote ni mazao ya hizi timu mbili.
mtabaki kutambiana lkn ukwel mnaujua lkn hamtak kuuweka wazi mfumo ndyo tatizo simba na yanga klabu kongwe zaid hpa nchini lkn hawana academy za kukuza vipaji vya wachezaji kila cku wanapigana vikumbo kugombea wachezaji wazee
 
Taifa stars n janga la kitaifa sana maana hakuna la maana anzia jezi mpaka mpira wanaocheza n sifuri tuu,hakuna la kueleweka zaidi ya porojo za tff tuu sioni lolote lile la mpira kuchezwa zaidi ya maneno hakuna jipya,
Tff haya maboresho yenu mungeyaleta mda mwafaka lakini c sasa mnatufanya tuanze kufikiria kuisusia hii timu yenu.
 
Back
Top Bottom