Basi miongoni mwa tahadhari na wafunge Kanisa lao ili waumini wao wasiambukizwe na mikusanyiko.
Ha ha ha haa! Nimejikuta nacheka bila kutarajia.
====
Herd immunity inaonekana ni moja ya muarobaini wa covid, na kuna uwezekano mkubwa Mungu alitulinda kwa njia hiyo mwaka jana. Kwa kuwa wanasema kirusi kimejibadili, basi na sisi tubadili mbinu yetu lakini kwa mtindo ule ule.
Mfano, Kama mwaka jana ratio ya kinywaji cha mchanganyiko wa tangawizi, ndimu/limao, vitunguu maji, vitunguu, swaumu, kashwagara ilikuwa 1:3:2:4:1.5:7 na mchanganyiko wa kujifukuzia ratio yake ya majani ya mpera, mkaratusi, kijeera(mmea wa Rombo na Madagascar), majani ya limao, nakadhalika ilikuwa 2:1:3:4.2 basi msimu huu ratios za kinywaji na kujifukizia ziwe 3:1:2.5:4:7:3:1 na 4:1:5:2. Baada ya kutumia michanganyiko hii huku tukichukua tahadhari lakini zisizo za kutishana kama mwaka jana tuendelee kupiga kazi kama kawaida bila woga.
Kwa mbinu ya mfano huo hapo juu, hicho kirusi kikija kufikia moja ya sita ya permutations na combinations za ratios hizo hapo juu katika kujibadilisha nina hakika badala ya kuwa ugonjwa ama mdudu mwenye madhara mwilini basi kitakapo kuwa kinaingia mwilini kitakuwa vitamini na protini muhimu kwa afya njema ya mtu!!
Kumbuka maneno yanaumba. Ni kwa imani hiyo hiyo huku nikimtanguliza Mungu aliyetuvusha wimbi la covid19 la mwaka jana, sasa nimeumba mbinu ya kukabiliana na wimbi la sasa na mawimbi yajayo ya namna hii ya ama covid ama vimelea vingine vya magonjwa. Amina.
Imani inaponya.
Tuendelee kuchapa kazi ndugu zangu tena kwa furaha isiyo na kifani.