MKWEAMINAZI
JF-Expert Member
- May 28, 2023
- 930
- 1,299
Inashangazwa kuona nguvu kubwa inatumika kwa viongozi wa wilaya mikoa manaibu mawaziri na mawaziri wajumbe wa halmashauri kuu ya ccm wakihaha huku na kule kuwahutubia wananchi waunge mkono sakata la bandari kupewa DP World ya Dubai.
Wahenga walishasema "Kizuri chajiuza ila kibaya chajitembeza". Usemi huu umethibitika kwenye sakata la bandari kwani CCM baada ya kugundua kuwa wananchi wanapinga mchakato wa bandari wameamua kujitembeza mitaani kuwahadaa wananchi ili wakubali uwekezaji ambao una mkataba wa hovyo.
Naamini mkataba wa bandari ungekuwa mzuri wenye tija kwa nchi na wananchi suala la bandari lingejiuza lenyewe bila CCM na viongozi wake kuzurura kuwashawishi wananchi.
Narudua tena suala la bandari wananchi tunataka mchakato uanze upya wenye nchi tushirikishwe.
Wahenga walishasema "Kizuri chajiuza ila kibaya chajitembeza". Usemi huu umethibitika kwenye sakata la bandari kwani CCM baada ya kugundua kuwa wananchi wanapinga mchakato wa bandari wameamua kujitembeza mitaani kuwahadaa wananchi ili wakubali uwekezaji ambao una mkataba wa hovyo.
Naamini mkataba wa bandari ungekuwa mzuri wenye tija kwa nchi na wananchi suala la bandari lingejiuza lenyewe bila CCM na viongozi wake kuzurura kuwashawishi wananchi.
Narudua tena suala la bandari wananchi tunataka mchakato uanze upya wenye nchi tushirikishwe.