Kizazi cha Gen Z kimekuwa na nguvu na mwiba mkubwa kwa mafisadi kwenye mataifa mbalimbali kuliko upinzani wa vyama vya siasa

Genius Man

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2024
Posts
3,560
Reaction score
7,914
Kizazi cha Gen z kimekuwa na nguvu na mwiba mkubwa kwa mafisadi kwenye mataifa mbalimbali kuliko upinzani wa vyama vya siasa.

Je, gen z wa Tanzania wanaweza kupindua serikali ya Tanzania? hili ni jibu ambalo linaweza kuwa ndio,

kulingana na uchunguzi idadi ya gen z ni zaidi ya asilimia 60% ya watanzania, hivi karibuni serikali ilipata upinzani mkubwa kutoka kwa gen z pasipo kutegemea hivyo uwezo wa gen z kuchukua nchi ni mkubwa na unaweza usitegemewe kwa sasa.
 
CCM ni wapumbavu sana.
Wali paralyse vyama vya upinzani wakiamini watatawala kirahisi ila mambo yamekua vice versa.

Matokea yake umeibuka upinzani mpya, tena upinzani wa Gen Z ni wa moto sana kushinda ule wa vyama vya upinzani.
 
Ogopa sana mtu anapigwa risas ..anaokolewa ila analazimisha arudi wakammalizie...ukiona binadamu amefikia stg hyo bac kama we ni kiongoz na unatumia mabavu..nenda kabatin angalia kitakachokufaa weka kweny begi..kimbia kabisaa..wala usiangalie nyuma due yajayo yatakufurahisha
 
Wa Madagascar alikimbia nchi yake
 
Je, gen z wa Tanzania wanaweza kupindua serikali ya Tanzania?
I'm telling you and trust me when I say I see I say.. vijana wakiamua ni suala la usiku mmoja tu serikali inaanguka. Hutoamini maneno yangu but believe me kuna kitu nimekiona ambacho sijui km kuna mtu anaona km mimi ndio maana wanapiga makelele majukwaani sababu wanaijua nguvu waliyonayo vijana wakiamua ile kuamua kweli usiku mmoja mwingi sana.. kwanini nasema usiku mmoja? Usiniulize mara mbili
 
Vyama vya upinzani au vyama vya siasa mara nyingi huwa vina agenda zao binafsi na mara nyingi huwa haviko real ni kama chama pinzani huwa kinaonea wivu chama tawala kwa kuwa karibu na jiko hivyo na wao pia wanatafuta namna ya kuwa karibu na jiko. Ukiwasikiliza genz mazungumzo yao wana mrefer sana JPM kwa mazuri aliyoyafanya kitu ambacho wapinzani hawakumuelewa kabisa sasa hapo ndio utajua utofauti wa genz na wanasiasa.
 
GEN Z wa tanzania awali walikuwa hawaeleweki kama wapo, walidharaulika ni watu wa mpira, kubeti, walevi na starehe zingine. Gafla wakaibuka na kuwa tishio kutaka kufanya yao. Bila maridhiano hawa wajuba ni obistacle na radical kwa watawala, all eyes on them kuliko vyama vya upinzani
 
Hivi UVCCM sio gen z? au hao vijana ni tofauti na wenzao? maana inaonekana gen z hawana itikadi za vyama wameamua kuwa symetrically kufanya siasa bila vyama. Uongozi wao haujulikani, sasa kama wakifanikiwa kupindua serikali watamuweka nani nafasi ya juu, je sirikali watakayoiunda itakuwa ni ya ma gen z watupu au watachanganya na generation zingine?
 
CCM ni wapumbavu sana.
Wali paralyse vyama vya upinzani wakiamini watatawala kirahisi ila mambo yamekua vice versa.

Matokea yake umeibuka upinzani mpya, tena upinzani wa Gen Z ni wa moto sana kushinda ule wa vyama vya upinzani.
Sasa kama gen z wamekuwa wa moto kuliko vyama vyama vya siasa kama chadema na mwenyekiti wake si wamuachie tu mjuba lissu atoke korokoroni? Maana upinzani wake ni cha mtoto kwa hawa ma gen z. Upinzani wa lissu hauna madhara kwa ccm tena, umeibuka upinzani mpya wa ma gen z. Sijui kina lissu na chadema yake watafanya siasa za aina gani kama upinzani sasa umehamia kwa gen z Hata hivyo gen z ni upepo fulani tu unaovuma kwa muda na utapita kama kimbunga, serikali imara ndio zitahimili upepo huo na zile dhaifu zitabanduliwa na upepo huo mkali unaovuma kwa sasa
 
Gen z watamkimbiza samuya nje ya nchi hiyo #D9
Sasa hivi inafanya tafrija kwa kificho, pambafuu kabisa! JW Mo29 walirahisishiwa kazi wakashindwa kumaliza mchezo, wacha vi Gen-Z vipambane vyenyewe!
 
Gen z ni fasheni tu ya mtazamo wa kisiasa katika kubadili mambo, fasheni hii itapita kama upepo wa kimbunga. The strong governpment will be survived but the weak one will quit, inategemeana na organ za nchi zikoje.
 
Bado wanaendelea kusearch wajue ni nani muhamasishaji mkuu ndio maana wanakamatakamata watu hovyo.
Wasilolijua kumbe Genz wanajiongeza wenyewe tu hawamtegemei Lissu wala heche
 
Kwa vile CCM wamekataa siasa za kistaarabu za kuheshimu demokrasia basi ngoja Gen Zee waseme nao kwa lugha ya kitaa
 
CCM kumejaa wasomi wasioweza kuusema ukweli hadharani, walipaswa kuhakikisha vyama vya upinzani hasa chadema vinanawiri ili kupunguza upinzani kutoka katika makundi mengine ambayo ni ngumu kuyadhibiti.
Kiuhalisia, machafuko ya mwaka 2025 yasingetokea kama chadema ingepewa uwanja sawa wa kushiriki siasa. Hili wajinga wa ccm hawakuliona.
Sasa wamezalisha makundi mengi yanayowapinga, unapambana na TEC, Chadema, GEN Z, vyombo vya habari vya nje, mitandao ya kijamii. Wanaharakati wa nje na ndani, Asasi za kiraia, na watu wotee wenye mlengo tofauti na mawazo yako.

Hii vita CCM hawawez kuishinda kamwe, kumbuka kijana aliyezaliwa 2012, mwaka 2030 atakuwa na sifa ya kupiga kura. CCM ijiandae kuua wananchi wengi zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…