DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Tanzania imebarikiwa utajiri wa kila kitu, lakini tunashangaa huduma ya afya ni mbovu, tumekuja hapa Tunduru kinamama wanalalamika wakienda kujifungua wanauziwa watoto, vifaa vya kujifungulia hakuna, wazee wanatozwa hela, lakini tunashangaa wenzetu wa Chama Cha Mapinduzi wanajisifia eti nchi nzima kuna majengo ya huduma ya afya, sisi tunawaambia wananchi hawataki majengo wanachohitaji ni huduma bora" Kiza Mayeye. Mwenyekiti wa ACT Mkoa wa Kigoma, akizungumza na wakazi wa Jimbo la Tunduru Kaskazini wilayani Tunduru mkoani Ruvuma.