Nakupa mfano mmoja:-
Benki iliamua kuwapa mkopo bwana A, na bwana B; kila mmoja kiasi cha milioni 5, na kila mmoja alitakiwa kuzirejesha pesa hizo baada ya miaka 2.
Bwana A aliamua kuwekeza pesa zile kwenye biashara yake ya uuzaji wa bia na soda; kwa sababu bidhaa alizokuwa auza si za kuharibika, aliweza kuziuza na kupata faida.
Bwana B aliamua kuchukua pesa ile na kununua kiwanja, bila kufanya uzalishaji wowote.
Muda wa marejesho ulipofika, bwana A aliweza kurudisha na kubaki na faida, ila bwana B hakuwa na pesa ya kurudisha zaidi ya kile kiwanja; kutokana na kutakiwa kurudisha lile deni kwa haraka, ilibidi bwana B auze kile kiwanja kwa bei ya hasara ili aweze kurejesha mkopo.
Swali; Je, Bwana A na Bwana B ni nani aliyetumia akili zaidi?