Kiwango cha juu kabisa cha uovu wa mwanadamu ni kumtukuza na kumwabudu mwanadamu mwenzake

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,547
41,060
Vitabu vyote vya dini vinatamka wazi kabisa kuwa anayetakiwa kuabudiwa, kutukuzwa na kusifiwa ni Mungu pekee yake. Biblia inaongeza kwa kusema, amelainiwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, na kumfanya mwanadamu kuwa kinga yake.

Nimerejea maandiko ya vitabu vya dini kwa sababu ndiko huko mifumo ya tawala zote ilirithiwa.

Kwa sasa bila shaka, nchi yetu imelaanika maana viongozi wote hakuna wanalolijua zaidi ya kumsifu na kumtukuza Rais, tena kwa kiwango kinachokaribia kumwabudu.

Anayewezesha yote kufanyika, kwa watu wanaomwamini Mungu, ni Mungu pekee yake. Sisi wanadamu, bila ya kujali vyeo vyetu, utajiri wetu, maarifa yetu, akili zetu na nguvu zetu, bado tumejawa na mapungufu mengi.

Leo tuna watu wanaonena na kutaka kuwaaminisha watu wote kuwa kila linalofanyika nchini mwetu limewezeshwa na Rais. Wameifuta nafasi ya Mungu, na kumkweza Rais. Na yeye, kwa kutolikemea hili, maana yake amekubali, na kama amekubali kuwa yeye ndiye mwezeshaji wa kila kitu, basi ina maana anajifananisha na Mungu. Na kama ndivyo, basi shauri yake.

Mimi siwezi kusema nini kitatokea au ni nini adhabu ya mtu kujifananisha na Mungu, kwa sababu mimi sina nafasi hata ile ndogo kabisa ya kumsemea Mungu. Mimi napaza sauti tu kwa wanadamu wenzangu ili waijue kufuru wanayoifanya, na adhabu wanayojitengenezea kwa nafsi zao na kwa yule waliyeamua kumtukuza.

Leo hii, ikijengwa barabara, ni Rais kajenga.

Maji yakitoka bombani, Rais kaleta maji.

Simba au Yanga ikishinda, Rais katuletea ushindi.

Kukiwa na umeme, Rais katuletea umeme.

Kukiwa na chakula cha kutosha, Rais katuletea chakula.

Leo hii kwa Tanzania, hakuna kinachowezeshwa na Mungu, bali ni Rais tu.

Wale walioamua kumpa rushwa ya utukufu na suia Rais, wanawaaminishwa watu wote kuwa Leo hii kwa Tanzania hakuna kinachofanywa na wananchi zaidi ya milioni 63, isipokuwa Rais pekee yake ndiye anafanya kila kitu. Rais ndiye anayejenga miradi yote. Rais ndiye mwenye akili kuliko Watanzania wote. Rais ndiye mwenye upendo kuzidi Watanzania wote. Na Rais ndiye anayependwa zaidi kuliko Mtanzania yeyote.

Rushwa ya sifa na utukufu ni rushwa sawa na rushwa nyingine, yenye malengo yale yale. Rushwa ya sifa na utukufu humpofusha mtawala sawa na rushwa ya pesa inavyompofusha mtumishi wa Serikali asiye na pesa.

Watanzania mliobakiwa na hekima, jitengene na laana za kuwatukuza wanadamu.

Mwalimu Nyerere hekima ilimwongoza hata aliweza kuishinda rushwa ya sifa:

1) Watu waliamua kumwita Musa, Mwalimu Nyerere aligomba na kukemea kabisa.

2) Alipotaka kung'atuka, watu walienda kwake na sifa kedekede, na kumwambia Mwalimu, 'nchi hii itaendaje bila wewe'. Mwalimu akang'aka na kuuliza, kama yeye ataishi milele; na kama siku akifa na nchi itakufa. Baadaye mwalimu alisema kuwa baada ya kufanya utafiti wake aligundua kuwa "nchi" wanayoiongelea ni familia zao. Hawakuwa na uhakika akitoka yeye, akaja Rais mwingine, kama wangeendelea kuwa kwenye nafasi alizokuwa amewaweka.

Kusema kuwa kila kitu kinafanywa na Rais, ni kuwadharau, kuwatusi na kuwakatisha tamaa Watanzania wanaoteseka usiku na mchana kuleta ustawi katika Taifa lao. Ni sawa na kuwaambia Watanzania wote kuwa hayo wanayoyafanya hayana maana yoyote wala hayana mchango wowote kwenye ustawi wa Taifa lao, maana mtu pekee anayefanya kazi katika nchi hii na kuistawisha ni Rais pekee yake.

Yatafakarini haya kwa hekima badala ya sifa, ubishi na ushindani.
 
Aisee.
Ati kwamba uovu mbaya zaidi ni kuabudu wanadamu badala ya mungu.
Wakati huo huo, unapuuza mambo saba ambayo Mungu anachukia, kama vile kusema uongo, kuua, na kuchonganisha watu au kupandikiza mifarakanyo.

Kutwa hapa huwa kuna Uzi za kuwatukuza na kuwasifia watu wa nchi zingine, mfano Waziri Mkuu wa zamani wa Singapore na sera zake za Uchumi n.k Ati ni watu wenye akili zaidi kupita Watanzania! Huo sio Unafiki? Sionagi vidole vikinyooshwa kwa wale wanaotukuza Wazungu wenzao na kuwashutumu kuwa wamelaaniwa, why the hypocrasy?

I think its there is alot of hypocrasy, inconsistent and divisive arguments herein.


Mnwaambia Watanzania waepuke na laana ya kuwaabudu na kuwatukuza wanadamu wenzao, haswa Rais wetu! How trustworthy is your advice? Does that that come from authenticated soul? Uzalendo wa Nchi na watu wake? I doubt.

Nadhani huwa watu wanapenda kuleta mifarakano kati ya Watanzania kwa husuda, wivu, insecurity na pure hatred na hasira tu.

Hii ni dhambi, sawa na wanaotukuza Raisi unaowakosoa.

Mmeshwahi kujiuliza kwamba some of these people are not glorifying "people" but aknowledging their contributions and achievments?

I for one, situkuzi mtu au watu lakini ninawaheshimu na kuwathamini wale ambao wameleta matokeo chanya na yanaoyoonekana kwa jamii yetu na nchi kwa ujumla.

Hayat Rais John Pombe Magufuli na Rais Samia Suluhu Hassan hawatukuzwi kimungu bali we are aknowledging their contribution na mafanikio yao.
 
Viongozi wenyewe kama hawa tusitegeme maendeleo
20231209_105134.jpg
 
Laana huwaingia wasio na akili hivihivi.Mwaka 1576 kwenye mji wa Galilaya kuna jamaa alisifiwa hadi kutwaa nafasi ya Yesu akaitwa Mungu.Waja wakadai kila goti litakunjwa mbele ya huyo "mungu"! Laana ikatamalaki.
 
Nakamuliwa Kodi kwenye mshahara, na biashara, magari na nyumba! Zote hizi serikali inachukua. Halafu sifa za kujenga nchi ni Kwa rais peke yake. Hakuna mahali walipa Kodi , wakubwa kwa wadogo wanatajwa. It's like wanachi katika nchi hii hawana maana, bali raisi tu.Inashangaza
 
Nakamuliwa Kodi kwenye mshahara, na biashara, magari na nyumba! Zote hizi serikali inachukua. Halafu sifa za kujenga nchi ni Kwa rais peke yake. Hakuna mahali walipa Kodi , wakubwa kwa wadogo wanatajwa. It's like wanachi katika nchi hii hawana maana, bali raisi tu.Inashangaza

Rais ambaye ni mtumiaji wa pesa za wananchi anaonekana ndiye pekee anayezalisha pesa na ndiye pekee mwenye maamuzi juu ya matumizi ya hiyo pesa wanayotuamisha ni pesa ya Rais.

Kama ndivyo, basi wafute kodi zote wanazotozwa wananchi, Rais ajenge nchi kwa hiyo pesa yake, kama wanavyosema wanaomhonga rushwa ya sifa na utukufu.
 
Samia love haina tatizo lolote huyo mangi ameonyesha Upendo tu
Haina tatizo, una uhakika? Huyo hajasema, I love Samia'; bali amesema Samia Love. Naamini anakusudia kusema kuwa Samia ni Upendo. Neno hili hutumika kwa Mungu na Masiha Kristo. Yesu ni Upendo. Mungu ni Upendo.
 
Vitabu vyote vya dini vinatamka wazi kabisa kuwa anayetakiwa kuabudiwa, kutukuzwa na kusifiwa ni Mungu pekee yake. Biblia inaongeza kwa kusema, amelainiwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, na kumfanya mwanadamu kuwa kinga yake.

Nimerejea maandiko ya vitabu vya dini kwa sababu ndiko huko mifumo ya tawala zote ilirithiwa.

Kwa sasa bila shaka, nchi yetu imelaanika maana viongozi wote hakuna wanalolijua zaidi ya kumsifu na kumtukuza Rais, tena kwa kiwango kinachokaribia kumwabudu.

Anayewezesha yote kufanyika, kwa watu wanaomwamini Mungu, ni Mungu pekee yake. Sisi wanadamu, bila ya kujali vyeo vyetu, utajiri wetu, maarifa yetu, akili zetu na nguvu zetu, bado tumejawa na mapungufu mengi.

Leo tuna watu wanaonena na kutaka kuwaaminisha watu wote kuwa kila linalofanyika nchini mwetu limewezeshwa na Rais. Wameifuta nafasi ya Mungu, na kumkweza Rais. Na yeye, kwa kutolikemea hili, maana yake amekubali, na kama amekubali kuwa yeye ndiye mwezeshaji wa kila kitu, basi ina maana anajifananisha na Mungu. Na kama ndivyo, basi shauri yake. Mimi siwezi kusema nini kitatokea au ni nini adhabu ya mtu kujifananisha na Mungu, kwa sababu mimi sina nafasi hata ile ndogo kabisa ya kumsemea Mungu. Mimi napaza sauti tu kwa wanadamu wenzangu ili waijue kufuru wanayoifanya, na adhabu wanayojitengenezea kwa nafsi zao na kwa yule waliyeamua kumtukuza.

Leo hii, ikijengwa barabara, ni Rais kajenga.

Maji yakitoka bombani, Rais kaleta maji.

Simba au Yanga ikishinda, Rais katuletea ushindi.

Kukiwa na umeme, Rais katuletea umeme.

Kukiwa na chakula cha kutosha, Rais katuletea chakula.

Leo hii kwa Tanzania, hakuna kinachowezeshwa na Mungu, bali ni Rais tu.

Wale walioamua kumpa rushwa ya utukufu na suia Rais, wanawaaminishwa watu wote kuwa Leo hii kwa Tanzania hakuna kinachofanywa na wananchi zaidi ya milioni 63, isipokuwa Rais pekee yake ndiye anafanya kila kitu. Rais ndiye anayejenga miradi yote. Rais ndiye mwenye akili kuliko Watanzania wote. Rais ndiye mwenye upendo kuzidi Watanzania wote. Na Rais ndiye anayependwa zaidi kuliko Mtanzania yeyote.

Rushwa ya sifa na utukufu ni rushwa sawa na rushwa nyingine, yenye malengo yale yale. Rushwa ya sifa na utukufu humpofusha mtawala sawa na rushwa ya pesa inavyompofusha mtumishi wa Serikali asiye na pesa.

Watanzania mliobakiwa na hekima, jitengene na laana za kuwatukuza wanadamu.

Mwalimu Nyerere hekima ilimwongoza hata aliweza kuishinda rushwa ya sifa:

1) Watu waliamua kumwita Musa, Mwalimu Nyerere aligomba na kukemea kabisa.

2) Alipotaka kung'atuka, watu walienda kwake na sifa kedekede, na kumwambia Mwalimu, 'nchi hii itaendaje bila wewe'. Mwalimu akang'aka na kuuliza, kama yeye ataishi milele; na kama siku akifa na nchi itakufa. Baadaye mwalimu alisema kuwa baada ya kufanya utafiti wake aligundua kuwa "nchi" wanayoiongelea ni familia zao. Hawakuwa na uhakika akitoka yeye, akaja Rais mwingine, kama wangeendelea kuwa kwenye nafasi alizokuwa amewaweka.

Kusema kuwa kila kitu kinafanywa na Rais, ni kuwadharau, kuwatusi na kuwakatisha tamaa Watanzania wanaoteseka usiku na mchana kuleta ustawi katika Taifa lao. Ni sawa na kuwaambia Watanzania wote kuwa hayo wanayoyafanya hayana maana yoyote wala hayana mchango wowote kwenye ustawi wa Taifa lao, maana mtu pekee anayefanya kazi katika nchi hii na kuistawisha ni Rais pekee yake.

Yatafakarini haya kwa hekima badala ya sifa, ubishi na ushindani.
CDM bana wamemtukuza mzee Mbowe na kumpachika kila jina
 
Vitabu vyote vya dini vinatamka wazi kabisa kuwa anayetakiwa kuabudiwa, kutukuzwa na kusifiwa ni Mungu pekee yake. Biblia inaongeza kwa kusema, amelainiwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, na kumfanya mwanadamu kuwa kinga yake.

Nimerejea maandiko ya vitabu vya dini kwa sababu ndiko huko mifumo ya tawala zote ilirithiwa.

Kwa sasa bila shaka, nchi yetu imelaanika maana viongozi wote hakuna wanalolijua zaidi ya kumsifu na kumtukuza Rais, tena kwa kiwango kinachokaribia kumwabudu.

Anayewezesha yote kufanyika, kwa watu wanaomwamini Mungu, ni Mungu pekee yake. Sisi wanadamu, bila ya kujali vyeo vyetu, utajiri wetu, maarifa yetu, akili zetu na nguvu zetu, bado tumejawa na mapungufu mengi.

Leo tuna watu wanaonena na kutaka kuwaaminisha watu wote kuwa kila linalofanyika nchini mwetu limewezeshwa na Rais. Wameifuta nafasi ya Mungu, na kumkweza Rais. Na yeye, kwa kutolikemea hili, maana yake amekubali, na kama amekubali kuwa yeye ndiye mwezeshaji wa kila kitu, basi ina maana anajifananisha na Mungu. Na kama ndivyo, basi shauri yake.

Mimi siwezi kusema nini kitatokea au ni nini adhabu ya mtu kujifananisha na Mungu, kwa sababu mimi sina nafasi hata ile ndogo kabisa ya kumsemea Mungu. Mimi napaza sauti tu kwa wanadamu wenzangu ili waijue kufuru wanayoifanya, na adhabu wanayojitengenezea kwa nafsi zao na kwa yule waliyeamua kumtukuza.

Leo hii, ikijengwa barabara, ni Rais kajenga.

Maji yakitoka bombani, Rais kaleta maji.

Simba au Yanga ikishinda, Rais katuletea ushindi.

Kukiwa na umeme, Rais katuletea umeme.

Kukiwa na chakula cha kutosha, Rais katuletea chakula.

Leo hii kwa Tanzania, hakuna kinachowezeshwa na Mungu, bali ni Rais tu.

Wale walioamua kumpa rushwa ya utukufu na suia Rais, wanawaaminishwa watu wote kuwa Leo hii kwa Tanzania hakuna kinachofanywa na wananchi zaidi ya milioni 63, isipokuwa Rais pekee yake ndiye anafanya kila kitu. Rais ndiye anayejenga miradi yote. Rais ndiye mwenye akili kuliko Watanzania wote. Rais ndiye mwenye upendo kuzidi Watanzania wote. Na Rais ndiye anayependwa zaidi kuliko Mtanzania yeyote.

Rushwa ya sifa na utukufu ni rushwa sawa na rushwa nyingine, yenye malengo yale yale. Rushwa ya sifa na utukufu humpofusha mtawala sawa na rushwa ya pesa inavyompofusha mtumishi wa Serikali asiye na pesa.

Watanzania mliobakiwa na hekima, jitengene na laana za kuwatukuza wanadamu.

Mwalimu Nyerere hekima ilimwongoza hata aliweza kuishinda rushwa ya sifa:

1) Watu waliamua kumwita Musa, Mwalimu Nyerere aligomba na kukemea kabisa.

2) Alipotaka kung'atuka, watu walienda kwake na sifa kedekede, na kumwambia Mwalimu, 'nchi hii itaendaje bila wewe'. Mwalimu akang'aka na kuuliza, kama yeye ataishi milele; na kama siku akifa na nchi itakufa. Baadaye mwalimu alisema kuwa baada ya kufanya utafiti wake aligundua kuwa "nchi" wanayoiongelea ni familia zao. Hawakuwa na uhakika akitoka yeye, akaja Rais mwingine, kama wangeendelea kuwa kwenye nafasi alizokuwa amewaweka.

Kusema kuwa kila kitu kinafanywa na Rais, ni kuwadharau, kuwatusi na kuwakatisha tamaa Watanzania wanaoteseka usiku na mchana kuleta ustawi katika Taifa lao. Ni sawa na kuwaambia Watanzania wote kuwa hayo wanayoyafanya hayana maana yoyote wala hayana mchango wowote kwenye ustawi wa Taifa lao, maana mtu pekee anayefanya kazi katika nchi hii na kuistawisha ni Rais pekee yake.

Yatafakarini haya kwa hekima badala ya sifa, ubishi na ushindani.
Kongole mkuu kwa andiko lenye hekima na busara tele. Upuuzi wote huu uliletwa na JPM. Sifa za utukufu, kuabudu pamoja na pambio zilipoanza kustawi na kutamalaki, hata Mzee Mkapa aliwahi kukemea hadharani tabia hii mbaya ya mawaziri, na alitaka kama endapo kuna pongezi, basi zisiende kwa Rais kama mtu binafsi, bali ziende kwa serikali inayoundwa na CCM chini ya uongozi wa Rais JPM.

Wameshupaza shingo zao, maji wamekwisha yavulia nguo hawana budi pia kuyaogea. Mazoea hujenga tabia, sasa imegeuka rasmi kuwa ndiyo kama "code of conduct" kwao. Ni lazima sasa usifu na kuabudu ili uonekane kuwa ni mmoja wao. Rais naye yupo katika "hangover" ya kiburi cha kinafamu, na hata kupata tamaa za kuzidi kuhofiwa, kusifiwa na kuabudiwa kutokana na utukufu wa kiti chake chenye mamlaka makuu ya kibinadamu

Laana hii kamwe haitaliacha Taifa letu salama.
 
Laana kubwa. Eti "Samia Love", halafu huyo anaweza kuwa ni kiongozi!!
Eti huyu home anawakoromea watoto na mke wake....haoni aibu kumtukuza Saa 100 hadi aibu wanaona familia yake?? Aibuu wanaume tena kichaga hawako hivyo too much jiamini .....sio kujikombaaabhivyoo bana
 
Vitabu vyote vya dini vinatamka wazi kabisa kuwa anayetakiwa kuabudiwa, kutukuzwa na kusifiwa ni Mungu pekee yake. Biblia inaongeza kwa kusema, amelainiwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, na kumfanya mwanadamu kuwa kinga yake.

Nimerejea maandiko ya vitabu vya dini kwa sababu ndiko huko mifumo ya tawala zote ilirithiwa.

Kwa sasa bila shaka, nchi yetu imelaanika maana viongozi wote hakuna wanalolijua zaidi ya kumsifu na kumtukuza Rais, tena kwa kiwango kinachokaribia kumwabudu.

Anayewezesha yote kufanyika, kwa watu wanaomwamini Mungu, ni Mungu pekee yake. Sisi wanadamu, bila ya kujali vyeo vyetu, utajiri wetu, maarifa yetu, akili zetu na nguvu zetu, bado tumejawa na mapungufu mengi.

Leo tuna watu wanaonena na kutaka kuwaaminisha watu wote kuwa kila linalofanyika nchini mwetu limewezeshwa na Rais. Wameifuta nafasi ya Mungu, na kumkweza Rais. Na yeye, kwa kutolikemea hili, maana yake amekubali, na kama amekubali kuwa yeye ndiye mwezeshaji wa kila kitu, basi ina maana anajifananisha na Mungu. Na kama ndivyo, basi shauri yake. Mimi siwezi kusema nini kitatokea au ni nini adhabu ya mtu kujifananisha na Mungu, kwa sababu mimi sina nafasi hata ile ndogo kabisa ya kumsemea Mungu. Mimi napaza sauti tu kwa wanadamu wenzangu ili waijue kufuru wanayoifanya, na adhabu wanayojitengenezea kwa nafsi zao na kwa yule waliyeamua kumtukuza.

Leo hii, ikijengwa barabara, ni Rais kajenga.

Maji yakitoka bombani, Rais kaleta maji.

Simba au Yanga ikishinda, Rais katuletea ushindi.

Kukiwa na umeme, Rais katuletea umeme.

Kukiwa na chakula cha kutosha, Rais katuletea chakula.

Leo hii kwa Tanzania, hakuna kinachowezeshwa na Mungu, bali ni Rais tu.

Wale walioamua kumpa rushwa ya utukufu na suia Rais, wanawaaminishwa watu wote kuwa Leo hii kwa Tanzania hakuna kinachofanywa na wananchi zaidi ya milioni 63, isipokuwa Rais pekee yake ndiye anafanya kila kitu. Rais ndiye anayejenga miradi yote. Rais ndiye mwenye akili kuliko Watanzania wote. Rais ndiye mwenye upendo kuzidi Watanzania wote. Na Rais ndiye anayependwa zaidi kuliko Mtanzania yeyote.

Rushwa ya sifa na utukufu ni rushwa sawa na rushwa nyingine, yenye malengo yale yale. Rushwa ya sifa na utukufu humpofusha mtawala sawa na rushwa ya pesa inavyompofusha mtumishi wa Serikali asiye na pesa.

Watanzania mliobakiwa na hekima, jitengene na laana za kuwatukuza wanadamu.

Mwalimu Nyerere hekima ilimwongoza hata aliweza kuishinda rushwa ya sifa:

1) Watu waliamua kumwita Musa, Mwalimu Nyerere aligomba na kukemea kabisa.

2) Alipotaka kung'atuka, watu walienda kwake na sifa kedekede, na kumwambia Mwalimu, 'nchi hii itaendaje bila wewe'. Mwalimu akang'aka na kuuliza, kama yeye ataishi milele; na kama siku akifa na nchi itakufa. Baadaye mwalimu alisema kuwa baada ya kufanya utafiti wake aligundua kuwa "nchi" wanayoiongelea ni familia zao. Hawakuwa na uhakika akitoka yeye, akaja Rais mwingine, kama wangeendelea kuwa kwenye nafasi alizokuwa amewaweka.

Kusema kuwa kila kitu kinafanywa na Rais, ni kuwadharau, kuwatusi na kuwakatisha tamaa Watanzania wanaoteseka usiku na mchana kuleta ustawi katika Taifa lao. Ni sawa na kuwaambia Watanzania wote kuwa hayo wanayoyafanya hayana maana yoyote wala hayana mchango wowote kwenye ustawi wa Taifa lao, maana mtu pekee anayefanya kazi katika nchi hii na kuistawisha ni Rais pekee yake.

Yatafakarini haya kwa hekima badala ya sifa, ubishi na ushindani.
Kinacho uma zaidi sifa anazopewa na uhalisia wa mambo tofauti utasikia amefungua nchi utasikia wawekezaji wameongezeka utasikia ana huruma atukatai kumsifia Bina adam akifanya jema ni vema kumsifia lakini wezetu wamezidi itafika hatua hata unaponyanyua mdomo hili umeze tonge utasikia mtu anasema namshukuru rais kwakuniweza mdomo kunyanyuka hili niweze kula utasikia na mshukuru rais kuniwezesha kupiga nguo pasi na kuivaa na mshukuru rais kwakuniwezesha kusikia usingizi na kulala na mshukuru rais kuniwezesha kupata mke bora namshukuru rais kuniwezesha kupata mtoto na mshukuru rais kuniwezesha kufika 2024 namshukuru rais kuniwezesha kwenda kusalimia wazee namshukuru rais kuniwezesha kukoment jamii forums cha ajabu kwenye sifa nzuri wanamueka rais kwenye mambo mabaya wana muhusisha Mungu umeme wa mgao Mungu ajaleta mvua ikitokea madawati wanachangishwa raia anakuja mkuu wa wilaya anakuambia tunamshukuru rais kwa kuboresha elimu shule zote zina madawati mwisho allahu sswamad yy ndie anaepaswa kuabudiwa kila sifa njema ni zake yeye MUNGU sio bina adamu
 
Mtu yeyote timamu, kamwe hawezi kuabudu mwanadamu mwenzake. Kinachoendelea nchini ni kufuru na ibada ya sanamu, ambayo, wahusika lazima watatoa hesabu yake siku ikifika kwa Mungu, Muumba wa nchi na wanadamu.
 
Vitabu vyote vya dini vinatamka wazi kabisa kuwa anayetakiwa kuabudiwa, kutukuzwa na kusifiwa ni Mungu pekee yake. Biblia inaongeza kwa kusema, amelainiwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, na kumfanya mwanadamu kuwa kinga yake.

Nimerejea maandiko ya vitabu vya dini kwa sababu ndiko huko mifumo ya tawala zote ilirithiwa.

Kwa sasa bila shaka, nchi yetu imelaanika maana viongozi wote hakuna wanalolijua zaidi ya kumsifu na kumtukuza Rais, tena kwa kiwango kinachokaribia kumwabudu.

Anayewezesha yote kufanyika, kwa watu wanaomwamini Mungu, ni Mungu pekee yake. Sisi wanadamu, bila ya kujali vyeo vyetu, utajiri wetu, maarifa yetu, akili zetu na nguvu zetu, bado tumejawa na mapungufu mengi.

Leo tuna watu wanaonena na kutaka kuwaaminisha watu wote kuwa kila linalofanyika nchini mwetu limewezeshwa na Rais. Wameifuta nafasi ya Mungu, na kumkweza Rais. Na yeye, kwa kutolikemea hili, maana yake amekubali, na kama amekubali kuwa yeye ndiye mwezeshaji wa kila kitu, basi ina maana anajifananisha na Mungu. Na kama ndivyo, basi shauri yake.

Mimi siwezi kusema nini kitatokea au ni nini adhabu ya mtu kujifananisha na Mungu, kwa sababu mimi sina nafasi hata ile ndogo kabisa ya kumsemea Mungu. Mimi napaza sauti tu kwa wanadamu wenzangu ili waijue kufuru wanayoifanya, na adhabu wanayojitengenezea kwa nafsi zao na kwa yule waliyeamua kumtukuza.

Leo hii, ikijengwa barabara, ni Rais kajenga.

Maji yakitoka bombani, Rais kaleta maji.

Simba au Yanga ikishinda, Rais katuletea ushindi.

Kukiwa na umeme, Rais katuletea umeme.

Kukiwa na chakula cha kutosha, Rais katuletea chakula.

Leo hii kwa Tanzania, hakuna kinachowezeshwa na Mungu, bali ni Rais tu.

Wale walioamua kumpa rushwa ya utukufu na suia Rais, wanawaaminishwa watu wote kuwa Leo hii kwa Tanzania hakuna kinachofanywa na wananchi zaidi ya milioni 63, isipokuwa Rais pekee yake ndiye anafanya kila kitu. Rais ndiye anayejenga miradi yote. Rais ndiye mwenye akili kuliko Watanzania wote. Rais ndiye mwenye upendo kuzidi Watanzania wote. Na Rais ndiye anayependwa zaidi kuliko Mtanzania yeyote.

Rushwa ya sifa na utukufu ni rushwa sawa na rushwa nyingine, yenye malengo yale yale. Rushwa ya sifa na utukufu humpofusha mtawala sawa na rushwa ya pesa inavyompofusha mtumishi wa Serikali asiye na pesa.

Watanzania mliobakiwa na hekima, jitengene na laana za kuwatukuza wanadamu.

Mwalimu Nyerere hekima ilimwongoza hata aliweza kuishinda rushwa ya sifa:

1) Watu waliamua kumwita Musa, Mwalimu Nyerere aligomba na kukemea kabisa.

2) Alipotaka kung'atuka, watu walienda kwake na sifa kedekede, na kumwambia Mwalimu, 'nchi hii itaendaje bila wewe'. Mwalimu akang'aka na kuuliza, kama yeye ataishi milele; na kama siku akifa na nchi itakufa. Baadaye mwalimu alisema kuwa baada ya kufanya utafiti wake aligundua kuwa "nchi" wanayoiongelea ni familia zao. Hawakuwa na uhakika akitoka yeye, akaja Rais mwingine, kama wangeendelea kuwa kwenye nafasi alizokuwa amewaweka.

Kusema kuwa kila kitu kinafanywa na Rais, ni kuwadharau, kuwatusi na kuwakatisha tamaa Watanzania wanaoteseka usiku na mchana kuleta ustawi katika Taifa lao. Ni sawa na kuwaambia Watanzania wote kuwa hayo wanayoyafanya hayana maana yoyote wala hayana mchango wowote kwenye ustawi wa Taifa lao, maana mtu pekee anayefanya kazi katika nchi hii na kuistawisha ni Rais pekee yake.

Yatafakarini haya kwa hekima badala ya sifa, ubishi na ushindani.
Hahahaa
 
Back
Top Bottom