nasrimgambo
JF-Expert Member
- Jan 10, 2017
- 1,898
- 2,473
Akiwa kashikilia nyaraka za kibenki mikononi mwake, kwa taratibu Johari alielekea chumba maalum cha maongezi cha benki yao. Chumba ambacho kilitengwa maalum kwa ajili ya kufanya maongezi na wateja wa hadhi kubwa wa huduma za kibenki zilizotolewa na benki ya National Investment Bank, ama NIB, ambayo ndiyo Johari alikuwa akiifanyia kazi. Moja ya majukumu ya Johari hapo benki ilikuwa ni kuonana na kufanya mazungumzo na wateja wakubwa wakubwa wenye uwezo na hadhi kubwa wa benki hiyo.
Ndani ya chumba alichokuwa akielekea mlikuwamo na bwana Jama Bhanji, ambaye alikuwa mfanyabiashara maarufu na mtu tajiri sana na aliyekuwa miongoni mwa wateja wakubwa kabisa wa benki ya NIB. Hivyo Johari alikuwa anaelekea kwenye mazungumzo na kumhudumia mteja mkubwa wa benki. Ndani ya hicho chumba bwana Jama Bhanji alikuwa kashikilia kikombe cha kahawa akiwa anainywa taratibu, huku macho yake kayarushia kwenye runinga ya kisasa iliyokuwamo ndani ya chumba hicho na ambayo kwa wakati huo ilirusha taarifa ya habari na wakati huo kiyoyozi kilipulizia hewa ya ubaridi kwenye chumba. Mara tu Johari alipofungua mlango wa chumba hicho na kuingia bwana Bhanji alitoa macho yake toka kwenye runinga na kumtazama Johari aliyeingia ndani ya chumba hicho, huku akiwa kajaza tabasamu usoni, akionekana nadhifu kwa suti aliyovalia.
Kwa bashasha Johari aliongeza tabasamu la uso wake na kuelekea kukaa kwenye kochi lililotazamana na kochi alilokaa bwana Bhanji, kisha akamkaribisha na kumwambia jinsi benki yao ya NIB ilivyo na furaha kuendelea kumhudumia mtu wa muhimu katika uwekezaji nchini. Maongezi yao yalihusisha mapitio ya faida za gawiwo ambazo bwana Bhanji alizipata kutokana na kuwekeza kwenye makampuni na miradi mbalimbali ambayo benki ya NIB ilimshauri mfanyabiashara huyo awekeze. Kwenye kikao hicho bwana Bhanji alijawa na furaha sana kwa maana miradi yote liyoshauriwa awekeze na watu wa benki hiyo ilikuwa imemuingizia faida nyingi sana na hivyo akamuahidi Johari kuwa ataendelea kutumia huduma za benki yao ya NIB na kufuata shauri za benki hiyo juu ya masuala ya uwekezaji.
Kikao cha siku hiyo na bwana Bhanji kilienda vizuri sana hivi kwamba Johari alisifiwa na wafanyakazi wezie na viongozi wake kazini kwa kuweza kushughulika na wateja wakubwa wakubwa wa benki hiyo, wateja ambao walikuwa wa hadhi kubwa na kila benki iliwalilia na kufanya jitihada kuwapata.
Johari alijawa na furaha na kujiona mwenye bahati na akili nyingi kwa kuweza kufanya kazi na kushughulika na watu wa hadhi ya juu. Alijivunia sana moyoni.
Kwa hakika Johari alikuwa ni mwanamke mwenye bahati sana. Alikuwa msomi, mrembo, mnyenyekevu, aliyependwa na watu kila mahala,maofisini, majirani na koote alikokwenda alipendwa, alikuwa na uwezo mkubwa kwa maana kazi yake ya benki ilimlipa vizuri na kumpa heshima. Na pia Johari alikuwa keshaolewa, na alimpenda sana mume wake ambaye aliitwa Malcom Munyisi. Malcom alikuwa akifanya kazi katika wizara ya mambo ya nje, kazi ambayo ilimfanya asafiri sana kwenda nje ya nchi katika nchi za ulaya, arabuni, uchina na hata amerika, Johari alifurahia sana kazi hiyo ya Malcom.
Hakika Johari alionekana mwenye bahati sana kwa wakati huo. Ila!, kama inavyosemekana miongoni mwa waswahili ya kuwa hakuna kizuri kisicho kasoro, basi ndivyo vivyo hivyo ilivyokuwa kwa Johari Chande Munyisi.
Na kichwani mwake Johari aliwaza sana mambo yaliyomtia kasoro. Pamoja na furaha zake na bahati zake alizo kirimiwa na mwenyezi mungu, katu hayakutoka kichwani mwake mambo yaliyomtia kasoro na aliyawaza sana.
Mambo yenyewe yaliyomtia kasoro yalianza kama miaka kumi na nne kabla ya wakati huo. Enzi ambazo Johari alikuwa binti yatima, mwenye maisha magumu ila binti aliyekuwa kajawa akili hivi kwamba alipata nafasi kujiunga na chuo kikuu.
Kwa ugumu wa maisha aliokuwa nao Johari kipindi hicho alichokuwa akisoma, alijikuta akiingia kwenye mahusiano na kijana mtukutu aliyeitwa ‘Kutu’. Kutu alimpenda sana Johari na alimpa kila kitu. Na akawa akimshawishi Johari ajiunge na kundi la kiharifu la kivamizi lililoitwa ‘mapanya’. Johari katu hakukubali kujiunga na kundi hilo la kiharifu.
Basi ikafika siku moja ambayo Johari alitimuliwa chuo na kuambiwa kuwa hatofanya mitihani ya mwisho wa ‘semester’ hadi atakapolipia ada ya chuo. Kitendo hicho kilimuuma sana na kumtia hasira, hivyo akafanya maamuzi mazito ya kuamua kujiunga na kundi la kiharifu la ‘mapanya’, ikiwa kama njia yake ya kujinasua toka kwenye ukata.
Hivyo kwa msaada wa bwana ake, Kutu, Johari alifanikiwa kujiunga na kundi hilo la kiharifu. Na akiwa ndani ya kundi hilo, haraka sana Johari alipata ada ya kulipa chuo na pesa nyingi za kufanyia mambo mengine. Na akawa mshirika mkubwa wa waharifu wa kundi hilo, ambalo lilifanya uharifu katika maeneo mbalimbali kwa kupora, kukaba na kuibia watu na kusaidia usambazaji wa madawa haramu ya kulevya.
Johari aliona kila kitu kinaenda sawa kwa kushiriki kwake kwenye uharifu wa kundi la ‘mapanya’. Mpaka usiku mmoja mambo yalipoanza kwenda kombo baada ya kuvamia nyumba ya mfanyabiashara mmoja wa madini mwenye asili ya kieshia.
Katika usiku huo mnene wa manane, kundi la ‘mapanya’ wakiwa wamevalia vinyago usoni, na silaha za bunduki, masime na mapanga, walivamia nyumba ya mfanyabiashara wa madini na vito vya thamani. Walifika na gari yao aina ya ‘Noah’, wakiwa kundi kubwa sana na waliojipanga wakiwa na uelewa wa ramani nzima ya nyumba ya mfanyabiashara huyo na walikuwa wakifahamu kila mahala ambapo vitu vya thamani vilikuwa vimefichwa kwenye nyumba mfanyabiashara huyo, tena walikuwa na funguo zao wenyewe za milango ya kila kona ya nyumba hiyo.
Bila huruma kundi la mapanya walimshushia mfanyabiashara huyo kipigo kikali mbele ya familia yake na kisha kuanza kupekua kila walipofahamu pana vitu vya thamani na kuanza kuchukua vitu hivyo.
Johari akiwa miongoni mwa waharifu wa kundi hilo la ‘mapanya’, tena mtoto wa kike pekee kundini, alishiriki vyema katika tukio hilo la kikatili. Na alishuhudia jinsi waharifu wezie walivyo mdhalilisha yule mfanyabiashara na mkewe mbele ya mabinti zao wawili. Alishuhudia jinsi yule mfanyabiashara na mkewe na mabinti zao walivyolazimishwa kulala kifudifudi kwenye sebule ya nyumba yao na kuzuiwa kutoa kelele za aina zozote na kupewa vitisho vya kukatishwa maisha dakika yeyote watakayo neng’eneka kwa namna yeyote ile. Mfanyabiashara wa watu alikuwa hoi kagalagazwa sakafuni, damu zikimtoka mdomoni na puani, alikuwa kakosa kabisa la kufanya zaidi ya kulia shahada kwa sauti ya chini, “la ilaha illa llah, la ilaha illa llah”, huku akiomba waharifu wabebe kila walichoona kinawafaa na kuondoka. Johari aliyekuwa kavalia kinyago alimuangalia mzee huyo na kuona jinsi alivyolia kwa mungu wake na kuwalilia wao, na mara akamuona Kutu akitoa bunduki na kumnyooshea mzee huyo na familia yake ili awaue.
Hapo sasa Johari alijikuta akiingiwa na huruma kidogo na akamuomba Kutu amwache mzee huyo na asimuue. Kutu ambaye alikuwa ni muharifu sugu alimtazama Johari na kuangua kicheko cha kishetani shetani kisha akafyatua risasi toka kwenye bunduki hiyo na kumuua mzee huyo. Hivyo Johari akashuhudia mzee huyo wa watu jinsi ambavyo risasi ilitawanyisha kichwa chake na kumpoteza uhai ndani ya sekunde, huku mke wa mzee huyo na mabinti zao wakishuhudia na walishindwa kujizuia na wakatoa ukelele wa kilio. Mara Kutu akawafyatulia risasi wote, huyo mama wa kiarabu na mabinti zake wawili na kuwaua.
Johari sasa hata kinyago akakivua hakuamini alichoshuhudia kikitendwa na Kutu. Johari alijikuta akitetemeka kwa kuogopa alichokiona. Macho yalimtoka na akajikuta kamvamia Kutu na kumhoji kwa hasira umuhimu hasa wa kuwaua yule mama na mabinti zake pamoja na baba yao mfanyabiashara. Kutu akamtazama Johari kwa jicho la ukali sana na kisha akamnyooshea bunduki na kumuwekea kichwani. Johari alikuwa na hasira sana wakati huo, hata hakuogopa hiyo bunduki aliyowekewa kwenye paji la uso. Tena wakati huo Johari mwenyewe alikuwa na bunduki yake mkononi. Mara wale waharifu wengine ambao hawakushtushwa na kilichotendwa na Kutu walikuwa washamaliza kubeba vitu vya thamani vya ndani ya nyumba hiyo, hivyo wakaamrisha Kutu na Johari waache upumbavu wao na kuamuru kuwa wote waondoke haraka toka kwenye nyumba hiyo. Hivyo wote wakiwamo Johari na Kutu walitoka nje haraka na Kurukia kwenye ‘Noah’ yao na ‘kuondoka’ pamoja na pesa na vito vya thamani walivyoiba.
Usiku wa siku hiyo na wiki kadhaa zilizofuatia Johari alishindwa kulala kabisa kwa maana kila mara alipolala ilikuwa lazima aote juu ya ile familia aliyoshuhudiwa ikiuwawa na Kutu. Kwenye ndoto moja, aliota wanawake watatu waliovalia mavazi meupe na kujifunika hijabu wamelala kifudifudi kwenye sakafu huku damu zikiwavuja toka vichwani mwao na kuchafua nguo zao nyeupe, aliota akihangaika kuwapindua ili aone sura zao na kujua ni akina nani, ila ghafla waliamka wenyewe na kumtazama na aliona sura zao ni zile za yule mama na mabinti zake wawili waliouwawa na Kutu. Kila mara taswira za yule mama na mabinti zake zilimjia, mara nyingine aliota wakimlilia kwa uchungu mwingi, mida mingine alilala akahisi wapo nje ya dirisha la chumba chake wakimlilia. Kila mara Johari aliisikia sauti ya yule mzee aliyokuwa akiitoa muda mchache kabla hajauwawa, aliyasikia maneno ya shahada ya yule mzee, alisikia “la ilaha illa llah, la ilaha illa llah”, alisikia sauti hiyo ikianza kidogo na kisha kupanda na mara ikawa inageuka na kuwa kilio kikubwa cha mzee yule akimlilia.
Kama hiyo haikutosha, miezi michache baadae, Kutu alihusika katika ajali mbaya sana. Johari ambaye alikuwa na mahusiano na Kutu alipopokea taarifa alishtuka sana kujua kuwa Kutu alikufa kinyama kwa kuteketea kwa moto huku akijiona baada ya basi alilokuwa akisafiria kupata ajali na kusha kuwaka moto, tena katika hali isiyo eleweka abiria wote wa basi hilo waliwahi kutoka kwenye basi kasoro Kutu peke yake, ambaye alinasa kwenye basi na alichelewa kutoka hivyo akateketea kwa moto huku watu wakishindwa kumuokoa kutokana na ukali na ukubwa wa moto hivyo akafa akijiona. Johari alishtuka sana kwa taarifa ya kifo cha Kutu, alitetemeka na moja kwa moja alielewa huo ulikuwa ni mkosi.
Kama haikutosha waharifu wengine wawili wa kundi la mapanya walipata ajali mbaya sana na kufariki huku ndani ya wiki hiyohiyo waharifu watatu wa kundi la mapanya waliuwawa kinyama na maaskari walipokwenda kufanya uvamizi katika nyumba moja mitaa yenye ulinzi mkali. Waharifu wengine wakapotea hivyo Johari hakuwasikia wala kuwaona tena zaidi ya kuona matangazo kwenye vyombo vya habari wakitafutwa na ndugu zao.
Johari aliuelewa mkosi huo, kuwa ulitokana na Kutu kuua ile familia ya yule mfanyabiahara wa madini pamoja na familia yake. Ila kichwani mwake Johari alijiuliza sana mbona yeye hayamkuti ya kumkuta, na hivyo aliishi kwa hofu na wasiwasi. Ila hakupatwa na lolote japo ndoto aliendelea kuota ndoto za ajabu ajabu hadi usiku mmoja alipopata ndoto ya kutisha.
Usiku huo aliota akitembea na kukimbia kimbia katikati ya msitu mnene wa kutisha, akiwa na kiu, jasho likimtoka, nywele zikiwa zimemtimka, gauni lake likiwa chafu kwelikweli, huku akiwa kajawa na hofu, wasi na mashaka, na huku huku akisikia sauti za vilio na vicheko.
Mara akajikuta katokea nje ya msitu huo mnene ulioshonana na kuufikia uwanja mkuubwa. Katikati ya huo uwanja Johari aliona kuna watu wamekaa kwenye jamvi, wamevalia mavazi meupe. Walikuwa watu kama sita hivi.
Johari alipoangalia kwa makini aliona kuwa kumbe miongoni mwa wale watu walikuwamo yule mfanyabiashara aliyeuwawa, pamoja na mkewe na mabinti zao wawili, huku wakiwa pamoja na wanaume watatu wengine warefu sana na waliovalia mavai meupe.
Kwa hofu Johari alishindwa kuwakimbilia akabaki akiwaangalia hadi walipomuona na kunong’onezana jambo. Kisha moja kati ya wale wanaume watatu akainuka na kusimama na kumuelekea Johari huku uso kaukunja, alijongea hadi akamfikia, Johari alijikuta akiishiwa nguvu na kushindwa kusimama na kujikuta akipiga magoti mbele ya mwanamume yule.
Yule mtu alipomfikia Johari alisimama pembeni yake na kuanza kuongea kwa sauti ya kutisha, “Johari, Johari, binti mrembo uliyeingia kwenye majanga. Binti uliyekosa imani juu ya mungu wako akupaye riziki ukachukua maamuzi ya kujiunga na kundi la kiharifu ili kufanya maovu ulijiaminisha kuwa yangeweza kukuondolea ukata na kukuondoa kwenye lindi la umaskini”, aliongea mtu huyo huku mavazi yake meupe yakiwa yanang’aa hata yakaweza kuumiza macho ya Johari.
“Wezio wewe Johari, wezio wa kundi lenu la kiharifu, wamepata mikosi na kupoteza uhai wao na hakika nakwambia wao ni wa motoni. Hivi wewe muharifu unaweza kujua uchungu wa yule baba na mkewe kupoteza uhai na kuona mabinti zao wakiwa pamoja nao akhera?”, aliuliza huo mwanaume huku kaakimnyooshea Johari mkono awaone yule baba na mkewe na mabinti zake waliokuwa wamekalia kwenye jamvi pale kati uwanjani. Na kisha akaendelea kumwambia “Wewe Johari utabeba mzigo wa utasa, ujue uchungu wa kukosa mwana. Huo ndio utakuwa mtihani wako wa kukufunza kuwa na imani.Huo utakuwa ni mtihani ili kukurudisha katika mstari wa binadamu mtenda mema, nenda tenda kwa akili ikiwezekana tubu popote itapobidi na fanya toba, mungu atakusamehe na utakuwa miongoni mwa waja wema, ila ukiendekeza ubinafsi wako mikosi zaidi itakuwa yako”, alimaliza kuongea huyo mtu na kutoweka kisha wale watu wengine wote waaliokuwamo uwanjani wamekalia jamvi, akiwamo yule baba na familia yake wakatoweka pia. Baada ya kuamka toka kwenye ndoto hiyo, Johari hakuota tena ndoto mbaya mbaya. Ila kutokana na imani yake ndogo alipuuzia ndoto hiyo na hakutilia maanani nini hasa ilimaanisha kwenye maisha yake kuanzia wakati huo na akaendelea na maisha yake ya kawaida.
Baadaye Johari alihitimu elimu yake ya chuo kwa ufaulu wa alama za juu sana na hivyo akapata ufadhili wa kuendelea kusoma kwa ngazi ya ‘masters’ na kupata ajira, hivyo akabadilisha kabisa hali ya maisha yake na ya shangazi yake aliyeitwa Roda ambaye ndiye aliyemlea baada ya wazazi wake kufariki alipokuwa mdogo. Johari akaja kufahamiana na mtu aliyeitwa Malcom Munyisi na kupendana na kufunga ndoa. Kisha akajaliwa kupata nafasi muhimu ya kufanya kazi katika benki ya NIB, iliyokuwa moja ya mabenki makubwa nchini. Kwa ujumla maisha yake yalionekana yamekamilika, yaliyobarikiwa na mungu na ambayo kila mwanamke wa angeyatamani. Ila!, Johari aliishi katika ndoa na mumewe kwa miaka kumi pasina kupata mtoto, wala ujauzito wala dalili yeyote na ‘unukio’ wa ujauzito.
Johari alifahamu vizuri tatizo lake lilitokana na mkosi ‘aliojiokotea’ kutokana na maasi yake aliyotenda huko nyuma ila akiwa pamoja na mume wake walihangaika mahospitali kwa wataalam wa tiba za uzazi ambako tatizo lilionekana liko upande wake, tena tatizo lililowastaajabisha wataalamu kwa maana viungo na maumbile yake hayakuwa na kasoro yeyote ile iliyoeleweka kusababisha asishike ujauzito kwa sababu za kuelezeka.
Kadiri miaka ilivyokuwa ikienda Johari alizidi kuwa mwenye wasiwasi kuwa ipo siku eidha Malcom ama ndugu zake watazidiwa na hamu ya kuwa na mtoto kwenye familia na pengine hata kulazimisha ndoa yao kuvunjika, aliwaza sana juu ya jambo hilo na aliombea lisimtokee.
Kwa upande wa Malcom yeye alikuwa ni mtu mwenye mambo ya kizunguzungu, pengine ilitokana na maisha yake yaliyojawa na kwenda ulaya kila mara kila mwezi, hivyo yeye aliangalia tatizo la mkewe la kutopata ujauzito kama tu tatizo la kuendelea kulishughulikia na alizidi kuonesha mapenzi kwa mkewe. Ila sasa tatizo lilikuwa ni mama yake Malcom na mdogo wake wa kike aliyeitwa Snura, ambao wao walikuwa ni waongeaji na wenye mambo ya ukorofi sana.
Basi siku moja Malcom alimchukua Johari na kwenda nae kwao kwa mama yake kutembea. Siku hiyo walikuta kuna wajomba, baba wadogo, shangazi, mama wadogo wa Malcom wote wapo, kwa mshangao walioupata kwa kutotarajia uwepo wa ndugu wote hao, Malcom na Johari wakaambiwa kuwa hao ndugu wote walialikwa wajumuike siku hiyo kuzungumza mambo mbalimbali ya msingi ya kifamilia ikiwemo na kumshauri Malcom kwenye masuala muhimu ya kimaisha.
Wakiwa ndugu wote wamekaa chini ya mwembe nje ya nyumba ya kina Malcom, na Johari akiwa yuko hapo akijinyenyekeza mbele ya maongezi yao, mara mmoja wa wajomba wa Malcom akaanza kuongelea jinsi alivyojaaliwa kuwa na watoto watano wa kiume ambao aliwaita majembe na kuwasifu ni vidume hasa, na mara shangazi yake Malcom akadakia na kueleza jinsi ambavyo alijaaliwa kuzaa watoto saba na mwenyezi mungu na kushangaa hasa kwanini vijana wa kileo hawaelewi umuhimu wa kuwa na watoto mapema ilihali uhai ni mfupi.
Johari hakufurahia maongezi hayo aliona kabisa yanamsakama yeye na mumewe kwa kukosa mtoto.
Mara katikati ya mazungumzo hayo alifika binti mdogo, mzuri na aliyeonekana mpole na kuwaamkia kwa heshima na kujieleza kuwa kaja kumtembelea Snura, yani mdogo wa kike wa Malcom, mama Malcom kwa furaha sana alimkaribisha binti huyo na kumuelekeza aelekee huko nyuma ya nyumba kwenye jiko ambako Snura alikuwako akipika, na binti huyo akaelekea huko huku nyuma yake hapo chini ya mwembe ndugu zake Malcom walimtupia macho huku wakiwa na furaha na kuanza kumsifu.
Alianza baba ake mdogo Malcom kusifia, “kabinti kapoole, kazuuri, kanafaa kweli kuwa mke wa mtu ila laa!, vijana wetu wanaokoteza wanaacha mawari kama hawa mikoani”, akadakia mama ake mdogo Malcom, “tena kwa jinsi alivyo mpole binti huyu akiolewa wala hababaiki anazaa ‘fasta’, sio mijanamke mingine miaka dahali ‘no’ mtoto ‘no’ nini”, mama mdogo huyo aliongea kwa sauti. Maneno hayo yalikuwa wazi yakimlenga Johari. Mara akadakia mama ake Malcom, “Unajua enzi zetu mtu ukienda ukweni unafikia jikoni, unakaa huko unapika siku hiyo wakwe zako wanakula chakula ulichopika”, kisha akamuangalia Johari na wakaonana macho. Johari ikabidi ajibalaguze na kujiongelesha, “unajua mama mimi ni mpishi hodari tu sasa ngoja nika wakaangazie huko jikoni leo mle msosi niloupika mimi na mtaufurahia”, aliongea Johari na kujichekesha na kuinuka kwenda huko nyuma ya nyumba kulikokuwa na jiko, alijua lazima aondoke hapo ili kumuacha Malcom aongee na ndugu zake.
Hapo chini ya mwembe ndugu zake Malcom walimjiaa juu, wakimtamkia kuwa umri unaenda anahitaji mtoto, na kwamba kama mkewe hazai aachane nae aoe mwanamke mwengine. Malcom ambaye alijawa mambo ya kizungu, huku kavalia mawani yake, alikosa maneno ya kujibizana nao hao waswahili wa maneno akawekwa mtu kati wakimshambulia na kumuelimisha, aache ‘uboya’.
Wakati huo, huko jikoni alikokwenda kukaa Johari apike hapakuwa na amani, kwa maana Snura aligoma kupisha ‘mtu’ apike. Hivyo Johari akawa kakaa pembeni akimsaidia kupika kwa kumsogezea kopo la mkaa, mara amsogezee kopo la vitunguu na chumvi ama maji . Halafu mbaya zaidi muda wote Snura alikuwa anaongea na rafiki yake kana kwamba hawamuoni Johari, waliongea mambo yao ya kijijini ambayo Johari hakuweza kuchangia.
Ila kilichomuuma zaidi Johari ni pale alipokatiza kuku nje ya jiko hilo, kuku huyo mtetea alipita pamoja na vifaranga vyake. Basi Snura akaanza kumsifia huyo kuku, “Kuku si ndo huyu, kuku kuku kweli, kuku anatotoa vifaranga tunaona faida yake, mana raha ya kuku atotoe, sio kuku miaka nenda rudi kuku hatotoi, yani huyu kuku jinsi anavyototoa mfugaji anakupa raha ambayo hata binadamu mwengine hawakupi”, maneno hayo yalimuuma sana Johari pale alipoyaelewa maana yake, na alipoelewa kuwa kwa Snura, yule kuku ‘mdudu’ alikuwa na thamani kwa kutotoa kwake kuliko yeye Johari.
Ilimuuma hivi kwamba alilia njia nzima kwenye gari wakati yeye na Malcom wanarejea Dar es Salaam. Na Malcom alielewa kilichomliza mkewe, na safari hii alishindwa hata kumfariji, kwa maana hakuwa na pa kuanzia ndugu zake walifanya mambo ya kiroho mbaya bila kuficha safari hiyo.
Wiki nzima iliyofuatia Johari alikuwa mtu mwenye huzuni, na alijaribu kuficha hisia zake asionekane huzuni yake. Ila huzuni ilimtawala hivi kwamba bosi wake kazini alimuuliza baada ya kikao kimoja , kama ana tatizo lolote lililomtatiza, pia wafanyakazi wezie ‘walinotisi’ na kumuuliza kulikoni. Hadi mteja wa benki hiyo bwana Jama Bhanji ambaye alihudumiwa ‘private’ kwenye benki hiyo mara kwa mara na Johari alinotisi huzuni ya Johari na alimuhoji kulikoni alipoa sana.
Kwa kuwa Malcom alikuwa tayari keshaenda nje nchi kama kawaida yake -maana yeye Malcom alikuwa akifanya kazi wizarani kuhusu masuala ya mashirikiano ya kimataifa- Johari hakuwa hata na hamu ya kuwahi kwake, alibakia ofisini hadi jioni sana, katika ofisi yake hata kama alikuwa hana la kufanya alibaki kakodolea macho yake dirisha la kioo la ofisi yake iliyokuwa ghorofa ya nne ya jengo la benki hiyo ya NIB, hivyo akabaki hapo akiangalia jinsi giza lilivotua na majengo marefu ya mjini kati yakiwashwa taa ndipo aondoke kwenda kwake, huko mitaa ya Kijitonyama.
Aliwaza na kuwazua na hatimaye akafanya maamuzi kuwa, kwa kuwa kashahangaika sana kwenda mahospitali ya nchini na nje ya nchi basi suluhisho lililobaki ni kwenda kwa mganga wa kienyeji. Maamuzi yake yalifika huko kwasababu alifahamu fika tatizo lake lilitokana na kuhusika na kundi la kiharifu na kiuaji la mapanya. Na alifahamu fika kuwa wezie waliokuwa katika kundi hilo eidha walikufa kinyama ama kupotea, aidha Johari alielewa kuwa yeye pekee ndiye alliyesalia katika lile kundi la mapanya na kwamba kukosa kwake kupata ujauzito ni sehemu ya lana ya matendo yale maovu. Hivyo kwa imani kubwa aliamini mganga wa kishirikina ndiye angekuwa na msaada mkubwa sana kwake kwa tatizo hilo lake la muda mrefu.
Basi, siku moja wakati mumewe yuko nje nchi, bi. Johari alifunga safari ya mbali hadi katika kijiji kilichoitwa Sadani, kilichokuwa porini mbali kweli na kwenye kutisha. Huko alienda kumuona mganga. Mganga aliyekuwa mashuhuri, na watu toka kona zote za Tanzania nzima walienda kwa nguli huyo wa kishirikina kupata nusura ya matatizo yao.
Na Johari alipowasili tu kwa mganga huyo alikubali kuwa kweli alienda kwa mganga na sio matani. Kwanza palikuwa chini ya mti mnene na mkubwa wa mbuyu uliotisha na kufuka moshi, ulioning’inizwa vitambaa vyeusi na vyekundu na mahirizi makubwa makubwa yaliyotuna na kupumua. Johari aliingia kwa mganga huyo huku akitetemeka na kujifunga vizuri kanga zake alizovaa huku kaukumbatia mkoba wake alokwenda nao hapo. Mganga mwenyewe alikuwa pande la mtu, aliyejaa mahirizi na macheni ya mifupa ya wanyama na yale maganda ya konokono na viumbe wa baharini, usoni kajichora kwa maandishi meupe, huku akiwa kavalia kaniki na huku yuko kifua wazi.
Kabla hata Johari hajaeleza shida yake huyo mganga alimtolea macho makali sana Johari, macho makali kama ya chuki na kuanza kuongea, “Kweli leo umenijia wewe mwanamke mbaya. Hata waungwana unawapa mtihani, mizimu ya mababu zetu wa Sadani unawapa wakati mgumu kukupokea wakiwa wametulia, wanatetemeka kwa uovu ulioshuhudia na uovu wa watu uliojihusisha nao”, aliongea mganga huyo, na Johari alijikuta akiangausha chozi alielewa kuwa mganga kashafahamu maovu yote yanayomletea mkosi uliomfanya afike hapo mizimuni.
“Wewe mama unaitwa Johari Chande na mumeo anaitwa Malcom”, aliongea mganga na Johari kwa uchungu akaitikia, “tawile ‘baba’ angu ndio mimi, Johari”, na mganga akaendelea, “shida yako ni kupata mtoto, ila hupati kutokana na mkosi na nuksi ulizopata baada ya kuwa moja ya wafuasi wa kundi la kijambazi waliowahi kuua familia nzima na wewe ulikuwako siku ya tukio ukishuhudia”, aliendelea mganga huyo nguli, na Johari akaitikia, “tawile mganga”.
“Wezio woote, waliohusika wamepatwa na vifo vya kutisha na wengine kupotea, ila wewe walau umepewa utasa tu. Ila bado hujakubali unahaha kupata mtoto kama hivi kwa kututafuta waganga”, aliongea mganga huyo na kuangalia juu mawinguni, huku Johari akimtazama pia kwa hofu, kwa muda mganga huyo alibaki akiangalia mawinguni na ghafla akamgeukia Johari na kumkazia macho na kuendelea kuongea kuwa, waungwana wake, yani akimaanisha mizimu ya mababu zake wanampa hizo nguvu za kimiujiza wanayo dawa ya kutibu utasa wa Johari na kumsaidia kupata watoto, ila tatizo ni ugumu wa masharti, na mganga akamuuliza Johari kama yu tayari kufuata masharti magumu ya mganga. Na mganga akamsisitizia kuwa si jambo la kirahisi tu kukubali masharti hayo, na kwamba hatomtajia hayo masharti mpaka Johari ayakubali kwa moyo wote kabisakabisa kuwa vyovyote yatakavyokuwa hayo masharti kwa ugumu wake, yawe mepesi ama magumu kwelikweli shurti lazima ayatimize. Kuwa Johari ilimbidi akubali kutenda masharti kabla hajatajiwa na kuwa akishatajiwa basi hakuwa na jinsi ingine zaidi ya kuyatimiza. Johari alijikuta katika wakati mgumu sana, akawa kabaki kamtolea macho mganga. Hivi kweli akubali tu masharti kabla hajatajiwa, aliwaza, yakiwa magumu je itakuwa vipi ilihali ndio mganganga keshasema akimtajia sharti ayafanye hayo masharti.
Basi mganga akamuamuru Johari aondoke akatafakari ili kuamua kama yu radhi kutimiza masharti yeyote atakayopewa na mganga ama la. Na mganga akamwambia Johari kuwa akirejea tena aende na mbuzi wa kafara wa rangi yeyote ili walau kufidia vile vifo vya familia ile iliyouwawa na kundi la Mapanya, na pia aende na fedha zisizopungua milioni tano. Na akamsisitizia Johari kuwa iwe ni siri yake kati yake na mganga kuwa anatafutia hapo dawa ya kupata ujauzito. Na mganga akamsisitizia Johari tena kuwa akiwa anaondoka akumbuke kuwa, atakapoamua kurejea kwa mganga huyo, awe tayari kaamua kufuata masharti ya kiganga, na kumkumbusha kuwa siku akishamtajia masharti hayo basi Johari atakuwa kama aliyevulia nguo maji hivyo sharti lake ayaoge.
Baada ya kuondoka kwa mganga Johari alitafakari sana, kwanza alionywa asimwambie mtu hivyo hakuwa na mwengine wa kushiriki nae hayo mawazo yake, pili sasa alitafakari kuwa hadi wakati huo, hakuwa akiyajua hayo masharti ya mganga, ila mganga alimuambia kuwa siku akienda tena na akatajiwa hayo masharti ni lazima ayakubali bila ya kuyakataa, hivyo Johari aliwaza kuwa lazima afikie mkataa na kuamua hasaa kufuata masharti ya mganga.
Johari aliwaza sana itakuwa vipi kama masharti ni magumu mno, ila kichwani mwake zikamjia picha akicheza na watoto wake ambao pengine mganga angemsaidia kuwapata, pia aliona jinsi Malcom angefurahia uzao huo na mkewe, hivyo Johari akaamua kuwa ataenda tena kwa mganga na kukubali masharti atakayopewa yawe magumu kwa vyovyote vile, yeye atakuwa yu radhi na tayari kuyafanya.
Basi siku ikawadia na Johari akaelekea tena huko kijiji cha Sadani kwa mganga. Na siku hiyo alienda na mbuzi mweusi na pesa taslim ambazo mganga alimwambia aende nazo.
Mganga alimtakia Johari kuwa ni mwanmke jasiri sana kwa kurejea tena kukabiliana na masharti magumu ambayo angemtajia. Basi mganga akamchinja yule mbuzi na kutoa kama kafara kwa mizimu ya mababu zake.
Kisha akaanza kumpa masharti Johari na kumuambia kuwa, namna pekee ya Johari kupata watoto ni kuzaa na kichaa, yani mwehu, mwendawazimu wa akili, mwanamume aliyechizi kabisa muokota makopo.
Johari alishtuka sana. Alishtuka kwa maana hakutarajia sharti hilo hata kidogo. Ila mganga akamsisitizia kuwa hiyo ndio njia pekee ya kwake Johari kuweza kupata watoto vyenginevyo, asahau uzao. Na mganga kwa hasira alimkumbusha Johari kuwa masharti hayo ni lazima ayafuate, kwamba sasa ilikuwa ni lazima kwa Johari kumtafuta chizi muokota makopo na kulala nae ili azae na huyo chizi na kwamba Johari hakuwa na chaguzi tafauti na kulitekeleza sharti hilo ‘la aina yake’ alilompa.
Huo ulikuwa ni mtrihani mkubwa kwa Johari. Hakufikiria kabisa kuwa mganga angeweza kumpa sharti kama hilo. Njia nzima akiwa anarejea Dar machozi yalimtirirka akiwaza wapi atapata mtu chizi, na ‘atamkovisi’ vipi chizi hadi alale nae na aliwaza sana kuwa ikigundulika ‘mishe’ yake hiyo ya kutembea na wehu wa akili waokota makopo, ili apate watoto kama masharti ya mganga yatakavyo, uso wake ataufichia wapi, na alifikiria sana kwanini yeye Johari mfanyakazi wa benki kubwa kama NIB na mke wa Malcom Munyisi, mtu tajiri na alojaa uzungu uzungu, mfanyakazi wizarani, kwanini yeye ilimlazimu kulala na machizi ili kuzaa. Ila alikumbuka kuwa ni maovu yake yanyomtafuta na kumkimbiza, yakimfuatilia kama kivuli kila aendako.
........................
Malcom aliporejea toka nje ya nchi na kutembelea kijijini kwa mama yake, ndugu zake walimjia juu zaidi na safari hiyo wakamwambia kuwa wamemtafutia mchumba hivyo kazi yake ilikuwa kumuacha tu Johari na kumuoa huyo mwari mpya wa uhakika wa kuleta mtoto katika familia yao ya akina Munyisi.
Na Malcom hakuficha kitu kwa mkewe akamwambia alichoambiwa na ndugu zake, mama zake wadogo, mashangazi na wajomba, kuwa katafutiwa mchumba. Mbaya zaidi sasa kwa Johari huyo mchumba aliyetafutwa akaanza kumpigia simu Malcom. Hivi kwamba wakati mmoja Johari alipokea moja ya simu hizo na kumtukana sana huyo mwanamke.
Basi, siku moja Johari alikuwa kampitia mfanyakazi mwezie aliyeishi maeneo ya huko Mbezi Beach, ili waende mahala. Johari akiwa kakaa kwenye gari lake akimsubiri huyo mwezie atoke, mara akamuona mwanamume mmoja aliyevalia rafu sana, nywele zimetimka, yuko peku, akikatiza mbele ya gari lake akielekea mbele ya duka la rejareja lililokuwa mtaa huo. Moja kwa moja Johari alielewa huyo mtu alikuwa ni chizi mwendawazimu muokota makopo. Na akabaki akimtazama jinsi yule chizi alivyokuwa akifanya uchizi wake na mambo ya hovyo akielekea kwenye duka la mtaa.
Johari aliona jinsi, watu waliokuwa wamekaa wakianza kumcheka yule chizi. Na mara muziki ukasikika toka ndani ya duka. Na yule chizi akaanza kucheza huo mziki kwa furaha kabisa na wale wa dukani wakaendelea kumshangilia na kumcheka sana, walimgeuza kituko chao. Johari mwenyewe alijikuta akicheka vituko ambavyo yule chizi alikuwa akifanya kwa ‘kusakata’ muziki.
Mara rafiki yake aliyekuwa akimsubiri aliingia kwenye gari na kukaa kwenye kiti cha pembeni ya Johari huku akiomba radhi kwa kumchelewesha.
Na Johari aliondoa gari eneo hilo kuelekea kwenye safari yao waliyokuwa wakielekea. Walipokuwa njiani Johari alimuuliza rafiki yake juu ya yule chizi aliyekuwa akicheza mziki, na rafiki yake akamwambia kuwa yule mtu ni kichaa kabisa muokota makopo ambaye huzururazurura mitaani kwao na kuwa aliishi kwenye boma la nyumba ambayo haijakamilika jirani kabisa na pale palipokuwa na duka. Na kwamba hakuna mtu aliyefahamu yule chizi anaitwa nani, ama ndugu zake ni akina nani na wapi ama kwa namna gani aliupata uchizi, ila watu walipenda tu kumuona akicheza muziki na kumgeuza kituko chao na kumcheka.
Johari alisisimka mwili wake kusikia habari za yule chizi. Alianza kufikiria sana kichwani mwake kuwa huenda kapata aina ya chizi sahihi ambaye angefaa katika kutimiza masharti aliyopewa na mganga ili alale nae na kupata ujauzito. Aliwaza sana Johari na kujiapia kuwa lazima amchunguze yule chizi vizuri ili amjue tabia zake na kuelewa namna gani atamuingia na kumshawishi hadi afanye nae tendo la ndoa.
Na kweli, Johari alifanya uchunguzi wake na akapajua yule chizi alipokuwa akilala, aina ya taka alizokuwa akila na zuri zaidi alilofurahia ni kuwa chizi yule hakuwa na tabia ya kupiga watu. Johari alidhamiria kabisa kuwa lazima alale na chizi yule.
Usiku mmoja baada ya chunguzi zake kwisha, Johari alimfungia safari yule chizi. Ilikuwa ni usiku wa manane, Johari alifika kwenye boma la nyumba ambayo haikukamilika ambako yule chizi alilala. Kwa hofu Johari aliingia hadi ndani ya boma hilo na kumkukuta yule chizi kalala. Kwa muda kidogo Johari alimmulika kwa tochi na kumtazama na Kuona jinsi alivyokuwa mchafu na kulala kwenye udongo na nyasi za boma hilo tena harufu ya uchafu wa mwili wa chizi huyo ilitapakaa boma zima, hakika Johari alihisi kinyaa.
Mara yule chizi akaamka kutokana na mwanga wa tochi ambao Johari alimmulika nao. Na chizi yule alishtuka sana kwa maana hakuzoea ugeni bomani humo, hasa usiku manane. Johari mwenyewe alipoona yule chizi anaamka alishtuka hakujua yule chizi angewaruka kwa mtindo gani baada ya kumuona humo bomani.
Basi Johari ambaye mkononi alikuwa kabeba mfuko wenye machungwa, aliingiza mkono mmoja mfukoni na kutoa chungwa na kuanza kula kwa kumringishia chizi yule. Mara yule chizi akamvamia Johari na kumpokonya mfuko wa machungwa aliobeba na lile chungwa alilokuwa akimlingishia kisha, yule chizi akaenda kujikunyata na kula yale machungwa haraka haraka. Wakati huo Johari alikuwa kamtolea macho yule chizi. Kwanza hadi wakati huo Johari alijiona jasiri sana kufika katika boma hilo na kendelea kuwamo humo usiku huo wa manane pamoja na huyo chizi. Ila sasa Johari alifikia ukomo wake wa kufikiri hakuelewa ataanzaanza vipi kuhamsha hisia za chizi, hivi kwamba wafanye tendo la ndoa humo bomani na yeye mwenyewe alijiwazia sana ‘msambwanda’ na mtu chizi hufanania vipi, kichwani mwake, Johari alikuwa na mawazo kama alfu hivi, aliwaza kama akifumwa bomani humo na chizi usiku huo watu wangemchukiliaje.
Basi yule chizi baada ya kumaliza kula yale machungwa, ghafla akatulia na kumtizama Johari. Alimtazama kwa kutulia kabisa kama mtu mzima na timamu awezavyo kumuangalia mtu mwezie akiwa katulia, hadi Johari akastaajabu sana. Alistaajabu kwa jinsi ile yule chizi alivyotulia. Yule chizi alimungalia Johari machoni moja kwa moja na kutulia kabisa kama vile hakuwa na kawehuka kichwani.
Kumbe yule chizi alitulia vile kutokana na uzuri aliokuwa nao Johari. Alimuona Johari kuwa ni mrembo sana. Pamoja na uchizi wake alitambua kuwa hakuwahi kuona mwanamke mzuri kama Johari. Yule chizi alimuangalia Johari hadi machozi yakaanza kumlenga na kuona haya akageukia pembeni.
Johari hakutarajia kuwa mtu chizi anaweza kutulia namna hiyo, akabaki kaduwaa. Ila sasa aligundua kuwa, kama yule chizi aliweza kutulia namna ile basi kazi yake ilompeleka bomani mule ilikuwa nyepesi sana.
Mara moja Johari akavua na kuangusha nguo zake alizovalia mwilini na kumfuata yule chizi, ambaye nae alipomuona Johari yuko utupu alishtuka sana. Pamoja na uchizi wake alitambua kuwa si kawaida kwa mwanamke kuwa utupu. Johari akamsogelea.
Nia ajabu ilioje hadi wakati huo kile kinyaa alichokuwa akiona Johari kilimtoka kabisa na hakukisikia, hadi wakati huo alilenga tu kulala nae tu yule mwendawazimu.
Katika hali ngeni kabisa kwa yule chizi, alijikuta kasisimka sana na mara Johari alikuwa juu yake. Naam!, kilichotendeka hapo ilikuwa ni starehe ambayo chizi yule hakuwahi kuipata. Ilikuwa ndio mara ya kwanza kwa yule chizi kufanya tendo lile la aina yake na kwa Johari ilikuwa ndio mara yake ya kwanza kufanya vile na mataahira, yani ni kama walijiondoa ubikira kila mmoja wa aina yake, khatari!.
Johari akawa kafanikiwa lengo lake la kulala na chizi. Na usiku huo aliporejea kwake alikesha bafuni akioga akiwa haamini namna alivyofanikisha lile tendo na yule chizi. Hakuamini kama kweli msomi kama yeye alifanya alichokifanya, hakuamini kuwa yeye alikuwa ni jasiri wa kufanya kitu kama kile wakati aliona kuwa ni sharti zito sana pale alipotajiwa na mganga kuwa afanye vile, na ajabu aliona kuwa mbona ilikuwa na kauwepesi kidogo katika kutekeleza kuliko alivyokuwa akifikiria ugumu wake. Na alijishangaa na kujiuliza kinyaa chake cha kulala na chizi mchafu, anukae asieoga kilienda wapi muda wa tendo. Ni maswali mengi aliyojiuliza na akakosa majibu kichwani mwake.
Basi, maisha yaliendelea na wiki chache tu mbele Johari alianza kupata dalili ambazo hakika yeye aliamini ni ujauzito. Na hata alipokwenda kumuona daktari majibu yalionesha hivyo kuwa alikuwa ni mjamzito. Ilikuwa ni furaha sana kwa Malcom, kwa maana alishamkatia tamaa mkewe, Malcom hakuwa akitarajia kama mkewe angeweza kuleta kiumbe duniani, ilikuwa ni miujiza kwenye ndoa yao.
Ndugu zake Malcom walistaajabishwa sana na taarifa hizo, hawakuamini hata kidogo. Walijiuliza sana iwaje mgumba kapata ujauzito. Miezi tisa baadae, Johari alijifungua mtoto wa kiume, na kwa furaha Malcom akamuita mtoto huyo, Miujiza, kwa maana alikuwa ni muujiza kwa familia yake. Sasa mama yake Malcom, mdogo wake Malcom na ndugu wengine wakajikuta wana mapenzi ya dhati na Johari na kusahau viroja walivyokuwa wakimtendea. Sasa safari hiyo, Johari nae akawa anawaletea nyodo za ‘kimtindo’ za waziwazi katika kile kiitwacho kutesa kwa zamu, sasa Johari alionesha dhahiri kutopenda mtoto wake ashikweshikwe na ndugu wa mumewe na kujifanya mtoto wake anamlea kizungu sana na si kiswahiliswahili kama ndugu wa Malcom aliowachukulia kuwa hawana elimu walivyotaka kujishirikisha kwenye malezi ya mtoto.
Johari alikuwa ndiye mwenye furaha zaidi baina ya wote waliofurahia kuzaliwa kwa Miujiza. Yeye kama mama alifahamu shuruba na masharti aliyopitia na kutimiza ili kumpata mtoto wake. N akichwani mwake Johari akawa kafikia mkataa mwengine kuwa lazima atembee tena na yule mwanamume chizi ili apate mtoto mwengine wa pili.
Kwake yeye Johari kutembea na yule chizi ilikuwa ni jambo rahisi sana, kwa maana Malcom alikuwa ni mtu mwenye kusafiri safiri sana kwenda nje ya nchi, hivyo Johari aliweza kuwa na uhuru wa kuamua kuchelewa kurudi nyumbani na kufanya lolote huko mitaani, ikiwemo kulala na machizi, bila ya kuhofia kujulikana na mtu yeyote wala kumtia wasi Malcom.
Baada ya mwaka mmoja kupita, Johari, kwa awamu ya pili alirejea bomani kwa yule chizi. Na safari hiyo Johari alishangazwa kugundua kuwa yule chizi alimkumbuka vyema. Kwa maana safari hiyo ya pili, yule chizi alipomuona tu Johari machozi yalimdondoka toka kwenye macho yake hadi Johari mwenyewe akajikuta machozi yakimdondoka, hata bila ya kuelewa yule kichaa alilia nini kwa kumuona yeye Johari. Kumbe yule chizi alilia kwa mapenzi. Alimkumbuka vizuri Johari na urembo wake, na toka usiku ule wa mara ya kwanza wafanye tendo bomani yule chizi alimkumbuka na kumuwazia.
Kwa namna hiyo, hiyo safari hiyo ya mara ya pili ilikuwa rahisi zaidi kwa Johari kumuingia chizi huyo na kulala nae , kwasababu chizi mwenyewe alikuwa kaingia ‘laini’, yani haleti papara, ‘mzigo’ kauelewa na picha alijua kulicheza, na chizi yule alikuwa na hamu kweli ya kulala na Johari.
Hivyo Kama kawaida kwa maraya pili mambo yalitiki tena kwa Johari. N kweli akapata ujauzito na kuzidi kumfurahisha Malcom na ndugu zake.
Na miezi tisa baadae akajifungua, safari hiyo alijifungua watoto mapacha wawili, wasiofanana, wa kike na wa kiume, na kuzidisha furaha maradufu kwenye familia hiyo ya Malcom na ndugu zake ya akina Munyisi.
Johari alifurahia sana mafanikio ya mchezo wake mchafu. Na akafurahi pia kuwa hana haja ya kuuendeleza kwasababu watoto watatu walimtosha sana yeye na Malcom. Hivyo Johari alijiona ni shujaa aliyeweza pambana na lana ya uovu aliowahi kuufanya na kuushinda. Na nyodo zake kwa ndugu wa Malcom zikazidi maradufu hadi wakajutia madhira waliyomfanyia. Kwanza Johari watoto zake hakutaka mtu awaguse, aliwalea kama kitu gani sijui!, aliwalea kama ‘maprince’ na ‘princess’. Ndugu wote kimdomomdomo ‘kikawakatika’ wakabaki kuangalia malezi ya kiulaya ulaya.
...................................
Basi miaka ikaenda, na kichwani mwake Johari akamsahau kabisa yule chizi utadhani hakuwahi kutokea kwenye maisha yake kutembea na mtu chizi, yeye aliwaza furaha yake na Malcom na watoto wao watatu, Miujiza, Flora na Florian. Kwake watoto walikuwa ni wa Malcom sio mtu chizi. Hakuwa hata na haja ya kujua yule mtu aliishia vipi maisha yake, hakuwa na umuhimu wowote kwake. Kwake kilichokuwa umuhimu ilikuwa ni furaha ya familia yake na mumewe.
Na kweli hakuna kilichowabughudhi tena familia yao, kwa upande wao. Waliishi kwa raha mustarehe. Ila sasa mikasa ikawa upnde wa yule chizi.
Wakati Johari, alisahau juu ya yule chizi, kwa upande wa yule chizi haikuwa hivyo. Kwa upande wake alimuwaza Johari kwa mapenzi makubwa.
Pamoja na uchizi wake, aliikumbuka vizuri sura ya Johari, harufu yake, sauti na miguno yake na hasa alikumbuka uzuri wake. Na alimuwaza sana na ‘kummiss’ sana. Alipokuwa akilala alimuota Johari. Mara nyengine alihisi Johari kamsimamia pembeni na kuamka kwa furaha kumkumbatia na kumkaribisha bomani kumbe hakukuwa na Johari bali mawazo yake tu ya kichizi. Na alipogundua kuwa Johari hakuwa akija tena bomani yule chizi alikuwa akilia. Haikuwa kawaida, siku moja alikatiza mbele ya duka moja la mtaani na akasikia wimbo wa mapenzi ukipigwa redioni. Wimbo ambao ulikuwa na mashairi ya mtu aliyemkosa mpenzi wake, na uliokuwa na ‘tune’ ya kusikitisha ikionesha huzuni ya mapenzi, kwa hali ya kushangaza kabisa yule chizi alitoa ‘mchozi’ na kulia, na kushindwa kuendela na safari zake za kichizi na akakaa chini kulia kwa uchungu. Watu waliomuona walishangazwa sana na kumjaalia na kumuwazia iwaje mtu taahira ashikwe na hisia kali za wimbo wa mapenzi toka redioni hivi kwamba atoe machozi.
Hali ilikuwa ya namna hiyo kwa yule chizi. Na hivyo ndivyo maisha yake ya uchizi mitaani yalivyoendelea. Huku watu wakiwa hawamjui alikuwa ni nani hasa, hakuna liyejua jina lake wala asili yake, ilionekana mungu kampangia maisha yake yawe ya uchizi na uzururaji.
Itaendelea.............................................................
Ndani ya chumba alichokuwa akielekea mlikuwamo na bwana Jama Bhanji, ambaye alikuwa mfanyabiashara maarufu na mtu tajiri sana na aliyekuwa miongoni mwa wateja wakubwa kabisa wa benki ya NIB. Hivyo Johari alikuwa anaelekea kwenye mazungumzo na kumhudumia mteja mkubwa wa benki. Ndani ya hicho chumba bwana Jama Bhanji alikuwa kashikilia kikombe cha kahawa akiwa anainywa taratibu, huku macho yake kayarushia kwenye runinga ya kisasa iliyokuwamo ndani ya chumba hicho na ambayo kwa wakati huo ilirusha taarifa ya habari na wakati huo kiyoyozi kilipulizia hewa ya ubaridi kwenye chumba. Mara tu Johari alipofungua mlango wa chumba hicho na kuingia bwana Bhanji alitoa macho yake toka kwenye runinga na kumtazama Johari aliyeingia ndani ya chumba hicho, huku akiwa kajaza tabasamu usoni, akionekana nadhifu kwa suti aliyovalia.
Kwa bashasha Johari aliongeza tabasamu la uso wake na kuelekea kukaa kwenye kochi lililotazamana na kochi alilokaa bwana Bhanji, kisha akamkaribisha na kumwambia jinsi benki yao ya NIB ilivyo na furaha kuendelea kumhudumia mtu wa muhimu katika uwekezaji nchini. Maongezi yao yalihusisha mapitio ya faida za gawiwo ambazo bwana Bhanji alizipata kutokana na kuwekeza kwenye makampuni na miradi mbalimbali ambayo benki ya NIB ilimshauri mfanyabiashara huyo awekeze. Kwenye kikao hicho bwana Bhanji alijawa na furaha sana kwa maana miradi yote liyoshauriwa awekeze na watu wa benki hiyo ilikuwa imemuingizia faida nyingi sana na hivyo akamuahidi Johari kuwa ataendelea kutumia huduma za benki yao ya NIB na kufuata shauri za benki hiyo juu ya masuala ya uwekezaji.
Kikao cha siku hiyo na bwana Bhanji kilienda vizuri sana hivi kwamba Johari alisifiwa na wafanyakazi wezie na viongozi wake kazini kwa kuweza kushughulika na wateja wakubwa wakubwa wa benki hiyo, wateja ambao walikuwa wa hadhi kubwa na kila benki iliwalilia na kufanya jitihada kuwapata.
Johari alijawa na furaha na kujiona mwenye bahati na akili nyingi kwa kuweza kufanya kazi na kushughulika na watu wa hadhi ya juu. Alijivunia sana moyoni.
Kwa hakika Johari alikuwa ni mwanamke mwenye bahati sana. Alikuwa msomi, mrembo, mnyenyekevu, aliyependwa na watu kila mahala,maofisini, majirani na koote alikokwenda alipendwa, alikuwa na uwezo mkubwa kwa maana kazi yake ya benki ilimlipa vizuri na kumpa heshima. Na pia Johari alikuwa keshaolewa, na alimpenda sana mume wake ambaye aliitwa Malcom Munyisi. Malcom alikuwa akifanya kazi katika wizara ya mambo ya nje, kazi ambayo ilimfanya asafiri sana kwenda nje ya nchi katika nchi za ulaya, arabuni, uchina na hata amerika, Johari alifurahia sana kazi hiyo ya Malcom.
Hakika Johari alionekana mwenye bahati sana kwa wakati huo. Ila!, kama inavyosemekana miongoni mwa waswahili ya kuwa hakuna kizuri kisicho kasoro, basi ndivyo vivyo hivyo ilivyokuwa kwa Johari Chande Munyisi.
Na kichwani mwake Johari aliwaza sana mambo yaliyomtia kasoro. Pamoja na furaha zake na bahati zake alizo kirimiwa na mwenyezi mungu, katu hayakutoka kichwani mwake mambo yaliyomtia kasoro na aliyawaza sana.
Mambo yenyewe yaliyomtia kasoro yalianza kama miaka kumi na nne kabla ya wakati huo. Enzi ambazo Johari alikuwa binti yatima, mwenye maisha magumu ila binti aliyekuwa kajawa akili hivi kwamba alipata nafasi kujiunga na chuo kikuu.
Kwa ugumu wa maisha aliokuwa nao Johari kipindi hicho alichokuwa akisoma, alijikuta akiingia kwenye mahusiano na kijana mtukutu aliyeitwa ‘Kutu’. Kutu alimpenda sana Johari na alimpa kila kitu. Na akawa akimshawishi Johari ajiunge na kundi la kiharifu la kivamizi lililoitwa ‘mapanya’. Johari katu hakukubali kujiunga na kundi hilo la kiharifu.
Basi ikafika siku moja ambayo Johari alitimuliwa chuo na kuambiwa kuwa hatofanya mitihani ya mwisho wa ‘semester’ hadi atakapolipia ada ya chuo. Kitendo hicho kilimuuma sana na kumtia hasira, hivyo akafanya maamuzi mazito ya kuamua kujiunga na kundi la kiharifu la ‘mapanya’, ikiwa kama njia yake ya kujinasua toka kwenye ukata.
Hivyo kwa msaada wa bwana ake, Kutu, Johari alifanikiwa kujiunga na kundi hilo la kiharifu. Na akiwa ndani ya kundi hilo, haraka sana Johari alipata ada ya kulipa chuo na pesa nyingi za kufanyia mambo mengine. Na akawa mshirika mkubwa wa waharifu wa kundi hilo, ambalo lilifanya uharifu katika maeneo mbalimbali kwa kupora, kukaba na kuibia watu na kusaidia usambazaji wa madawa haramu ya kulevya.
Johari aliona kila kitu kinaenda sawa kwa kushiriki kwake kwenye uharifu wa kundi la ‘mapanya’. Mpaka usiku mmoja mambo yalipoanza kwenda kombo baada ya kuvamia nyumba ya mfanyabiashara mmoja wa madini mwenye asili ya kieshia.
Katika usiku huo mnene wa manane, kundi la ‘mapanya’ wakiwa wamevalia vinyago usoni, na silaha za bunduki, masime na mapanga, walivamia nyumba ya mfanyabiashara wa madini na vito vya thamani. Walifika na gari yao aina ya ‘Noah’, wakiwa kundi kubwa sana na waliojipanga wakiwa na uelewa wa ramani nzima ya nyumba ya mfanyabiashara huyo na walikuwa wakifahamu kila mahala ambapo vitu vya thamani vilikuwa vimefichwa kwenye nyumba mfanyabiashara huyo, tena walikuwa na funguo zao wenyewe za milango ya kila kona ya nyumba hiyo.
Bila huruma kundi la mapanya walimshushia mfanyabiashara huyo kipigo kikali mbele ya familia yake na kisha kuanza kupekua kila walipofahamu pana vitu vya thamani na kuanza kuchukua vitu hivyo.
Johari akiwa miongoni mwa waharifu wa kundi hilo la ‘mapanya’, tena mtoto wa kike pekee kundini, alishiriki vyema katika tukio hilo la kikatili. Na alishuhudia jinsi waharifu wezie walivyo mdhalilisha yule mfanyabiashara na mkewe mbele ya mabinti zao wawili. Alishuhudia jinsi yule mfanyabiashara na mkewe na mabinti zao walivyolazimishwa kulala kifudifudi kwenye sebule ya nyumba yao na kuzuiwa kutoa kelele za aina zozote na kupewa vitisho vya kukatishwa maisha dakika yeyote watakayo neng’eneka kwa namna yeyote ile. Mfanyabiashara wa watu alikuwa hoi kagalagazwa sakafuni, damu zikimtoka mdomoni na puani, alikuwa kakosa kabisa la kufanya zaidi ya kulia shahada kwa sauti ya chini, “la ilaha illa llah, la ilaha illa llah”, huku akiomba waharifu wabebe kila walichoona kinawafaa na kuondoka. Johari aliyekuwa kavalia kinyago alimuangalia mzee huyo na kuona jinsi alivyolia kwa mungu wake na kuwalilia wao, na mara akamuona Kutu akitoa bunduki na kumnyooshea mzee huyo na familia yake ili awaue.
Hapo sasa Johari alijikuta akiingiwa na huruma kidogo na akamuomba Kutu amwache mzee huyo na asimuue. Kutu ambaye alikuwa ni muharifu sugu alimtazama Johari na kuangua kicheko cha kishetani shetani kisha akafyatua risasi toka kwenye bunduki hiyo na kumuua mzee huyo. Hivyo Johari akashuhudia mzee huyo wa watu jinsi ambavyo risasi ilitawanyisha kichwa chake na kumpoteza uhai ndani ya sekunde, huku mke wa mzee huyo na mabinti zao wakishuhudia na walishindwa kujizuia na wakatoa ukelele wa kilio. Mara Kutu akawafyatulia risasi wote, huyo mama wa kiarabu na mabinti zake wawili na kuwaua.
Johari sasa hata kinyago akakivua hakuamini alichoshuhudia kikitendwa na Kutu. Johari alijikuta akitetemeka kwa kuogopa alichokiona. Macho yalimtoka na akajikuta kamvamia Kutu na kumhoji kwa hasira umuhimu hasa wa kuwaua yule mama na mabinti zake pamoja na baba yao mfanyabiashara. Kutu akamtazama Johari kwa jicho la ukali sana na kisha akamnyooshea bunduki na kumuwekea kichwani. Johari alikuwa na hasira sana wakati huo, hata hakuogopa hiyo bunduki aliyowekewa kwenye paji la uso. Tena wakati huo Johari mwenyewe alikuwa na bunduki yake mkononi. Mara wale waharifu wengine ambao hawakushtushwa na kilichotendwa na Kutu walikuwa washamaliza kubeba vitu vya thamani vya ndani ya nyumba hiyo, hivyo wakaamrisha Kutu na Johari waache upumbavu wao na kuamuru kuwa wote waondoke haraka toka kwenye nyumba hiyo. Hivyo wote wakiwamo Johari na Kutu walitoka nje haraka na Kurukia kwenye ‘Noah’ yao na ‘kuondoka’ pamoja na pesa na vito vya thamani walivyoiba.
Usiku wa siku hiyo na wiki kadhaa zilizofuatia Johari alishindwa kulala kabisa kwa maana kila mara alipolala ilikuwa lazima aote juu ya ile familia aliyoshuhudiwa ikiuwawa na Kutu. Kwenye ndoto moja, aliota wanawake watatu waliovalia mavazi meupe na kujifunika hijabu wamelala kifudifudi kwenye sakafu huku damu zikiwavuja toka vichwani mwao na kuchafua nguo zao nyeupe, aliota akihangaika kuwapindua ili aone sura zao na kujua ni akina nani, ila ghafla waliamka wenyewe na kumtazama na aliona sura zao ni zile za yule mama na mabinti zake wawili waliouwawa na Kutu. Kila mara taswira za yule mama na mabinti zake zilimjia, mara nyingine aliota wakimlilia kwa uchungu mwingi, mida mingine alilala akahisi wapo nje ya dirisha la chumba chake wakimlilia. Kila mara Johari aliisikia sauti ya yule mzee aliyokuwa akiitoa muda mchache kabla hajauwawa, aliyasikia maneno ya shahada ya yule mzee, alisikia “la ilaha illa llah, la ilaha illa llah”, alisikia sauti hiyo ikianza kidogo na kisha kupanda na mara ikawa inageuka na kuwa kilio kikubwa cha mzee yule akimlilia.
Kama hiyo haikutosha, miezi michache baadae, Kutu alihusika katika ajali mbaya sana. Johari ambaye alikuwa na mahusiano na Kutu alipopokea taarifa alishtuka sana kujua kuwa Kutu alikufa kinyama kwa kuteketea kwa moto huku akijiona baada ya basi alilokuwa akisafiria kupata ajali na kusha kuwaka moto, tena katika hali isiyo eleweka abiria wote wa basi hilo waliwahi kutoka kwenye basi kasoro Kutu peke yake, ambaye alinasa kwenye basi na alichelewa kutoka hivyo akateketea kwa moto huku watu wakishindwa kumuokoa kutokana na ukali na ukubwa wa moto hivyo akafa akijiona. Johari alishtuka sana kwa taarifa ya kifo cha Kutu, alitetemeka na moja kwa moja alielewa huo ulikuwa ni mkosi.
Kama haikutosha waharifu wengine wawili wa kundi la mapanya walipata ajali mbaya sana na kufariki huku ndani ya wiki hiyohiyo waharifu watatu wa kundi la mapanya waliuwawa kinyama na maaskari walipokwenda kufanya uvamizi katika nyumba moja mitaa yenye ulinzi mkali. Waharifu wengine wakapotea hivyo Johari hakuwasikia wala kuwaona tena zaidi ya kuona matangazo kwenye vyombo vya habari wakitafutwa na ndugu zao.
Johari aliuelewa mkosi huo, kuwa ulitokana na Kutu kuua ile familia ya yule mfanyabiahara wa madini pamoja na familia yake. Ila kichwani mwake Johari alijiuliza sana mbona yeye hayamkuti ya kumkuta, na hivyo aliishi kwa hofu na wasiwasi. Ila hakupatwa na lolote japo ndoto aliendelea kuota ndoto za ajabu ajabu hadi usiku mmoja alipopata ndoto ya kutisha.
Usiku huo aliota akitembea na kukimbia kimbia katikati ya msitu mnene wa kutisha, akiwa na kiu, jasho likimtoka, nywele zikiwa zimemtimka, gauni lake likiwa chafu kwelikweli, huku akiwa kajawa na hofu, wasi na mashaka, na huku huku akisikia sauti za vilio na vicheko.
Mara akajikuta katokea nje ya msitu huo mnene ulioshonana na kuufikia uwanja mkuubwa. Katikati ya huo uwanja Johari aliona kuna watu wamekaa kwenye jamvi, wamevalia mavazi meupe. Walikuwa watu kama sita hivi.
Johari alipoangalia kwa makini aliona kuwa kumbe miongoni mwa wale watu walikuwamo yule mfanyabiashara aliyeuwawa, pamoja na mkewe na mabinti zao wawili, huku wakiwa pamoja na wanaume watatu wengine warefu sana na waliovalia mavai meupe.
Kwa hofu Johari alishindwa kuwakimbilia akabaki akiwaangalia hadi walipomuona na kunong’onezana jambo. Kisha moja kati ya wale wanaume watatu akainuka na kusimama na kumuelekea Johari huku uso kaukunja, alijongea hadi akamfikia, Johari alijikuta akiishiwa nguvu na kushindwa kusimama na kujikuta akipiga magoti mbele ya mwanamume yule.
Yule mtu alipomfikia Johari alisimama pembeni yake na kuanza kuongea kwa sauti ya kutisha, “Johari, Johari, binti mrembo uliyeingia kwenye majanga. Binti uliyekosa imani juu ya mungu wako akupaye riziki ukachukua maamuzi ya kujiunga na kundi la kiharifu ili kufanya maovu ulijiaminisha kuwa yangeweza kukuondolea ukata na kukuondoa kwenye lindi la umaskini”, aliongea mtu huyo huku mavazi yake meupe yakiwa yanang’aa hata yakaweza kuumiza macho ya Johari.
“Wezio wewe Johari, wezio wa kundi lenu la kiharifu, wamepata mikosi na kupoteza uhai wao na hakika nakwambia wao ni wa motoni. Hivi wewe muharifu unaweza kujua uchungu wa yule baba na mkewe kupoteza uhai na kuona mabinti zao wakiwa pamoja nao akhera?”, aliuliza huo mwanaume huku kaakimnyooshea Johari mkono awaone yule baba na mkewe na mabinti zake waliokuwa wamekalia kwenye jamvi pale kati uwanjani. Na kisha akaendelea kumwambia “Wewe Johari utabeba mzigo wa utasa, ujue uchungu wa kukosa mwana. Huo ndio utakuwa mtihani wako wa kukufunza kuwa na imani.Huo utakuwa ni mtihani ili kukurudisha katika mstari wa binadamu mtenda mema, nenda tenda kwa akili ikiwezekana tubu popote itapobidi na fanya toba, mungu atakusamehe na utakuwa miongoni mwa waja wema, ila ukiendekeza ubinafsi wako mikosi zaidi itakuwa yako”, alimaliza kuongea huyo mtu na kutoweka kisha wale watu wengine wote waaliokuwamo uwanjani wamekalia jamvi, akiwamo yule baba na familia yake wakatoweka pia. Baada ya kuamka toka kwenye ndoto hiyo, Johari hakuota tena ndoto mbaya mbaya. Ila kutokana na imani yake ndogo alipuuzia ndoto hiyo na hakutilia maanani nini hasa ilimaanisha kwenye maisha yake kuanzia wakati huo na akaendelea na maisha yake ya kawaida.
Baadaye Johari alihitimu elimu yake ya chuo kwa ufaulu wa alama za juu sana na hivyo akapata ufadhili wa kuendelea kusoma kwa ngazi ya ‘masters’ na kupata ajira, hivyo akabadilisha kabisa hali ya maisha yake na ya shangazi yake aliyeitwa Roda ambaye ndiye aliyemlea baada ya wazazi wake kufariki alipokuwa mdogo. Johari akaja kufahamiana na mtu aliyeitwa Malcom Munyisi na kupendana na kufunga ndoa. Kisha akajaliwa kupata nafasi muhimu ya kufanya kazi katika benki ya NIB, iliyokuwa moja ya mabenki makubwa nchini. Kwa ujumla maisha yake yalionekana yamekamilika, yaliyobarikiwa na mungu na ambayo kila mwanamke wa angeyatamani. Ila!, Johari aliishi katika ndoa na mumewe kwa miaka kumi pasina kupata mtoto, wala ujauzito wala dalili yeyote na ‘unukio’ wa ujauzito.
Johari alifahamu vizuri tatizo lake lilitokana na mkosi ‘aliojiokotea’ kutokana na maasi yake aliyotenda huko nyuma ila akiwa pamoja na mume wake walihangaika mahospitali kwa wataalam wa tiba za uzazi ambako tatizo lilionekana liko upande wake, tena tatizo lililowastaajabisha wataalamu kwa maana viungo na maumbile yake hayakuwa na kasoro yeyote ile iliyoeleweka kusababisha asishike ujauzito kwa sababu za kuelezeka.
Kadiri miaka ilivyokuwa ikienda Johari alizidi kuwa mwenye wasiwasi kuwa ipo siku eidha Malcom ama ndugu zake watazidiwa na hamu ya kuwa na mtoto kwenye familia na pengine hata kulazimisha ndoa yao kuvunjika, aliwaza sana juu ya jambo hilo na aliombea lisimtokee.
Kwa upande wa Malcom yeye alikuwa ni mtu mwenye mambo ya kizunguzungu, pengine ilitokana na maisha yake yaliyojawa na kwenda ulaya kila mara kila mwezi, hivyo yeye aliangalia tatizo la mkewe la kutopata ujauzito kama tu tatizo la kuendelea kulishughulikia na alizidi kuonesha mapenzi kwa mkewe. Ila sasa tatizo lilikuwa ni mama yake Malcom na mdogo wake wa kike aliyeitwa Snura, ambao wao walikuwa ni waongeaji na wenye mambo ya ukorofi sana.
Basi siku moja Malcom alimchukua Johari na kwenda nae kwao kwa mama yake kutembea. Siku hiyo walikuta kuna wajomba, baba wadogo, shangazi, mama wadogo wa Malcom wote wapo, kwa mshangao walioupata kwa kutotarajia uwepo wa ndugu wote hao, Malcom na Johari wakaambiwa kuwa hao ndugu wote walialikwa wajumuike siku hiyo kuzungumza mambo mbalimbali ya msingi ya kifamilia ikiwemo na kumshauri Malcom kwenye masuala muhimu ya kimaisha.
Wakiwa ndugu wote wamekaa chini ya mwembe nje ya nyumba ya kina Malcom, na Johari akiwa yuko hapo akijinyenyekeza mbele ya maongezi yao, mara mmoja wa wajomba wa Malcom akaanza kuongelea jinsi alivyojaaliwa kuwa na watoto watano wa kiume ambao aliwaita majembe na kuwasifu ni vidume hasa, na mara shangazi yake Malcom akadakia na kueleza jinsi ambavyo alijaaliwa kuzaa watoto saba na mwenyezi mungu na kushangaa hasa kwanini vijana wa kileo hawaelewi umuhimu wa kuwa na watoto mapema ilihali uhai ni mfupi.
Johari hakufurahia maongezi hayo aliona kabisa yanamsakama yeye na mumewe kwa kukosa mtoto.
Mara katikati ya mazungumzo hayo alifika binti mdogo, mzuri na aliyeonekana mpole na kuwaamkia kwa heshima na kujieleza kuwa kaja kumtembelea Snura, yani mdogo wa kike wa Malcom, mama Malcom kwa furaha sana alimkaribisha binti huyo na kumuelekeza aelekee huko nyuma ya nyumba kwenye jiko ambako Snura alikuwako akipika, na binti huyo akaelekea huko huku nyuma yake hapo chini ya mwembe ndugu zake Malcom walimtupia macho huku wakiwa na furaha na kuanza kumsifu.
Alianza baba ake mdogo Malcom kusifia, “kabinti kapoole, kazuuri, kanafaa kweli kuwa mke wa mtu ila laa!, vijana wetu wanaokoteza wanaacha mawari kama hawa mikoani”, akadakia mama ake mdogo Malcom, “tena kwa jinsi alivyo mpole binti huyu akiolewa wala hababaiki anazaa ‘fasta’, sio mijanamke mingine miaka dahali ‘no’ mtoto ‘no’ nini”, mama mdogo huyo aliongea kwa sauti. Maneno hayo yalikuwa wazi yakimlenga Johari. Mara akadakia mama ake Malcom, “Unajua enzi zetu mtu ukienda ukweni unafikia jikoni, unakaa huko unapika siku hiyo wakwe zako wanakula chakula ulichopika”, kisha akamuangalia Johari na wakaonana macho. Johari ikabidi ajibalaguze na kujiongelesha, “unajua mama mimi ni mpishi hodari tu sasa ngoja nika wakaangazie huko jikoni leo mle msosi niloupika mimi na mtaufurahia”, aliongea Johari na kujichekesha na kuinuka kwenda huko nyuma ya nyumba kulikokuwa na jiko, alijua lazima aondoke hapo ili kumuacha Malcom aongee na ndugu zake.
Hapo chini ya mwembe ndugu zake Malcom walimjiaa juu, wakimtamkia kuwa umri unaenda anahitaji mtoto, na kwamba kama mkewe hazai aachane nae aoe mwanamke mwengine. Malcom ambaye alijawa mambo ya kizungu, huku kavalia mawani yake, alikosa maneno ya kujibizana nao hao waswahili wa maneno akawekwa mtu kati wakimshambulia na kumuelimisha, aache ‘uboya’.
Wakati huo, huko jikoni alikokwenda kukaa Johari apike hapakuwa na amani, kwa maana Snura aligoma kupisha ‘mtu’ apike. Hivyo Johari akawa kakaa pembeni akimsaidia kupika kwa kumsogezea kopo la mkaa, mara amsogezee kopo la vitunguu na chumvi ama maji . Halafu mbaya zaidi muda wote Snura alikuwa anaongea na rafiki yake kana kwamba hawamuoni Johari, waliongea mambo yao ya kijijini ambayo Johari hakuweza kuchangia.
Ila kilichomuuma zaidi Johari ni pale alipokatiza kuku nje ya jiko hilo, kuku huyo mtetea alipita pamoja na vifaranga vyake. Basi Snura akaanza kumsifia huyo kuku, “Kuku si ndo huyu, kuku kuku kweli, kuku anatotoa vifaranga tunaona faida yake, mana raha ya kuku atotoe, sio kuku miaka nenda rudi kuku hatotoi, yani huyu kuku jinsi anavyototoa mfugaji anakupa raha ambayo hata binadamu mwengine hawakupi”, maneno hayo yalimuuma sana Johari pale alipoyaelewa maana yake, na alipoelewa kuwa kwa Snura, yule kuku ‘mdudu’ alikuwa na thamani kwa kutotoa kwake kuliko yeye Johari.
Ilimuuma hivi kwamba alilia njia nzima kwenye gari wakati yeye na Malcom wanarejea Dar es Salaam. Na Malcom alielewa kilichomliza mkewe, na safari hii alishindwa hata kumfariji, kwa maana hakuwa na pa kuanzia ndugu zake walifanya mambo ya kiroho mbaya bila kuficha safari hiyo.
Wiki nzima iliyofuatia Johari alikuwa mtu mwenye huzuni, na alijaribu kuficha hisia zake asionekane huzuni yake. Ila huzuni ilimtawala hivi kwamba bosi wake kazini alimuuliza baada ya kikao kimoja , kama ana tatizo lolote lililomtatiza, pia wafanyakazi wezie ‘walinotisi’ na kumuuliza kulikoni. Hadi mteja wa benki hiyo bwana Jama Bhanji ambaye alihudumiwa ‘private’ kwenye benki hiyo mara kwa mara na Johari alinotisi huzuni ya Johari na alimuhoji kulikoni alipoa sana.
Kwa kuwa Malcom alikuwa tayari keshaenda nje nchi kama kawaida yake -maana yeye Malcom alikuwa akifanya kazi wizarani kuhusu masuala ya mashirikiano ya kimataifa- Johari hakuwa hata na hamu ya kuwahi kwake, alibakia ofisini hadi jioni sana, katika ofisi yake hata kama alikuwa hana la kufanya alibaki kakodolea macho yake dirisha la kioo la ofisi yake iliyokuwa ghorofa ya nne ya jengo la benki hiyo ya NIB, hivyo akabaki hapo akiangalia jinsi giza lilivotua na majengo marefu ya mjini kati yakiwashwa taa ndipo aondoke kwenda kwake, huko mitaa ya Kijitonyama.
Aliwaza na kuwazua na hatimaye akafanya maamuzi kuwa, kwa kuwa kashahangaika sana kwenda mahospitali ya nchini na nje ya nchi basi suluhisho lililobaki ni kwenda kwa mganga wa kienyeji. Maamuzi yake yalifika huko kwasababu alifahamu fika tatizo lake lilitokana na kuhusika na kundi la kiharifu na kiuaji la mapanya. Na alifahamu fika kuwa wezie waliokuwa katika kundi hilo eidha walikufa kinyama ama kupotea, aidha Johari alielewa kuwa yeye pekee ndiye alliyesalia katika lile kundi la mapanya na kwamba kukosa kwake kupata ujauzito ni sehemu ya lana ya matendo yale maovu. Hivyo kwa imani kubwa aliamini mganga wa kishirikina ndiye angekuwa na msaada mkubwa sana kwake kwa tatizo hilo lake la muda mrefu.
Basi, siku moja wakati mumewe yuko nje nchi, bi. Johari alifunga safari ya mbali hadi katika kijiji kilichoitwa Sadani, kilichokuwa porini mbali kweli na kwenye kutisha. Huko alienda kumuona mganga. Mganga aliyekuwa mashuhuri, na watu toka kona zote za Tanzania nzima walienda kwa nguli huyo wa kishirikina kupata nusura ya matatizo yao.
Na Johari alipowasili tu kwa mganga huyo alikubali kuwa kweli alienda kwa mganga na sio matani. Kwanza palikuwa chini ya mti mnene na mkubwa wa mbuyu uliotisha na kufuka moshi, ulioning’inizwa vitambaa vyeusi na vyekundu na mahirizi makubwa makubwa yaliyotuna na kupumua. Johari aliingia kwa mganga huyo huku akitetemeka na kujifunga vizuri kanga zake alizovaa huku kaukumbatia mkoba wake alokwenda nao hapo. Mganga mwenyewe alikuwa pande la mtu, aliyejaa mahirizi na macheni ya mifupa ya wanyama na yale maganda ya konokono na viumbe wa baharini, usoni kajichora kwa maandishi meupe, huku akiwa kavalia kaniki na huku yuko kifua wazi.
Kabla hata Johari hajaeleza shida yake huyo mganga alimtolea macho makali sana Johari, macho makali kama ya chuki na kuanza kuongea, “Kweli leo umenijia wewe mwanamke mbaya. Hata waungwana unawapa mtihani, mizimu ya mababu zetu wa Sadani unawapa wakati mgumu kukupokea wakiwa wametulia, wanatetemeka kwa uovu ulioshuhudia na uovu wa watu uliojihusisha nao”, aliongea mganga huyo, na Johari alijikuta akiangausha chozi alielewa kuwa mganga kashafahamu maovu yote yanayomletea mkosi uliomfanya afike hapo mizimuni.
“Wewe mama unaitwa Johari Chande na mumeo anaitwa Malcom”, aliongea mganga na Johari kwa uchungu akaitikia, “tawile ‘baba’ angu ndio mimi, Johari”, na mganga akaendelea, “shida yako ni kupata mtoto, ila hupati kutokana na mkosi na nuksi ulizopata baada ya kuwa moja ya wafuasi wa kundi la kijambazi waliowahi kuua familia nzima na wewe ulikuwako siku ya tukio ukishuhudia”, aliendelea mganga huyo nguli, na Johari akaitikia, “tawile mganga”.
“Wezio woote, waliohusika wamepatwa na vifo vya kutisha na wengine kupotea, ila wewe walau umepewa utasa tu. Ila bado hujakubali unahaha kupata mtoto kama hivi kwa kututafuta waganga”, aliongea mganga huyo na kuangalia juu mawinguni, huku Johari akimtazama pia kwa hofu, kwa muda mganga huyo alibaki akiangalia mawinguni na ghafla akamgeukia Johari na kumkazia macho na kuendelea kuongea kuwa, waungwana wake, yani akimaanisha mizimu ya mababu zake wanampa hizo nguvu za kimiujiza wanayo dawa ya kutibu utasa wa Johari na kumsaidia kupata watoto, ila tatizo ni ugumu wa masharti, na mganga akamuuliza Johari kama yu tayari kufuata masharti magumu ya mganga. Na mganga akamsisitizia kuwa si jambo la kirahisi tu kukubali masharti hayo, na kwamba hatomtajia hayo masharti mpaka Johari ayakubali kwa moyo wote kabisakabisa kuwa vyovyote yatakavyokuwa hayo masharti kwa ugumu wake, yawe mepesi ama magumu kwelikweli shurti lazima ayatimize. Kuwa Johari ilimbidi akubali kutenda masharti kabla hajatajiwa na kuwa akishatajiwa basi hakuwa na jinsi ingine zaidi ya kuyatimiza. Johari alijikuta katika wakati mgumu sana, akawa kabaki kamtolea macho mganga. Hivi kweli akubali tu masharti kabla hajatajiwa, aliwaza, yakiwa magumu je itakuwa vipi ilihali ndio mganganga keshasema akimtajia sharti ayafanye hayo masharti.
Basi mganga akamuamuru Johari aondoke akatafakari ili kuamua kama yu radhi kutimiza masharti yeyote atakayopewa na mganga ama la. Na mganga akamwambia Johari kuwa akirejea tena aende na mbuzi wa kafara wa rangi yeyote ili walau kufidia vile vifo vya familia ile iliyouwawa na kundi la Mapanya, na pia aende na fedha zisizopungua milioni tano. Na akamsisitizia Johari kuwa iwe ni siri yake kati yake na mganga kuwa anatafutia hapo dawa ya kupata ujauzito. Na mganga akamsisitizia Johari tena kuwa akiwa anaondoka akumbuke kuwa, atakapoamua kurejea kwa mganga huyo, awe tayari kaamua kufuata masharti ya kiganga, na kumkumbusha kuwa siku akishamtajia masharti hayo basi Johari atakuwa kama aliyevulia nguo maji hivyo sharti lake ayaoge.
Baada ya kuondoka kwa mganga Johari alitafakari sana, kwanza alionywa asimwambie mtu hivyo hakuwa na mwengine wa kushiriki nae hayo mawazo yake, pili sasa alitafakari kuwa hadi wakati huo, hakuwa akiyajua hayo masharti ya mganga, ila mganga alimuambia kuwa siku akienda tena na akatajiwa hayo masharti ni lazima ayakubali bila ya kuyakataa, hivyo Johari aliwaza kuwa lazima afikie mkataa na kuamua hasaa kufuata masharti ya mganga.
Johari aliwaza sana itakuwa vipi kama masharti ni magumu mno, ila kichwani mwake zikamjia picha akicheza na watoto wake ambao pengine mganga angemsaidia kuwapata, pia aliona jinsi Malcom angefurahia uzao huo na mkewe, hivyo Johari akaamua kuwa ataenda tena kwa mganga na kukubali masharti atakayopewa yawe magumu kwa vyovyote vile, yeye atakuwa yu radhi na tayari kuyafanya.
Basi siku ikawadia na Johari akaelekea tena huko kijiji cha Sadani kwa mganga. Na siku hiyo alienda na mbuzi mweusi na pesa taslim ambazo mganga alimwambia aende nazo.
Mganga alimtakia Johari kuwa ni mwanmke jasiri sana kwa kurejea tena kukabiliana na masharti magumu ambayo angemtajia. Basi mganga akamchinja yule mbuzi na kutoa kama kafara kwa mizimu ya mababu zake.
Kisha akaanza kumpa masharti Johari na kumuambia kuwa, namna pekee ya Johari kupata watoto ni kuzaa na kichaa, yani mwehu, mwendawazimu wa akili, mwanamume aliyechizi kabisa muokota makopo.
Johari alishtuka sana. Alishtuka kwa maana hakutarajia sharti hilo hata kidogo. Ila mganga akamsisitizia kuwa hiyo ndio njia pekee ya kwake Johari kuweza kupata watoto vyenginevyo, asahau uzao. Na mganga kwa hasira alimkumbusha Johari kuwa masharti hayo ni lazima ayafuate, kwamba sasa ilikuwa ni lazima kwa Johari kumtafuta chizi muokota makopo na kulala nae ili azae na huyo chizi na kwamba Johari hakuwa na chaguzi tafauti na kulitekeleza sharti hilo ‘la aina yake’ alilompa.
Huo ulikuwa ni mtrihani mkubwa kwa Johari. Hakufikiria kabisa kuwa mganga angeweza kumpa sharti kama hilo. Njia nzima akiwa anarejea Dar machozi yalimtirirka akiwaza wapi atapata mtu chizi, na ‘atamkovisi’ vipi chizi hadi alale nae na aliwaza sana kuwa ikigundulika ‘mishe’ yake hiyo ya kutembea na wehu wa akili waokota makopo, ili apate watoto kama masharti ya mganga yatakavyo, uso wake ataufichia wapi, na alifikiria sana kwanini yeye Johari mfanyakazi wa benki kubwa kama NIB na mke wa Malcom Munyisi, mtu tajiri na alojaa uzungu uzungu, mfanyakazi wizarani, kwanini yeye ilimlazimu kulala na machizi ili kuzaa. Ila alikumbuka kuwa ni maovu yake yanyomtafuta na kumkimbiza, yakimfuatilia kama kivuli kila aendako.
........................
Malcom aliporejea toka nje ya nchi na kutembelea kijijini kwa mama yake, ndugu zake walimjia juu zaidi na safari hiyo wakamwambia kuwa wamemtafutia mchumba hivyo kazi yake ilikuwa kumuacha tu Johari na kumuoa huyo mwari mpya wa uhakika wa kuleta mtoto katika familia yao ya akina Munyisi.
Na Malcom hakuficha kitu kwa mkewe akamwambia alichoambiwa na ndugu zake, mama zake wadogo, mashangazi na wajomba, kuwa katafutiwa mchumba. Mbaya zaidi sasa kwa Johari huyo mchumba aliyetafutwa akaanza kumpigia simu Malcom. Hivi kwamba wakati mmoja Johari alipokea moja ya simu hizo na kumtukana sana huyo mwanamke.
Basi, siku moja Johari alikuwa kampitia mfanyakazi mwezie aliyeishi maeneo ya huko Mbezi Beach, ili waende mahala. Johari akiwa kakaa kwenye gari lake akimsubiri huyo mwezie atoke, mara akamuona mwanamume mmoja aliyevalia rafu sana, nywele zimetimka, yuko peku, akikatiza mbele ya gari lake akielekea mbele ya duka la rejareja lililokuwa mtaa huo. Moja kwa moja Johari alielewa huyo mtu alikuwa ni chizi mwendawazimu muokota makopo. Na akabaki akimtazama jinsi yule chizi alivyokuwa akifanya uchizi wake na mambo ya hovyo akielekea kwenye duka la mtaa.
Johari aliona jinsi, watu waliokuwa wamekaa wakianza kumcheka yule chizi. Na mara muziki ukasikika toka ndani ya duka. Na yule chizi akaanza kucheza huo mziki kwa furaha kabisa na wale wa dukani wakaendelea kumshangilia na kumcheka sana, walimgeuza kituko chao. Johari mwenyewe alijikuta akicheka vituko ambavyo yule chizi alikuwa akifanya kwa ‘kusakata’ muziki.
Mara rafiki yake aliyekuwa akimsubiri aliingia kwenye gari na kukaa kwenye kiti cha pembeni ya Johari huku akiomba radhi kwa kumchelewesha.
Na Johari aliondoa gari eneo hilo kuelekea kwenye safari yao waliyokuwa wakielekea. Walipokuwa njiani Johari alimuuliza rafiki yake juu ya yule chizi aliyekuwa akicheza mziki, na rafiki yake akamwambia kuwa yule mtu ni kichaa kabisa muokota makopo ambaye huzururazurura mitaani kwao na kuwa aliishi kwenye boma la nyumba ambayo haijakamilika jirani kabisa na pale palipokuwa na duka. Na kwamba hakuna mtu aliyefahamu yule chizi anaitwa nani, ama ndugu zake ni akina nani na wapi ama kwa namna gani aliupata uchizi, ila watu walipenda tu kumuona akicheza muziki na kumgeuza kituko chao na kumcheka.
Johari alisisimka mwili wake kusikia habari za yule chizi. Alianza kufikiria sana kichwani mwake kuwa huenda kapata aina ya chizi sahihi ambaye angefaa katika kutimiza masharti aliyopewa na mganga ili alale nae na kupata ujauzito. Aliwaza sana Johari na kujiapia kuwa lazima amchunguze yule chizi vizuri ili amjue tabia zake na kuelewa namna gani atamuingia na kumshawishi hadi afanye nae tendo la ndoa.
Na kweli, Johari alifanya uchunguzi wake na akapajua yule chizi alipokuwa akilala, aina ya taka alizokuwa akila na zuri zaidi alilofurahia ni kuwa chizi yule hakuwa na tabia ya kupiga watu. Johari alidhamiria kabisa kuwa lazima alale na chizi yule.
Usiku mmoja baada ya chunguzi zake kwisha, Johari alimfungia safari yule chizi. Ilikuwa ni usiku wa manane, Johari alifika kwenye boma la nyumba ambayo haikukamilika ambako yule chizi alilala. Kwa hofu Johari aliingia hadi ndani ya boma hilo na kumkukuta yule chizi kalala. Kwa muda kidogo Johari alimmulika kwa tochi na kumtazama na Kuona jinsi alivyokuwa mchafu na kulala kwenye udongo na nyasi za boma hilo tena harufu ya uchafu wa mwili wa chizi huyo ilitapakaa boma zima, hakika Johari alihisi kinyaa.
Mara yule chizi akaamka kutokana na mwanga wa tochi ambao Johari alimmulika nao. Na chizi yule alishtuka sana kwa maana hakuzoea ugeni bomani humo, hasa usiku manane. Johari mwenyewe alipoona yule chizi anaamka alishtuka hakujua yule chizi angewaruka kwa mtindo gani baada ya kumuona humo bomani.
Basi Johari ambaye mkononi alikuwa kabeba mfuko wenye machungwa, aliingiza mkono mmoja mfukoni na kutoa chungwa na kuanza kula kwa kumringishia chizi yule. Mara yule chizi akamvamia Johari na kumpokonya mfuko wa machungwa aliobeba na lile chungwa alilokuwa akimlingishia kisha, yule chizi akaenda kujikunyata na kula yale machungwa haraka haraka. Wakati huo Johari alikuwa kamtolea macho yule chizi. Kwanza hadi wakati huo Johari alijiona jasiri sana kufika katika boma hilo na kendelea kuwamo humo usiku huo wa manane pamoja na huyo chizi. Ila sasa Johari alifikia ukomo wake wa kufikiri hakuelewa ataanzaanza vipi kuhamsha hisia za chizi, hivi kwamba wafanye tendo la ndoa humo bomani na yeye mwenyewe alijiwazia sana ‘msambwanda’ na mtu chizi hufanania vipi, kichwani mwake, Johari alikuwa na mawazo kama alfu hivi, aliwaza kama akifumwa bomani humo na chizi usiku huo watu wangemchukiliaje.
Basi yule chizi baada ya kumaliza kula yale machungwa, ghafla akatulia na kumtizama Johari. Alimtazama kwa kutulia kabisa kama mtu mzima na timamu awezavyo kumuangalia mtu mwezie akiwa katulia, hadi Johari akastaajabu sana. Alistaajabu kwa jinsi ile yule chizi alivyotulia. Yule chizi alimungalia Johari machoni moja kwa moja na kutulia kabisa kama vile hakuwa na kawehuka kichwani.
Kumbe yule chizi alitulia vile kutokana na uzuri aliokuwa nao Johari. Alimuona Johari kuwa ni mrembo sana. Pamoja na uchizi wake alitambua kuwa hakuwahi kuona mwanamke mzuri kama Johari. Yule chizi alimuangalia Johari hadi machozi yakaanza kumlenga na kuona haya akageukia pembeni.
Johari hakutarajia kuwa mtu chizi anaweza kutulia namna hiyo, akabaki kaduwaa. Ila sasa aligundua kuwa, kama yule chizi aliweza kutulia namna ile basi kazi yake ilompeleka bomani mule ilikuwa nyepesi sana.
Mara moja Johari akavua na kuangusha nguo zake alizovalia mwilini na kumfuata yule chizi, ambaye nae alipomuona Johari yuko utupu alishtuka sana. Pamoja na uchizi wake alitambua kuwa si kawaida kwa mwanamke kuwa utupu. Johari akamsogelea.
Nia ajabu ilioje hadi wakati huo kile kinyaa alichokuwa akiona Johari kilimtoka kabisa na hakukisikia, hadi wakati huo alilenga tu kulala nae tu yule mwendawazimu.
Katika hali ngeni kabisa kwa yule chizi, alijikuta kasisimka sana na mara Johari alikuwa juu yake. Naam!, kilichotendeka hapo ilikuwa ni starehe ambayo chizi yule hakuwahi kuipata. Ilikuwa ndio mara ya kwanza kwa yule chizi kufanya tendo lile la aina yake na kwa Johari ilikuwa ndio mara yake ya kwanza kufanya vile na mataahira, yani ni kama walijiondoa ubikira kila mmoja wa aina yake, khatari!.
Johari akawa kafanikiwa lengo lake la kulala na chizi. Na usiku huo aliporejea kwake alikesha bafuni akioga akiwa haamini namna alivyofanikisha lile tendo na yule chizi. Hakuamini kama kweli msomi kama yeye alifanya alichokifanya, hakuamini kuwa yeye alikuwa ni jasiri wa kufanya kitu kama kile wakati aliona kuwa ni sharti zito sana pale alipotajiwa na mganga kuwa afanye vile, na ajabu aliona kuwa mbona ilikuwa na kauwepesi kidogo katika kutekeleza kuliko alivyokuwa akifikiria ugumu wake. Na alijishangaa na kujiuliza kinyaa chake cha kulala na chizi mchafu, anukae asieoga kilienda wapi muda wa tendo. Ni maswali mengi aliyojiuliza na akakosa majibu kichwani mwake.
Basi, maisha yaliendelea na wiki chache tu mbele Johari alianza kupata dalili ambazo hakika yeye aliamini ni ujauzito. Na hata alipokwenda kumuona daktari majibu yalionesha hivyo kuwa alikuwa ni mjamzito. Ilikuwa ni furaha sana kwa Malcom, kwa maana alishamkatia tamaa mkewe, Malcom hakuwa akitarajia kama mkewe angeweza kuleta kiumbe duniani, ilikuwa ni miujiza kwenye ndoa yao.
Ndugu zake Malcom walistaajabishwa sana na taarifa hizo, hawakuamini hata kidogo. Walijiuliza sana iwaje mgumba kapata ujauzito. Miezi tisa baadae, Johari alijifungua mtoto wa kiume, na kwa furaha Malcom akamuita mtoto huyo, Miujiza, kwa maana alikuwa ni muujiza kwa familia yake. Sasa mama yake Malcom, mdogo wake Malcom na ndugu wengine wakajikuta wana mapenzi ya dhati na Johari na kusahau viroja walivyokuwa wakimtendea. Sasa safari hiyo, Johari nae akawa anawaletea nyodo za ‘kimtindo’ za waziwazi katika kile kiitwacho kutesa kwa zamu, sasa Johari alionesha dhahiri kutopenda mtoto wake ashikweshikwe na ndugu wa mumewe na kujifanya mtoto wake anamlea kizungu sana na si kiswahiliswahili kama ndugu wa Malcom aliowachukulia kuwa hawana elimu walivyotaka kujishirikisha kwenye malezi ya mtoto.
Johari alikuwa ndiye mwenye furaha zaidi baina ya wote waliofurahia kuzaliwa kwa Miujiza. Yeye kama mama alifahamu shuruba na masharti aliyopitia na kutimiza ili kumpata mtoto wake. N akichwani mwake Johari akawa kafikia mkataa mwengine kuwa lazima atembee tena na yule mwanamume chizi ili apate mtoto mwengine wa pili.
Kwake yeye Johari kutembea na yule chizi ilikuwa ni jambo rahisi sana, kwa maana Malcom alikuwa ni mtu mwenye kusafiri safiri sana kwenda nje ya nchi, hivyo Johari aliweza kuwa na uhuru wa kuamua kuchelewa kurudi nyumbani na kufanya lolote huko mitaani, ikiwemo kulala na machizi, bila ya kuhofia kujulikana na mtu yeyote wala kumtia wasi Malcom.
Baada ya mwaka mmoja kupita, Johari, kwa awamu ya pili alirejea bomani kwa yule chizi. Na safari hiyo Johari alishangazwa kugundua kuwa yule chizi alimkumbuka vyema. Kwa maana safari hiyo ya pili, yule chizi alipomuona tu Johari machozi yalimdondoka toka kwenye macho yake hadi Johari mwenyewe akajikuta machozi yakimdondoka, hata bila ya kuelewa yule kichaa alilia nini kwa kumuona yeye Johari. Kumbe yule chizi alilia kwa mapenzi. Alimkumbuka vizuri Johari na urembo wake, na toka usiku ule wa mara ya kwanza wafanye tendo bomani yule chizi alimkumbuka na kumuwazia.
Kwa namna hiyo, hiyo safari hiyo ya mara ya pili ilikuwa rahisi zaidi kwa Johari kumuingia chizi huyo na kulala nae , kwasababu chizi mwenyewe alikuwa kaingia ‘laini’, yani haleti papara, ‘mzigo’ kauelewa na picha alijua kulicheza, na chizi yule alikuwa na hamu kweli ya kulala na Johari.
Hivyo Kama kawaida kwa maraya pili mambo yalitiki tena kwa Johari. N kweli akapata ujauzito na kuzidi kumfurahisha Malcom na ndugu zake.
Na miezi tisa baadae akajifungua, safari hiyo alijifungua watoto mapacha wawili, wasiofanana, wa kike na wa kiume, na kuzidisha furaha maradufu kwenye familia hiyo ya Malcom na ndugu zake ya akina Munyisi.
Johari alifurahia sana mafanikio ya mchezo wake mchafu. Na akafurahi pia kuwa hana haja ya kuuendeleza kwasababu watoto watatu walimtosha sana yeye na Malcom. Hivyo Johari alijiona ni shujaa aliyeweza pambana na lana ya uovu aliowahi kuufanya na kuushinda. Na nyodo zake kwa ndugu wa Malcom zikazidi maradufu hadi wakajutia madhira waliyomfanyia. Kwanza Johari watoto zake hakutaka mtu awaguse, aliwalea kama kitu gani sijui!, aliwalea kama ‘maprince’ na ‘princess’. Ndugu wote kimdomomdomo ‘kikawakatika’ wakabaki kuangalia malezi ya kiulaya ulaya.
...................................
Basi miaka ikaenda, na kichwani mwake Johari akamsahau kabisa yule chizi utadhani hakuwahi kutokea kwenye maisha yake kutembea na mtu chizi, yeye aliwaza furaha yake na Malcom na watoto wao watatu, Miujiza, Flora na Florian. Kwake watoto walikuwa ni wa Malcom sio mtu chizi. Hakuwa hata na haja ya kujua yule mtu aliishia vipi maisha yake, hakuwa na umuhimu wowote kwake. Kwake kilichokuwa umuhimu ilikuwa ni furaha ya familia yake na mumewe.
Na kweli hakuna kilichowabughudhi tena familia yao, kwa upande wao. Waliishi kwa raha mustarehe. Ila sasa mikasa ikawa upnde wa yule chizi.
Wakati Johari, alisahau juu ya yule chizi, kwa upande wa yule chizi haikuwa hivyo. Kwa upande wake alimuwaza Johari kwa mapenzi makubwa.
Pamoja na uchizi wake, aliikumbuka vizuri sura ya Johari, harufu yake, sauti na miguno yake na hasa alikumbuka uzuri wake. Na alimuwaza sana na ‘kummiss’ sana. Alipokuwa akilala alimuota Johari. Mara nyengine alihisi Johari kamsimamia pembeni na kuamka kwa furaha kumkumbatia na kumkaribisha bomani kumbe hakukuwa na Johari bali mawazo yake tu ya kichizi. Na alipogundua kuwa Johari hakuwa akija tena bomani yule chizi alikuwa akilia. Haikuwa kawaida, siku moja alikatiza mbele ya duka moja la mtaani na akasikia wimbo wa mapenzi ukipigwa redioni. Wimbo ambao ulikuwa na mashairi ya mtu aliyemkosa mpenzi wake, na uliokuwa na ‘tune’ ya kusikitisha ikionesha huzuni ya mapenzi, kwa hali ya kushangaza kabisa yule chizi alitoa ‘mchozi’ na kulia, na kushindwa kuendela na safari zake za kichizi na akakaa chini kulia kwa uchungu. Watu waliomuona walishangazwa sana na kumjaalia na kumuwazia iwaje mtu taahira ashikwe na hisia kali za wimbo wa mapenzi toka redioni hivi kwamba atoe machozi.
Hali ilikuwa ya namna hiyo kwa yule chizi. Na hivyo ndivyo maisha yake ya uchizi mitaani yalivyoendelea. Huku watu wakiwa hawamjui alikuwa ni nani hasa, hakuna liyejua jina lake wala asili yake, ilionekana mungu kampangia maisha yake yawe ya uchizi na uzururaji.
Itaendelea.............................................................