Kituo cha Ubungo Bus terminal Kimehamia Simu 2000

Kituo cha Ubungo Bus terminal Kimehamia Simu 2000

Egwugu

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2011
Posts
17,558
Reaction score
8,552
Jamani mliobahatika kufika kituo kipya kutoka Ubungo kuamia sim 2000 waliofika hapo kituoni leo tupeni habari yake kwa harakaharaka mpangilio ukoje wa mandhari
========================


KUHAMISHIA DALADALA KITUO CHA SIMU 2000
(NYUMA YA MAWASILIANO TOWERS) KUANZIA ALHAMIS TAREHE 23.10.2014



Baada ya kituo cha Simu 2000 kukamilika SUMATRA kwa kushirikiana na Manispaa ya Kinondoni na Kikosi cha usalama barabarani Mkoa wa Kinondoni tumekubaliana kufungua kituo hiki tarehe 23.10.2014 asubuhi kwa daladala ambazo zilikuwa zinaishia au kuanza safari katika kituo cha daladala Ubungo.

Kila dereva anatakiwa kufuata utaratibu ulioelekezwa hapa chini ili kuondoa usumbufu usio na tija.

1. DALADALA ZINAZOTOKA MASAKI

zikifika barabara ya Shekilango zitaingia kulia kwa kutumia barabara ya TANESCO inayokwenda moja kwa moja kituoni simu 2000 na zitarudi barabara ya Shekilango kwa kutumia njia hiyo hiyo ya TANESCO.

2. DALADALA ZINAZOTOKA KARIAKOO, POSTA na KIVUKONI
zikifika mataa ya Ubungo zitaingia kulia (barabara ya Sam Nujoma) kwenda kituoni Simu 2000, zitarejea zilikotoka kwa kutumia barabara hiyo hiyo

3. DALADALA ZINAZOTOKEA BARABARA YA MANDELA

zitavuka mataa ya Ubungo (kwa kutumia barabara ya Sam Nujuma) na kwenda kituoni Simu 2000, zitarejea zilikotoka kwa kutumia barabara hiyo hiyo.

4. DALADALA ZINAZOTOKEA MWENGE
zikikaribia jengo la Mawasiliano Towers zitachepukia kushoto kwa kutumia service road inayopita mbele ya Mawasiliano Towers hadi kituoni simu 2000, zitarejea zilikotoka kwa kutumia barabara ya Sam Nujoma (sio servive road).

5. DALADALA ZINAZOTOKEA KIMARA NA MBEZI
zikifika mataa ya Ubungo zitaingia kulia kwenda kituoni simu 2000. zitarejea zilikotoka kwa kutumia barabara hiyo hiyo.

Conrad Shio
Afisa Mfawidhi SUMATRA –DSM
0755 660 016
 
1. Jina la simu 2000 limetokana na nini kwanini kituo kisijulikane kama mawasiliano

2. Kuboresha kituo kuendane na uboreshaji wa barabara na mifereji ya maji kwakuwa eneo hilo huwa na kero nyingi sana kipindi cha masika kutokana na maji kutotiririkia bondeni na badala yake yanajaa barabarani
 
Jamani mliobahatika kufika kituo kipya kutoka Ubungo kuamia sim 2000 ......
========================

ImageUploadedByJamiiForums1414074329.026232.jpg

Zitaingia kulia!!!!!!!!!!!!
 
1. Jina la simu 2000 limetokana na nini kwanini kituo kisijulikane kama mawasiliano

2. Kuboresha kituo kuendane na uboreshaji wa barabara na mifereji ya maji kwakuwa eneo hilo huwa na kero nyingi sana kipindi cha masika kutokana na maji kutotiririkia bondeni na badala yake yanajaa barabarani

namba 2 nice observation mkuu! waangalie sana kuhusu hilo maana eneo liko chini na huwa hapafai hapo kipindi cha mvua kubwa. isje baadae kuwa kero.
 
Hili jina litawasumbua wapiga debe... Ubungo..Ubungoo...! Ilikuwa rahisi....Lakini Simu elfu mbili Simu elfu mbiliiii..!! wala hainogi.....Labda wafupishe...Sim... Sim...Simuuuuu...!!

Kutoshirikishwa wadau ni jadi ya watawala wetu.

Nadhani hili jina la simu 2000 halitakuwa famous hata kidogo.
 
Dah darajani palikuwa panaboa sana pale. Ila nchi hii, baada ya miaka mitatu watakihamisha tena.
 
Hili jina litawasumbua wapiga debe... Ubungo..Ubungoo...! Ilikuwa rahisi....Lakini Simu elfu mbili Simu elfu mbiliiii..!! wala hainogi.....Labda wafupishe...Sim... Sim...Simuuuuu...!!

Hahahah mkuu mbona unawatetea wapiga debe hivo au na ww ndo shughuli yako nini?
 
yani hawa jamaa wanazidi kufanya maisha kua magumu juu ya usafiri wa uma.
Na nitoe angalizo naona wanazidi kukuza kituo cha river side darajani hasahasa kwenye zile eneo la tanesco transfoma. hivi unategemea dereva atokae tabata au buguruni au gogo la mboto atakua na muda wa kusubiri taa ziwake ndio aende huko kwenye hizo simu zenu? labda kama na wao mnawawekea kituo hapo river side otherwise ni mwendo wa "kukunja chapati" kuwaongezea majanga abiria watokao mwenge kwenda uelekeo wa barabara ya mandela.
 
Back
Top Bottom