Kituo cha Ubungo Bus terminal Kimehamia Simu 2000

Kituo cha Ubungo Bus terminal Kimehamia Simu 2000

Hahahah mkuu mbona unawatetea wapiga debe hivo au na ww ndo shughuli yako nini?

Mkuu wajiriamali wale...na kumbuka tuko kwenye soko huria/ulia...wale wanauza huduma kijariamali...wahusika walitakiwa kuwashirikisha wadau hawa kuchagua jina la kituo. Nina watetea sababu hiyo tu..!
 
hapatakuwa na wapiga debe wala makonda hawataruhusiwa kupiga debe, ni kimya kimya.
 
Pamoja na kukaa dsma miaka kadhaa lakini hilo jina ni geni kabisa kwangu!
 
Kuna walakini hapo


Yani watanzania ni kama tumerogwa vile. na hiyo ni Prress release kabisa kwa ajili ya umma? Utoke kimara/Mbezi ukate kulia utokee Sam Nujoma kweli? Kulia si Mandela Road????
 
Plan ya kujenga Mall au majengo yenye hadhi kimejengwa kituo cha daradara, mpaka kituo kimejengwa ilikua hamna jinsi,kituo kimejengwa kwa amri ya mkubwa baada ya kukosa eneo mbadala baada ya ubungo
 
Yani watanzania ni kama tumerogwa vile. na hiyo ni Prress release kabisa kwa ajili ya umma? Utoke kimara/Mbezi ukate kulia utokee Sam Nujoma kweli? Kulia si Mandela Road????

Mkuu umejiuliza kama Mimi mpaka nikapotea! Eti ukifika mataa ya ubungo unalala kulia! Nikawa nawaza huo mzunguko Wa nini? Jamaa anaandika press release huku anawaza kwenda kufumania! Kazi kweli kweli!!
 
Hili jina litawasumbua wapiga debe... Ubungo..Ubungoo...! Ilikuwa rahisi....Lakini Simu elfu mbili Simu elfu mbiliiii..!! wala hainogi.....Labda wafupishe...Sim... Sim...Simuuuuu...!!

Unawajua makonda wewe,litapikwa mpaka litakaa sawa mwenyewe utakubar
 
Back
Top Bottom