Kituko cha uandikishaji wa wapiga kura - Kasulu

Kituko cha uandikishaji wa wapiga kura - Kasulu

NyakaiIkagogo

Senior Member
Joined
Nov 5, 2013
Posts
182
Reaction score
46
Wakati nakatiza mtaa wa Nyachijima, Kijiji cha Kidyama kilichopo Kata ya Kigondo Wilaya ya Kasulu, nimekutana na Mzee KUDONA BALAKUBHA MFUMYA aliyekuwa ametoka kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura linaloendelea katika Shule ya Msingi Kidyama.

Kituko, nilipoangalia Kadi yake ya mpiga kura nimesitaajabu baada ya kuona mwaka wake wa kuzaliwa ni 1995 na Jinsia yake KE. Mzee huyu kwa mjibu wa maelezo yake amewambia ana umri wa miaka 90 na ni Mwanaume.

Nadhani umakini unahitajika katika zoezi hili.
 

Attachments

  • 1433596984615.jpg
    1433596984615.jpg
    41.2 KB · Views: 1,113
Hii mpya kabisa, nadhani bado single albam itatoka badae.
 
Nakumbuka tume ya uchaguzi moja ya changamoto walizozitaja ni kuwa na wataalamu wachache wa kufanya kazi hii.
Sasa unakuja kujiuliza je, walikurupushwa na zoezi hili au la???Na kama walijiandaa kwanini kunakuwa na uzembe wa namna hii???
 
Nakumbuka tume ya uchaguzi moja ya changamoto walizozitaja ni kuwa na wataalamu wachache wa kufanya kazi hii.
Sasa unakuja kujiuliza je, walikurupushwa na zoezi hili au la???Na kama walijiandaa kwanini kunakuwa na uzembe wa namna hii???
Du, watanzania tunapenda sana kuhalalisha uzembe wetu kwa sababu zisizo na kichwa wala miguu! Hata kama ni changamoto la wataalam lakini hii ni kali zaidi! Siku zote mimi nasema kutokuwa makini ni ugonjwa wa watanzania wengi sana! BTW hata mpiga picha nae hayuko makini kwani haku-focus vizuri!
 
Ukistaajabu hili utashangazwa na kijana wa miaka chini ya miaka 18 (Mwanafunzi) kuandikishwa mara 2 vituo tofauti.Hii ndio JMT.
 
Kupeana kazi hovyohovyo kwa kujuana na kupewa papuchi, upuuzi mtu, aibu kwa mratibu
 
Cha ajabu wakati wa kupiga kura huyu mzee atakaliwa...kisa kadi yake imekosewa. Zaidi, hiyo haki anayohubiliwa hana tena pakuitafuta.
 
Nakumbuka tume ya uchaguzi moja ya changamoto walizozitaja ni kuwa na wataalamu wachache wa kufanya kazi hii.
Sasa unakuja kujiuliza je, walikurupushwa na zoezi hili au la???Na kama walijiandaa kwanini kunakuwa na uzembe wa namna hii???
Hapana tatizo ni kuwa ajira hizi ziliachwa kwa wapambIe wa chama na mashabiki wa kisiasa. Mlengo wa kisiasa ulichukua kipaumbele
 
Haya ni matokeo ya kuwekana, kupeana ajira kindugu bila kujali uwezo wa mtu.

Rais ajaye anatakiwa awe mwenye uwezo wa kusimamia maadili. Ajira za uma ziwe kulingana na merit na sio kujuana juana tu!
 
Kwenye ofisi yetu tuliomba hiyo kazi tukiambatanisha na ushahidi Wa vivuli kuwa tunaujuzi Wa koomputer,wote tulio na sifa tuliachwa wakachukiliwa ambao hawajawahi kuzitumia wakaelekezwa,herufi inatafutwa kama keybord imekosewa.
 
uliyetuwekea hii picha hebu weka iliyo nzuri. hiko kigiza zaidi. kwa kuwa niko kslu nione tutafanyaje kumpata huyu mzee
 
Yani huyo aliyekuwa anaandikisha hata kwa kutumia akili ya kawaida tu hakuona kuwa huyo mzee ni mwanaume?!!!
 
Ningependa kujua nini maana ya wataalamu
Tuanzie hapo
 
Back
Top Bottom