Kitu Gani Hiki Kusheherekea Mauti?

Kitu Gani Hiki Kusheherekea Mauti?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
22,455
Reaction score
32,981
KITU GANI HIKI WATU KUSHEHEREKEA MAUTI?

Nimeinamisha kichwa changu toka alfajir nawaza hili la watu kusheherekea kifo.

Mtume (SAW) katuasa kasema tuseme mema ya maiti zetu.
Hawa wamepitiliza angalau wangesema.

Hawa wanacheza ngoma kusheherekea kifo.
Nimeinamisha kichwa changu nawafikiria watoto na mke wa marehemu.

Msiba walionao wa mpendwa wao unawatosha hapana haja ya kuwabebesha na hili.

Lilipata kutokea jambo kama hili Dar es Salaam katika miaka ya 1970.
Bwana mkubwa mmoja kapata ajali kafariki dunia.

Mtu mkubwa sana huyu kisha mpigania uhuru na katika wanachama wa mwanzo wa TANU na mtu aliyekuwa karibu sana na Mwalimu Nyerere.

Waliokuwa wanamjua wanasema alikuwa hana miadi ya Mwalimu anawekwenda kwake iwe Ikulu au nyumbani kwa Mwalimu muda wowote na atapokelewa.

Mji wa Dar es Salaam wote una taarifa ya kifo cha bwana huyu.
Jambo la kushangaza.

Kwa kawaida sisi watu wa Pwani msiba ukitokea tu kitu cha kwanza ni kupelea taarifa msikitini kisha nyumbani panafungwa maturubai nje na kutandika majamvi kwa kivuli na watu kukaa.

Na huwa haichukui muda nje barazani watu huanza kujazana.

Wanaume wanakaa barazani wanawake uani na ikiwa ua mdogo hautoshi watatengewa nyumba ya jirani.

Msibani nyumbani kwa marehemu huyu lau taarifa za msiba zimeshafika hapaonekani watu kukusanyika nje nyumbani kwake.

Hili dogo.
Lililofanywa na msikiti wa jirani ndilo kubwa.

Waliufunga msikiti wao ili wasiitwe kushiriki kwa chochote katika msiba wa marehemu huyu.

Waliokwenda msikitini ama kwa kutoa taarifa au kuchukua jeneza hawakukuta mtu.

Lakini wakubwa wa serikali na chama wamefika nyumbani kwa marehemu.
Hali waliyoikuta pale iliwasononesha sana na kupita kiasi.

Iko siku nimekaa nazungumza na Mzee Aboud Jumbe nyumbani kwake Mji Mwema.

Wakati huo wa kifo cha marehemu huyu yeye alikuwa Makamo wa Rais.

Mzee Jumbe anasema yeye ndiye aliyetoa wazo kuwa vijana wa TANU Youth League haraka wakusanywe waletwe nyumbani kwa marehemu kusimamia maziko.

Mtu mmoja kamkuta mwenzie kwenye barza nje ya hoteli anacheza dhumna.

Anamwambia, ‘’Eee bwana we hebu acha huo mchezo twende mazikoni.’’
Mwenzie anamjibu, ‘’Kwani nani kafariki?

Anamtajia jina ingawa anajua kuwa anamcheza shere kwani Dar es Salaam nzima ilikuwa na taarifa.

Hampi jibu anabakia kimya anaendelea na mchezo na waliomzunguka kuangalia mchezo wito ule wa kwenda mazikoni pia unawahusu lakini na wao wamempuuza wako kimya wameshughulishwa na dhumna.

Sasa anawapigia kelele wote wale.
‘’Jamani Eeeh! Twendeni mazikoni.’’

Anajibiwa, ‘’Hii ni fardhi kifaya ukienda wewe kuzika umetuondolea sote dhima mbele ya Allah.’’

Ndugu yao hakutaka kuendelea taratibu alijiondoa mahali pale.

Huyu marehemu aliwafanyia nini nduguze kiasi cha wao kumsusa katika umauti wake?

Ninaitalii upya taazia aliyoandika Mohamed Mlamali Adam katika jarida la Africa Events kuhusu kiongozi mmoja Zanzibar aliyefariki zaidi ya miaka 30 sasa.

Mlamali ni Sheikh.

Sijapatapo kuchoka kuikumbuka taazia hii kwa sababu nashindwa kuiweka mahali pake kuwa ni taazia au kitu kingine cha ‘’satire,’’ yaani kichekesho kumfanya msomaji badala ya kuingiwa na majonzi ya kifo acheke.

Unafanya nini unapomuona mtu anacheza muziki kwa furaha akifurahi msiba mkononi kashika chupa ya bia?

Ikiwa utacheka ni kicheko lakini si kicheko kama kicheko kinavyofahamika.
 
Tuko vizuriii
1000082447.jpg
 
wenye mamlaka wajirekebishe --- kama wana akili waunganishe dots wajitafakari upya
 
Watanzania tumesha ambiwa kuwa kifo ni kifo tu, kwa hiyo ni maamuzi yako tu unaweza sherekea au kuto-kusherekea.
Hapohapo dishi limekamata usiachie, angekuwa na uchungu wa kweli angehusianisha anachoandika na kauli hii kwenye moja ya aya zake. Nami nimalizie kusema kwa mwalimu wangu Mohamed kuwa “usiangalie ulipodondokea bali angalia ulipojikwaa”
Wasalaam.
 
Kwa wafiwa kuna mke na watoto, kwao ni baba, KIONGOZI wa familia na mume pia.. watapata huzuni kwa jinsi walivyoishi nae, alivyowapambania ugali wa nyumbani upatikane na vya nyongeza.

Kwetu sisi alikuwa KIONGOZI je, alifanya mazuri kiasi cha sisi kupata huzuni na mauti yake.
tuishi vema na watu, tupendane, tutende wema.
Nyerere watu walilia sana unadhani ni kisa tu alikuwa rais hapana, je kilio cha Nyerere,magufuli, mkapa na mwinyi vinafanana!?? Wote hao ni maraisi wetu kuna walioliliwa kwa uchungu, kuna wengine kawaida.

Sasa huyu wa msoga ama pandikizi lake akianguka usishangae watu wakanywa na pombe kabisa, na kufunga vibwebwe.
 
Tuitengeneze kesho yetu iliobora kwa jamii, sasa hivi kuna mpasuko mkubwa kati ya wananchi na Viongozi. Kama Taifa tunapoelekea ni pabaya sana, Uzalendo unazikwa hivi hivi tukiona, Wananchi wameshaiona kama Tanzania imeporwa na Viongozi (CCM) nani abadilike ? Mwananchi ama CCM ?
 
Kwa sababu viongozi siku hizi hawana uchungu na wananchi wao. sasa kwa nini wasisheherekee?
 
%Hapohapo dishi limekamata usiachie, angekuwa na uchungu wa kweli angehusianisha anachoandika na kauli hii kwenye moja ya aya zake. Nami nimalizie kusema kwa mwalimu wangu Mohamed kuwa “usiangalie ulipodondokea bali angalia ulipojikwaa”
Wasalaam.

Hapohapo dishi limekamata usiachie, angekuwa na uchungu wa kweli angehusianisha anachoandika na kauli hii kwenye moja ya aya zake. Nami nimalizie kusema kwa mwalimu wangu Mohamed kuwa “usiangalie ulipodondokea bali angalia ulipojikwaa”
Wasalaam.
Hatari sana mkuu. Taratibu taratibu hata wale waliopo nyumba nyeupe kuna situ hali itakuwa tofauti. Tuishi kwa amani na haki kwa kila binadamu. 🙏
 
Kwa viongozi makini mzee wangu hii ni ishara mbaya sana.kuna ufa mkubwa kati ya viongozi na wananchi.ukiacha maneno ya kejeli hawa mabwana wanaiba sana bila aibu.wananchi wanaanza kuamka kidogo kidogo kwenye usingizi wa pono.Mungu atuepushe na hili balaa.
 
Kwanini mnazunguka?

Utamaduni wa kushangilia vifo umeanza lini na chanzo ni nini?
 
KITU GANI HIKI WATU KUSHEHEREKEA MAUTI?

Nimeinamisha kichwa changu toka alfajir nawaza hili la watu kusheherekea kifo.

Mtume (SAW) katuasa kasema tuseme mema ya maiti zetu.
Hawa wamepitiliza angalau wangesema.

Hawa wanacheza ngoma kusheherekea kifo.
Nimeinamisha kichwa changu nawafikiria watoto na mke wa marehemu.

Msiba walionao wa mpendwa wao unawatosha hapana haja ya kuwabebesha na hili.

Lilipata kutokea jambo kama hili Dar es Salaam katika miaka ya 1970.
Bwana mkubwa mmoja kapata ajali kafariki dunia.

Mtu mkubwa sana huyu kisha mpigania uhuru na katika wanachama wa mwanzo wa TANU na mtu aliyekuwa karibu sana na Mwalimu Nyerere.

Waliokuwa wanamjua wanasema alikuwa hana miadi ya Mwalimu anawekwenda kwake iwe Ikulu au nyumbani kwa Mwalimu muda wowote na atapokelewa.

Mji wa Dar es Salaam wote una taarifa ya kifo cha bwana huyu.
Jambo la kushangaza.

Kwa kawaida sisi watu wa Pwani msiba ukitokea tu kitu cha kwanza ni kupelea taarifa msikitini kisha nyumbani panafungwa maturubai nje na kutandika majamvi kwa kivuli na watu kukaa.

Na huwa haichukui muda nje barazani watu huanza kujazana.

Wanaume wanakaa barazani wanawake uani na ikiwa ua mdogo hautoshi watatengewa nyumba ya jirani.

Msibani nyumbani kwa marehemu huyu lau taarifa za msiba zimeshafika hapaonekani watu kukusanyika nje nyumbani kwake.

Hili dogo.
Lililofanywa na msikiti wa jirani ndilo kubwa.

Waliufunga msikiti wao ili wasiitwe kushiriki kwa chochote katika msiba wa marehemu huyu.

Waliokwenda msikitini ama kwa kutoa taarifa au kuchukua jeneza hawakukuta mtu.

Lakini wakubwa wa serikali na chama wamefika nyumbani kwa marehemu.
Hali waliyoikuta pale iliwasononesha sana na kupita kiasi.

Iko siku nimekaa nazungumza na Mzee Aboud Jumbe nyumbani kwake Mji Mwema.

Wakati huo wa kifo cha marehemu huyu yeye alikuwa Makamo wa Rais.

Mzee Jumbe anasema yeye ndiye aliyetoa wazo kuwa vijana wa TANU Youth League haraka wakusanywe waletwe nyumbani kwa marehemu kusimamia maziko.

Mtu mmoja kamkuta mwenzie kwenye barza nje ya hoteli anacheza dhumna.

Anamwambia, ‘’Eee bwana we hebu acha huo mchezo twende mazikoni.’’
Mwenzie anamjibu, ‘’Kwani nani kafariki?

Anamtajia jina ingawa anajua kuwa anamcheza shere kwani Dar es Salaam nzima ilikuwa na taarifa.

Hampi jibu anabakia kimya anaendelea na mchezo na waliomzunguka kuangalia mchezo wito ule wa kwenda mazikoni pia unawahusu lakini na wao wamempuuza wako kimya wameshughulishwa na dhumna.

Sasa anawapigia kelele wote wale.
‘’Jamani Eeeh! Twendeni mazikoni.’’

Anajibiwa, ‘’Hii ni fardhi kifaya ukienda wewe kuzika umetuondolea sote dhima mbele ya Allah.’’

Ndugu yao hakutaka kuendelea taratibu alijiondoa mahali pale.

Huyu marehemu aliwafanyia nini nduguze kiasi cha wao kumsusa katika umauti wake?

Ninaitalii upya taazia aliyoandika Mohamed Mlamali Adam katika jarida la Africa Events kuhusu kiongozi mmoja Zanzibar aliyefariki zaidi ya miaka 30 sasa.

Mlamali ni Sheikh.

Sijapatapo kuchoka kuikumbuka taazia hii kwa sababu nashindwa kuiweka mahali pake kuwa ni taazia au kitu kingine cha ‘’satire,’’ yaani kichekesho kumfanya msomaji badala ya kuingiwa na majonzi ya kifo acheke.

Unafanya nini unapomuona mtu anacheza muziki kwa furaha akifurahi msiba mkononi kashika chupa ya bia?

Ikiwa utacheka ni kicheko lakini si kicheko kama kicheko kinavyofahamika.
Mzee Mohamed Said ukipata muda malizia hili kisa, kuna kitu cha kujifunza.
 
KITU GANI HIKI WATU KUSHEHEREKEA MAUTI?

Nimeinamisha kichwa changu toka alfajir nawaza hili la watu kusheherekea kifo.

Mtume (SAW) katuasa kasema tuseme mema ya maiti zetu.
Hawa wamepitiliza angalau wangesema.

Hawa wanacheza ngoma kusheherekea kifo.
Nimeinamisha kichwa changu nawafikiria watoto na mke wa marehemu.

Msiba walionao wa mpendwa wao unawatosha hapana haja ya kuwabebesha na hili.

Lilipata kutokea jambo kama hili Dar es Salaam katika miaka ya 1970.
Bwana mkubwa mmoja kapata ajali kafariki dunia.

Mtu mkubwa sana huyu kisha mpigania uhuru na katika wanachama wa mwanzo wa TANU na mtu aliyekuwa karibu sana na Mwalimu Nyerere.

Waliokuwa wanamjua wanasema alikuwa hana miadi ya Mwalimu anawekwenda kwake iwe Ikulu au nyumbani kwa Mwalimu muda wowote na atapokelewa.

Mji wa Dar es Salaam wote una taarifa ya kifo cha bwana huyu.
Jambo la kushangaza.

Kwa kawaida sisi watu wa Pwani msiba ukitokea tu kitu cha kwanza ni kupelea taarifa msikitini kisha nyumbani panafungwa maturubai nje na kutandika majamvi kwa kivuli na watu kukaa.

Na huwa haichukui muda nje barazani watu huanza kujazana.

Wanaume wanakaa barazani wanawake uani na ikiwa ua mdogo hautoshi watatengewa nyumba ya jirani.

Msibani nyumbani kwa marehemu huyu lau taarifa za msiba zimeshafika hapaonekani watu kukusanyika nje nyumbani kwake.

Hili dogo.
Lililofanywa na msikiti wa jirani ndilo kubwa.

Waliufunga msikiti wao ili wasiitwe kushiriki kwa chochote katika msiba wa marehemu huyu.

Waliokwenda msikitini ama kwa kutoa taarifa au kuchukua jeneza hawakukuta mtu.

Lakini wakubwa wa serikali na chama wamefika nyumbani kwa marehemu.
Hali waliyoikuta pale iliwasononesha sana na kupita kiasi.

Iko siku nimekaa nazungumza na Mzee Aboud Jumbe nyumbani kwake Mji Mwema.

Wakati huo wa kifo cha marehemu huyu yeye alikuwa Makamo wa Rais.

Mzee Jumbe anasema yeye ndiye aliyetoa wazo kuwa vijana wa TANU Youth League haraka wakusanywe waletwe nyumbani kwa marehemu kusimamia maziko.

Mtu mmoja kamkuta mwenzie kwenye barza nje ya hoteli anacheza dhumna.

Anamwambia, ‘’Eee bwana we hebu acha huo mchezo twende mazikoni.’’
Mwenzie anamjibu, ‘’Kwani nani kafariki?

Anamtajia jina ingawa anajua kuwa anamcheza shere kwani Dar es Salaam nzima ilikuwa na taarifa.

Hampi jibu anabakia kimya anaendelea na mchezo na waliomzunguka kuangalia mchezo wito ule wa kwenda mazikoni pia unawahusu lakini na wao wamempuuza wako kimya wameshughulishwa na dhumna.

Sasa anawapigia kelele wote wale.
‘’Jamani Eeeh! Twendeni mazikoni.’’

Anajibiwa, ‘’Hii ni fardhi kifaya ukienda wewe kuzika umetuondolea sote dhima mbele ya Allah.’’

Ndugu yao hakutaka kuendelea taratibu alijiondoa mahali pale.

Huyu marehemu aliwafanyia nini nduguze kiasi cha wao kumsusa katika umauti wake?

Ninaitalii upya taazia aliyoandika Mohamed Mlamali Adam katika jarida la Africa Events kuhusu kiongozi mmoja Zanzibar aliyefariki zaidi ya miaka 30 sasa.

Mlamali ni Sheikh.

Sijapatapo kuchoka kuikumbuka taazia hii kwa sababu nashindwa kuiweka mahali pake kuwa ni taazia au kitu kingine cha ‘’satire,’’ yaani kichekesho kumfanya msomaji badala ya kuingiwa na majonzi ya kifo acheke.

Unafanya nini unapomuona mtu anacheza muziki kwa furaha akifurahi msiba mkononi kashika chupa ya bia?

Ikiwa utacheka ni kicheko lakini si kicheko kama kicheko kinavyofahamika.
Hivi huyu mzee yupo kweli maana kapiga kimya kweli kweli
 
Back
Top Bottom