Kakke
JF-Expert Member
- Dec 4, 2010
- 1,883
- 1,483
- Thread starter
- #21
Na Boniface Meena, Mwananchi
Posted Novemba22 2014 saa 11:36 AM
Kwa ufupi
- Kauli hiyo ya Zungu aliitoa jana bungeni baada ya wabunge kuanza kuhoji kuwapo kwa taarifa za barua ya mahakama kutaka kuzuia mjadala wa ripoti hiyo.
SHARE THIS STORY
0
inShare
inShare
Dodoma. Mwenyekiti wa Bunge, Muss Azzan Zungu amesema kuwa ripoti ya uchunguzi wa sakata la Tegeta Escrow itawasilishwa bungeni kama ilivyopangwa na kwamba hakuna zuio lolote la mahakama linalotaka suala hilo lisijadiliwe bungeni.
Kauli hiyo ya Zungu aliitoa jana bungeni baada ya wabunge kuanza kuhoji kuwapo kwa taarifa za barua ya mahakama kutaka kuzuia mjadala wa ripoti hiyo.
Zungu ambaye pia ni Mbunge wa Ilala (CCM) alisema, Nitoe taarifa tu ya kiti kwamba hakuna barua yoyote ya mahakama iliyozuia kujadili Escrow. Uhusiano wa Bunge na mahakama ni mzuri mno, alisema Zungu na kuongeza:
Hakuna katazo lolote, hakuna zuio lolote.
Alisema ripoti hiyo itawasilishwa na Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) inayoongozwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini(Chadema), Zitto Kabwe kama ilivyopangwa.
Juzi na jana madai ya kuwapo kwa barua hiyo yalizua mtafaruku bungeni na wabunge wa pande zote mbili waliwasha moto wakitaka kujua kama kuna ukweli wowote kuhusu barua hiyo.
Wabunge David Kafulila (Kigoma Kusini), Esther Bulaya (Viti Maalumu), Lekule Laizer (Longido), Peter Msigwa (Iringa Mjini), James Lembeli (Kahama) na Tundu Lissu (Iramba Mashariki) walitaka kujua ukweli kuhusu barua hiyo na kama kweli ipo basi jaji aliyeiandika awekwe mezani ili ajadiliwe.
Hali hiyo ilimfanya Naibu Spika, Job Ndugai juzi kusema, Mambo haya ni magumu sana. Kazi ya Jaji Mkuu ni kulinda mhimili wa mahakama tena kwa wivu kabisa na kazi ya Spika ni kulinda Bunge tena kwa wivu mkubwa. Alipoyasema hayo alishangiliwa na wabunge.
Alisema wakati Sitta alipokuwa Spika aliwahi kuwaambia kuwa, tukiwa viongozi hatuwezi kutengeneza umoja katika maovu.
Ndugai alisema kutokana na kauli hiyo, Bunge haliwezi kuficha uovu katika jambo hilo na kwamba litashughulikiwa vizuri na haki itatendeka.