DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
“Kazi ya serikali ukiacha mambo ya ulinzi na usalama ni kutengeneza fursa kwenye maisha ya watu wake kwa kufungua fursa za wananchi kutengeneza ajira na biashara na katika hili Mama Samia amefanikiwa sana, wakati anaingia madarakani tulikuwa tunasajili miradi 207 tu leo tunasajili zaidi ya miradi 900 na ajira nyingi zimezalishwa. La pili ni serikali kuweka mazingira ya kupunguza gharama za maisha kwa watu wake ili kipato wanachopata kibaki mfukoni, serikali ya Mama Samia imeweza kupeleka kwa wananchi moja kwa moja kwenye mifuko yao zaidi ya shilingi Trilioni 5.7 na wananchi Milioni 11 wamenufaika.
Wananchi wamenufaika kupitia hatua muhimu nne ambazo ni kupitia mpango wa Kaya maskini ambapo alipeleka shilingi Bilioni 961 na watu Milioni 5 waliweza kunufaika, la pili ni kupitia programu yake ya ruzuku za mbolea, Bilioni 693 na wananchi Milioni 2.2 wamenufaika moja kwa moja.
Hatua nyingine ni kupitia programu ya elimu bila ada, Mama Samia amepeleka shilingi Trilioni 1.138 na wanafunzi zaidi ya Milioni 3 wamenufaika na hatua ya nne ni kupitia programu ya kuwakopesha wanafunzi wa elimu ya juu ambapo Shilingi Trilioni 2.607 zimekwenda kwa wanafunzi na hizi ni fedha ambazo kwa namna moja ama nyingine ilibidi wazazi wazilipe lakini zimebaki mifukoni mwao na ni serikali ya Mama Samia iliyosaidia fedha hizi zibaki mifukoni mwa mwananchi ziongeze kipato na zipunguze gharama za maisha.”- Prof. Kitila Mkumbo, Mwanasiasa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya 2025/30, akizungumza Moshi Mjini kwenye Kampeni za Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Oktoba Mosi, 2025.
Wananchi wamenufaika kupitia hatua muhimu nne ambazo ni kupitia mpango wa Kaya maskini ambapo alipeleka shilingi Bilioni 961 na watu Milioni 5 waliweza kunufaika, la pili ni kupitia programu yake ya ruzuku za mbolea, Bilioni 693 na wananchi Milioni 2.2 wamenufaika moja kwa moja.
Hatua nyingine ni kupitia programu ya elimu bila ada, Mama Samia amepeleka shilingi Trilioni 1.138 na wanafunzi zaidi ya Milioni 3 wamenufaika na hatua ya nne ni kupitia programu ya kuwakopesha wanafunzi wa elimu ya juu ambapo Shilingi Trilioni 2.607 zimekwenda kwa wanafunzi na hizi ni fedha ambazo kwa namna moja ama nyingine ilibidi wazazi wazilipe lakini zimebaki mifukoni mwao na ni serikali ya Mama Samia iliyosaidia fedha hizi zibaki mifukoni mwa mwananchi ziongeze kipato na zipunguze gharama za maisha.”- Prof. Kitila Mkumbo, Mwanasiasa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya 2025/30, akizungumza Moshi Mjini kwenye Kampeni za Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Oktoba Mosi, 2025.