Nancyjoa13
Senior Member
- May 18, 2018
- 167
- 97
"Serikali imeanzisha kitengo kipya cha kupokea malalamiko ya kodi na kitaratibiwa na Wizara ya Fedha na Mipango,
kitahusisha kupokea malalamiko kutoka kwa walipa kodi yakiwamo ya kuombwa rushwa na Watumishi wa Mamlaka ya Kodi TRA."
SERIKALI imependekeza kuchukua hatua za kisera na utawala kwa lengo la kuimarisha na kurahisisha ukusanyaji mapato ikiwemo kuanzisha kitengo huru cha kupokea malalamiko na taarifa za kodi kitakachoratibiwa na Wizara ya Fedha na Mipango. Kitengo hicho kitakuwa na jukumu la kupokea na kupitia malalamiko ya taarifa za kodi zitakazotolewa na walipakodi au watu wenye nia njema.
Aidha serikali inapendekeza kufanya marekebisho ya Sheria ya Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kwenye usimamizi wa viwango unaojumuisha ubora na usalama wa chakula na vipondozi ili Shirika la Viwango Tanzania (TBS) liendelee kusimamia eneo la chakula na vipodozi kwa ujumla kama ilivyo kuwa tangu mwaka 1975.
Serikali pia imependekeza kuimarisha na kurahisisha ukusanyaji mapato na kubuni mfumo wa kudhibiti michezo ya kubahatisha. Hayo yalisemwa bungeni jana na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alipokuwa akiwasilisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka ujao wa fedha.
Akizungumzia kuanzishwa kwa kitengo cha kodil; Waziri Mpango alisema;“Baadhi ya majukumu ya kitengo hiki ni kupokea malalamiko ya rushwa dhidi ya watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
“Pia kupokea malalamiko ya ukadiriaji wa kodi na uthamanishaji wa bidhaa usio wa haki wala uhalisia dhidi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania; Kupokea malalamiko ya matumizi ya nguvu katika ukusanyaji kodi dhidi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania; Kupokea malalamiko ya ufungaji wa biashara bila kufuata sheria na taratibu dhidi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania.” Kuhusu TFDA na TBS, Waziri Mpango alisema katika bajeti hiyo serikali inapendekeza kurekebisha sheria ya TFDA.
kitahusisha kupokea malalamiko kutoka kwa walipa kodi yakiwamo ya kuombwa rushwa na Watumishi wa Mamlaka ya Kodi TRA."
SERIKALI imependekeza kuchukua hatua za kisera na utawala kwa lengo la kuimarisha na kurahisisha ukusanyaji mapato ikiwemo kuanzisha kitengo huru cha kupokea malalamiko na taarifa za kodi kitakachoratibiwa na Wizara ya Fedha na Mipango. Kitengo hicho kitakuwa na jukumu la kupokea na kupitia malalamiko ya taarifa za kodi zitakazotolewa na walipakodi au watu wenye nia njema.
Aidha serikali inapendekeza kufanya marekebisho ya Sheria ya Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kwenye usimamizi wa viwango unaojumuisha ubora na usalama wa chakula na vipondozi ili Shirika la Viwango Tanzania (TBS) liendelee kusimamia eneo la chakula na vipodozi kwa ujumla kama ilivyo kuwa tangu mwaka 1975.
Serikali pia imependekeza kuimarisha na kurahisisha ukusanyaji mapato na kubuni mfumo wa kudhibiti michezo ya kubahatisha. Hayo yalisemwa bungeni jana na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alipokuwa akiwasilisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka ujao wa fedha.
Akizungumzia kuanzishwa kwa kitengo cha kodil; Waziri Mpango alisema;“Baadhi ya majukumu ya kitengo hiki ni kupokea malalamiko ya rushwa dhidi ya watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
“Pia kupokea malalamiko ya ukadiriaji wa kodi na uthamanishaji wa bidhaa usio wa haki wala uhalisia dhidi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania; Kupokea malalamiko ya matumizi ya nguvu katika ukusanyaji kodi dhidi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania; Kupokea malalamiko ya ufungaji wa biashara bila kufuata sheria na taratibu dhidi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania.” Kuhusu TFDA na TBS, Waziri Mpango alisema katika bajeti hiyo serikali inapendekeza kurekebisha sheria ya TFDA.