Kwetu-Mbagala
JF-Expert Member
- Jun 26, 2013
- 203
- 39
WanaJF, katika miaka ya hivi karibuni, ktk jamii na familia zetu, kumekua na mashamsham hasa wenzetu wanapofunga ndoa. Miongoni mwa shamrashamra hizo imekua ni kuwafanyia dada zetu 'sherehe ya jikoni' (kitchen party).Lengo kuu la sherehe hiyo ni kuwaandaa dada zetu ili waweze kutimiza vyema majukumu yao ya kifamilia ndani ya ndoa. Kwa sasa binafsi inashangaza kwa wanandoa wapya (pamoja na wadada kufanyia kparty) utakuta bw harusi kavaa shati limejikunja(halijanyooshwa), mabwana harusi wapya asubuhi tunakunywa nao chai magenge (inamaanisha asb wanatoka bila ya kuandaliwa chochote), wengine mpk jioni wanakula magengeni. Pia wengine ndani wiki moja wanaanza kuchepuka nje (inamaanisha kuwa ndani hawatosheki/waharidhishwi?).Hakika haya yananipa wasiwasi kuhusu kparty, je ni kweli zina faida au tunapoteza muda tu? Tafakari, chukua hatua.Karibuni Mbagala..