Kitachompata Iran, kitaweka Historia

Russia na China wame balance nguvu ya Marekani kijeshi na kiuchumi
Mkuu unaota au?china na Russia combined hawafikii military bases za USA,ndege za kijeshi,ikiwa ni pamoja na bajeti ya jeshi na hata satellites za jeshi wameachwa mbali sana.

Ukija kiuchumi ndio kabisa hapo ukijumlisha uchumi wa china na Russia bado hawafiki kwa USA,maana uchumi wa Russia tu umepitwa na Jimbo moja tu la USA California.

Mkuu karudie kusoma au kusikiliza ulipopatia hizo habari za uzushi,

World super power ni USA na si vinginevyo.
 
Habar wadau. Hivi naomba kujua hawa marekani ni kama wao wanapenda sana vita hivi wananchi wao wanajua madhara ya hizi vita huko wanakovamia? Natamani vita ambayo ije kupiganwa kwenye ardhi ya marekani ili nao wajue utamu wa vita. Huwa nashangaa sana humu jukwaani watu tunashabikia vita utadhani inakopiganwa ni game au wanaokufa sio watu.
 
Mbona wahusika wamesha jisema
 
Trump siyo mpenzi wa vita!
Hii imenikumbusha enzi zile za Ghaddaff watu walikuwa wanachangia kwamba akiingia kijeshi kwa Ghaddaff washirika wao Russia na China wataingilia lakini yalivyokuja tokea mpaka leo ni historia mzeee baba akakamatwa kwy mtaro wakampa kipigo cha paka mwizi. Kama naona Ayatollahs Khomeini yakimkuta ya sddam Hussein
 
Nimeona leo live Aljazeera na CNN......Saudi wameandaa press conference ya kama lisaa limoja wakionesha ushahidi kwamba Iran inahusika!
Wa Soudia..wabaya sana..
Wako radhi kumwaga damu za wengi kwa kuutetea ufalme wao...
Halafu ni wapotoshaji wakubwa ..na wanamkaribisha Us..tayari maadili na silka zao zinaanza kupotezwa.
Watakuja juta mbeleni huko!
 
Huyo mmarekani ..hiyo tec na maendeleo yake yote ni kazi ya Yahudi na Mjerumani!
 
Ok. Kinachomfanya Marekani hasite site kumshambulia Iran ni nini ?
 
Nani kakudanganya, marekani ni super power tuombe tu Mungu wasiipige Iran maana amani na utulivu wa eneo hilo vitapotea

Mkuu:
Ni vyema turejee ktk historia. Hivi Marekani ktk vita zote alizowahi kupigana nje ya nchi yake ni ipi aliyoshinda? (Anza na mfano wa Vietnam,Somalia nk..,).
 
Wamguse waone..

Iran ana backup ya Mrusi na Mchina ambao ni bitter rivals wa marekani
Mara ngapi marekani na washirika wake wameenda kuwapiga Iraq, Libya na hata Yugoslavia hao uliowataja CHINA NA RUSSIA waliingilia????

Je unafahamu WARSAW PACT ???? Je, unafahamu kuwa Yugoslavia na Russia ni washirika wamoja (yaani wala hamini)??? warusi walikuwa wapi wakt ule Yugoslavia ikipigwa kipigo cha mbwa mwitu?

Leo hii Eti America akimpiga Iran eti Watusi na wachina wataingilia. Kamwe haitatokea hao ni watu wa mdomo tu, utasikia tu wakilalamika.
America ni super power hao wote uliowataja wamewekewa vikwazo na America, yaani Russia & China. Jiulize mbona hao hawawezi kumwekea vikwazo America????
 
Mikwara ya marekani, ile meli wamerekani walitaka kuikamata adrian darya 1, ilienda ikatia nanga syria na kupumzika hapo kisha kuelekea Mediterranean na hamna aliyeigusa pamoja na vitisho vyote vya us...us walaini sana kwa mhajemi
 
Kwani America kapigana vita na Vietnam na Somalia tu. Jaza nyama taja na nchi zingine si hizo tu ulizotaja. Kuhusu Vietnam hasara waliopata wavietnam ilikuwa kubwa sana kuliko hicho unachodhani kuwa walishindwa pia vita vya somalia havikuwa na maslahi kwa marekani ndipo akaamua kujitoa. Nitajie kipi marekani angefaidi pale somalia km ww unavyofikiria?
Mkuu:
Ni vyema turejee ktk historia. Hivi Marekani ktk vita zote alizowahi kupigana nje ya nchi yake ni ipi aliyoshinda? (Anza na mfano wa Vietnam,Somalia nk..,).
 

Kwahiyo unadhani us anaweza kumpiga iran kama wewe unavyomchapa mdogo wako hapo kwenu?its a big men fight mzee, hamna mwenye uhakika wa kuchomoka hapo
 
Hahaha inashangaza sana watu wanaamini Iran kuwa na uwezo kupambana na USA.

Hawa ni mbingu na ardhi.

Taifa ambalo lina military base karibia elfu 5 kote duniani.

Taifa ambalo military budget yake inazidi kwa mbali jumla ya budget za nchi zote duniani.

China na urusi hata iweje hawawezi ingilia sehemu ambapo USA anapiga,watabakia kubwabwaja tu,lakini wanajua mataifa yao yana maslahi mapana na USA kuliko hayo maficho mengine.
 
Kwahiyo unadhani us anaweza kumpiga iran kama wewe unavyomchapa mdogo wako hapo kwenu?its a big men fight mzee, hamna mwenye uhakika wa kuchomoka hapo
Watu sijuwi kwa nini wana fananisha Libya na Iraq na iran technology hawajuwi kuwa Iran ipo masafa mengine kabisa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…