Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 10,890
- 18,836
Na R. Mwaruka. Unaweza kukisoma free ndani ya app ya Maktaba Sauti. Ipo playstore.
Hatuna hakika ya tarehe maalumu ya kusehelea, ila twafahamu hayo katika masimulizi ya mgawanyiko wa koo mbalimbali za Uzaramo ambazo nyingi zinasimuliwa kwamba zimetoka katika makabila mengine ya Kibantu na kujiunga katika Uzaramo. Lakini wazee wengi wanakubaliana kwamba mkubwa wa Uzaramo alikuwa Pazi Kilama Lukali mwenye asili ya Ukutu.
Pazi huyo aliitwa kwa majina mbalimbali ya ushujaa na kutukuzwa kama hivi ‘Pazi Kibamandu, kihabamanduka na Ulanga wela', maana yake, ‘Pazi Kifuniko, Kikifunuka na mbinguni kweupe!' Na tena aliitwa 'Mwana Mkungwi pala' na 'Mwana Mwizila Kumogo', maana yake 'Mwana wa Utukufu' na 'Mwana ajiwaye kwa heshima'. Na katika kutukuzwa kwake aliitwa 'Gulu Jasi' yaani, 'Mfalme Mkuu'.
Pazi huyo asili yake hasa alitoka Kibwemandu, katika Ukutu, nchi iliyo sasa magharibi ya Uzaramo. Kwa upande mwingine ndio sababu aliitwa Pazi Kibamandu. Ukoo wake ni Mulugoma, na mtala wake ni Kilama na Lukali. Baba yake aliitwa Pazi Mvilama. Huyu Pazi Mvilama alimwoa Mulambena katika kizazi cha Nyambiza, akamzaa Pazi Kilama.
Pazi Kilama aliondokea kuwa shujaa tangu alipokuwa mvulana, maana alikuwa hashindiki katika mapigano na watoto wengine. Alikuwa hodari katika kutupa mishale na mikuki katika uwindaji. Alipokuwa mtu mzima, watu wakamheshimu kwa sababu ya ushujaa wake, maana katika vita vya kabila yeye aliweza kuongoza jeshi na kuwashinda adui. Kwa ajili hiyo, wakamtukuza na kumwita Gulu Jasi. Na kila mtu aliyekwenda mbele yake kumwamkia alijiinamisha na kunyoosha mikono yake mbele na kusema, 'Simbamwenee'! Na Pazi aliitikia, ‘Utwaa!' Kisha mtu huyo humwita kwa jina lake, 'Pazi'! Na Pazi hujibu, ‘Nene Mwana Mkungwi pala, Mwana Mwizila kumogo'. Maamkio hayo ndiyo yaliyotumika katika utawala wa Pazi.
Lakini jambo la kusikitisha ni ya kwamba maamkio hayo ya asili yalianza kupotea baada ya kuingia Waarabu nchi hii. Watu wote waliwatukuza Waarabu na kumheshimu Sultani Said, ndipo maamkio yakawa hivi: aamkiaye husema, 'Mwinyi'! maana yake ‘Bwana' na aitikiaye hujibu, 'Mwinyi Mkuu Saidi', yaani bwana mkubwa ni Saidi tu. Na kwa sababu ya watumwa kuwaheshimu mabwana zao amkio la 'shikamoo' likatukuka zaidi. Shikamoo ni neno lenye maneno mawili pamoja, yaani, 'Nashika miuu'. Miuu maana yake ni miguu, kwa Kimwambao, na umoja wake ni muu. Kwa sababu ya mabadiliko ya matamshi baadaye ikawa ‘shikamuu' na siku hizi ni 'Shikamoo'. Marahaba maana yake ni 'Ahsante'. Kumheshimu mtu kwa kumshika miguu ni adabu nzuri ikiwa mwenye kuamkia anaifahamu maana yake.
Basi tuendelee na habari za Pazi. Pazi alikuwa na miji yake miwili, wa kwanza uliitwa Zongomelo, na wa pili ulikuwa Kinyangulu. Miji hiyo miwili ndiyo iliyokuwa ikivuma kwa fahari ya Pazi Kilama. Pazi alikuwa na dada zake wanne ambao nao walitoa vizazi vya wapwa wa Pazi. Dada zake walikuwa hawa:
(1) Nyamhazi (2) Mulalukali (3) Vinhama, na (4) Matata- hala. Mzao wa wapwa wa Pazi kwa maumbu zake ulikuwa hivi:
Nyamhazi alimzaa Temodimogoke na dada zake wawili, Kidang’hali na Kitumbe. Mulalukali alimzaa Hega. Vinhama aliolewa na Mluguru akamzaa Kingalu. Na Matatahala aliolewa na Mdowe akamzaa Mwene.
Pazi Kilama alikuwa na ndugu zake wawili waliozaliwa kwa baba na mama zao mbalimbali, nao ni Nyamitombo na Dilunga. Huyu Dilunga alikuwa na wapwa zake sita wanaohusika katika urithi wa Uzaramo, nao ni Bofi, Lugeng'he, Malamula, Ditali, Zamvi na Lunyovu; hawa waliishi pamoja na Pazi Gulu Jasi kule Kinyangulu.
Sifa zake Pazi Kilama zinafahamika kwamba alikuwa mkakamavu, nywele zake zilikuwa ndefu hata mara nyingine zilifunika uso wake, nazo hazikunyolewa tangu utoto wake, alikuwa na umbo la kutisha. Mara kwa mara alionekana akitembea na mbwa wake mkubwa aliyefanana na chui, huyu alimtumia zaidi katika mawindo. Watu waliokutana naye hawakuthubutu kumkaribia kwa jinsi alivyojipamba kishujaa. Kinyangulu ni mahali pazuri penye udongo wenye rutuba uwezao kustawisha aina nyingi za mimea.
Mahali alipoishi Pazi palijengwa ngome imara ya kukinga maadui wa kila upande. Ngome hiyo ilizungushiwa miti imara, na mji wa Pazi ulikuwa katikati ya ngome. Ngome ya namna hii iliitwa 'mhongono'. Ngome hiyo ililindwa na askari hodari wenye silaha. Kila siku askari sita walikuwa na zamu ya kuilinda ngome.
Mke wa Pazi Kilama alikuwa Mulamtumbikwa, na kwa sababu alikuwa mke wa Sultani aliitwa 'Sano'. Sano maana yake ni 'Bibi mheshimiwa' au Malkia. Pazi Kilama alijulikana sana tangu Ukutu mpaka Zaramo ya Mwambao. Watu wengi wa nyakati zile walimtegemea kwa sababu ya ushujaa wake. Katika siku alizoishi kule Kinyangulu huko pwani ya Mzizima, Wakamba waliingia na kuanza kuihujumu nchi hii. Vita na unyang'anyi wa Wakamba uliwafanya Wamashomvi walioishi mwambao kutawanyika huko na huko. Wengine walikimbilia visiwani, na wengine walikimbilia bara ya Uzaramo wakajificha misituni. Wakati huo Pazi Kilama hakuwa na habari yo yote juu ya Wakamba walioingia Mzizima. Wakamba walikuwa jeuri na hodari kwa mapigano, nao waliwaogofisha mno watu walioishi Zaramo ya Mwambao siku zile.
SURA YA 1
PAZI KILAMA KATIKA UZARAMO
WAZARAMO ni jumla ya mchanganyiko wa makabila ya Kibantu. Sehemu kubwa ya mchanganyiko huo ni Wakutu na watu wengine wenye asili ya Mwambao. Neno hili 'Uzaramo' linatokana katika 'Kuzalama' na maana yake ni 'Kusehelea'. Kwa hivi, Wazaramo hasa maana yake ni Waseheleaji, yaani watu waliotoka katika nchi mbalimbali na kufanya masikani katika nchi hii. Mabadiliko ya neno hili yalitokea kwa sababu ya matamshi ya watu; neno lenyewe hasa ni Zalamo, yaani nchi iliyosehelewa, lakini baadaye ikabadilika na kuwa Zaramo au pengine hutamkwa Zaramu.PAZI KILAMA KATIKA UZARAMO
Hatuna hakika ya tarehe maalumu ya kusehelea, ila twafahamu hayo katika masimulizi ya mgawanyiko wa koo mbalimbali za Uzaramo ambazo nyingi zinasimuliwa kwamba zimetoka katika makabila mengine ya Kibantu na kujiunga katika Uzaramo. Lakini wazee wengi wanakubaliana kwamba mkubwa wa Uzaramo alikuwa Pazi Kilama Lukali mwenye asili ya Ukutu.
Pazi huyo aliitwa kwa majina mbalimbali ya ushujaa na kutukuzwa kama hivi ‘Pazi Kibamandu, kihabamanduka na Ulanga wela', maana yake, ‘Pazi Kifuniko, Kikifunuka na mbinguni kweupe!' Na tena aliitwa 'Mwana Mkungwi pala' na 'Mwana Mwizila Kumogo', maana yake 'Mwana wa Utukufu' na 'Mwana ajiwaye kwa heshima'. Na katika kutukuzwa kwake aliitwa 'Gulu Jasi' yaani, 'Mfalme Mkuu'.
Pazi huyo asili yake hasa alitoka Kibwemandu, katika Ukutu, nchi iliyo sasa magharibi ya Uzaramo. Kwa upande mwingine ndio sababu aliitwa Pazi Kibamandu. Ukoo wake ni Mulugoma, na mtala wake ni Kilama na Lukali. Baba yake aliitwa Pazi Mvilama. Huyu Pazi Mvilama alimwoa Mulambena katika kizazi cha Nyambiza, akamzaa Pazi Kilama.
Pazi Kilama aliondokea kuwa shujaa tangu alipokuwa mvulana, maana alikuwa hashindiki katika mapigano na watoto wengine. Alikuwa hodari katika kutupa mishale na mikuki katika uwindaji. Alipokuwa mtu mzima, watu wakamheshimu kwa sababu ya ushujaa wake, maana katika vita vya kabila yeye aliweza kuongoza jeshi na kuwashinda adui. Kwa ajili hiyo, wakamtukuza na kumwita Gulu Jasi. Na kila mtu aliyekwenda mbele yake kumwamkia alijiinamisha na kunyoosha mikono yake mbele na kusema, 'Simbamwenee'! Na Pazi aliitikia, ‘Utwaa!' Kisha mtu huyo humwita kwa jina lake, 'Pazi'! Na Pazi hujibu, ‘Nene Mwana Mkungwi pala, Mwana Mwizila kumogo'. Maamkio hayo ndiyo yaliyotumika katika utawala wa Pazi.
Lakini jambo la kusikitisha ni ya kwamba maamkio hayo ya asili yalianza kupotea baada ya kuingia Waarabu nchi hii. Watu wote waliwatukuza Waarabu na kumheshimu Sultani Said, ndipo maamkio yakawa hivi: aamkiaye husema, 'Mwinyi'! maana yake ‘Bwana' na aitikiaye hujibu, 'Mwinyi Mkuu Saidi', yaani bwana mkubwa ni Saidi tu. Na kwa sababu ya watumwa kuwaheshimu mabwana zao amkio la 'shikamoo' likatukuka zaidi. Shikamoo ni neno lenye maneno mawili pamoja, yaani, 'Nashika miuu'. Miuu maana yake ni miguu, kwa Kimwambao, na umoja wake ni muu. Kwa sababu ya mabadiliko ya matamshi baadaye ikawa ‘shikamuu' na siku hizi ni 'Shikamoo'. Marahaba maana yake ni 'Ahsante'. Kumheshimu mtu kwa kumshika miguu ni adabu nzuri ikiwa mwenye kuamkia anaifahamu maana yake.
Basi tuendelee na habari za Pazi. Pazi alikuwa na miji yake miwili, wa kwanza uliitwa Zongomelo, na wa pili ulikuwa Kinyangulu. Miji hiyo miwili ndiyo iliyokuwa ikivuma kwa fahari ya Pazi Kilama. Pazi alikuwa na dada zake wanne ambao nao walitoa vizazi vya wapwa wa Pazi. Dada zake walikuwa hawa:
(1) Nyamhazi (2) Mulalukali (3) Vinhama, na (4) Matata- hala. Mzao wa wapwa wa Pazi kwa maumbu zake ulikuwa hivi:
Nyamhazi alimzaa Temodimogoke na dada zake wawili, Kidang’hali na Kitumbe. Mulalukali alimzaa Hega. Vinhama aliolewa na Mluguru akamzaa Kingalu. Na Matatahala aliolewa na Mdowe akamzaa Mwene.
Pazi Kilama alikuwa na ndugu zake wawili waliozaliwa kwa baba na mama zao mbalimbali, nao ni Nyamitombo na Dilunga. Huyu Dilunga alikuwa na wapwa zake sita wanaohusika katika urithi wa Uzaramo, nao ni Bofi, Lugeng'he, Malamula, Ditali, Zamvi na Lunyovu; hawa waliishi pamoja na Pazi Gulu Jasi kule Kinyangulu.
Sifa zake Pazi Kilama zinafahamika kwamba alikuwa mkakamavu, nywele zake zilikuwa ndefu hata mara nyingine zilifunika uso wake, nazo hazikunyolewa tangu utoto wake, alikuwa na umbo la kutisha. Mara kwa mara alionekana akitembea na mbwa wake mkubwa aliyefanana na chui, huyu alimtumia zaidi katika mawindo. Watu waliokutana naye hawakuthubutu kumkaribia kwa jinsi alivyojipamba kishujaa. Kinyangulu ni mahali pazuri penye udongo wenye rutuba uwezao kustawisha aina nyingi za mimea.
Mahali alipoishi Pazi palijengwa ngome imara ya kukinga maadui wa kila upande. Ngome hiyo ilizungushiwa miti imara, na mji wa Pazi ulikuwa katikati ya ngome. Ngome ya namna hii iliitwa 'mhongono'. Ngome hiyo ililindwa na askari hodari wenye silaha. Kila siku askari sita walikuwa na zamu ya kuilinda ngome.
Mke wa Pazi Kilama alikuwa Mulamtumbikwa, na kwa sababu alikuwa mke wa Sultani aliitwa 'Sano'. Sano maana yake ni 'Bibi mheshimiwa' au Malkia. Pazi Kilama alijulikana sana tangu Ukutu mpaka Zaramo ya Mwambao. Watu wengi wa nyakati zile walimtegemea kwa sababu ya ushujaa wake. Katika siku alizoishi kule Kinyangulu huko pwani ya Mzizima, Wakamba waliingia na kuanza kuihujumu nchi hii. Vita na unyang'anyi wa Wakamba uliwafanya Wamashomvi walioishi mwambao kutawanyika huko na huko. Wengine walikimbilia visiwani, na wengine walikimbilia bara ya Uzaramo wakajificha misituni. Wakati huo Pazi Kilama hakuwa na habari yo yote juu ya Wakamba walioingia Mzizima. Wakamba walikuwa jeuri na hodari kwa mapigano, nao waliwaogofisha mno watu walioishi Zaramo ya Mwambao siku zile.