Kitabu kipya: Dola, Kanisa na Tatizo la Udini Tanzania

Mkuu, nimecheka sana, imebidi niende kwenye uzi wake nione hiyo picha ya avator yake, kweli kaweka picha ya Coca Cola. Haa ha haha, halafu anashindwa kutuwekea hayo majarida yalionukuu HOJA zke huko kwenye vyuo "bora". Anyway, back to the topic; kujua kama Nyerere ndiye aliyewadidimiza Waislamu au la ni hivi, kwanini majarida yake huyu mzee anayapeleka kwenye vyuo vya nchi ambazo waislamu wengi wanadai ni za Kikristo badala ya kupeleka kwenye vyuo vya nchi za Kiislamu? Jibu lake ni rahisi tu, huko Uislamuni hawaheshimu elimu na ndicho walicho kiambukiza hadi huku kwa wamatumbi, na wenyewe hawapendi elimu halafu wanakuja kuilamu serikali kwa uzembe wao wenyewe. Gadafi pamoja na kutoa elimu bure kwa Walibya, je ni Walibywa wangapi walioamua kwa moyo mmoja kuwapeleka watoto wao shule? Juzi kati hapa nimeona kwenye taarifa ya habari ITV kwamba wanafunzi 17000 kule Lindi (Lindi ni miongoni mwa mikoa yenye waislamu wengi) wamegoma kuripoti shule/sekondari. Hapa na penyewe tuilamu serikali? Huwezi kuusambaza uislamu bila kueneza CHUKI, huwezi. Uislamu na chuki pamoja na fitina ni mapacha.
Mazindu...
Kwa kuleta suala la picha za chupa za Coca Cola sidhani kama ndiyo tunachojadili hapa.

Wala sijashindwa kuweka ''reviews,'' za vitabu vyangu.

''Reviews'' zote ninazo wala si kazi kubwa kuziweka hapa.

Nilichomweleza Ndjabu ni kuwa wala asijiitabishe kuwa nimeandika kitabu kwa kuwa hili linamsumbua kwa miaka mingi hapa Barzani.

Nimemwambia kuwa na achukulie kuwa mimi sijaandika chochote na kama sijaandika chochote ''review'' itatoka wapi?

Kinachonichekesha mimi kama wewe unavyocheka kuona picha za Coca Cola ni mtu kushughulishwa na ''review'' ya kitabu asishughulishwe na kitabu chenyewe.

Mimi nikikusoma na hizi kejeli za ''huyu mzee'' basi nakuwa nimeshakufahamu na wala sipati tabu na wewe kwani wewe si wa kwanza wala hutakuwa wa mwisho kunikejeli hadi ukweli utakapokudhihirikia.

Wengi wanaponifahamu taratibu heshima hurejea.

Wewe hunijui na inawezekana ndiyo mara yako ya kwanza kunisoma au kunisikia.

Nimeandika vitabu saba na kipo kingine In Shaa Allah kitabu cha nane kinakuja.

Ninazo pia ''paper'' kadhaa wala sijui hesabu yake nilizoandika kuwasilisha katika vyuo mbalimbali hapa nyumbani na nje ya mipaka ya Tanzania.

Lakini mimi furaha yangu huzidi pale unapotokea mtu kama wewe ukanikejeli.

Wala mimi sitakuuliza wewe umeandika nini kwani nakujua kutokana na unavyoandika na kujenga hoja hapa Barzani na kutiatia maneno ya Kiiingereza kuwa lipo tatizo.

Wewe kama nilivyomfahamisha mwenzio nakuomba jiaminishe kuwa mimi si lolote wala sijaandika chochote cha kutambulikana katika dunia ya usomi.

Hayo mengine wala sijaona haja ya kuyasemea.

Kitabu changu cha mwisho kimeingia Tanzania mwanzo wa mwaka huu hicho hapo chini pamoja na baadhi ya vingine.

Kitabu cha watoto nimekusudia kuwafunza Kiingereza na historia ya Zanzibar.

Sidhani kama bado unacheka.
 

Attachments

  • SYKES BOOK ALL EDITIONS.jpg
    SYKES BOOK ALL EDITIONS.jpg
    54.1 KB · Views: 5
  • THE SCHOOL TRIP GUGU.jpg
    THE SCHOOL TRIP GUGU.jpg
    71.5 KB · Views: 5
  • THE TORCH ON KILIMANJARO SECOND EDITION.png
    THE TORCH ON KILIMANJARO SECOND EDITION.png
    33.3 KB · Views: 5
McMahoon,

''Lakini tuende kielimu. Ninayo ripoti ya mwaka huu. Waliofanya mtihani wa darasa la saba kuingia darasa la tisa, asilimia 71 Waislamu. Asilimia 29 ni wengine. Walioshinda katika wale asilimia 71 ni asilimia 21. Katika wale 29 walioshinda tena sema mwenyewe. Katika asilimia 29 waliokwenda shuleni ni asilimia 79. Katika asilimia 71 waliokwenda darasa la tisa ni asilimia 21.

Sasa kuna moja, ama Waislamu wajinga ama akili yao haifanyi kazi, ama mtu ukiwa Muislamu wewe huna kitu, ama kuna kitu. Sasa namwomba Waziri anayehusika, anaposema aseme ya kwamba kwa hali ilivyo Waislamu wameumbwa wajinga. Au kwa hali ilivyo kuna sababu kadha, kadha. Mwalimu Nyerere alisema zamani ifanywe bidii ya kuwanyanyua waliokuwa chini. Sasa bidii hii siyo ya kuwanyanyua waliokuwa chini. Bidii hii ni ya kuwakandamiza waliokuwa chini.''

(Hotuba ya Mh. Kitwana Kondo (MB) aliyoitoa Bungeni Dodoma, 1999)

Mzee nimesoma alichoandika
Kitwana Kondo lakini sijaona ushahidi wowote ule kuthibitisha alichoandika

Nilitarajia kuona takwimu zilizoshiba ushahidi na sio porojo za aliyekusudia kuwajengea imani kuwa mnaonewa
 
Huu uzi ulipaswa kufungwa hapa.
Mohamed Said, Ukiona watu baada ya kutatua matatizo,kisayansi,wanaanza kuleta sababu,na kuhusisha dini,kabila na matatizo yaliyopo,basi ujue balaa limefika,

Kuna kipindi miaka hiyooo,Serikali baada ya kuona watoto kutoka shule za kagera wanafaulu sana kwenye mitiani,na kuchukua nafasi nyingi katika shule za serikali,iliamuliwa viwango vya kufaulu kwa mkoa was kagera vipandishwe!! Ili kudhibiti wingi wao!wala haikusaidia,wasomi nchi hii bado wanatoka kwa wingi mikoa ya Kagera,Mbeya,Kilimanjaro.

Sasa kama unatafuta kwanini mikoa ya Lindi na Mtwara,haina ufaulu wa kutosha,sabsbu sio ufaulu wa Kagera na mikoa mingine.

Nyerere hayupo tena,kuna mabaya alifsnya,je Mwinyi,Kikwete walishindwa kurekebisha!
Maana tukisema unajua sisi wa afrika,ni maskini,kwa sababu utumwa,ukoloni,na ukoloni mamboleo,umetuumiza sana,ndio maana hatuendeli kama wazungu,tutaendelea tu pale watakapo tuomba msamaha! What!!

Sasa kama ndio hivyo,Bakhresa,Mo,Dangote,Diamond,Ben Carson,Obama,walitoka wapi! Mbona wao ni wenzetu na wameendelea,?

There is no future in the past! Westage of time
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom