Kitabu cha Khamis Abdulla Ameir kipo tayari

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,915
30,259
KITABU CHA KHAMIS ABDULLA AMEIR KIPO TAYARI

Rafiki yangu mmoja katika uongozi wa juu Zanzibar na aliyeshuhudia yote yaliyotokea kabla na baada ya mapinduzi alipata kuniambia kuwa ili kuielewa historia ya Zanzibar inataka mtu apinde mgongo kuisoma.

Akaendelea kusema na ubongo wako ufungue uwe wazi kujifunza bila kutanguliza mbele hisia zako.

"Historia ya Zanzibar ni tofauti sana na historia ya kwenu Tanganyika.
Hivi mnavyotuona sisi Wanzanzibari sote sie ni ndugu.

Sote sisi Waislam.
Mkiyajua haya na kuyakubali hamtopata shida na sisi."

Sijayasahau maneno haya.

Kila kitabu cha historia ya Zanzibar kilichoandikwa na Wanzanzibar wenyewe nje ya waandishi walioko au walikuwa ndani ya "Mapinduzi Daima," ukifungua tu ukurasa wa kwanza utahisi kama vile vidole vyako vimeshika bakuli la bati la uji wa moto uliotoka jikoni huku unatokota.

Msomaji wangu kwanza ningependa utambue kuwa hiki niandikacho si pitio la kitabu.

Hapana la hasha.
Si pitio la kitabu.

Sijakimaliza kukisoma kitabu.

Lakini ninachoweza kueleza ni kuwa hiki si kitabu cha kawaida kama alivyo mwandishi wa kitabu hiki kuwa si mtu wa kawaida pia.

Si ajabu pia kwahiyo kuwa historia ya maisha ya Khamis Abdulla Ameir yasingeweza kuwa ya kawaida.

Yeyote awae yule atakaekuwa na ujasiri wa kukipitia kitabu hiki na kukichambua kitamuacha taabani na si yeye mptiaji bali na wasomaji wake sawia.

"The Eagle Has Landed."
Hii ilikuwa Apollo 11 ilipotua mwezini mwaka wa 1969.

Hapa kwetu nyumbani ni tai katua juu ya mti.
Kitabu hiki ni tai aliyetua juu ya mti tena mti wenyewe mjengaua ulioko uani kwetu.

1647708795012.png
 
Ameeleza kwamba aliyepindua ni John Okello


Zanzibar Revolution

Article Talk

Language

Download PDF

Watch

Edit

The Zanzibar Revolution (Arabic: ثورة زنجبار Thawrat Zanjibār) occurred in 1964 and led to the overthrow of the Sultan of Zanzibar and his mainly Arab government by local African revolutionaries. Zanzibar was an ethnically diverse state consisting of a number of islands off the east coast of Tanganyika which had been granted independence by Britain in 1963. In a series of parliamentary elections preceding independence, the Arab minority succeeded in retaining the hold on power it had inherited from Zanzibar's former existence as an overseas territory of Oman. Frustrated by under-representation in Parliament despite winning 54% of the vote in the July 1963 election, the mainly African Afro-Shirazi Party (ASP) allied itself with the left-wing multiracial Umma Party, and early in the morning of 12 January 1964 ASP member John Okello mobilised around 600–800 revolutionaries on the main island of Unguja (Zanzibar Island). Having overrun the country's police force and appropriated their weaponry, the insurgents proceeded to Zanzibar Town where they overthrew the Sultan and his government. Reprisals against Arab and South Asian civilians on the island followed; the resulting death toll is disputed, with estimates ranging from several hundred to 20,000. The moderate ASP leader Abeid Karume became the country's new president and head of state, and positions of power were granted to Umma party
 
KITABU CHA KHAMIS ABDULLA AMEIR KIPO TAYARI

Rafiki yangu mmoja katika uongozi wa juu Zanzibar na aliyeshuhudia yote yaliyotokea kabla na baada ya mapinduzi alipata kuniambia kuwa ili kuielewa historia ya Zanzibar inataka mtu apinde mgongo kuisoma.

Akaendelea kusema na ubongo wako ufungue uwe wazi kujifunza bila kutanguliza mbele hisia zako.

"Historia ya Zanzibar ni tofauti sana na historia ya kwenu Tanganyika.

Hivi mnavyotuona sisi Wanzanzibari sote sie ni ndugu.

Sote sisi Waislam.

Mkiyajua haya na kuyakubali hamtopata shida na sisi."

Sijayasahau maneno haya.

Kila kitabu cha historia ya Zanzibar kilichoandikwa na Wanzanzibar wenyewe nje ya waandishi walioko au walikuwa ndani ya "Mapinduzi Daima," ukifungua tu ukurasa wa kwanza utahisi kama vile vidole vyako vimeshika bakuli la bati la uji wa moto uliotoka jikoni huku unatokota.

Msomaji wangu kwanza ningependa utambue kuwa hiki niandikacho si pitio la kitabu.

Hapana la hasha.
Si pitio la kitabu.

Sijakimaliza kukisoma kitabu.

Lakini ninachoweza kueleza ni kuwa hiki si kitabu cha kawaida kama alivyo mwandishi wa kitabu hiki kuwa si mtu wa kawaida pia.

Si ajabu pia kwahiyo kuwa historia ya maisha ya Khamis Abdulla Ameir yasingeweza kuwa ya kawaida.

Yeyote awae yule atakaekuwa na ujasiri wa kukipitia kitabu hiki na kukichambua kitamuacha taabani na si yeye mptiaji bali na wasomaji wake sawia.

"The Eagle Has Landed."

Hii ilikuwa Apollo ilipotua mwezini mwaka wa 1969.

Hapa kwetu nyumbani ni tai katua juu ya mti.

Kitabu hiki ni tai aliyetua juu ya mti tena mti wenyewe mjengaua ulioko uani kwetu.
Umekisifia sana kitabu. Yes the Eagle has landed lakini angalau tuwekee picha ya hicho kitabu kwa mbele na nyuma. Mchapishaji wake ni nani? Kinapatikana wapi?
 
Ameeleza kwamba aliyepindua ni John Okello


Zanzibar Revolution

Article Talk

Language

Download PDF

Watch

Edit

The Zanzibar Revolution (Arabic: ثورة زنجبار Thawrat Zanjibār) occurred in 1964 and led to the overthrow of the Sultan of Zanzibar and his mainly Arab government by local African revolutionaries. Zanzibar was an ethnically diverse state consisting of a number of islands off the east coast of Tanganyika which had been granted independence by Britain in 1963. In a series of parliamentary elections preceding independence, the Arab minority succeeded in retaining the hold on power it had inherited from Zanzibar's former existence as an overseas territory of Oman. Frustrated by under-representation in Parliament despite winning 54% of the vote in the July 1963 election, the mainly African Afro-Shirazi Party (ASP) allied itself with the left-wing multiracial Umma Party, and early in the morning of 12 January 1964 ASP member John Okello mobilised around 600–800 revolutionaries on the main island of Unguja (Zanzibar Island). Having overrun the country's police force and appropriated their weaponry, the insurgents proceeded to Zanzibar Town where they overthrew the Sultan and his government. Reprisals against Arab and South Asian civilians on the island followed; the resulting death toll is disputed, with estimates ranging from several hundred to 20,000. The moderate ASP leader Abeid Karume became the country's new president and head of state, and positions of power were granted to Umma party
Hiyo pfd iko wapi mkuu?
 
Mohamed Said,

..hebu tumegee kwa uchache wasifu wa khamis abdulla ameir.
JK,
Sijui kama uliona hii hapo chini:

KUMBUKUMBUKU ZA ''THEORETICIAN'' KHAMIS ABDULLAH AMEIR ZIKO UWANJANI

Haya ndiyo maajabu makubwa katika historia za Afrika kuwa wanaostahili kupewa sifa hawasifiwi wala hawapewi medali sifa zinakwenda kwa wale Waingereza wanawaita, ''syncopaths.''

Hawa ni wale watu ambao bila aibu hata chembe watapinda migongo yao hadharani sa saba mchana hadharani wakainama kumfunga viatu muhisani wao.

Mifano iko mingi na watu hawa hawagusiki.
Wako juu ya sheria zote.

Hii ni fani maalum ambayo kwa hakika na bahati nzuri ni watu wachache sana wanaiweza na kuimudu.

Lakini ni fani ya yenye manufaa makubwa sana inapodumu na wewe na halikadhalika ni fani yenye kubeba hatari nyingi inapokugeukia ikawa kibidu na kukupa mgongo.

Sikupatapo kumsikia Khamis Abdullah Ameir kabla mpaka siku moja Ahmed Rajab aliponiandikia kuhusu kitabu cha Hashil Seif, ''Mimi Umma Party na Mapinduzi ya Zanzibar, '' akanitajia jina lake na kunitahadharisha kuwa huyu mtu si mtu wa kawaida katika historia ya Zanzibar.

Ahmed Rajab akamtaja kwa sifa kubwa akamwita, ''Theoretician.''
Hakika nilishtuka na nikapigwa na mshangao.

Nimeshtuka kwa sababu namjua Ahmed Rajab si mtu wa kutupa maneno yake ovyo ovyo.
Nilipigwa na mshangao kwa kuwa nilijiuliza imekuwaje mtu muhimu kama huyu sijamsikia nusu karne ya mimi kusoma historia ya Zanzibar na propaganda zote za Mapinduzi Daima?

Nilikutana na Khamis ''Theoretician'' Abdullah Ameir katika ukumbi wa ZIRPP nilipoalikwa kuwasilisha kitabu cha Hashil Seif, ''Mimi, Umma Party na Mapinduzi ya Zanzibar.''

Niikwenda kumsalimu na mara moja nilitambua kuwa Khamis Abdullah Ameir ni aina ya wale watu ambao wapo lakini hawaonekani.

Yupo lakini huisikii sauti yake.
Hasemi lakini yuko wala huhisi kuwepo kwake.

Lakini yupo ila wewe humuoni.
Anasikiliza zaidi ya yeye kuzungumza.

Huisikii sauti yake.

Utamfahamu na kumtambua katika yale atakayofanya.
Tulisalimiana na nikamtia katika mazungumzo na kumuulza kama anaandika kumbukumbu zake.
Yeye ananisikiliza na tabasamu kubwa liko usoni kwake.

Nikamuomba tupige picha ya pamoja na nikamfahamisha picha hizi ni kwa ajili ya Maktaba yangu na akanikubalia.

Kuanzia pale nikataka kumjua huyu ''Theoretician,'' Khamis Abdullah Ameir.
Naam nilifurahi na nafsi yangu.

Alinifikisha London ya miaka ya 1950 kabla hata lile wimbi la ''Wind of Change,'' la Harold Macmillan halijajikusanya.

Hii ilikuwa London iliyokuwa inafukuta na joto la siasa za kujikombia na ukoloni.

Khamis Abdullah Ameir yuko London kijana mdogo wa Kizanzibari kajikuta yuko pamoja na vijana wengine kutoka nyumbani Zanzibar na nchi nyingine za Afrika ya Mashariki, vijana ambao watakuja kuacha alama katika historia za ukombozi wa nchi zao kutoka katika ukoloni.

Vijana ambao wengine maisha yao yalikatika ndani ya nchi zao katika juhudi za ukombozi na wengine baadae.

Kwa kawaida vitabu vinavyoandikwa na wanamapinduzi huwa ''drab,''' nikiazima msamiati wa Kiingereza kutoka kwa mwalimu wangu Sheikh Mohamed Mlamali Adam, Allah amrehemu.

Yaani vitabu vinakosa mvuto kwa kukosa ya kuandika lakini mwandishi hakubali kuwa hana la kuandika ambalo halifahamiki.

Matokeo yake badala ya kuwa na kitabu kunakuwa na kabrasha la mkutano mkuu wa chama chake.

Mwandishi haelewi kuwa ili kitabu kiwe kitabu ni lazima kiwe na elimu mpya ambayo jamii haina.
Hii ni tofauti na vitabu vingine katika historia ya Zanzibar vilivyoandikwa na Wazanzibari wengine, ''removed,'' yaani waliombali na hawa kwa fikra.

Nina hakika Khamis ''Theoretician'' Abdullah Khamis anakuja na kitabu kitakacho tusomesha mengi tuliyokuwa hatuyajui hata kwa mbali sana.

 
Back
Top Bottom