Scolari Ndenga
JF-Expert Member
- Aug 4, 2008
- 271
- 43
Wakuu Habari zilizonifikia ni kwamba viongozi wakuu wa BAVICHA John Heche Mwenyekiti na Katibu Mkuu Deogratias Munishi jana waliutetemesha mji wa Mpanda kwa kuishukia vikali CCM na Sekikali yake kwa kuidhoofisha Tanzania kimaendeleo.
Wakati John Heche akiwataka polisi kumtia mbaroni Martini Shegela kwa uchochezi wa kuwataka vijana wa ccm kupambana na wale wa Chadema na pia kuongeza kuwa hata kama ni kupambana basi watoto wa ccm ni watoto wa laktojeji na wale wa Chadema ni ngangari kweli kweli katibu mkuu wa Bavicha Deo Munishi amesema mikutano ya Chadema hailindi na jeshi la polisi ama kikundi chochote kile bali wananchi wenyewe hivyo CCM wanapojipanga kuvamia mikutano hiyo daima wataangukia pua.
Wakati John Heche akisema kuwa umasikini wa Tanzania unasababishwa na uchovu na udhaifu wa serikali ya CCM chini ya Kikwete, Pinda na Makinda, Munishi aliwaambia wananchi wa mpanda kuwa katika kushughulikia tatizo la umasikini Tanzania hakuna njia ya mkato zaidi ya kuunganisha uchumi wa vijijini na wa mjini na hii ni kwa kupitia mapinduzi ya KILIMO ambacho ni msingi wa mapinduzi ya viwanda nchini na si kwa ngonjera na mapambio ya kilimo kwanza ya serikali ya CCM.
Munishi alisema kuwa CCM ni janga la taifa, ni laana kwa taifa na ni mkosi kwa taifa na ana uhakika thabiti kuwa kuendelea kuwepo kwake Tanzania ni kuendelea kuhatarisha utulivu uliopo ambao wao CCM wanauita amani. Wakati John Heche akiendelea kuonyesha udhaivu wa serikali ya CCM kwa kusema kuwa ni aibu kwa rais Kikwete kuendelea kuiabisha Tanzania kwa kuwa matonya na kumtaka aone aibu kwa kupishana angani akiwa na misaada ya vyandarua akitokea ughaibuni huku akipishana na wazungu angani wakitokea Tanzania wakiwa na dhahabu Deo Munishi aliwageuzia kibao CCM kwa kuwaita chama cha Magaidi kwani kimekua kikiratibu vitendo vya kigaidi akitolea mfano vile vya Sigida chini ya Mwigulu Nchemba aliyekodi vijana kutoka Dar es salaam kufanya vurugu kwenye mikutano ya Chadema na vile vya Iringa alivyofanyiwa Mchungaji Msigwa kwenye mikutano ya Chadema.
Munishi aliendelea kuwataka wananchi wa Rukwa na mpanda kuwa makini katika mchakato wa katiba mpya kwa kuwaomba wananchi wakatae uwepo wa vyeo vya wakuu wa wilaya na mikoa kwa kuwa ni sehemu ya mzigo kwa walipa kodi kwani hawana kazi wanazozifanya.
Leo vijana hawa wataendelea kutikisa katika jimbo la Mpanda Vijijini na kesho watamshukia Waziri Mkuu kwenye jimbo la Mpanda Mashariki na Ijumaa watautetemesha Mji wa Sumbawanga.
Wakati John Heche akiwataka polisi kumtia mbaroni Martini Shegela kwa uchochezi wa kuwataka vijana wa ccm kupambana na wale wa Chadema na pia kuongeza kuwa hata kama ni kupambana basi watoto wa ccm ni watoto wa laktojeji na wale wa Chadema ni ngangari kweli kweli katibu mkuu wa Bavicha Deo Munishi amesema mikutano ya Chadema hailindi na jeshi la polisi ama kikundi chochote kile bali wananchi wenyewe hivyo CCM wanapojipanga kuvamia mikutano hiyo daima wataangukia pua.
Wakati John Heche akisema kuwa umasikini wa Tanzania unasababishwa na uchovu na udhaifu wa serikali ya CCM chini ya Kikwete, Pinda na Makinda, Munishi aliwaambia wananchi wa mpanda kuwa katika kushughulikia tatizo la umasikini Tanzania hakuna njia ya mkato zaidi ya kuunganisha uchumi wa vijijini na wa mjini na hii ni kwa kupitia mapinduzi ya KILIMO ambacho ni msingi wa mapinduzi ya viwanda nchini na si kwa ngonjera na mapambio ya kilimo kwanza ya serikali ya CCM.
Munishi alisema kuwa CCM ni janga la taifa, ni laana kwa taifa na ni mkosi kwa taifa na ana uhakika thabiti kuwa kuendelea kuwepo kwake Tanzania ni kuendelea kuhatarisha utulivu uliopo ambao wao CCM wanauita amani. Wakati John Heche akiendelea kuonyesha udhaivu wa serikali ya CCM kwa kusema kuwa ni aibu kwa rais Kikwete kuendelea kuiabisha Tanzania kwa kuwa matonya na kumtaka aone aibu kwa kupishana angani akiwa na misaada ya vyandarua akitokea ughaibuni huku akipishana na wazungu angani wakitokea Tanzania wakiwa na dhahabu Deo Munishi aliwageuzia kibao CCM kwa kuwaita chama cha Magaidi kwani kimekua kikiratibu vitendo vya kigaidi akitolea mfano vile vya Sigida chini ya Mwigulu Nchemba aliyekodi vijana kutoka Dar es salaam kufanya vurugu kwenye mikutano ya Chadema na vile vya Iringa alivyofanyiwa Mchungaji Msigwa kwenye mikutano ya Chadema.
Munishi aliendelea kuwataka wananchi wa Rukwa na mpanda kuwa makini katika mchakato wa katiba mpya kwa kuwaomba wananchi wakatae uwepo wa vyeo vya wakuu wa wilaya na mikoa kwa kuwa ni sehemu ya mzigo kwa walipa kodi kwani hawana kazi wanazozifanya.
Leo vijana hawa wataendelea kutikisa katika jimbo la Mpanda Vijijini na kesho watamshukia Waziri Mkuu kwenye jimbo la Mpanda Mashariki na Ijumaa watautetemesha Mji wa Sumbawanga.