Congo
JF-Expert Member
- Mar 13, 2008
- 2,079
- 2,334
Nimewataja hao waheshimiwa wabunge wetu. Naheshimu ubunge wao. Lakini baadhi ya maneno yatokayo midomoni mwao yanaleta ukakasi.
1. Mtu atakuwaje mwalimu wa biashara wakati hana hata kiosk. Huu ni upotoshaji. Elimu ilianza bila kuandika mahali pppote. Maandishi yalippanza elimu ile ikaanza kuwekwa kwenye maandishi. Maandishi na elimu hiyo imekuwa ikiboreshwa siku hata siku mpaka tuliyonayo sasa hivi.
Hivyo iko kwenye maandishi. Yale maandishi ndio yanayofundishwa mashuleni na vyuoni. Faida inakuwa kabisa kama una elimu ile na ukafanya kile ulichosomea. Na mfano elimu ya biashara imetokana na matukio ya kawaida kabisa ya kibiashara yanayotokea kila siku.
Ola sasa matukio hayo yako kwenye maandishi. Mfano mfanya biashara yeyote awe amesoma au hajasoma anajua neno MTAJI WA BIASHARA.
Na heshima inatotakiwa kuwekwa ukishasema huu ni mtaji wa biashara. Elimu ikauweka kwenye vitabu ikauita CAPITAL na OWNER'S EQUITY.
Hivyo kusema mtu atafundishaje biashara hana kiosk ni upotoshaji mkubwa sana. Kuna elimu ya ujenzi wa barabara, je anayefundisha elimu hiyo unataka awe amejenga barabaraba yake?
2. Kulaumu wasomi kila kukicha. Nashangaa sana. Hivi barabara zetu, mahospitali yetu, mabenki yetu, maji, n.k. yataendeshwaje bila kutumia wasomo wetu? Wasichanganye taaluma na siasa. Hakuna taaluma ya wizi. Wizi ni uhalifu unashughulikiwa kama uhalifu mwingine. Kama watu wameiba wakajenga muundombinu mbovu sio kwamba walifundishwa hivyo. Hao ni wahalifu, na uhalifu wao ni jambo lao binafsi.
3. Sasa likaja kubwa zaidi. Hoja ya.kuvalisha ng'ombe hereni (ear tags) ikapongwa kwa nguvu zote, mtu akafikia kusema kumvalisha ng'ombe hereni ni ushoga. Hapo ndio tunajiuliza tunaelekea wapi. Mimi naelewa kuwa sio ng'ombe anatakiwa kivalishwa hereni, anatakiwa pia.kuwa na LOGBOOK yake.
Itakayoandikwa kila taarifa kuanzia siku anazaliwa, matibabu anayopata, lini ameoshwa, amebadilisha wamiliki wangapi n.k. Huwezi kuuza nyama nje kwenye nchi zilizoendelea bila kuwa na taarifa sahihi ya ng'ombe na hatimaye nyama.
Wenzetu wamefikia wanawamezesha vifaa maalumu vya kielektroniki. Taarifa zao zinasomwa kila hatua. KUPIGA CHAPA NG'OMBE ni mtindo umeshapitwa na wakati.
Mwisho, niwaulize hao Waheshimiwa. Hivi biashara zao hawana wahasibu? Je, nyumba zao wanajengewa na wasio mainjinia? Wanakiumwa wanaenda kwa waganga wa kienyeji?
Katiba yetu inasema ili kuwa mbunge LAZIMA ujue kusoma na kuandika.
1. Mtu atakuwaje mwalimu wa biashara wakati hana hata kiosk. Huu ni upotoshaji. Elimu ilianza bila kuandika mahali pppote. Maandishi yalippanza elimu ile ikaanza kuwekwa kwenye maandishi. Maandishi na elimu hiyo imekuwa ikiboreshwa siku hata siku mpaka tuliyonayo sasa hivi.
Hivyo iko kwenye maandishi. Yale maandishi ndio yanayofundishwa mashuleni na vyuoni. Faida inakuwa kabisa kama una elimu ile na ukafanya kile ulichosomea. Na mfano elimu ya biashara imetokana na matukio ya kawaida kabisa ya kibiashara yanayotokea kila siku.
Ola sasa matukio hayo yako kwenye maandishi. Mfano mfanya biashara yeyote awe amesoma au hajasoma anajua neno MTAJI WA BIASHARA.
Na heshima inatotakiwa kuwekwa ukishasema huu ni mtaji wa biashara. Elimu ikauweka kwenye vitabu ikauita CAPITAL na OWNER'S EQUITY.
Hivyo kusema mtu atafundishaje biashara hana kiosk ni upotoshaji mkubwa sana. Kuna elimu ya ujenzi wa barabara, je anayefundisha elimu hiyo unataka awe amejenga barabaraba yake?
2. Kulaumu wasomi kila kukicha. Nashangaa sana. Hivi barabara zetu, mahospitali yetu, mabenki yetu, maji, n.k. yataendeshwaje bila kutumia wasomo wetu? Wasichanganye taaluma na siasa. Hakuna taaluma ya wizi. Wizi ni uhalifu unashughulikiwa kama uhalifu mwingine. Kama watu wameiba wakajenga muundombinu mbovu sio kwamba walifundishwa hivyo. Hao ni wahalifu, na uhalifu wao ni jambo lao binafsi.
3. Sasa likaja kubwa zaidi. Hoja ya.kuvalisha ng'ombe hereni (ear tags) ikapongwa kwa nguvu zote, mtu akafikia kusema kumvalisha ng'ombe hereni ni ushoga. Hapo ndio tunajiuliza tunaelekea wapi. Mimi naelewa kuwa sio ng'ombe anatakiwa kivalishwa hereni, anatakiwa pia.kuwa na LOGBOOK yake.
Itakayoandikwa kila taarifa kuanzia siku anazaliwa, matibabu anayopata, lini ameoshwa, amebadilisha wamiliki wangapi n.k. Huwezi kuuza nyama nje kwenye nchi zilizoendelea bila kuwa na taarifa sahihi ya ng'ombe na hatimaye nyama.
Wenzetu wamefikia wanawamezesha vifaa maalumu vya kielektroniki. Taarifa zao zinasomwa kila hatua. KUPIGA CHAPA NG'OMBE ni mtindo umeshapitwa na wakati.
Mwisho, niwaulize hao Waheshimiwa. Hivi biashara zao hawana wahasibu? Je, nyumba zao wanajengewa na wasio mainjinia? Wanakiumwa wanaenda kwa waganga wa kienyeji?
Katiba yetu inasema ili kuwa mbunge LAZIMA ujue kusoma na kuandika.